Ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Hamisi

KJ07

JF-Expert Member
Dec 17, 2021
2,243
5,000
Dunia ina mengi ya kushangaza ukiachana na maajabu saba ya ulimwengu lakini pia kuna maajabu ya walimwengu wenyewe, Najua umewahi kushuhudia na kusikia habari za watu kujinunulia Jeneza kwa ajili ya maandalizi ifikapo siku ya mwisho, Leo tumekutana na Kijana anayelala kwenye Jeneza kwa zaidi ya miaka kumi na tano sasa yaani hadi usiku wa leo hii kijana huyu atalala kwenye jeneza.

Kutana na Hamisi mkazi wa Dar Es Salaam kijana ambaye ameamua kuishi kwenye Jeneza badala ya kulala kitandani, Kila mtu huwa na matamanio ya kulala sehemu nzuri pale mambo yanaponyooka ila ni tofauti kwa Hamisi licha ya kuwa na Miradi pamoja na kipato kikubwa lakini amechagua kulala kwenye Jeneza.

Hamisi anasema kuwa ana amani na furaha pia suala la kulala kwenye Jeneza wala halimpi shida na haogopi kabisa kwani anaamini kuwa kuna siku atakufa hivyo hakiogopi kifo kwasasa anafurahia maisha yake na kufanya anachokitaka. Amebahatika kujenga nyumba zaidi ya moja japo anatamani sana apate mke wa kufunga naye ndoa na kupata watoto kwani aliyewahi kuwa mchumba wake alimkimbia kwa aina ya maisha aliyonayo.

Licha ya kuwa tajiri mwenye mali za kutosha lakini nyumbani kwake wanaishi watu wawili tu yeye na dada wa kazi. Dada wa kazi hutakiwa kufanya usafi nyumba yote pamoja na kumuamsha kwa ajili ya chakula, Endapo dada wa kazi akitaka kumuamsha bosi wake basi hutakiwa kugonga Jeneza mara sita na kusubiri kwa dakika tano ili bosi wake atoke nje.

Hamisi anasema kuwa haofii maneno ya watu na hata kutengwa na jamii bali anachojua yeye kuwa ana pesa na yuko huru kufanya chochote anachojisikia kikubwa zaidi anajivunia

kwa kitendo chake cha kuwasaidia watu wenye mahitaji.

CREDIT: EFM TANZANIA
 
Pesa tamu
Hakuna raha hapo hafu chaajabu sasa anaishi mwenyew ila ana mfanyakazi ambaye haishi hapo ila akienda kumuamsha anatakiwa agonge jeneza mara 6 halafu asubiri kwa dakika tano.
 
Back
Top Bottom