Uliwahi kupata mikasa gani kwa kuishi kwa ndugu?

Morg

JF-Expert Member
Oct 20, 2018
1,301
1,767
Habari za muda huu, ni siku tulivu sana hapa. Jiji la Dar es Salaam kumekucha salama, ingawa kulikuwa na upepo wa baridi sana, poleni na natumaini kila mmoja wetu ni mzima kabisa. Nawatakia kila la kheri katika pilika za kuijenga Tanzania kuwa kubwa tena, yenye amani na upendo. Twende kwenye mada.

Kuna kipindi kwenye Life cycle ya kimaisha ilinifanya nihamie kwa uncle wangu kuishi nae ili kuangalia uwezekano wa kufanya maisha. Enzi zile ndio nimemaliza masomo nipo home tu nikapata mchong huo, nilikuwa very excited sana na hili, maana nilikuwa ninavuta picha fulani hivi kabla ya kufika kwa uncle Dar.

Siku mbili baada ya kupewa taarifa ya safari nilijiandaa lakini ilikuwa ghafla sana kutokana na uchu wa safari ya kuja huku hata watu niliokuwa nawadai pesa zangu wengi niliwapotezea, kitu ninachojutia sana.

Siku ya safari ikawadia, panda nikapanda basi safari mpaka Dar, nifika mida ya saa moja hivi enzi za ubungo terminal pale, akaja mshakaji aliyekuwa anakaa kwa huyo uncle, wakanichukua freshi mpaka home.

Hapo nipo so excited na wishes nying sana how it's going to be in the up coming day's, nikachil, nikafika home. Yale mapokezi tuu yakanidropisha point. Yule mke wake alikuwa anagubu sana, nilivyofika nikaona hapa chakike.

Picha linaanza kulipokucha tunaamshwa saa kumi na moja tufanye usafi, duuhh nilichoka. Kumbe wanafuga mbwa, sehemu padogo mbwa wanajisaidia, morning ni kuzoa na kusafisha kumwaga maji, nilichoka. Ila nikajikaza kumbe bado kuna kuosha magari usiku unaamshwa uoshe, kibaya zaidi ni kila siku iwe mvua au jua.

Kibaya zaidi ni huyo mke wake alikuwa na visa na maneno ya shombo, mara hataki watu watoke nje ya geti anafunga, mara hataki watu wakae sebuleni, hata kunywa maji ya kwenye friji jau, akinunua matunda mpaka akupe yeye na atakupa wakati linaanza kuharibika ukila atakuja kuongea mpaka ujute.

Kwa kipindi kile ilikuwa ni mateso sana, sabuni ya kuogea unajinunilia, mafuta ya kujipaka pia, tulikuwa tunajitegemea kama tumepanga hata kipindi tunaenda K/Koo ilikuwa ni taabu sana.

Ilinipasa kuishi kama mtoto wa miaka kumi kushuka chini, maana ni kama sikuwa najielewa. Maana watu walikuwa wanakuja pale wanashangaa tunawezaje kuishi na hawa, hata wadogo zake na yule mama walishindwa kukaa nae, wengine walikimbia na kutoroka. Ila ndo changamoto tunazokutana nazo katika maisha ya wengi wetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwakuwa ni kwa ndugu yako ulitaka uwe unajifungulia tu friji unakula unachotaka sio?

Hutaki kuzoa mavi ya mbwa unataka azoe Nani?
Kufungua friji ni normal things Sana hasa kama kipind cha joto maji lazima unywe ya barid so sio kitu cha kumind Sana kufungua friji kama na ww na hii mindset acha gubu Ndugu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nilikuwa nakaa kwa shemeji yan mke alie muoa kaka yangu tulikuwa marafiki sana mpaka matatizo yake na kaka ananiambia sasa siku nilitakiwa kwenda kukaa uko kwa ajili ya field sasa sehemu napajua ila landmark ilinitoka nikawa nampigia simu hapokei piga simu hapokei af hapo yeye alikuwa amesafiri nikampigiq mama nikamwambia yeye akampiga kaka maana mimi nahasira nishaaza kutoa maneno ya hasira

Bro akanipigia umefika wapi nikamjibu kituoni hapa haya ulizia sehemu fulani nikafika nikaingia an begi langu tukawq tunakaa mimi na kaka kesho yake nikiwa field nikampigia tena simu shemeji piga simu kapokea anaongea kama ataki nikajiongeza hapa sitakiw

Sasa sikuio mimi sina hili wala lile niko home nimekaa kaka kachelewa kurudi siku iyo nashanga mlango unafunguliwa kumbe shemeji nikampokea pale na bashasha na nilivyo mcheshi kijana wa watu za kwenu ulikotoka mambo mengi mtu ananijibu shot mh nikauchuna

Tumekaa gala nashangaa mtu kachukua ngazi anasafisha feni na ni mjamzito ikabidi nimwambie shuka nipande nikasafisha usiku ule ule kaka alipo rudi katukuta tunasafisha ndani akauchuna tu basi wakati tunakula sisi tunakula ugali na dagaa yeye kumbe katoka kwao na kuku anakula peke yake kaka akakamuomba akamkatalia dah nikasema hapa cha kike

Basi siku iyo ikapita sasa nikiwa field nasema niwahi kurudi nikapige story na shemeji yangu ee nikifika ananikataa kabisa analala nikasema huyu anijui nikawa nabaki field mpaka saa mbili akawa anafoka siku nayo ondoka siku waambia nilikuja kuwaambia asubuhi maana niliona bro naye anamuonga mkon mkewe morning anaoga na mimi naoga najiandaa akaniuliza unaenda wapi nikamjibu naondoka leo narudi home mbona ujasema mapema huyo. Shemeji nikamuuliza ulikuwa unataka ufanyeje? Akaa kimya

Na alikuwa na tabia anaingia chumban atakama umelala anaingia tu bila hodi nilipotoka hapo sikumpigia simu kuwa nimefika wala nini alipiga simu mama kuwapa taarifa kak akapiga simu mbona ujasema kama umefika mimi majibu yangu short kwani ukupewa taarifa na mama? Mzozo ulikuwa mkubwa nikakata simu sikuja kuongea nao mpaka mkewe alipojifungua nikampa hongera ikapita hiyo
 
Back
Top Bottom