GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 57,114
- 110,494
Siku zote Watu wa Simba SC ambao 99.99% si tu kwamba ni Wasomi bali pia tumebarikiwa Akili Kubwa ili tuweze kutoa Elimu kwa Mashabiki wenye bahati mbaya ya kuwa na Upeo mdogo pamoja na Uelewa mbovu kama wa Yanga SC.
Hivyo basi kwa Faida ya Watu wenye Uelewa mdogo wa Kufikiri kutoka Yanga SC wakiongozwa na Msemaji wao Hassan Bumbuli na Mawakili wao Vihiyo (Uchwara) akina Chacha na Mgongolwa bila kusahau Watangazaji wa Redio na Wachambuzi kadhaa wenye Uyanga Uyanga GENTAMYCINE naenda 'Kuwaelimisha' juu ya Sakata zima na itakayokuwa Hatima ya Kesi imhusuyo Mchezaji Bernard Morrison.
KESI ZILIZOKO CAS YANGA SC ILIZOFUNGUA NI MBILI TU
Ya Kwanza ni kuhusu Mkataba wa Yanga SC na Mchezaji Bernard Morrison.
Ya Pili ni kuhusu Viongozi wa Simba (na siyo Klabu ya Simba) Kumshawishi Mchezaji Bernard Morrison Kujiunga Simba SC kinyume na utaratibu.
KWANINI MAAMUZI YATAKAYOTOLEWA NA CAS HAYATOIATHIRI SIMBA SC?
Ukweli ni kwamba Washtakiwa wa Kimsingi huko CAS ni Mchezaji Bernard Morrison na Viongozi Wawili wa Simba SC Zackaria Hanspoppe na Poti wangu kutoka Mkoani Mara (Musoma) Crescentius Magori na siyo Klabu ya Simba kama ambavyo Watu wa Yanga SC wanavyojaribu Kupotosha na bahati mbaya Wapuuzi wanawaamini.
KWANINI TFF IKO SALAMA KATIKA KESI HII HUKO CAS?
Taarifa iwafikie kuwa Yanga SC imeshtaki CAS Maamuzi ya Kamati iliyosimamia Mwenendo wa Kesi (ambayo kwa Kanuni za TFF) hii huwa ni Kamati iliyo Huru Kimaamuzi na haiingiliwi na TFF na Yanga SC haijaishtaki TFF huko CAS kama Wapuuzi wanavyoeneza.
KWANINI MAAMUZI YA CAS HAYATOATHIRI UBINGWA WA SIMBA SC?
Ifahamike kuwa iliyoshtakiwa huko CAS siyo Simba SC wala TFF bali ni Mchezaji Bernard Morrison na Mkataba wake Yanga SC pamoja na Viongozi Wawili wa Simba SC hivyo hata Maamuzi yatakayotolewa hayatoiathiri Klabu ya Simba na Simba SC hapa iko salama tena 100% kabisa.
MAKOSA YA KIUFUNDI YALIYOFANYWA NA YANGA SC AMBAYO YANAIWEKA SALAMA SIMBA SC KUTOPOKONYWA UBINGWA WAKE HALALI NI HAYA
Yanga SC walitakiwa kuachana na Kumshtaki Mchezaji Bernard Morrison na Kuishtaki Simba kama Klabu ili wawe na Hoja nzito kisha hawa akina Hanspoppe na Magori wakawajumuisha pamoja.
Ili Simba SC ipokwe Ubingwa wake Yanga SC walitakiwa Kuishtaki Simba kama Klabu (tena wakati Ligi Kuu ya VPL inaendelea) na siyo Kumshtaki Mchezaji Bernard Morrison ili CAS iihukumu haraka Simba SC wakati Ligi ikiendelea na siyo kwa sasa ambapo Yanga SC wameingia katika Mtego wa Kisheria uitwao 'Time Barred' hivyo hawataweza Kufua dafu.
MAAMUZI AMBAYO HUENDA CAS ITAYATOA BAADA YA LEO KUMALIZA KUISIKILIZA KESI NI KAMA YAFUATAYO
a) Mchezaji Bernard Morrison ama Kuamriwa kuwa alikuwa ni Mchezaji halali wa Yanga SC kwa Kipindi kile ila kutokana na ukiukwaji wa Mkataba alikuwa na Haki ya Kutafuta Klabu nyingine.
au
b) Mchezaji Bernard Morrison kuwa Huru ila atapigwa Faini kutokana na kuwahi Kwake Kuzungumza na Viongozi wa Vilabu vingine huku akijua Shauri lake lilipelekwa katika Kamati ya Maamuzi.
au
c) Viongozi wa Simba SC Hanspoppe na Magori Kuhukumiwa Kujihusisha na Soka kutokana na Kumrubuni (Kumshawishi) Mchezaji Bernard Morrison kabla ya Mkataba wa Mchezaji kumalizika au Shauri lake kutolewa Maamuzi na Kamati iliyokuwa inasikiliza.
au
d) Mashtaka yote ya Yanga SC dhidi ya Mchezaji Bernard Morrison na Viongozi Wawili wa Simba SC kutupiliwa mbali na Mahakama ya Usuluhishi Michezoni (CAS) na Yanga SC Kuamriwa kurudi tena upya katika Kamati ya Rufaa ya Tanzania (chini ya TFF) ili Malalamiko yao kupitiwa tena upya.
au
e) Yanga SC Kuonywa na hata Kupigwa Faini kwa Usumbufu na Kukiuka Utaratibu wa Kisheria ambao uliitaka Kwanza kabla ya Kukimbilia kwenda CAS Yanga SC ingekata Rufaa katika Kamati ile ile iliyoamua Kesi ya Mchezaji Bernard Morrison huku Dar es Salaam ( Tanzania ) na kama ilikuwa haina Imani na Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamati hiyo husika bado Kisheria Yanga SC walikuwa na Haki ya Kuomba wabadilishwe ili Rufaa yao isikilizwe na siyo kuruka hatua na Kukimbilia CAS.
Baada ya Elimu hii na Ufafanuzi huu ambao GENTAMYCINE nimewapa wana Yanga SC wote Usiku huu nimalize tu kwa Kuwaambia muda wa Maandalizi ya Ligi Kuu ijayo ni Mdogo na Michuano ya Klabu Bingwa inaanza hivi karibuni tu hivyo nyie endeleeni Kupoteza muda na hii Kesi yenu huko CAS kisha mjikute mmechelewa na mkaanza Kuharibu katika Mechi zenu na Simba SC iendelee kufanya vyema kisha muendelee kusema kuwa inabebwa na TFF.
Na Simba SC wala hatusajili kama nyie bali tunajazilia tu (Kufukia Mashimo) tofauti na nyie Wenzetu ambao masikia mmejipanga Kusajili Wachezaji wengi 'Magalasa' kama Kawaida yenu halafu wakija mnajazana JNIA Kuwapokea kwa mbwembwe na baadae Ligi ikiwa inaendelea na kupamba Moto huku Simba SC ikiwa inagawa Dozi zake tu mnaanza Kuwakataa na Kukimbilia ile Kauli yenu mliyoizoea pale mkifanya vibaya kuwa bado mnajenga Kikosi chenu.
Uzi huu uwafikie wana Yanga SC wote!
Hivyo basi kwa Faida ya Watu wenye Uelewa mdogo wa Kufikiri kutoka Yanga SC wakiongozwa na Msemaji wao Hassan Bumbuli na Mawakili wao Vihiyo (Uchwara) akina Chacha na Mgongolwa bila kusahau Watangazaji wa Redio na Wachambuzi kadhaa wenye Uyanga Uyanga GENTAMYCINE naenda 'Kuwaelimisha' juu ya Sakata zima na itakayokuwa Hatima ya Kesi imhusuyo Mchezaji Bernard Morrison.
KESI ZILIZOKO CAS YANGA SC ILIZOFUNGUA NI MBILI TU
Ya Kwanza ni kuhusu Mkataba wa Yanga SC na Mchezaji Bernard Morrison.
Ya Pili ni kuhusu Viongozi wa Simba (na siyo Klabu ya Simba) Kumshawishi Mchezaji Bernard Morrison Kujiunga Simba SC kinyume na utaratibu.
KWANINI MAAMUZI YATAKAYOTOLEWA NA CAS HAYATOIATHIRI SIMBA SC?
Ukweli ni kwamba Washtakiwa wa Kimsingi huko CAS ni Mchezaji Bernard Morrison na Viongozi Wawili wa Simba SC Zackaria Hanspoppe na Poti wangu kutoka Mkoani Mara (Musoma) Crescentius Magori na siyo Klabu ya Simba kama ambavyo Watu wa Yanga SC wanavyojaribu Kupotosha na bahati mbaya Wapuuzi wanawaamini.
KWANINI TFF IKO SALAMA KATIKA KESI HII HUKO CAS?
Taarifa iwafikie kuwa Yanga SC imeshtaki CAS Maamuzi ya Kamati iliyosimamia Mwenendo wa Kesi (ambayo kwa Kanuni za TFF) hii huwa ni Kamati iliyo Huru Kimaamuzi na haiingiliwi na TFF na Yanga SC haijaishtaki TFF huko CAS kama Wapuuzi wanavyoeneza.
KWANINI MAAMUZI YA CAS HAYATOATHIRI UBINGWA WA SIMBA SC?
Ifahamike kuwa iliyoshtakiwa huko CAS siyo Simba SC wala TFF bali ni Mchezaji Bernard Morrison na Mkataba wake Yanga SC pamoja na Viongozi Wawili wa Simba SC hivyo hata Maamuzi yatakayotolewa hayatoiathiri Klabu ya Simba na Simba SC hapa iko salama tena 100% kabisa.
MAKOSA YA KIUFUNDI YALIYOFANYWA NA YANGA SC AMBAYO YANAIWEKA SALAMA SIMBA SC KUTOPOKONYWA UBINGWA WAKE HALALI NI HAYA
Yanga SC walitakiwa kuachana na Kumshtaki Mchezaji Bernard Morrison na Kuishtaki Simba kama Klabu ili wawe na Hoja nzito kisha hawa akina Hanspoppe na Magori wakawajumuisha pamoja.
Ili Simba SC ipokwe Ubingwa wake Yanga SC walitakiwa Kuishtaki Simba kama Klabu (tena wakati Ligi Kuu ya VPL inaendelea) na siyo Kumshtaki Mchezaji Bernard Morrison ili CAS iihukumu haraka Simba SC wakati Ligi ikiendelea na siyo kwa sasa ambapo Yanga SC wameingia katika Mtego wa Kisheria uitwao 'Time Barred' hivyo hawataweza Kufua dafu.
MAAMUZI AMBAYO HUENDA CAS ITAYATOA BAADA YA LEO KUMALIZA KUISIKILIZA KESI NI KAMA YAFUATAYO
a) Mchezaji Bernard Morrison ama Kuamriwa kuwa alikuwa ni Mchezaji halali wa Yanga SC kwa Kipindi kile ila kutokana na ukiukwaji wa Mkataba alikuwa na Haki ya Kutafuta Klabu nyingine.
au
b) Mchezaji Bernard Morrison kuwa Huru ila atapigwa Faini kutokana na kuwahi Kwake Kuzungumza na Viongozi wa Vilabu vingine huku akijua Shauri lake lilipelekwa katika Kamati ya Maamuzi.
au
c) Viongozi wa Simba SC Hanspoppe na Magori Kuhukumiwa Kujihusisha na Soka kutokana na Kumrubuni (Kumshawishi) Mchezaji Bernard Morrison kabla ya Mkataba wa Mchezaji kumalizika au Shauri lake kutolewa Maamuzi na Kamati iliyokuwa inasikiliza.
au
d) Mashtaka yote ya Yanga SC dhidi ya Mchezaji Bernard Morrison na Viongozi Wawili wa Simba SC kutupiliwa mbali na Mahakama ya Usuluhishi Michezoni (CAS) na Yanga SC Kuamriwa kurudi tena upya katika Kamati ya Rufaa ya Tanzania (chini ya TFF) ili Malalamiko yao kupitiwa tena upya.
au
e) Yanga SC Kuonywa na hata Kupigwa Faini kwa Usumbufu na Kukiuka Utaratibu wa Kisheria ambao uliitaka Kwanza kabla ya Kukimbilia kwenda CAS Yanga SC ingekata Rufaa katika Kamati ile ile iliyoamua Kesi ya Mchezaji Bernard Morrison huku Dar es Salaam ( Tanzania ) na kama ilikuwa haina Imani na Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamati hiyo husika bado Kisheria Yanga SC walikuwa na Haki ya Kuomba wabadilishwe ili Rufaa yao isikilizwe na siyo kuruka hatua na Kukimbilia CAS.
Baada ya Elimu hii na Ufafanuzi huu ambao GENTAMYCINE nimewapa wana Yanga SC wote Usiku huu nimalize tu kwa Kuwaambia muda wa Maandalizi ya Ligi Kuu ijayo ni Mdogo na Michuano ya Klabu Bingwa inaanza hivi karibuni tu hivyo nyie endeleeni Kupoteza muda na hii Kesi yenu huko CAS kisha mjikute mmechelewa na mkaanza Kuharibu katika Mechi zenu na Simba SC iendelee kufanya vyema kisha muendelee kusema kuwa inabebwa na TFF.
Na Simba SC wala hatusajili kama nyie bali tunajazilia tu (Kufukia Mashimo) tofauti na nyie Wenzetu ambao masikia mmejipanga Kusajili Wachezaji wengi 'Magalasa' kama Kawaida yenu halafu wakija mnajazana JNIA Kuwapokea kwa mbwembwe na baadae Ligi ikiwa inaendelea na kupamba Moto huku Simba SC ikiwa inagawa Dozi zake tu mnaanza Kuwakataa na Kukimbilia ile Kauli yenu mliyoizoea pale mkifanya vibaya kuwa bado mnajenga Kikosi chenu.
Uzi huu uwafikie wana Yanga SC wote!