Ukoloni umefikia daraja la tano, la sita liko njiani na inatisha

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,199
10,932
Tumezoea kusoma na kufanyia mitihani nadharia za wazungu.Leo na mimi mswahili naleta nadharia yangu juu ya mgawanyo wa ukoloni.Napendekeza wasomeshwe vijana wetu wa masomo ya DS mwaka wa mwanzo na wa pili chini ya kipengele chenye jina la Ami's colonial classification.

Hapa nitazitaja hatua tano za mwanzo kwa ufupi bila kuingia kwenye undani wake.Pia nitaidokeza hatua ya sita ambayo bado hatujaifikia kikamilifu.

Hatua ya mwanzo ni pale binadamu alipopata ladha ya vitu mbali mbali na kuvipenda halafu vikakosekana maeneo alipo na akafikiria uwezekano wa kupatikana maeneo ya mbali na anapoishi.Vitu hivyo vizuri ama alivijua kwa kuwepo maeneo yake halafu vikaadimika au vililetwa kibahati na wasafiri kutoka mbali.Walipofika huko mbali akakuta kuna watu kama yeye lakini wanatumia vitu vyengine tofauti na vile walivyovipenda wao,
Ili kuvipata vitu hivyo binadamu akawaza jinsi ya kuvichukua bila kuingia ugomvi na wenyeji waliovikalia.Sehemu hii imegawanyika makundi matatu.

a)Wazungu kutoka Ulaya walitumia vifaa vya kimaendelel ya kiteknolojia kama bunduki na vioo na mapambo ili kujikuribisha na wenyeji.Vile vile walitumia dini na kujifanya wachamungu ili kubadili fikra za wenyeji.

b)Waarabu: Kutokana na njaa na ukame na ugomvi katika maeneo yao wakasafiri kwenda mbali Afrika na Asia.Kila walipofika walijifanya kama wamefika na kutopenda kurudi kwao kwa namna yoyote ile.Wakaowana na wenyeji na kuingia miradi ya kiuchumi na kulima vile walivyovikosa kwao.Kwa vile wengi wao walikuwa na dini ya Uislamu basi na Uislamu ukaingia maeneo waliyojiimarisha.

c)Kugombea maeneo kwa vita na hatimae kugawana maeneo.
Kipindi hicho ni kirefu sana mpaka 1884

Hatua ya pili ni pale wakoloni walipoendelea kufaidi kupata matunda waliyoyataka bila msuguano na wenyeji kwa muda mrefu mpaka pale walipoanza kukwaruzana na wenyeji kwa kutokutaka kuishi kwa wema na kugawana mapato.Kipindi hiki kulikuwepo na malalamiko ya chini kwa chini na uchochezi wa kugombanisha watu ili wasiwe wamoja.Wakoloni ili kujilinda walitia fitna kwa watu kwa faida zao.

Hatua ya tatu ni wenyeji wa maeneo mbali mbali kuanzisha harakati za kutaka kuwa huru ili na wao wasibaguliwe na wafaidi matunda yaliyowazunguka ambayo kwa sasa na wao wamejuwa ladha zake na kujua thamani zao.Matokeo ya hatua hii maeneo mengi yakafanikiwa kujiweka huru kwa njia ama kupigana au wakoloni kuona bora waachie tu wajitawale.Lakini hawakuondoka kwa kupenda ikabidi wafanye njama za kuondoka na kubaki wakati huo huo.

Hatua ya nne ni wale walioachiwa madaraka kutokuweza kujiendesha ikawa nafasi ya wakoloni kurudi kwa mlango wa nyuma wa ukoloni mamboleo.Wenyeji wa maeneo mengi hatimae wakashtukia kwamba wakoloni waliondoka lakini bado wao ndio wanaoendesha mambo yao na kufaidika na matunda yaliyowazunguka.
Kiwango cha juu cha ukoloni mamboleo ni pale wakoloni walipoona kutofanikiwa sana kutumia vita vya kidini ili watu wapigane vita vibaya.Hapo yalitumika makundi ya kigaidi kama kisingizio.

Hatua ya tano.Nchi nyingi zenye vijana waliozisoma kwa namna zao hatua nne za mwanzo na kupata elimu za kisasa kuamua kutaka kujitenga moja kwa moja na ukoloni mambo leo hata hivyo inaonekana hawajakuwa na nyenzo za kujitenga moja kwa moja,

Hatua ya sita ni pale wakoloni kutokutaka kuondoka kwa namna yoyote ile na watakapokuwa tayari kutumia nguvu na huku wenyeji nao wakiwa na nia ya kujitawala hata kwa nguvu ili wasinyang'anywe vitu vizuri walivyonavyo.Hatua hii itahusisha vita vikali na kuifanya dunia isiwe mahali pazuri pa kuishi .Watu watatamani kiama kifike na waliokufa wakijua mambo yalivyo duniani watafurahi kufa mapema na hawatotamani kurudi tena.
 
Tumezoea kusoma na kufanyia mitihani nadharia za wazungu.Leo na mimi mswahili naleta nadharia yangu juu ya mgawanyo wa ukoloni.Napendekeza wasomeshwe vijana wetu wa masomo ya DS mwaka wa mwanzo na wa pili chini ya kipengele chenye jina la Ami's colonial classification.

Hapa nitazitaja hatua tano za mwanzo kwa ufupi bila kuingia kwenye undani wake.Pia nitaidokeza hatua ya sita ambayo bado hatujaifikia kikamilifu.

Hatua ya mwanzo ni pale binadamu alipopata ladha ya vitu mbali mbali na kuvipenda halafu vikakosekana maeneo alipo na akafikiria uwezekano wa kupatikana maeneo ya mbali na anapoishi.Vitu hivyo vizuri ama alivijua kwa kuwepo maeneo yake halafu vikaadimika au vililetwa kibahati na wasafiri kutoka mbali.Walipofika huko mbali akakuta kuna watu kama yeye lakini wanatumia vitu vyengine tofauti na vile walivyovipenda wao,
Ili kuvipata vitu hivyo binadamu akawaza jinsi ya kuvichukua bila kuingia ugomvi na wenyeji waliovikalia.Sehemu hii imegawanyika makundi matatu.

a)Wazungu kutoka Ulaya walitumia vifaa vya kimaendelel ya kiteknolojia kama bunduki na vioo na mapambo ili kujikuribisha na wenyeji.Vile vile walitumia dini na kujifanya wachamungu ili kubadili fikra za wenyeji.

b)Waarabu: Kutokana na njaa na ukame na ugomvi katika maeneo yao wakasafiri kwenda mbali Afrika na Asia.Kila walipofika walijifanya kama wamefika na kutopenda kurudi kwao kwa namna yoyote ile.Wakaowana na wenyeji na kuingia miradi ya kiuchumi na kulima vile walivyovikosa kwao.Kwa vile wengi wao walikuwa na dini ya Uislamu basi na Uislamu ukaingia maeneo waliyojiimarisha.

c)Kugombea maeneo kwa vita na hatimae kugawana maeneo.
Kipindi hicho ni kirefu sana mpaka 1884

Hatua ya pili ni pale wakoloni walipoendelea kufaidi kupata matunda waliyoyataka bila msuguano na wenyeji kwa muda mrefu mpaka pale walipoanza kukwaruzana na wenyeji kwa kutokutaka kuishi kwa wema na kugawana mapato.Kipindi hiki kulikuwepo na malalamiko ya chini kwa chini na uchochezi wa kugombanisha watu ili wasiwe wamoja.Wakoloni ili kujilinda walitia fitna kwa watu kwa faida zao.

Hatua ya tatu ni wenyeji wa maeneo mbali mbali kuanzisha harakati za kutaka kuwa huru ili na wao wasibaguliwe na wafaidi matunda yaliyowazunguka ambayo kwa sasa na wao wamejuwa ladha zake na kujua thamani zao.Matokeo ya hatua hii maeneo mengi yakafanikiwa kujiweka huru kwa njia ama kupigana au wakoloni kuona bora waachie tu wajitawale.Lakini hawakuondoka kwa kupenda ikabidi wafanye njama za kuondoka na kubaki wakati huo huo.

Hatua ya nne ni wale walioachiwa madaraka kutokuweza kujiendesha ikawa nafasi ya wakoloni kurudi kwa mlango wa nyuma wa ukoloni mamboleo.Wenyeji wa maeneo mengi hatimae wakashtukia kwamba wakoloni waliondoka lakini bado wao ndio wanaoendesha mambo yao na kufaidika na matunda yaliyowazunguka.
Kiwango cha juu cha ukoloni mamboleo ni pale wakoloni walipoona kutofanikiwa sana kutumia vita vya kidini ili watu wapigane vita vibaya.Hapo yalitumika makundi ya kigaidi kama kisingizio.

Hatua ya tano.Nchi nyingi zenye vijana waliozisoma kwa namna zao hatua nne za mwanzo na kupata elimu za kisasa kuamua kutaka kujitenga moja kwa moja na ukoloni mambo leo hata hivyo inaonekana hawajakuwa na nyenzo za kujitenga moja kwa moja,

Hatua ya sita ni pale wakoloni kutokutaka kuondoka kwa namna yoyote ile na watakapokuwa tayari kutumia nguvu na huku wenyeji nao wakiwa na nia ya kujitawala hata kwa nguvu ili wasinyang'anywe vitu vizuri walivyonavyo.Hatua hii itahusisha vita vikali na kuifanya dunia isiwe mahali pazuri pa kuishi .Watu watatamani kiama kifike na waliokufa wakijua mambo yalivyo duniani watafurahi kufa mapema na hawatotamani kurudi tena.
Uzi mzuri sana
 
Watatutawala saana, kwanza wenzetu taifa linaanza, kisha maslahi binafsi yanafata.
Sisi ni maslahi binafsi, taifa litajijua lenyewe, wakati huo sintokuwepo na tayari nishajiwekeza.
 
Uzi mzuri sana

Nakushauri utunge kitabu ueleze nadharia zako kwa ufasaha. Tupende kuandika vitabu tusiishie kuweka maoni tu mitandaoni. Hongera kwa kujaribu
Nakushukuru sana kwa ushauri mzuri.Na nakuunga mkono kuwa fikra halisi na enelevu ni zile zinazowekwa kwenye vitabu na wala sio kuwekwa kwenye mitandao ya kijamii.
Faida ya vitabu vinatunzika na kubaki kwa wasomaji wa mbeleni.Nyuzi za mitandao ya kijamii inategemea wamiliki wana malengo gani na wataishi na huo mtandao muda gani.Mtandao ukizimika na kila kilichoandikwa hupotea
Faida nyengine za kitabu ni kuwa ni rahisi kufanya marejeo kwa kuangalia kurasa na kufunua unapokusudia.Kwenye mtandao inakuwa shida na mara search engines zinakupeleka kwenye utititri wa kile unachokitafuta mpaka unachanganyikiwa usome kila ulichokusudia au ufuate fikra zinazofanana.
Baada ya yote hayo kwa ushauri wako Mwenyezi Mungu akinipa umri nakusudia kufanya hivyo na nakisia nitahitaji kama kitabuj cha ukubwa wa B5 chenye kurasa 600 hivi.Kila hatua inahitaji kufafanuliwa kwa kuweka mwanzo na ukomo wake na kutolea mifano kadhaa ya matukio,
 
Kila industrial revolution inaambatana na vita....Hii ni pattern iliyojitengeneza...So tujiandaye ki psychology, vita vya tatu vimeshaanza ila vimeanza taratibu
Vimeanzia Ukraine vinaingia Afrika Magharibi.
Nchi za magharibi zinalazimisha mapinduzi ya Niger yabatilishwe kwa faida zao.Wanataka kuwatumia waafrika wenyewe wafanye kazi hiyo.
 
Matatizo mengi yaliyo katika bara la Afrika hasa baada ya 1960s,nchi nyingi kupata uhuru yaliletwa na waafrika wenyere hasa viongozi wa kwanza ambao walishindwa kuleta maendeleo sababu ya uchu wa madaraka na ubinafsi.

Ukoloni ulikuwepo hata katika nchi za Asia na America,lakini leo hii baadhi ya makoloni yamepiga hatua kubwa sana ya kimaendeleo(USA, Thailand,China,Singapo,nk) kuliko Africa ambapo nalo lilikuwa kwenye ukoloni kama ulivyo kuwa katika mabara mengine.kwenye kitabu chake Mwl.Nyerere anasema kwamba "Tunashindwa kutatua matatizo yetu,kwa sababu ya kutoa lawama bila kufanya tafiti ili tuweze kuhitimisha sababu ya matatizo yetu".

Nchi nyingi zilizopo kusini mwa Sahara desert zina umasikini wa kunuka,kulinganisha na nchi za North Africa na hii ina changizwa na ukweli kwamba watu weusi tumenyima "matumizi ya akili katika kufanya mambo yetu"
 
Matatizo mengi yaliyo katika bara la Afrika hasa baada ya 1960s,nchi nyingi kupata uhuru yaliletwa na waafrika wenyere hasa viongozi wa kwanza ambao walishindwa kuleta maendeleo sababu ya uchu wa madaraka na ubinafsi.

Ukoloni ulikuwepo hata katika nchi za Asia na America,lakini leo hii baadhi ya makoloni yamepiga hatua kubwa sana ya kimaendeleo(USA, Thailand,China,Singapo,nk) kuliko Africa ambapo nalo lilikuwa kwenye ukoloni kama ulivyo kuwa katika mabara mengine.kwenye kitabu chake Mwl.Nyerere anasema kwamba "Tunashindwa kutatua matatizo yetu,kwa sababu ya kutoa lawama bila kufanya tafiti ili tuweze kuhitimisha sababu ya matatizo yetu".

Nchi nyingi zilizopo kusini mwa Sahara desert zina umasikini wa kunuka,kulinganisha na nchi za North Africa na hii ina changizwa na ukweli kwamba watu weusi tumenyima "matumizi ya akili katika kufanya mambo yetu"
Sahiiii kabisa ila ungesema tu matatizo ya Afrka yameletwa na viongozi wa Afrika bila ya kufafanua ninge kupuuza tu na Cha ziada umetaja waliowai kutawala na Sasa wapo vizuri tu USA,China mifano dhairi kwahiyo Afrika tujifunze

Ila viongozi wetu waafrika mara tu baada ya kupata uhuru huenda hawakuchangamka kufanya mambo ya kimikakati yenye tija kama China na U.S.A na huenda pia waliona mambo magumu wakaacha upenyo wakoloni wakarudi tena(SAPs 1980s) kiufupi walizani reremama kumbe sio poa
Rushwa
Akili za kibinafsi
Uwoga(sio reremama)
 
Sahiiii kabisa ila ungesema tu matatizo ya Afrka yameletwa na viongozi wa Afrika bila ya kufafanua ninge kupuuza tu na Cha ziada umetaja waliowai kutawala na Sasa wapo vizuri tu USA,China mifano dhairi kwahiyo Afrika tujifunze

Ila viongozi wetu waafrika mara tu baada ya kupata uhuru huenda hawakuchangamka kufanya mambo ya kimikakati yenye tija kama China na U.S.A na huenda pia waliona mambo magumu wakaacha upenyo wakoloni wakarudi tena(SAPs 1980s) kiufupi walizani reremama kumbe sio poa
Rushwa
Akili za kibinafsi
Uwoga(sio reremama)
Sijui sherehe za kusherehekea uhuru ni za nini wakati kumbe wale waliotuletea Uhuru walidanganywa na wakoloni.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom