Umeme wa Solar : Nini Kinahitajika na Kiasi Gani..?

Mambo ya kuangalia unapotaka kunua mfumo wa sola.

Watu wengi wametamani kuwa na nyumba nzuri na yenye umeme wa uhakika .Tatizo linakuja kwamba Tanesco imeshindwa na pengine kwa miaka 10 ijao itaendelea kushindwa ku supply umeme wa kutosha wa kukidhi mahitaji yaliopo na yatakayo ongezeka , hili limeweka familia nyingi- ukiachilia mbali viwanda katika power nightmare.

Wengi wanajiuliza nini wafanye kwanza waweze pata umeme kama hawajafungiwa umeme[ hapa sitaki kuelezea usumbufu uatakao upata wa kufuatilia wafanyakazi wa Tanesco pesa utakayolipa kulobby na hata muda kwa kweli ni kizungumkuti] pili wale waliofungiwa ni kama hawana umeme kwani muda mwingi wamekuwa kwenye giza na hata ratiba ya mgao wenyewe haieleweki labda kwa taneso pekee.

Wengi wamezunguka huku na huku na hata kwenda kwenye maduka mbalimbali ya umeme mbadala kama magenereta na sola. wale wa majenereta kama wemeweza pata generta nzuri nyingi ziko kati ya Mil 2.5- mpaka 12. kwa saizi ya nyumba ya kawaida lakini pia hii itaambatana na ununuzi wa mafuta kila siku[ bei yake nayo haieleki kama umeme wa tanesko], pia umeme huu umbatana na kelele na maintenence isiyoisha.

wale walioweza nunua za bei raisi nazungumzia kati ya laki 1.5-mill 2 basi nyingi labda hazifanyo kazi ndani ya miezi miwili au mitatu na hapa baada ya maintenenace cost ya kila wk kumwita fundi. bila kusahau kelele na matumizi makubwa ya mafuta bila kujai kupanda kwa gharama za mafuta.

Kwa wale walioweka sola na kubahatika kukutana na bora sale dealer basi wame hesabu maumivu kwani nyingi pia zimeacha kufanya kazi ndani ya miezi miwili mpaka mitano bila kujali gharama kiasi gani ulilipia hasa unafuu ulipotumika kama kigezo cha manunuzi.

Kwa wale waliobahatika kuwapata wataalam thabit wanaothamini kazi zao na mteja basi walipata maumuvu ya mwanzoni ya kutoa pesa lakini wameendelea kupata furaha ya muda mrefu ya system inayofanya kazi vizuri na bila kuhitaji tena kuingia mfukoni kumtafuta fundi wala kunua mafuta .

Sasa basi wengi mtajiuliza ni nini tufanye kuondoka na adha hii ......


Majibu ni marefu na kwa leo nitawaletea kiasi kwa kadri nitakavyoweza.
  1. Kununua sola inahitaji maandalizi na kupanga kwa muda mrefu ikiwezekana kabla ya kuanza kujenga nyumba. kumbuka sola nzuri intosha kuendesha shughuli zote za nyumbani na ksuiwe na haja ya umeme wa tanesco tena.
  2. Unahitaji kuzunguka na kuwaona wataalamu wanaoweza kukufanyia makadilio mazuri ya mahitaji yako na kukupa option mbalimbali ili kukusaidia kufanya uamuzi.
  3. Unahitaji kujua maduka yenye uzoefu na biashara hiyo na hata kwenda online kupata uelewa zaidi. kumbuka usije ukajisumbua kununua online, unaweza pata kanyanga ni vizuri ununue kwa certified registered solar contractor ili upate guantee ya vifaa vyako. kwani kumbuka sola ni investment kubwa inayoitaji guarantee.
  4. Unahitaji kujua sifa na specification na kuweza kutafsiri kwa lugha rahisi hasa manufaa yake kwako. Nitawaletea taratibu somo hili kila nitakapokuwa napata nafasi kwani nahamini mteja anapofahamu zaidi anakuwa katika wakati mzuri wa kufanaya maamuzi hata kutunza kifaa chake.
  5. Unahitaji kujua upatikanaji wa spea kwani kifaa kimoja tu kikiharibika cha sola na ukishindwa kuki replace basi mfumo mzima utazimika na investment yako kwenda bure.
  6. Unahitaji kuwa na dealer amabaye atakuwa anakupa ushauri pindi utakapohisi mfumo wako unatatizo na ndio maana nasisistiza kunua hapa ncini ili muaazaji wake awe ndio mshauri wako.
Nitarejea kesho kwa maelezo zaidi.... mnaopitia forum hii msichokee kupitia kila siku ili kuelimika zaidi......

Mie ni nayo solar system nimeitumia mwaka wa pili sasa. Zipo panels mbili, battery mbili njaa inventor. Inawasha taa muda wote (nyumba yangu ina taa zaidi ya 20), vile vile Anaweza kuonesha TV kwa saa nne mpaka tano. Pamoja na mambo madogo madogo kama kucharge simu nk.

Swali langu ni je naweza kui upgrade iweze kurun fridge kwa mfano au hata kunyoosha nguo? Ninahitaji kununua nini zaidi?
 
Mie ni nayo solar system nimeitumia mwaka wa pili sasa. Zipo panels mbili, battery mbili njaa inventor. Inawasha taa muda wote (nyumba yangu ina taa zaidi ya 20), vile vile Anaweza kuonesha TV kwa saa nne mpaka tano. Pamoja na mambo madogo madogo kama kucharge simu nk.

Swali langu ni je naweza kui upgrade iweze kurun fridge kwa mfano au hata kunyoosha nguo? Ninahitaji kununua nini zaidi?

Panel 2 na betri 2 ni ndogo sana, sina uhakika na ukubwa wa panel zako na betri lakini najua friji na pasi huwezi kutumia.

Isipokuwa kuna pasi za DC (wanaita pasi za solar), umeme wake unatoka moja kwa moja kwenye betri unaweza kutumia, unahitaji kupata mtaalamu akuthaminishie.
 
wakati solar panel ya China ni kati ya $1-1.5/ w solar za Europe German inclusine ni kati ya 2-2.5/ w ... Na uwezi kuagiza PANEL moja ni Gharama zaidi .. kwani shipping ni gharama kwa item moja hasa freight cost
 
Mkuu naona kama hii bei huja-update kwa sababu kwa hapa TZ pannel za Mjerumani naweza kupata Watt 1000 kwa sh 3,000,000 ambayo ni equivalent na USD 1,700.

Panel zimeshuka sana bei huku ukilinganisha na 2011. Jaribu kutazama upya bei then tuwasiliane.
Nımekutajıa bei hıyo kwa ajili

usafirishaji wa haraka ukituma pesa zako ili uweze kupata hizo Panel zako kwa muda usiopunguwa Siku 10 nitakusafirishia kwa njia ya

kargo za watu binafsi la kama unataka nikutumie kwa njia ya kawaida usafirishaji wa posta gharama yake itakuwa ni dollar 2500 kwa

Panel yenye Wattt 1000. ukihitaji wasiliana na mimi kwa njia ya Email Baruwa ya pepe Email Address yangu hii hapa fewgoodman@hotmail.com
 
Kyenju Nime attach quoatation za 1000W, 2000W na 3000w .. summary tu ni kwamba

1000w solar PV system

  1. solar panel 4 za 250W/24v
  2. solar dry battery 4 za 150AH/12
  3. Charger controller 1 ya 40A
  4. Inverter ya 1000W
  5. Accessories na labour charger
Inaweza washa
  1. Taa 11 za 7w for 6hrs
  2. LCD tv 32" na accessories zake 6hrs
  3. Washing machine 1 for 1 hrs
  4. Fridge 180W MOJA for 24 hrs
  5. Fan 2 for 8 hrs
  6. printer na lap top 1 for 2 hrs
  7. Total $3712

2000W solar PV system

  1. Solar panel 8 za 250W/24V
  2. Solar dry battery 8 za 150AH
  3. Charger controller ya 60A
  4. Inverter ya 2000w/24v
  5. Accessories na labour charge

Inaweza washa

  1. Taa 11 za 7w for 6hrs
  2. LCD tv 32" na accessories zake 6hrs
  3. Washing machine 1 for 1 hrs
  4. Fridge 180W MOJA for 24 hrs
  5. Fan 2 for 8 hrs
  6. printer na lap top 1 for 2 hrs
  7. Pasi moja for 0.5 hr
Total $6192

3000W solar PV system

  1. Solar panel 12 za 250W/24V
  2. Solar dry battery 12 za 150AH
  3. Charger controller ya 60A @ 2
  4. Inverter ya 2000w/24v@ 1
  5. Accessories na labour charge

Inaweza washa

  1. Taa 20 za 7w for 8hrs
  2. LCD tv 32" mbili na accessories zake 8hrs
  3. Washing machine 1 for 1 hrs
  4. Fridge 180W MOJA for 24 hrs
  5. Fan 2 for 8 hrs
  6. printer na lap top 1 for 2 hrs
  7. Pasi moja for 0.5 hr
Total $8813


Kwa maelezo zaidi wasiliana nami kwa PM
VoiceOfReason; M-pesa, Paje, Bukyanagand, MziziMkavu, Mwanaharakati, BAK Misterdennis Papizo Baba_Enock, KIBURUDISHO Osaba SHAROBALO m_kishuri
watu wanataka bei rahisi hizo bei ulizoweka sizani kama watanunuwa si unajuwa wabongo kwa kupenda ubwete!!!!
 
Hizi bei siyo mbaya, anayetaka bei rahisi zaidi huyo atakuwa anahitaji device za kichina.
Na Hizo Solar Panel za kichina ni Feki utatumia labda mwaka au miak 2 kwisha kazi hazidumu sana kwa sababu ya bei zake rahisi zinakuw ani Feki solar Panel toka china. Solar Panel zangu mimi toka Ulaya sio za kichina.
 
Kwanza kabisa napenda kutokukubaliana na wewe kwamba kila kitu kinachotengenezwa China ni FEKI!!!. kwa sasa hata Europe na AMERIKA karibu Asilimia 60% ya vifaa vinavyotumika vinatengenezwa china.

China wana viwango tofauti kwa kadili ya mahitaji ya mteja...Lakini kwa kiwango kikubwa solar Panel zinazotoka china zina viwango vya ubora wa hali ya juu .. na ndio bidhaa nying zinazouzwa Europe na America kwa brainding ya viwanda vya Europe na America.

WA europe wana- chofanya ni kuzipackage vizuri na kuzibrand zaidi ili zionekane kwamba ni bora zaidi lakini zote zimetengenezwa china kutokana na unafuu wa labour force na material.

Na bidhaa nyingi tunazonunua sisi zinapitia kwenye vyombo husika za ku control quality and specification zake ni za kiwango cha kimataifa.

Panel nying zina life span ya 45 years na huja na warranty ya 25 years .. kwa hiyo sio kweli kuwa Panel za china ni FEKI na kwamba zinakaa miaka 2 tu ... huu ni uongo wa asubuhi


Na Hizo Solar Panel za kichina ni Feki utatumia labda mwaka au miak 2 kwisha kazi hazidumu sana kwa sababu ya bei zake rahisi zinakuw ani Feki solar Panel toka china. Solar Panel zangu mimi toka Ulaya sio za kichina.
 
Nikitaka panel ya 100wtt, control charger 20am na inverter ya 300wtt itanigharimu kiasi gani pesa ya hapa bongo?
Ukitaka panel ya 100wtt, control charger 20am na inverter ya 300wtt kwa gharama za huku nilipo mpa kukufikia wewewe kwa pesa za Tanzania itakugharimu Shillingi Millioni 2 na laki 2. mimi nipo nje ughaibuni ukiweza wasiliana na mimi kwa njia ya Email yangu hii fewgoodman@hotmail.com
 
Kwanza kabisa napenda kutokukubaliana na wewe kwamba kila kitu kinachotengenezwa China ni FEKI!!!. kwa sasa hata Europe na AMERIKA karibu Asilimia 60% ya vifaa vinavyotumika vinatengenezwa china.

China wana viwango tofauti kwa kadili ya mahitaji ya mteja...Lakini kwa kiwango kikubwa solar Panel zinazotoka china zina viwango vya ubora wa hali ya juu .. na ndio bidhaa nying zinazouzwa Europe na America kwa brainding ya viwanda vya Europe na America.

WA europe wana- chofanya ni kuzipackage vizuri na kuzibrand zaidi ili zionekane kwamba ni bora zaidi lakini zote zimetengenezwa china kutokana na unafuu wa labour force na material.

Na bidhaa nyingi tunazonunua sisi zinapitia kwenye vyombo husika za ku control quality and specification zake ni za kiwango cha kimataifa.

Panel nying zina life span ya 45 years na huja na warranty ya 25 years .. kwa hiyo sio kweli kuwa Panel za china ni FEKI na kwamba zinakaa miaka 2 tu ... huu ni uongo wa asubuhi
Usifananishe Solar Panel wanayoleta Wachina huko Kwenye Dunia ya Tatu

na Solar Panel ya kichina wanayoleta bara la Ulaya kuwa ni sawasawa? ukifikiria hivyo itakula kwako. Solar Panel wanayoleta

Wachina huku ulaya ni quality ni bora mara 100 zaidi ya hiyo Solar Panel wanayoleta huko nyumbani. Wachina wanatengeneza vitu

kwa ajili ya watu wa Bara la Ulaya na bara la Afrika vitu vinavyo kwenda Bara la la ulaya ni imara na ni bora zaidi ya vitu vinavyokuja

huko bara la Afrika. Kwa mfano simu ya ulaya huwezi kufananisha na simu mnazo nunuwa huko kwenu kwenye maduka yenu huko

zinakuwa simu sio imara zaidi. Ukubali au ukatae shauri yako.
 
Na mwenzetu sijui hivyo vifaa vyako vimetengenezwa nchi gani , halafu kuhusu panels hujasema kama ni zile za kijani au nyeusi isiyokoza!
 
Kaka MziziMkavu... unazungumza na mtu aliyeishi Ulaya na kutembelea karibu nchi nyingi za Ulaya... Vifaa vya kichina vyipo kwa wingi barani ulaya na vimekuwa ndio kimbilio la wengi.
Vifaa vyingi vya sola vinafata standard za kimataifa na ndio maana kwa sasa ubora na bei ya vifaa vyingi haina tofauti.either umenunua ulaya au Africa.. tofauti kubwa ipo kwenye kodi na uwezo ww kukwepa kodi.. ndik maana unaona Africa bei wakati mwingine ni nafuu kuliko Ulaya pamoja.na kuwa na high shipping cost.
Nakushauri acha ulimbukeni wa kufulikiri kila kinachotoka China ni feki wakati wenye Asili ya Ulaya nao wanavitumia bila shida.

Usifananishe Solar Panel wanayoleta Wachina huko Kwenye Dunia ya Tatu

na Solar Panel ya kichina wanayoleta bara la Ulaya kuwa ni sawasawa? ukifikiria hivyo itakula kwako. Solar Panel wanayoleta

Wachina huku ulaya ni quality ni bora mara 100 zaidi ya hiyo Solar Panel wanayoleta huko nyumbani. Wachina wanatengeneza vitu

kwa ajili ya watu wa Bara la Ulaya na bara la Afrika vitu vinavyo kwenda Bara la la ulaya ni imara na ni bora zaidi ya vitu vinavyokuja

huko bara la Afrika. Kwa mfano simu ya ulaya huwezi kufananisha na simu mnazo nunuwa huko kwenu kwenye maduka yenu huko

zinakuwa simu sio imara zaidi. Ukubali au ukatae shauri yako.
 
Last edited by a moderator:
Kaka MziziMkavu... unazungumza na mtu aliyeishi Ulaya na kutembelea karibu nchi nyingi za Ulaya... Vifaa vya kichina vyipo kwa wingi barani ulaya na vimekuwa ndio kimbilio la wengi.
Vifaa vyingi vya sola vinafata standard za kimataifa na ndio maana kwa sasa ubora na bei ya vifaa vyingi haina tofauti.either umenunua ulaya au Africa.. tofauti kubwa ipo kwenye kodi na uwezo ww kukwepa kodi.. ndik maana unaona Africa bei wakati mwingine ni nafuu kuliko Ulaya pamoja.na kuwa na high shipping cost.
Nakushauri acha ulimbukeni wa kufulikiri kila kinachotoka China ni feki wakati wenye Asili ya Ulaya nao wanavitumia bila shida.
Ninarudia tena kukwambia Solar Panel ya kutoka china inayokuja huku ulaya huwezi kuifananisha na Solar Panel ya kutoka

China wanayoleta huko Bara la Afrika ni Tofauti Uimara wake. Jaribu kuchunguza maneno yangu utakuja kupata ukweli ndani yake.

kwa Mfano simu mnazo nunuwa huko kwenu kwenye Maduka Makubwa ya hapo mjini Dares-Salaam Maduka ya Mlimani au Shopping

Centre Simu hizo zinatoka china na sio imara tofauti na simu nitakayo kuja nayo huku ingwa ni Wachina hao hao wanaotengeneza

vituı imara na vitu feki kazi kwako.
 
wandugu kwanza poleni ni ukweli usiopingika kwamba solar panel per watt ni aghali Tz compare na China. Kwanza ilikuwa USD 6.2 kwenye miaka miwili iliyopita na bei imeendelea kupungua mpaka kufika $ 3.6 per watt kwa sasa . lakini mkumbuke ya kuwa kuweka solar ya 2KW kwa household bado ni investment kubwa kwani unahitaji zaidi ya sola panel kukamilisha mfumo . nitawapa mchanganuo kwa kifupi

Solar panel 2000w @$3.6 = $7200; Charger controller za kutosha kuimili hizo panel ya 60A= 2 @ $225=$450 utahitaji inverter angalau ya 7000W kwa matumizi ya kuweza kupower Freedge na jiko anagalau la plate 2 za 1000W each =$5200 bado utahitaji Batteries kwa kuweza kustore umeme wako na kwa mfumo huo wa 2KW utahitaji angalau battery 24 za 150AH amabazo kwa bei ya sasa ni karibu $263 @24=$ 6312 hapo utahitaji pia mamabo ya waya na mounting pia na gharama za ufundi ambazo hazitapungua $300 . kwa hiyo utaona kupata mfumo wa sola wa 2000W per day itakughalimu karibu $19,462 kama utanunua vifaa hapa nchini. karibu 32.1M TZS. kuweka umeme utakaokuwa na karibu nguvu sawa na umeme wa tanesko. Bila shaka mtakubaliana nami kwamba hii ni investment kubwa kufanywa na Mtanzania wa kawaida na ndio maana L's solution tunakuja na suluhisho la kukupatia umeme kulingana na mahitaji muhimu bila kuathiri mfuko wako.


Tunazo option mbalimbali za kukupatia umeme utakaokidhi nagalau mahitaji muhimu kama taa, TV system c/w decoder, music systems na DVD players etc, Fridge whether ni double door or single na Kuacha matumizi ya Jiko kutumika kwa sorce nyingine kama Gas, Mkaa, kuni n.k

Option hizi zime prove kutatua mahitaji karibu asilimia 80 ya mahitaji ya kila siku ya familia. Tafadhali wasiliana nami kwa simu namba +255 787 00 1525 au +255 715 00 15 25 kwa free quote na ushauri zaidi . Karibu L's solution kwa suluhisho lako la umeme wa jua.

Mzee ngungi safi sana..Nitakutafuta
 
Mkuu naomba unifahamishe kidogo juu ya hivi vipimo vya battery yaani mAh (MicroAmpere-Hour) inamaana gani kima matuzi
 
Back
Top Bottom