mchonjoya
Member
- Aug 17, 2016
- 80
- 198
Habari members,
Kiukweli haya maisha hayana mwenyewe.
Nikirudisha nyuma kumbukumbu zangu za kimaisha siamini kama leo hii nakula ninachotaka na sio ninachopata.
Kuna kipindi wakuu maisha yanakupitisha katika mapitio magumu ili iwe fundisho kwako na kukujenga kimaarifa. Pia, pia upate kutambua nani rafiki na nani adui.
WANDUGU
kuna kipindi nilikula msoto tena msoto hasa kiasi nikiaa mwenyewe machozi yananitoka. Maisha magumu hakuna mfano wake. Best zangu wote hawana habari tena na Mimi.
Naishi kwa kuzurula tu hapa mjini. Nyuma nina mke na watoto wawili. Nyumba ya kupanga Kodi inakaribia kuisha, chakula shida, kila kitu shida.
Nilipigika aisee vibaya sana. Pamoja na lumba hilo nilikuwa nawai kuondoka nyumbani kwenda kusiko julikana na kurudi usiku. Sikuchoka kuondoka nyumba na kwenda kutafuta riziki, sikuwahi kuonyesha unyonge kwa wapangaji wezangu, sikuwahi kujishusha kama MWANAMME nilijikaza kama sifa ya wanaume inavyosema (mateso).
Siku moja nikiwa nyumbani siku ya jpili nikiwa na family yangu nyumbani wife aliniambia amechoka kuishi maisha ambayo hayafuraii. Anataka kuondoka aende kwao na watoto atawachukua. Hakusema kwa maana mbaya no, lengo kunipunguzia mzigo wa majukumu.
Kiukweli niliumia sana mpaka mwanamke ananionea huruma, maana yake mimi sitoshi, na siwezi tena kulea familia. Nikamwambia nijibu maswali haya matatu kisha uende.
(1)Una uhakika na huko uendako maisha yatakuwa unavyotaka?
(2)Je, unaikumbuka kanuni ya NDOA?
(3)Nani mwenye kujua kesho yake?
Wazee sikuongea tena. Tumelala tumemka salama. Nikiwa kitandani wife akanigusa bega na KUSEMA TUTAKUFA WOTE, TUTADHALILIKA WOTE.
Wazee nilipata nguvu ya ajabu sana kuona mke kaongea maneno ya kishujaa. Kiukweli kuazia hapo sikuchagua cha KUFANYA hatimae nimevuka kipindi kigumu kilichodumu takriban miaka na miezi toka kufilisiwa na bank.
Je, Wewe uliishije kipindi huna mishe?
Njia gani ulikufanya ukatoboa?
WASHIKAJI SIO WATU. USIWEKE KISASA ILA USIWASAHAU.
Kiukweli haya maisha hayana mwenyewe.
Nikirudisha nyuma kumbukumbu zangu za kimaisha siamini kama leo hii nakula ninachotaka na sio ninachopata.
Kuna kipindi wakuu maisha yanakupitisha katika mapitio magumu ili iwe fundisho kwako na kukujenga kimaarifa. Pia, pia upate kutambua nani rafiki na nani adui.
WANDUGU
kuna kipindi nilikula msoto tena msoto hasa kiasi nikiaa mwenyewe machozi yananitoka. Maisha magumu hakuna mfano wake. Best zangu wote hawana habari tena na Mimi.
Naishi kwa kuzurula tu hapa mjini. Nyuma nina mke na watoto wawili. Nyumba ya kupanga Kodi inakaribia kuisha, chakula shida, kila kitu shida.
Nilipigika aisee vibaya sana. Pamoja na lumba hilo nilikuwa nawai kuondoka nyumbani kwenda kusiko julikana na kurudi usiku. Sikuchoka kuondoka nyumba na kwenda kutafuta riziki, sikuwahi kuonyesha unyonge kwa wapangaji wezangu, sikuwahi kujishusha kama MWANAMME nilijikaza kama sifa ya wanaume inavyosema (mateso).
Siku moja nikiwa nyumbani siku ya jpili nikiwa na family yangu nyumbani wife aliniambia amechoka kuishi maisha ambayo hayafuraii. Anataka kuondoka aende kwao na watoto atawachukua. Hakusema kwa maana mbaya no, lengo kunipunguzia mzigo wa majukumu.
Kiukweli niliumia sana mpaka mwanamke ananionea huruma, maana yake mimi sitoshi, na siwezi tena kulea familia. Nikamwambia nijibu maswali haya matatu kisha uende.
(1)Una uhakika na huko uendako maisha yatakuwa unavyotaka?
(2)Je, unaikumbuka kanuni ya NDOA?
(3)Nani mwenye kujua kesho yake?
Wazee sikuongea tena. Tumelala tumemka salama. Nikiwa kitandani wife akanigusa bega na KUSEMA TUTAKUFA WOTE, TUTADHALILIKA WOTE.
Wazee nilipata nguvu ya ajabu sana kuona mke kaongea maneno ya kishujaa. Kiukweli kuazia hapo sikuchagua cha KUFANYA hatimae nimevuka kipindi kigumu kilichodumu takriban miaka na miezi toka kufilisiwa na bank.
Je, Wewe uliishije kipindi huna mishe?
Njia gani ulikufanya ukatoboa?
WASHIKAJI SIO WATU. USIWEKE KISASA ILA USIWASAHAU.