Ukweli kuhusu mpaka wa Tanzania na Malawi

Hili ni tatizo la kihistoria na inaonekana halifuatiliwi tena tokea Nyerere aondoke madarani. Kwanza kuna tatizo kuhusu jina la ziwa. Malawi wanasema ziwa linaitwa "Lake Malawi wakati sisi tunadai ni "Lake Nyasa". Nchi nyingine na ramani za kimataifa zinalitambua jina la Lake Nyasa. Tatizo lilizanza baada ya Malawi kupata uhuru wake mwaka 1964. Kwa wale waliosoma historia watakumbuka kuwa kabla ya uhuru wake, Malawi ilikuwa ikiitwa Nyasaland. Walipopata uhuru na kubadilisha jina, walitaka pia kubadilisha jina la ziwa kutoka ziwa Nyasa kwenda Ziwa Malawi.

Kitu kingine kilichochangia huu mgogoro ni Banda kuanzisha uhusiano wa kibalozi na serikali ya makaburu Afrika Kusini miaka ya 1960s. Viongozi wengi wa Kiafrika akiwemo Nyerere alipinga sana hili. Hii iliongeza chachu ya mgogoro juu ya jina na ramani ya ziwa Nyasa kati ya Tanzania na Malawi. Kwa sasa mgogoro juu ya jina la ziwa ni dormant.

Ukija kwenye ramani, Tanzania inadai mpaka unapita katikati ya ziwa. Huu ni mpaka uliowekwa kati ya Uingereza na Ujerumani wakati wa Berlin Conference juu ya kuigawa Afrika katika makoloni. Malawi wanadai ziwa lote liko Malawi ispokuwa ile sehemu ya chini iliyo Msumbiji. Tatizo ni pale Ujerumani iliponyang'anywa makoloni yake baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia, ambapo Tanganyika iliwekwa chini ya Uningereza. Kitu ambacho serikali ya kikoloni ya Uingereza ilifanya ni kuweka maeneo yote ya maji ya Ziwa Nyasa chini ya mamlaka ya Malawi (wakati huo Nyasaland) ikiwemo pia ile sehemu ya maji iliyokuwa upande wa Tanganyika. Hiki ndicho kiini cha tatizo kwa sababu baada ya Malawi kupata uhuru, automatically walidhani maji yote ya Ziwa Nyasa yako kwao kwa sababu yaliwekwa chini ya mamlaka yao tokea ukoloni.

Japokuwa kumekuwa na migogoro ya hapa na pale, Malawi imekataa kusema wazi kuwa ziwa ni lao. Kulikuwa na mgogoro miaka ya 1990s na miaka ya 2000s lakini haukufika mahali. Hata hiyo imeadhiri kwa kiasi kikubwa haki za wavuvi hasa wale wa upande wa Tanzania wanaoishi kando kando ya ziwa. Mara nyingi wamekuwa wakilaumiwa na wenza wa Malawi kuwa wanavua kwenye maji ya Malawi.

Serikali ya pande zote husika zinabidi kulichukulia hili suala kwa uzito zaidi. Vingenevyo ukitokea mgogoro wa wananchi wa pande zote husika hapa, itakuwa ngumu kusuluhisha. Haya mambo sijui ya kuunda tume, yatachukuwa miaka na miaka kutatua hili tatizo. Resources are very scarce. Siku ikugundulika kuna madini ndani ya ziwa itakuwa ni balaa.

Chini hapo ramani ya Google inaonyesha Ziwa Malawi halipo Tanzania. Serikali ilishawahi hata kuwaandikia Google kujua ni vigezo gani walivyotumia kuchora hii ramani?


attachment.php


 

Attachments

  • Lake Nyasa.PNG
    Lake Nyasa.PNG
    85 KB · Views: 5,346
Au ndio sababu kuna wakati ikalewta hoja kwamba Oscar Kambona hakuwa mtanzania na kwa muda wakamnyang'ana passport, hadi na yeye aliposema hata Nyerere baba yake alitokea karibu na Rwanda.
 
Mnaukumbuka huu wimbo:
Bandaaa wa Malawi, umetuvalia ngozi ya Simba
Kututishia watanzania, hatujali, hatujali.
 
Ntafurah sana Kama Kyela itakuwa upande wa Malawi kwani Malawi hawana Tatizo la umeme kama huu na hata Viongozi wakituletea longolongo tutakuwa tunaandamana na kudai haki yetu...
 
Inapatikana pia kwenye Hansard ya July 30, 2007 ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mpaka.jpg
 
Mpaka wake ni mto songwe kwa upande wa wilaya ya kyela na upande mwingine ni ziwa nyasa
 
Any county is entitled to print its own maps. However, international maps I have seen show that Lake Nyasa is in Malawi. The British administrators allocated the section of the lake that was under German East Africa to Malawi. I don't why they did it. But I guess they thought they will be in Africa forever. They didn't and they left Africans with tones of problems to solve.
 
Mpaka wake ni mto songwe kwa upande wa wilaya ya kyela na upande mwingine ni ziwa nyasa

Mkuu mpaka huu umekuwa na utata kwa miaka mingi. Kwa upande wa Tanzania tunasema mpaka upo katikati ya ziwa Nyasa lakini Wamalawi wao wanasema Mpka ni mto Songwe na ufukwe wa Ziwa Nyasa kwa upande wa Tanzania. Hii imekuwa ni ero ya miaka mingi sana. Kumbukumbu zinaonyesha kwamba kwenye miaka ya tisini kuna ramani ziliingizwa hapa nchini zikionyesha kwamba mpaka ni ufukwe wa Ziwa Nyasa, serikali ikazipiga marufuku.
 
Kunakisa niliskia malawi wakadai ziwa nyasa lote lao., ko watanzania mnatakiwa kulipia kwa matumizi yoyote ya ziwa. Nyerere akakubali na akasema kama ufukwe ndo mpaka basi kila wimbi linalopiga ufukwe wetu mtaulipia tsh1. Wamalawi wakanyosa mikono juu.
 
Lilw ni ziwa Nyasa au ziwa Malawi? School texts za Kenya hazifahamu kuhusu uwepo wa ziwa Nyasa, kwa mfano.
 
na ile sheria ya UN Convention on law of the Sea huko haitumia, au ni kwa jusa tu
 
duh! hi kweli inachanganya sana, ukiwa malawi wao hawana ziwa nyasa, ila wana ziwa Malawi na ndo maana lote linaonekana kuwa la kwao
 
Jamani jiografia nmejifunzia wapi? tuna bandari pale kyela na mbambabay sasa hizo meli zenafloot eneo lka wamalawi? haiwezekani zima tumepakana nalo kwa mikoa mitatu, yaani mbeya, iringa(sasa Njombe) an Ruvuma alufu liwe ilanamilikiwa kwa 100% na jirani yako, ina maana angeweka wanajeshi wake mpaka kwetu! huo mto songwe uko chini sana, lakini kuna matema beach ambay iko mbali sana , kwa hiyo mto songwe sio mpaka sahii, mkuu wa majeshi wa sasa anavuka mto songwe kwenda kijiji kwao na yuko ziwani kabisa, na hapo sio mwishi kuna watanzania wengine wakwenda mbali zaidi toka alipo yeye

Mpaka wake ni mto songwe kwa upande wa wilaya ya kyela na upande mwingine ni ziwa nyasa
 
Mawawi zamani walikuwa wanajulikana kama Nyasa land, hii historia ndio inawafanya wafikilie wanyasa wote hata wale wa rudewa ni wamalawi

duh! hi kweli inachanganya sana, ukiwa malawi wao hawana ziwa nyasa, ila wana ziwa Malawi na ndo maana lote linaonekana kuwa la kwao
 
Kuna haja ya kutangaza kabisa ziwa nyasa kuwa linaitwa ziwa nyasa. Niliona kipindi fulani cha e-tv ya s.a wakisema lake malawi ni moja maziwa nafuu zaidi duniani kutumia maji yake. Nikastuka sana.

Anyway inaonekana nchi yetu ni kubwa sana ndo maana hata tunatangaza sehemu moja tu ya tanzania na kusahau sehemu nyingine.
 
Jamani jiografia nmejifunzia wapi? tuna bandari pale kyela na mbambabay sasa hizo meli zenafloot eneo lka wamalawi? haiwezekani zima tumepakana nalo kwa mikoa mitatu, yaani mbeya, iringa(sasa Njombe) an Ruvuma alufu liwe ilanamilikiwa kwa 100% na jirani yako, ina maana angeweka wanajeshi wake mpaka kwetu! huo mto songwe uko chini sana, lakini kuna matema beach ambay iko mbali sana , kwa hiyo mto songwe sio mpaka sahii, mkuu wa majeshi wa sasa anavuka mto songwe kwenda kijiji kwao na yuko ziwani kabisa, na hapo sio mwishi kuna watanzania wengine wakwenda mbali zaidi toka alipo yeye

kaka usibishe vitu vingine usivojua. Mimi ni mwanakijiji mwenzake unaemsema mku wa majeshi, na mwakyembe wote wanatoka kijiji kimoja.. We mto unaousema ni kiwira ndo unavuka unenda kina mwamunyange. Ila songwe ni mpaka toka uku kasumulu hadi katumba songwe. Na huwaga mto huu songwe unamatatizo ya kuhamahama na kuingia tz zaidi pind yatokeapo mafuriko. Nafkiri umenipata ee..
 
Back
Top Bottom