MchunguZI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2008
- 4,009
- 2,173
Hii tabia ya serikali kuanza kuirudisha nchi kwenye mfumo wa ujamaa, ambao ulithibitika kwa vitendo kuwa mfumo wa kijinga, usiotekelezeka, unaogandisha mawazo na unaowafanya viongozi kuwa watawala pekee na siyo viongozi kweli; ni upotofu na udikteta wa hali ya juu. Serikali yoyote inayopanga bei ni serikali ya wajinga, wenye mawazo mgando na madikteta!
Hivi karibuni serikali ya ccm na magufuli wametangaza kuzuia shule binafsi kupandisha ada eti wangoje kile ambacho ikulu walikiita "ada elekezi".
Nasema huu ni ujinga kwa sababu kinachopaswa kuihusu serikali katika shule binafsi ni kuhakikisha wanafuata mtaala wa nchi tu. Tofauti na hapo hakuna kingine. Kumbukeni hakuna kodi yoyote ya mtu iliyotumika kujenga ama kugharamia chochote kwenye hizi shule!
Sasa kwa nini waingiliwe?! Hivi serikali haitupi ujumbe kwamba kwenye shule binafsi ndiko kuliko na elimu bora na kwa hiyo haki ya kupata elimu bora maana yake ni haki ya kusoma kwa bei ndogo kwenye shule binasi?!
Boresheni shule za walipa kodi. Porojo hatutaki!
Punguza jazba!
Kwanza nakupa pole kama ulianzisha kijishule ukidhani ni mradi wa kujipatia kipato. Elimu ni huduma kwa jamii na ndivyo ilivyo ktk nchi zote duniani. Hapa kwetu hao wanaojiita wenye shule binafsi wamekimbilia wakidhani ni biashara na wanajaribu sana kuendesha elimu kama biashara. Ada za kipuuzi kabisa, au ada wastani na kuongeza mambo ya kipuuzi.
Mara mchango wa maktaba, mara mchango wa gari la shule, mara mchango wa masomo ya kompyuta, nk.
Usilaani maamuzi ya ikulu. ukitaka biashara fungua guest house au restaurant. Pamba utakavyo, pika na weka viungo utakavyo kuvutia wateja. Elimu, Hapanaaa! lazima iongozwe na serikali. Kama unataka kuwachezea disco wanafunzi wako kila siku jioni kwa gharama za wazazi, acha! hao ni vijana wa Taifa la Tanzania.