Kanda ya Kusini imependelewa kwa kuwa na Wabunge ambao wengi wao ni Mawaziri ambapo kwa Mkoa wa Mtwara: Mtwara Vijijini Mbunge wake ni Mh: Hawa Ghasia ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Raisi Menejimenti ya Utumishi wa Umma; Newala Mbunge wake ni Mh: Capt Mstaafu George Mkuchika ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Kwa Mkoa wa Lindi kuna jimbo la Mtama ambalo mbunge wake ni Mh: Benard Membe Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa; Ruangwa Mbunge wake ni Kassim Majaliwa ambaye ni Naibu Waziri TAMISEMI; Nachingwea mbunge wake ni Mathias Chikawe ambaye ni Waziri Ofisi ya Raisi Utawala Bora.
Kwa nini viongozi hawa si wazalendo; Uchumi wa wananchi wa kanda ya Kusini kwa mikoa ya Lindi na Mtwara unategemea sana zao la korosho ambalo kwa mwaka wa uchaguzi wa mwaka 2010 bei ya korosho ilifika mpaka shilingi 2300/=kwa kilo moja ambapo mfumo wa stakabadhi ghalani unatumika ambapo malipo yaweza kufanyika mara tatu; Msimu wa mwaka 2010 wakulima wapata malipo ya kwanza sh.850/= malipo ya pili sh.350/= na malipo ya tatu ambayo ni ya majaliwa mpaka sh.850/= makato mengine ni ya ushuru wa halmashauri, vyama vikuu, usafirishaji, ushaufu.
Msimu wa mwaka jana wakulima walivutiwa sana na soko la mwaka 2010 na kuzalisha kwa wingi sana korosho lakini mpaka sasa kuna mwingiliano wa viongozi wakubwa kwa mkoa wa Mtwara na Lindi kiasi kwamba mpaka sasa wakulima hawajapata kabisa malipo ya kwanza ya sh.850/=. Mpaka sasa si wabunge wala madiwani wa Chama cha Mapinduzi ambao wamethubutu kuwaeleza wananchi tatizo liko wapi, kitu ambacho kimepelekea wananchi kukata tamaa ya maisha maana pesa zilitumika ktk kuandaa mashamba ya korosho, kiasi kwamba sasa imekuwa ngumu hata kulipia ada watoto wa shule. Mbaya zaidi Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho ni Mh: Mama Anna Abdallah ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Nagaga Wilaya ya Masasi. Kuna haja ya wananchi kubadili viongozi kwa chaguzi zijazo ili wananchi wapate viongozi watakaowatumikia. Naomba michango yenu wana JF
Kwa nini viongozi hawa si wazalendo; Uchumi wa wananchi wa kanda ya Kusini kwa mikoa ya Lindi na Mtwara unategemea sana zao la korosho ambalo kwa mwaka wa uchaguzi wa mwaka 2010 bei ya korosho ilifika mpaka shilingi 2300/=kwa kilo moja ambapo mfumo wa stakabadhi ghalani unatumika ambapo malipo yaweza kufanyika mara tatu; Msimu wa mwaka 2010 wakulima wapata malipo ya kwanza sh.850/= malipo ya pili sh.350/= na malipo ya tatu ambayo ni ya majaliwa mpaka sh.850/= makato mengine ni ya ushuru wa halmashauri, vyama vikuu, usafirishaji, ushaufu.
Msimu wa mwaka jana wakulima walivutiwa sana na soko la mwaka 2010 na kuzalisha kwa wingi sana korosho lakini mpaka sasa kuna mwingiliano wa viongozi wakubwa kwa mkoa wa Mtwara na Lindi kiasi kwamba mpaka sasa wakulima hawajapata kabisa malipo ya kwanza ya sh.850/=. Mpaka sasa si wabunge wala madiwani wa Chama cha Mapinduzi ambao wamethubutu kuwaeleza wananchi tatizo liko wapi, kitu ambacho kimepelekea wananchi kukata tamaa ya maisha maana pesa zilitumika ktk kuandaa mashamba ya korosho, kiasi kwamba sasa imekuwa ngumu hata kulipia ada watoto wa shule. Mbaya zaidi Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho ni Mh: Mama Anna Abdallah ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Nagaga Wilaya ya Masasi. Kuna haja ya wananchi kubadili viongozi kwa chaguzi zijazo ili wananchi wapate viongozi watakaowatumikia. Naomba michango yenu wana JF