90sgeneration
JF-Expert Member
- Dec 18, 2022
- 275
- 375
Habari wakuu. Mimi sio mtu wa siasa sana, lakini ni mtu ambae nafatilia mambo mbalimbali hasa habari za maendeleo ya nchi na mienendo ya siasa zetu na kijamii, na maisha kwa ujumla. Asante JF imenipa elimu kubwa sana ya mambo tangu nijiunge 2011 nikiwa secondary (kwa ID ya zamani nilisahau pass code).
Kuna matatizo mengi sana ambayo sijui ni either kwa makusudi au basi tunaamua yaendelee na sielewi ni kwa faida ya nani. Ni kwamba Rais wetu (aliepo na waliopita) hana washauri wazuri? Au washauri wake hawazingatii sana haya mambo?
ell pengine wanamajukumu mengi yanayowakeep busy kuliko haya ambayo kimsingi ni ya muhimu sababu serikali ipo kwa jili ya kulinda watanzania wote bila kujali mjinga au mwerevu.
Naomba ni act kwa muda huu kama Waziri asiye na Wizara (nadeal na wizara zote kama mshauri na bwana mipango). Labda naweza kusaidia mahali ambapo pengine mawaziri hawajapaona kama pana umuhimu.
Kwako Raisi na Waziri wa Ardhi;
Nianze na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Raisi, waziri aliepo madarakani ni kweli anajitahidi ila hajatilia hili jambo la utapeli wa viwanja na nyumba ambao umeota mizizi kila kona ya nchi hii. Watu wengi wanadhulumiwa ardhi na viwanja na hata nyumba zao.
Wengi wamelalamika, wamelia, wamekufa kwa presha, wamerudishwa nyuma kimaendeleo, wameletewa umaskini na hawa matapeli.
Wengine wanamagenge kabisa makubwa na wanafanya utapeli kwa kujiamini sababu wanajua mwisho wa siku hawawezi kufungwa kwa kesi ya utapeli, zaidi ya kupata dhamana, na mdai kuzungushwa na mwisho kukata tamaa na kuamua kuacha, na hapo akiwa ameathiliwa vibaya.
Kwa nini hili tatizo halitatuliwi na matapeli wanaongezeka?
SABABU ni hii, matapeli wanajua kabisa kesi ya utapeli wa aina hii hua sio jinai, huishia kua kesi ya madai na blabla then case closed. Na anaeumia zaidi sio tapeli, bali alietapeliwa.
Only watu wenye guts za kuwakomesha personally hao matapeli ndio hua wanaweza kwa kuwadhulu (kitu kinachoongeza kesi za mauaji mitaani), japo only 10% kati ya 100% ambao huweza kurudishiwa hasara, na 10% kulipwa half, waliobaki hubaki na vilio. Hivyo kwa hili utapeli huu kamwe hautaisha tukiendelea na hii trendy.
Mh Raisi na Mh waziri wa ardhi, Mimi kama waziri mshauri, nashauri sasa umefika muda wa makosa ya utapeli huu wakipumbavu unaowaletea umasikini watanzania wanaojaribu kupambana kujiletea maendeleo kukomeshwa. Nashauri mashauri ya aina hii ya utapeli wa viwanja, nyumba na ardhi yahamishiwe katika category ya makosa ya jinai.
*Mtu anaetuhumiwa kutapeli, iwe kuuza kiwanja, nyumba, ardhi na chochote kisicho chake, kutengeneza document na mihuri fake na kujifanya mwenyekiti, au kiongozi wa sehemu husika (wanaotapeli hua na mihuri na hujifanya wenyekiti wa mitaa na hua na docs zote) basi ashitakiwe kwa kosa la jinai na si la madai.
- Na mashauri haya yawe yanaharakishwa, na wakithibika bila shaka, basi wawe wanatangazwa hadharani.
FAIDA
Raisi na Waziri wa Ardhi
Haya mambo yanarudisha sana nyuma watanzania, badala ya kuendelea watu wanarudishwa nyuma. Serikali inapambana kuwezesha wananchi na wananchi wanapambana na mwisho wa siku mapato ya jasho lao yanamalizwa na wahuni wachache ambao wanadharau hafi mahakama zetu. Wanaotapeliwa sio wajinga, ila situation zinawakuta tu either kwa kukosa elimu au shida. Ni kazi ya serikali kuwalinda watu wake na utapeli huu.
Faida ni kwamba, kwa kuhamisha kesi hizi kuwa jinai, kwanza kabisa, watu wataogopa (haitaisha for 100%) lakini watu wataogopa, sababu sasa hawatapata dhamana, ambayo kwa hili inasemekana wanashirikiana na police wasio waaminifu kuwaachia huru na wanaamini sio rahisi kwao kufungwa.
Ila kama hakuna dhamana basi itakua kama ilivyo kesi za mauaji, sio kwamba watu hawauwai, lakini sheria ya jinai inapunguza mauaji. Na pia itawapa confidence wananchi kununua viwanja.
Hii itapunguza sana huu utapeli sababu sasa matapeli watakua wanajua kabisa kua wakikamatwa basi wameishia jela hakuna cha dhamana wala ujinga wa kulipa na kuachiwa, bahati nzuri kesi hizi za matapeli hua zina evidence nyingi mala nyingi.
Raisi;
Maendeleo ya wananchi hayawezi kuja ikiwa kila siku wanatapeliwa, mala pyramid schemes, mala kylinda sjui D9 sjui global, sjui matakataka gani, msiachie tu watu wakatapeliwa, wekeni sheria kali kuwakomesha matapeli.
USHAURI MUHIMU WA ZIADA
Pia Mh. Waziri wa ardhi, wizara yako ni wakati sasa wa kuweka kitengo maalumu cha uuzaji wa viwanja, ambacho ndio kitakua kinatoa document maalum za mauziano. Kitengo hichi kiwepo chini ya halmashauri zetu au ofisi za ardhi ambapo:
Mtu akiwa anauza kiwanja chake, au nyumba au shamba, akishapatana na mteja wake, akaenda kukiona, wakakubaliana bei, basi waelekee katika ofisi hiyo wakiwa na batua ya serikali za mitaa husika au kijiji au mji, kisha wakifika ofisi hiyo ijiridhishe kuwa kiwanja ni cha muuzaji kwa kuweka utaratibu ambao upo (sina hakika).
Kisha mauziano yafanyike chini ya wizara ya ardhi na iingie kwenye data base, kwamba 90sgeneration kamuuzia Hamad Rashid kiwanja no x,mtaa x kwa kiasi cha sh 900, tarehe 22/02/2023.
Shahidi ni Mwenyekiti wa mtaa Mbwana Ally, imethibitishwa na afisa ardhi bwana David Mshana. (Hili pia litaingizia serikali mapato, ambapo mnaweza weka only 2% au chini au zaidi (ila isimuumize mtu) ya bei ya mauziano iingie serikalini kama kodi)
NOTE: Kama hamna database ya kutambua kila mmiliki wa ardhi please anzisheni. Watu wasajiri ardhi zao, nyumba, shamba nk.
Kila eneo ambalo serikali itagawa viwanja, basi watu wataopewa taarifa zao ziwekwe kwenye database, kila kampuni ya kuuza viwanja ikiuza viwanja, basi taarifa zikasajiliwe ardhi na ziweke kwenye data base, kwamba eneo fulani sasa linamilikiwa na fulani, likiuzwa au kurithishwa basi taarifa zibadirishwe pia, na asiefanya hivyo basi hata eneo likiuzwa kitapeli asilalamike.
Ifike mahali Raisi mambo ya kijinga yaliyozoeleka yatatuliwe kibabe, sio kuvumilia upuuzi na watu wapuuzi. Sheria ya makosa ya utapeli yawe ya jinai, ili kukomesha Tanzania kua shamba la bibi au nchi ya wajinga.
Ni kazi yetu kama serikali kuwalinda watu wetu na aibu za kuonekana Taifa la wajinga wanaodhurumiwa ovyo, hata makosa ya wizi wa mtandao yawekwe category ya jinai, yasiwe na dhamana na adhabu ziwe kali ikithibitishwa. Kesi ziendeshwe kwa uwazi kuepuka mahakimu wala rushwa. I
fike mahali kesi za ardhi ziendeshe live TBC Taifa, hii itasambaza uelewa zaidi wa mambo ya ardhi, na tutakomesha upuuzi.
Hata viongozi wa serikali ambao wanatabia ya kuuza maeneo ya wanavijiji hovyo na kuwadhurumu haki zao ardhi zao, wapewe kesi za jinai. Hawa ndio wanasababisha kila siku migogoro kati ya wawekezaji na wananchi. Ni wakati sasa wa kuondoa ukiritimba kwenye ardhi. Yani hadi watu wanaogopa kununua viwanja kuogopa utapeli.
Aisee nina mengi ningeweza kushauri, najua mnajua mengi mawaziri wenzangu, hapa najaribu kuwakumbusha na kuwapa mbinu mpya au idea.
Niishie hapa kwenye wizara ya ardhi. Nakuja na Wizara ya kazi, vijana,ajira na wenye ulemavu.
Ni mimi 90sgeneration,
Waziri asie na wizara,
ofisi ya Raisi kazi maalum na ushauri.
Kuna matatizo mengi sana ambayo sijui ni either kwa makusudi au basi tunaamua yaendelee na sielewi ni kwa faida ya nani. Ni kwamba Rais wetu (aliepo na waliopita) hana washauri wazuri? Au washauri wake hawazingatii sana haya mambo?
ell pengine wanamajukumu mengi yanayowakeep busy kuliko haya ambayo kimsingi ni ya muhimu sababu serikali ipo kwa jili ya kulinda watanzania wote bila kujali mjinga au mwerevu.
Naomba ni act kwa muda huu kama Waziri asiye na Wizara (nadeal na wizara zote kama mshauri na bwana mipango). Labda naweza kusaidia mahali ambapo pengine mawaziri hawajapaona kama pana umuhimu.
Kwako Raisi na Waziri wa Ardhi;
Nianze na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Raisi, waziri aliepo madarakani ni kweli anajitahidi ila hajatilia hili jambo la utapeli wa viwanja na nyumba ambao umeota mizizi kila kona ya nchi hii. Watu wengi wanadhulumiwa ardhi na viwanja na hata nyumba zao.
Wengi wamelalamika, wamelia, wamekufa kwa presha, wamerudishwa nyuma kimaendeleo, wameletewa umaskini na hawa matapeli.
Wengine wanamagenge kabisa makubwa na wanafanya utapeli kwa kujiamini sababu wanajua mwisho wa siku hawawezi kufungwa kwa kesi ya utapeli, zaidi ya kupata dhamana, na mdai kuzungushwa na mwisho kukata tamaa na kuamua kuacha, na hapo akiwa ameathiliwa vibaya.
Kwa nini hili tatizo halitatuliwi na matapeli wanaongezeka?
SABABU ni hii, matapeli wanajua kabisa kesi ya utapeli wa aina hii hua sio jinai, huishia kua kesi ya madai na blabla then case closed. Na anaeumia zaidi sio tapeli, bali alietapeliwa.
Only watu wenye guts za kuwakomesha personally hao matapeli ndio hua wanaweza kwa kuwadhulu (kitu kinachoongeza kesi za mauaji mitaani), japo only 10% kati ya 100% ambao huweza kurudishiwa hasara, na 10% kulipwa half, waliobaki hubaki na vilio. Hivyo kwa hili utapeli huu kamwe hautaisha tukiendelea na hii trendy.
Mh Raisi na Mh waziri wa ardhi, Mimi kama waziri mshauri, nashauri sasa umefika muda wa makosa ya utapeli huu wakipumbavu unaowaletea umasikini watanzania wanaojaribu kupambana kujiletea maendeleo kukomeshwa. Nashauri mashauri ya aina hii ya utapeli wa viwanja, nyumba na ardhi yahamishiwe katika category ya makosa ya jinai.
*Mtu anaetuhumiwa kutapeli, iwe kuuza kiwanja, nyumba, ardhi na chochote kisicho chake, kutengeneza document na mihuri fake na kujifanya mwenyekiti, au kiongozi wa sehemu husika (wanaotapeli hua na mihuri na hujifanya wenyekiti wa mitaa na hua na docs zote) basi ashitakiwe kwa kosa la jinai na si la madai.
- Kusiwe na dhamana.
- Kifungo kiambatane na fidia na adhabu zingine ikiwemo kufilisiwa.
- Na mashauri haya yawe yanaharakishwa, na wakithibika bila shaka, basi wawe wanatangazwa hadharani.
FAIDA
Raisi na Waziri wa Ardhi
Haya mambo yanarudisha sana nyuma watanzania, badala ya kuendelea watu wanarudishwa nyuma. Serikali inapambana kuwezesha wananchi na wananchi wanapambana na mwisho wa siku mapato ya jasho lao yanamalizwa na wahuni wachache ambao wanadharau hafi mahakama zetu. Wanaotapeliwa sio wajinga, ila situation zinawakuta tu either kwa kukosa elimu au shida. Ni kazi ya serikali kuwalinda watu wake na utapeli huu.
Faida ni kwamba, kwa kuhamisha kesi hizi kuwa jinai, kwanza kabisa, watu wataogopa (haitaisha for 100%) lakini watu wataogopa, sababu sasa hawatapata dhamana, ambayo kwa hili inasemekana wanashirikiana na police wasio waaminifu kuwaachia huru na wanaamini sio rahisi kwao kufungwa.
Ila kama hakuna dhamana basi itakua kama ilivyo kesi za mauaji, sio kwamba watu hawauwai, lakini sheria ya jinai inapunguza mauaji. Na pia itawapa confidence wananchi kununua viwanja.
Hii itapunguza sana huu utapeli sababu sasa matapeli watakua wanajua kabisa kua wakikamatwa basi wameishia jela hakuna cha dhamana wala ujinga wa kulipa na kuachiwa, bahati nzuri kesi hizi za matapeli hua zina evidence nyingi mala nyingi.
Raisi;
Maendeleo ya wananchi hayawezi kuja ikiwa kila siku wanatapeliwa, mala pyramid schemes, mala kylinda sjui D9 sjui global, sjui matakataka gani, msiachie tu watu wakatapeliwa, wekeni sheria kali kuwakomesha matapeli.
USHAURI MUHIMU WA ZIADA
Pia Mh. Waziri wa ardhi, wizara yako ni wakati sasa wa kuweka kitengo maalumu cha uuzaji wa viwanja, ambacho ndio kitakua kinatoa document maalum za mauziano. Kitengo hichi kiwepo chini ya halmashauri zetu au ofisi za ardhi ambapo:
Mtu akiwa anauza kiwanja chake, au nyumba au shamba, akishapatana na mteja wake, akaenda kukiona, wakakubaliana bei, basi waelekee katika ofisi hiyo wakiwa na batua ya serikali za mitaa husika au kijiji au mji, kisha wakifika ofisi hiyo ijiridhishe kuwa kiwanja ni cha muuzaji kwa kuweka utaratibu ambao upo (sina hakika).
Kisha mauziano yafanyike chini ya wizara ya ardhi na iingie kwenye data base, kwamba 90sgeneration kamuuzia Hamad Rashid kiwanja no x,mtaa x kwa kiasi cha sh 900, tarehe 22/02/2023.
Shahidi ni Mwenyekiti wa mtaa Mbwana Ally, imethibitishwa na afisa ardhi bwana David Mshana. (Hili pia litaingizia serikali mapato, ambapo mnaweza weka only 2% au chini au zaidi (ila isimuumize mtu) ya bei ya mauziano iingie serikalini kama kodi)
NOTE: Kama hamna database ya kutambua kila mmiliki wa ardhi please anzisheni. Watu wasajiri ardhi zao, nyumba, shamba nk.
Kila eneo ambalo serikali itagawa viwanja, basi watu wataopewa taarifa zao ziwekwe kwenye database, kila kampuni ya kuuza viwanja ikiuza viwanja, basi taarifa zikasajiliwe ardhi na ziweke kwenye data base, kwamba eneo fulani sasa linamilikiwa na fulani, likiuzwa au kurithishwa basi taarifa zibadirishwe pia, na asiefanya hivyo basi hata eneo likiuzwa kitapeli asilalamike.
Ifike mahali Raisi mambo ya kijinga yaliyozoeleka yatatuliwe kibabe, sio kuvumilia upuuzi na watu wapuuzi. Sheria ya makosa ya utapeli yawe ya jinai, ili kukomesha Tanzania kua shamba la bibi au nchi ya wajinga.
Ni kazi yetu kama serikali kuwalinda watu wetu na aibu za kuonekana Taifa la wajinga wanaodhurumiwa ovyo, hata makosa ya wizi wa mtandao yawekwe category ya jinai, yasiwe na dhamana na adhabu ziwe kali ikithibitishwa. Kesi ziendeshwe kwa uwazi kuepuka mahakimu wala rushwa. I
fike mahali kesi za ardhi ziendeshe live TBC Taifa, hii itasambaza uelewa zaidi wa mambo ya ardhi, na tutakomesha upuuzi.
Hata viongozi wa serikali ambao wanatabia ya kuuza maeneo ya wanavijiji hovyo na kuwadhurumu haki zao ardhi zao, wapewe kesi za jinai. Hawa ndio wanasababisha kila siku migogoro kati ya wawekezaji na wananchi. Ni wakati sasa wa kuondoa ukiritimba kwenye ardhi. Yani hadi watu wanaogopa kununua viwanja kuogopa utapeli.
Aisee nina mengi ningeweza kushauri, najua mnajua mengi mawaziri wenzangu, hapa najaribu kuwakumbusha na kuwapa mbinu mpya au idea.
Niishie hapa kwenye wizara ya ardhi. Nakuja na Wizara ya kazi, vijana,ajira na wenye ulemavu.
Ni mimi 90sgeneration,
Waziri asie na wizara,
ofisi ya Raisi kazi maalum na ushauri.