Ulishughulika vipi na kisa cha namna hii?

Daniel Adrian

JF-Expert Member
Jan 1, 2019
311
322
Huyu msichana nilisoma nae 'A' level katika shule fulani hapa Dar es salaam. Darasani kwetu hakuna ambae hakumjua maana alikuwa msichana mwenye sura nzuri sana tena kuliko wote darasani. Ila hakuwa social kiviile. Alikuwa na rafiki zake aliowazoea na hakupenda mazoea sana.

Sasa mi nikawa nimempenda. Nikaanza kumtongoza tokea tunaanza form five. Kipindi ambacho mimi ndo nilikuwa mtu wa kwanza kumtongoza pale shuleni lakini alinikataa. Baada ya miezi mitatu nikapiga moyo konde nikamtongoza tena akakataa nikapotezea.

Tukiwa tunafanya mitihani ya mwisho tunaingia form 6 nikasema ngoja nijaribu tena nikamtongoza tena kwa mara ya tatu akakataa. Nikamuomba namba ili tuwe tunawasiliana maana kuna rafiki yangu mmoja 'Kishoro' (bado marafiki mpaka sasa) alinishauri bora niwe naenda nae taratibu niwe nawasiliana nae namuhonga honga vocha, na ukizingatia kilikuwa kipindi cha mitihani tunakaribia kwenda likizo. Nikamuomba namba akaninyima.

Baadae tukiwa likizo nikaitafuta namba yake kwa mtu mwingine. Nikampigia simu akawa ananijibu kwa mkato ili maongezi yaishe nikimtumia meseji hajibu kabisa.

Nikaacha kuongea nae tukaingia form 6. Nikawa najaribu kwenda nae taratibu nikawa nalazimisha urafiki. Akawa ananikwepa kwepa. Hataki story na mimi. (Inauma sana aiseee!). Kuna siku nilimuomba twende Kunduchi beach jumamosi kila kitu nitalipa mimi (baada ya kukopa sana maana mwanafunzi hela unatoa wapi ?). Akakataa nikaja kuskia Jumamos alienda Beach kombo na monitor wetu nilikuja kuambiwa baada ya kumaliza kuwa wakati tunakaribia kumaliza alianza mahusiano na monitor.

Tukiwa tunakaribia kufanya paper ya Form 6 nikataka nimtongoze tena akakataa kuongea namimi. Ila tu nikamwambia "Sawa. Ila hakuna msichana nilikuwa nampenda kama wewe". Hakujibu akaondoka. Tukafanya paper tukamaliza.

Toka tumemaliza form 6 sikuwahi kuonana nae tena. Nimemaliza chuo miaka miwili iliyopita(degree). Kazi nnayoifanya ni tofauti na niliyosomea. Sio ya maslahi ila inaniwezesha kuishi Dar. Nilishamsahau maana hatujaonana mda mrefu. Sasa juzi(jumatatu) niko makumbusho nasubiri daladala ya ubungo nikashangaa naguswa bega. Kugeuka ni yeye. Moyo ukapiga paa. Nilishangaa sana maana hakuwahi nianza mazungumzo wala kunisalimia popote.

Akaniambia Danny za siku nyingi nikamwambia safi. Tukaongea sana. Sana, tukakumbushana watu tuliosoma nao, mambo ya shule. Ila Gari la Kunduchi lilipofika akataka kupanda aondoke. Akaniambia "Danny naomba namba yako tuwasiliane." Nikashangaa sana. Nikampa namba.

Nilivofika nyumbani nikawaza sana kwamba kinachotokea ninaota? Prisca wakuniomba mimi namba ? Mimi ambae miaka kadhaa iliyopita alininyima namba yake nikaitafuta kwa mtu mwingine ?

Ilivyofika saa tano kasoro akanipigia simu nikapokea. Tukaongea stori kibao. Hakusema kwanini amenipigia zaidi ya story za hapa na pale. Akanipa story za UDSM (mimi nilisoma SAUT). Baadae tukaagana nikalala. Ila asubuhi wazo la kwanza lililonijia ni kuwa yawezekana Prisca anataka kunikubali sasa hivi. Maana haiwezekani Prisca anipigie mimi Danny simu hivihivi. Tena Prisca, anipigie mie simu ?

Jumannne hatukuwasiliana ila Jana jumatano alinipigia simu mchana akanilaumu sana kwa sauti ya mapenzi mbona sikumtafuta siku ya Jumanne ? Mi nikamwambia 'sikuwa na vocha' ila sikuwa na sababu ya kumtafuta kusema ukweli. Tukiwa tunaongea na simu hiyo jana akaniuliza vipi wifi mzima ? Nikamwambia sina mwanamke. Akaniambia anataka kuja kunitembelea Jumamosi. Nikamwambia nikipata muda ntakwambia.

Nikakutana na Kishoro kumuomba ushauri. Alichoniambia ndicho kinachonifanya nilete uzi hapa.

Kishoro alisema: "Hakupendi huyo, ila tu anakuja kwako kupooza machungu kwa sababu aliowataka yawezekana kagombana nao. Sasa we jiangalie wewe unampenda ama humpendi?".

Mimi, naweza sema nampenda ila sio sana kama nilivyokuwa nampenda kipindi kile; ni kama alinitoka kiukweli, ila sijiskii vizuri kumpotezea. Nipo single na nataka KUOA(sitaki mahusiano ya kucheza cheza) lakini nafsi yangu inasita kumuoa yeye.

Ila pia maneno ya Kishoro yanajirudia rudia sana kwenye akili yangu "Hakupendi huyo, do for your own risk."

Halafu mimi mwenyewe nashangaa. Alivyokuwa ananitreat kipindi kile, leo hii Prisca ananipigia simu ? Ananiuliza mbona sijamtafuta ? Halafu anataka kuja kunitembelea ? Huyu ni Prisca kweli au naota ndoto za mchana ?

Anyway, Yawezekana humu kuna watu waliwahi kupitia kisa kinachofanana na changu na wangependa kushare uzoefu wao jinsi walivyoshughulika na hivyo visa. Ntafurahi nikipata kuskia kutoka kwenu.

Lakini pia dada zangu mtanisaidia maoni yenu; Je, inawezekana kwa mwanamke ambae alikuwa hakupendi miaka ya nyuma akaja kwako kwa upendo wa dhati?

NB:Kuna vitu vingi nimevitoa ili kufupisha story, kama bado ndefu mniwie radhi
 
Kaka apo 100% ni Jumba Bovu sikushauri kuwa nae...Apo karuka ruka wee kaona mambo sio mambo anae mtaka hamtaki sasa anatafuta atakae mtaka...cha kufia nini si alijitia jeuri funika kombe nasema funika. Nakushauri ivi kwasababu lolote litakalo kuja kutokea uko mbeleni tofauti na matarajio yako ndugu yangu utakuja kulalamika sana na utapata stress mbaya haijawai tokea.

Good thing ni kwamba alisha kutoka japo sio mazima as you said ila fanya mishe zingine mpotezee atakutoka kabisa. Wanawake wapo wengi Kaka songa mbele kama ambulance uku unalia. ukifika utanyamaza
 
Wengi wamekushauri eiza uachane nae au uchape usepe. Mimi nitakushauri tofauti kidogo. Hebu kwa sasa mtazame Prisca kama mtu aliyepevuka na anaejitambua. Unakosea kumlaumu mtu wa form 5 kukukataa kimapenzi!!! Huyo alikuwa mtoto jomba.

Kweli wewe ulivyokuwa form 5 kiakili ndio ulivyo sasa? Na inaonekana bado unampenda Prisca, acha ligi zisizo na future, kwa sasa wote mmeshapevuka tuliza mpira.

Mpe nafasi wala usichukulie maubishani ya form 5. Mpe nafasi, pimeni afya jenga familia kijana. Kweli ulinganishe maisha ya kwenda bichi komba na monita ndio yakunyime future na umpendae?
 
Acha ufala wewe.....

Mkubalie aje Jumamosi kisha piga vizuri.... na mfulishe nguo kabisa.

Akishaondoka kwako zima simu na umkatie mawasiliano.

Huyo hakupendi hata kidogo maisha yamempiga anajitongozesha.

Wakati wa kumwaacha kuwa makini maana maisha hayahitaji hasira.
 
Wengi wamekushauri eiza uanchane nae au uchape usepe. Mimi nitakushauri tofauti kidogo. Hebu kwa sasa mtazame Prisca kama mtu aliyepevuka na anaejitambua. Unakosea kumlaumu mtu wa form 5 kukukataa kimapenzi!!! Huyo alikuwa mtoto jomba. Kweli wewe ulivyokuwa form 5 kiakili ndio ulivypo sasa? Na inaonekana bado unampenda Prisca, acha ligi zisizo na future, kwa sasa wote mmeshapevuka tuliza mpira. Mpe nafasi wala usichukulie maubishani ya form 5. Mpe nafasi, pimeni afya jenga familia kijana. Kweli ulinganishe maisha ya kwenda bichi komba na monita ndio yakunyime future na umpendae?
Wanawake wengi wengi wengi wa hivi huwezi ukafanya nao maisha mkuu.
 
Kaka apo 100% ni Jumba Bovu sikushauri kuwa nae...Apo karuka ruka wee kaona mambo sio mambo anae mtaka hamtaki sasa anatafuta atakae mtaka...cha kufia nini si alijitia jeuri funika kombe nasema funika. Nakushauri ivi kwasababu lolote litakalo kuja kutokea uko mbeleni tofauti na matarajio yako ndugu yangu utakuja kulalamika sana na utapata stress mbaya haijawai tokea.


Good thing ni kwamba alisha kutoka japo sio mazina as you said ila fanya mishe zingine mpotezee atakutoka kabisa. Wanawake wapo wengi Kaka songa mbele kama ambulance uku unalia. ukifika utanyamaza
Nashukuru kwa kunishauri. Ntazingatia ushauri wako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom