Kijana analala kwenye jeneza zaidi ya miaka 15

OgaBoy

JF-Expert Member
Aug 22, 2022
771
1,033
Kiranga Unazungumziqje hiki kisa TOA mtazamo wako.

---

Dunia ina mengi ya kushangaza ukiachana na maajabu saba ya ulimwengu lakini pia kuna maajabu ya walimwengu wenyewe, Najua umewahi kushuhudia na kusikia habari za watu kujinunulia Jeneza kwa ajili ya maandalizi ifikapo siku ya mwisho, Leo tumekutana na Kijana anayelala kwenye Jeneza kwa zaidi ya miaka kumi na tano sasa yaani hadi usiku wa leo hii kijana huyu atalala kwenye jeneza.

Kutana na Hamisi mkazi wa Dar Es Salaam kijana ambaye ameamua kuishi kwenye Jeneza badala ya kulala kitandani, Kila mtu huwa na matamanio ya kulala sehemu nzuri pale mambo yanaponyooka ila ni tofauti kwa Hamisi licha ya kuwa na Miradi pamoja na kipato kikubwa lakini amechagua kulala kwenye Jeneza.

Hamisi anasema kuwa ana amani na furaha pia suala la kulala kwenye Jeneza wala halimpi shida na haogopi kabisa kwani anaamini kuwa kuna siku atakufa hivyo hakiogopi kifo kwasasa anafurahia maisha yake na kufanya anachokitaka. Amebahatika kujenga nyumba zaidi ya moja japo anatamani sana apate mke wa kufunga naye ndoa na kupata watoto kwani aliyewahi kuwa mchumba wake alimkimbia kwa aina ya maisha aliyonayo.

Licha ya kuwa tajiri mwenye mali za kutosha lakini nyumbani kwake wanaishi watu wawili tu yeye na dada wa kazi. Dada wa kazi hutakiwa kufanya usafi nyumba yote pamoja na kumuamsha kwa ajili ya chakula, Endapo dada wa kazi akitaka kumuamsha bosi wake basi hutakiwa kugonga Jeneza mara sita na kusubiri kwa dakika tano ili bosi wake atoke nje.

Hamisi anasema kuwa haofii maneno ya watu na hata kutengwa na jamii bali anachojua yeye kuwa ana pesa na yuko huru kufanya chochote anachojisikia kikubwa zaidi anajivunia kwa kitendo chake cha kuwasaidia watu wenye mahitaji.

 
Hapa Duniani ni watu waafrika ndiyo tunakiogopa sana kifo.

Hilo jeneza ni fenicha kama kitanda tu hakuna cha kuogopa Wala kukufuru.

Enzi zile G Nako alipoganya video ya wimbo wa "lucky me" alipata ukosoaji mkubwa sana anajitabiria kifo. Leo huyu hapa anadunda.
 
😂😂😂😂ma slay queen wamemshindwa hiyo pesa yake anaipata kwa masharti ya waziwazi.
Angekua msiri asingekimbiwa maisha yenyewe ya kulenga kwa manati🙌🙌😃😃.
 
sijaelewa Kwanini unamuita kiranga asemee hili tukio la mtu kuamua kulala kwenye jeneza.

Kuna maajabu gani ya mtu kulala kwenye jeneza?
Sijaona sehemu waandishi wakiwa wanarekodi tukio toka asubuhi mpaka jioni akiwa ndani ya jeneza.

Sababu watu wengi wanapenda miujiza hapa kafanya marketing strategies ya kuanza kutafuta pesa za wajinga kwa kuona hichi.

Mpaka sasa sioni cha maana au ajabu kilichopo hapa.
 
Maagano hayo..

Firimansoni.
bora huyo analala kwenye jeneza na ndan kwake mi nalala kwenye kaburi asubuh nikiamka napiga zangu mswak nakula pamba huyoo kwenye mishe kabur langu nimeweka na ac lina friji na tv kabisa kama huamin kesho asubu pita mitaa ya kino makaburin utaniona ninavyoamka na kutoka kaburn uje uandike uzi hapa mana ushamb umekuzid
 
Unamsumbua kiranga. Siku ukiona shetani likimshawishi mtu afanye dhambi ndo muite Kiranga umwambie kama huyu yupo MUNGU na ye yupo.
 
Hapa Duniani ni watu waafrika ndiyo tunakiogopa sana kifo.

Hilo jeneza ni fenicha kama kitanda tu hakuna cha kuogopa Wala kukufuru.

Enzi zile G Nako alipoganya video ya wimbo wa "lucky me" alipata ukosoaji mkubwa sana anajitabiria kifo. Leo huyu hapa anadunda.
Jamaa anasema alikuwa na mchumba ambaye walitaka funga ndoa ila alipomwonyesha anapolala alikimbiwa. Sasa jeneza kwa asili sio sehemu ya Kulala MTU aliye hai wewe unachukulia poa? Wewe unaweza kununua jeneza na kuwa mbadala WA kitanda tena Una Mali na nyumba Kali namna hii?
 
sijaelewa Kwanini unamuita kiranga asemee hili tukio la mtu kuamua kulala kwenye jeneza.

Kuna maajabu gani ya mtu kulala kwenye jeneza?
Sijaona sehemu waandishi wakiwa wanarekodi tukio toka asubuhi mpaka jioni akiwa ndani ya jeneza.

Sababu watu wengi wanapenda miujiza hapa kafanya marketing strategies ya kuanza kutafuta pesa za wajinga kwa kuona hichi.

Mpaka sasa sioni cha maana au ajabu kilichopo hapa.
Eti enh
 
Unamsumbua kiranga. Siku ukiona shetani live likimshawishi mtu afanye dhambi mrikodi ndo muite Kiranga umwambie kama huyu yupo MUNGU na ye yupo.
Bado atasema yeye hakuwepo so haamini huenda nimeediti video kama jamaa yako hapo juu anasema wanafanya marketing
 
Kila mmoja apambane kivyake kwa namna yoyote ile atakayo ona inafaa yeye kuwa na kipato......as long as tu havunji sheria za nchi wala kuumiza raia wengine. Acheni jamaa aendelee kula pesa zake anazozitaabikia yeye mwenyew.
 
Ndagu aka maagano aka freemason aka maokoto.

Tembeleeni geita na Kahama muone vijana walivyojifungamanisha na watoa pesa.

Madogo wamejilipua
 
Hapa Duniani ni watu waafrika ndiyo tunakiogopa sana kifo.

Hilo jeneza ni fenicha kama kitanda tu hakuna cha kuogopa Wala kukufuru.

Enzi zile G Nako alipoganya video ya wimbo wa "lucky me" alipata ukosoaji mkubwa sana anajitabiria kifo. Leo huyu hapa anadunda.
Mtuu anafanyaa kilee anachoona kina mpa furahaa Cha ajabu anaambiwa n mwanga ,mara mashartii ya mgangaa ...
 
sijaelewa Kwanini unamuita kiranga asemee hili tukio la mtu kuamua kulala kwenye jeneza.

Kuna maajabu gani ya mtu kulala kwenye jeneza?
Sijaona sehemu waandishi wakiwa wanarekodi tukio toka asubuhi mpaka jioni akiwa ndani ya jeneza.

Sababu watu wengi wanapenda miujiza hapa kafanya marketing strategies ya kuanza kutafuta pesa za wajinga kwa kuona hichi.

Mpaka sasa sioni cha maana au ajabu kilichopo hapa.
Hkn maajabu Wala uchawi n vilee tu mtu kaamua kufanya anachokipendaa ila wabongo ss kwakukuzaa jambo n konyo..
 
Back
Top Bottom