Ukweli kuhusu Mabilioni ya NIDA: Kulinganisha NEC na NIDA Kimantiki

Nimefuatilia mjadala kwa umakini sana na binafsi nilimwelewa mleta hoja. Nilichoelewa ni;

1. Kumbe hizo 176bn ni za tangu mwaka 2011 si kwamba zinatolewa kila mwaka!

2. Kumbe fedha hizi ni si kwa ajili ya kutengenezea kitambulisho pekee kwa kila anayestahili bali ni pamoja mobilization, elimu, kufungua ofisi ktk kila wilaya, kulipa consultants, ununuzi wa vifaa vya kazi kama magari, computers nk na kufunga mfumo na pengine mishahara ya wafanyakazi na gharama zingine za uendeshaji.

Kama hii ndivyo, basi kuna picha kubwa kuwa fedha hii inaweza kuwa imetumika kama ilivyokusudiwa na ili kukamilisha zoezi nchi nzima defenetely zinahitajika fedha nyingi zaidi na zaidi!!

Lakini serikali sometimes nayo inapaswa kusikiliza ushauri wa kitaalamu unaotolewa na ma expert wetu na kuacha kufanya kila jambo kisiasa siasa tu ambayo matokeo yake ni kuingia kwa gharama kuubwa zisizokuwa na tija!

Serikali ilishauriwa mara nyingi sana kuwa mfumo wa NEC uunganishwe na wa NIDA ili kila mwananchi apate kitambulisho kimoja tu cha Uraia na hicho hicho kiwe ni cha kutambuliwa kupigia kura.

Hii si tu tungeweza kupiga ndege wawili kwa jiwe moja bali ingeweza kuokoa gharama kubwa na pengine mpaka sasa kila mtu angekuwa na National ID yake!!

Sina hakika ni kwa sbb zipi zilifanya wazo hili lisikubalike.

Binafsi sina tatizo na kuchunguzwa kwa matumizi ya fedha hizi ambazo kwa picha hii pekee kwa mtu yeyote mwenye fikra huru atakuwa ameshaona kuwa hakuna ufisadi wowote hapo.

Nadhani Rais asiwe ni mtu wa kutafuta kukamata mwizi tu na kumfunga bali tunataka awe ni mtu wa kutatuta kasoro za kimfumo ya kiutendaji na kuzirekebisha ili kupata suluhisho la kudumu la matatizo yetu!!

Lakini mimi tayari nilishaanza kupata mashaka na kasi ya JPM kwani imefikia time inakosa mwelekeo kwa kauli na matendo. Ni kama tunarudi kule kule tu ambako tunataka tutoke.

Kiukweli hisia zangu zinakataa kabisa kama JPM atatupeleka kwenye nchi tofauti na ya JMK iwapo anafanya kazi na mfumo ule ule waliomwachia watangulizi wake.

Haiwezekani tukawa na Tanzania mpya kama JPM amezungukwa na washauri wale wale waliotengeneza matatizo haya ambayo tunaaminishwa kuwa anapambana nayo ili kuyaondoa zaidi ya kuona visa na visasi tu kwa walio na mrengo tafauti na wa kwao. Hili la NIDA nalo liko ktk mwelekeo huohuo tu!!
 
Mimi sidhani raisi alikuwa mbali sana NEC na NIDA kiutafiti wote wanatakiwa wawe na hakika wanatoa vitambulisho kwa wazawa halali na hivyo matumizi yao kiuchunguzi yatalingana kwa quality ya vitambulisho si bishi uko sahihi na tusingehitaji kuwa na NEC kama tungekuwa wote tumepata vitambulisho vya NIDA. Hivyo kwa wao NIDA kusuasua ndiyo kumesababisha hasara ya NEC kuhitajika. Na je tofauti ya matumizi sio kubwa ya kutisha kulinganisha na idadi ya waliyopatiwa vitambulisho maana angalia cost ya mtu mmoja kwa cha NIDA compare na NEC ni kubwa sana ndugu kuna walakini hapo
 
Sawa umesomeka

Si mchezo usikimbie mkuu.

Naona umetambua namna tunavyo
Mkuu kuna mchangiaji huko juu alitaka ufafanuzi kuhusu ununuzi wa "server" 100. Ikikupendeza fafanua hiyo kitu ili sasa nijazie hoja yangu ni nirudi hapa kwa kina zaidi

Hii ngumu hawezi kujibu huyo.

Data zipo around the corner lakini nafikiri yeye amesoma magazeti tu.
 
Si mchezo usikimbie mkuu.

Naona umetambua namna tunavyo


Hii ngumu hawezi kujibu huyo.

Data zipo around the corner lakini nafikiri yeye amesoma magazeti tu.

Mi nimewakilisha nnacho kijua.... siko hapa ku speculate au kuleta utetezi au upotoshwaji.... ndo maana nikasema mengi yatafahamika baada ya uchunguzi alio uagiza mh. Raisi.... kwani umesikia hizo sever hazikutakiwa kununuliwa, je umesikia sio sehem ya package ya vitendea kazi vyao? Je umesikia alie nunua amesema alinunua kwa sababu gani? .... jambo usilo lijua usipende kuhukumu maana unaweza kuwa kwenye page tofauti kabisa na ukweli.......
 
Mi nimewakilisha nnacho kijua.... siko hapa ku speculate au kuleta utetezi au upotoshwaji.... ndo maana nikasema mengi yatafahamika baada ya uchunguzi alio uagiza mh. Raisi.... kwani umesikia hizo sever hazikutakiwa kununuliwa, je umesikia sio sehem ya package ya vitendea kazi vyao? Je umesikia alie nunua amesema alinunua kwa sababu gani? .... jambo usilo lijua usipende kuhukumu maana unaweza kuwa kwenye page tofauti kabisa na ukweli.......

Mkuu, habari za likizo?

Usijali sana mimi nimechokoza mada tu sote twasubiri uchunguzi.
 
Nimefurahishwa na watumishi wa NIDA kujitetea. Hoja zenu nzuri lakini hakukuwa na haja ofisi nzima kujazana kwenye uzi huu, kwa muda mtoa mada ni bingwa wa kujieleza na ameeleweka.
 
Mkuu

Mkuu hapo ndo kwenye shida..... lakini sielewi kwa nini NIDA hawaweki ukweli hadharani.... labda wanaogopa insurbodination. ... kuonekana wamemjibu mheshimiwa Raisi, lakini NIDA wana yao mazuri tu..... tena mazuri sana...


Hawawezi kuweka ukweli hadharani kwani wamechota mamilioni ya fedha kwa manufaa yao. Wana mali ambazo hazielezeki. Vijana wadogo kati ya miaka 38 na 50 wanamiliki majumba ya kifahari fedha wamepata wapi? Wakijaribu kueleza ukweli wataumbuka.
 
Nashauri na NEC pia wachunguzwe kwa matumizi yao yote ikiwemo uchapishaji wa vitambulisho vya mpiga kura.
Kwa uwezo mdogo nilio nao isije ikawa wao ndio wamewachonhea NIDA ili kuficha ubadhirifu wao uliokidhiri.
Nec hawatakiwi kuguswa kwasasa wamemfanyia makubwa sana Magufuri atakua hana shukrani akiwagusa
 
Hawawezi kuweka ukweli hadharani kwani wamechota mamilioni ya fedha kwa manufaa yao. Wana mali ambazo hazielezeki. Vijana wadogo kati ya miaka 38 na 50 wanamiliki majumba ya kifahari fedha wamepata wapi? Wakijaribu kueleza ukweli wataumbuka.
Ha haaa.... jina lako ni umri wa TANU huo.... lete ushahidi hapa na onyesha hati za majumba hayo nami ntajifunza..... nachelea kukubaliana na wewe maana watz wanapenda sana kuhukumu hata wasilo lijua..... thibitisha mkuu.....
 
Mie nadhani kuwa server za Nida kutokana na architecture yake ni centralized kwa maana taarifa zote zinakusanywa kutoka kwenye wilaya na kuletwa central kwa ajili ya kutoa rudufu na kuzalisha kitambulisho . Aidha kwa mantiki hiyo kila wilaya inatakiwa kuwa na server yake kwa ajili ya kuhifadhi taarifa zake kiwilaya na pia kwa technolojia ya sasa kuna matumizi ya blade servers nyembamba na zinakuwa nyingi kulingana na architecture
 
Utafiti ni mzuri sana tu,ila sasa zika patikanaje tena hela za kununulia mtaa mzima mikocheni nyuma ya Shopper's plaza na kujenga apartments za nguvu, hii inaingia kwenye matumizi gani katika huo mchanganuo wako na pengine ukatupa na gharama zake,nahofia usije uka tumika kama Sabuni.
Sabini tu,kama k o n d o m u,then inatupwa choooni
 
Hapo penye kujitafutia viada ndo penye shida kwa kuwa baada ya kukamilisha ada halafu kukawa hakuna noma, jitihada sasa zinahamia kwenye idadi ya nyumba za kupangisha, magari ya kifahari n.k. hawa watu wa nida wamekutwa na assets walizoshindwa kuelezea vyanzo vyake.....tutumbuane tu kwanza.
Umesahau na kuongoza wake za watu,na kupangishia nyumba videmu vya chuo maeneo ya masaki na sinza,bado kukaa stuli ndefu na kuzungusha round b bar,hongera bar nk
 
Wacha uchunguzi ufanyike hapa kuna jipu kubwa hata mm sina hicho kitambulisho ukienda nikoani hta awajui wanasikia kwenye TV na redio
 
Ha haaa haaaa..... kwa kweli sijabanduka niko likizo kidogo ila nilitaka kuhakikisha naondoa upotoshwaji unao letwa, suala la smart card, contact less etc ni mambo mapya hapa kwetu..... cha muhim ni je uzi huu una mashiko? Je kuna kitu tunaweza jifunza hapo maana ratiba za watu sio juu yako mkuu....
Tena inaonekana anayejibu sio mmoja wanaacha kufanya kaz walizoajiriwa na serikali wapo kutafuta huruma ya watanzania kwenye mitandao kwa wiz wao walioufanya
 
Nimesoma Magazeti mbali mbali na kumsikiliza mhe.Rais, baadhi ya mitandao ya kijamii na utafiti wangu mwenyewe , ki mantiki NEC na NIDA ni mbingu na Ardhi.

Wakati NIDA ni taasisi mpya na zoezi linalofanyika halijawahi kufanyika nchini kwetu kwa maana ya kumtambua mtanzania, mazoezi mengine yalikuwa ni ya usajili tu kama NEC wanavo fanya.

Madhumuni ya NIDA ni kumtambua nani Raia, nani Mgeni mkaazi na nani mkimbizi. Hili zoezi sio rahisi maana nchi yetu inapakana na nchi nyingi na kuwatofautisha watu wake sio rahisi.

Zoezi la NEC ni la kisiasa wakati mfumo wa NIDA una manufaa kiuchumi, kijamii na kiusalama ndo maana kazi yao inafanywa kwa umakini sana kwa kuhusisha vyombo vingine Kama RITA, Uhamiaji, Tamisemi na vyombo vingine vya ulinzi.

NIDA vs NEC.

1. Card ya NEC ni ya plastic na ina expire in 3 yrs kulingana na material iliyo tumika wakati ya NIDA ni smart card na life span yake ni miaka 10. Hivo ununuzi wa card za NIDA utakuwa ni wa juu kuliko wa card za NEC.

2. Kwa kuwa card za NIDA ni smart Card, hata printers zake ni specialized ili kuweza kuingiza data kwenye chip (watu wa IT watanielewa) wakati NEC ni printer za kawaida unazo weza print popote. Hivo ununuzi wa printa za NIDA utakuwa ghali.

3. Teknolojia ya NIDA ni ya kisasa na
ndo inayo tumika kwa sasa ulimwenguni na ni takwa la E. Africa comunity.

4. Kwa mujibu wa gazeti la Mtanzania la leo tarehe 08.02.2016, ukurasa wa 4 , mwandishi amegawanya pesa za usajili za NEC (70b) kwa idadi ya vitambulisho (23m) na kupata kila
kimoja ni sh. 3,010 na kwa NIDA kachukua 179.6b kagawa kwa vitambulisho 2m. Kimsingi 70b ya NEC ni ya usajili tu bila kuweka gharama za BVR. Kama sikosei wakati wa zoezi la usajili wa NEC magazeti yaliwahi kureport gharama ya BVR moja kuwa ni kama $ 6,800 na walinunua BVR 8,000 hivo basi NEC walitumia kama $54,400,000 sawa na karibu 120b bila gharama za usafiri (logistics), karatasi nk hivo si kweli NEC walitumia 70b tu. Wakati gharama za NIDA sh179.6b ni pamoja na gharama za kujenga mfumo wa kielectronic, kumlipa mkandarasi, kununua mashine za usajili na consultant aliye andikwa gazeti la Mtanzania la leo, magari, ofisi zao kila wilaya, na jukumu kubwa la utambuzi linalohusisha vyombo mbalimbali ambalo NEC hawalifanyi (nilivo vitaja hapo juu) na kama mnavyojua uanzishwajiwa ofisi ni pamoja na ununuzi wa samani etc.

5. Wakati NEC hizi pesa walipewa ndani ya mwaka mmoja, na kwa sababu ya uchaguzi NEC walikuwa na cut off time, NIDA pesa hizi
wamepewa tangu mradi uanze mwaka 2011.


6. Kama expiration ya card za NEC ni 3 yrs na NIDA ni 10 yrs hivo cost of investment ya NEC ni mara 3 ya NIDA.

7. Kuhusu sahihi (signature) kuto kuwa kwenye kitambulisho ni suala la kiteknolojia na kiusalama zaidi.Vitambulisho vingi vya kisasa na hata vya nchi nyingi tu havina signature on the face ya kitambulisho maana data zimo ndani ya kitambulisho na zinasomeka kielectronic. Vitambulisho vya Nigeria, Malaysia, Philippines etc havina signature . Data za mhusika husomwa na kitu kinaitwa Card reader. Ni kwa sababu za kiusalama tu maana signature inaweza kugushiwa lakini finger prints haziwezi. Nimeona kwenye magazeti mengi NIDA wamepata award (tuzo) mbili za kimataifa kuhusiana na teknolojia yao lakini hapa kwetu hatuvithamini, mi naona kuna shida.

Mpaka sasa hivi, kwa utafiti wangu, toka 2011 NIDA ilipo anza, NIDA imepata 20% ya pesa zilizo idhinishwa na bunge kwa miaka yote hiyo na sababu hii ya ukata ndo maana zoezi linasuasua na hawajaweza malizia usajili na wameshindwa toa elimu kwa Umma sababu ya Ukata.

Sio nia yangu kutetea ufisadi na ndo maana najiita "Tanzania Njema Yaja". Naiona Tanzania ikielekea kwenye nuru lakini hatutafika kilele cha uzuri huo kama ukweli hautaelezwa... ni vema Watanzania wakauelewa ukweli kabla ya kuhukumu. Mh. Raisi alisema, "msema kweli ni mpenzi wa Mungu" nami naona nimetimiza usemi huo. Na ninaamini baada ya uchunguzi ambao mh. Raisi ameelekeza ufanyike, ukweli utafahamika na haki itatendeka.

Long live Tanzania. Ukweli utatuweka huru.......
UTAELEZA HAYA KWENYE TUME UTAKAPOITWA KUHOJIWA HIZO PESA MLIZOLIPANA POSHO
 
1. Hoja iliyopo ni kwamba lazima uchunguzi ufanyika objectively kabla ya kufikia hitimisho la kuhukumu nani kaiba nini.
2. JPM anapaswa kushauriwa ajue tangu tulipojikwaa sio tulipoangukia tu. Huu mradi wa NIDA ulipingwa sana na wadau lkn
ukaanza kutekelezwa kwa kasi ya umeme kisha ukapoa tena. Yaani unashindwa kuelewa lengo la serikali lilikuwa hasa ni nini
na kwa nini lengo hilo halijakamilika hadi leo. Hili jipu halianzii kwenye matumizi tu ya fedha na ubora wa kadi, ni tangu pale kinachoitwa
'upembuzi yakinifu' ulipofanyika.
3. Hivi bajeti huwa haipitishwi kabla ya mradi kuanza? Na kama ilipitishwa ina maana NIDA walishapewa mpunga wote huo wa 179 bi na
kisha wakatoa vitambulisho 2m tu bila taarifa kwa baraza la mawaziri na Rais kwa ujumla?
 
Back
Top Bottom