UJIJI: Wazee wa UJIJI -KIGOMA wasema hawajawahi kuona Kiongozi aliyeujaza Uwanjani wa Lake Tanganyika kama Rais Samia

Mwananchi Huru

JF-Expert Member
Nov 20, 2021
1,448
1,003
KIGOMA WAMPA MAPOKEZI YA KIHISTORIA RAIS SAMIA SULUHU, ANATAJWA KUWA NDIO KIONGOZI ALIYEVUTA WATU WENGI ZAIDI LAKE TANGANYIKA

IMG-20221018-WA0158.jpg


Wananchi wa mkoa wa Kigoma wampa mapokezi makubwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan uwanja wa CCM Lake Tangayika.

IMG-20221018-WA0166.jpg


Mapenzi haya makubwa kwa Rais Samia yanahusishwa na jitihada zake kupitia serikali anayoiongoza ya kuifanya mkoa wa Kigoma kuwa kitovu cha biashara ukanda wa Magharibi.

IMG-20221018-WA0159.jpg


Serikali ya awamu ya sita anayoiongoza Rais Samia inakamilisha ujenzi wa barabara za lami zinazouunganisha mkoa wa Kigoma na mikoa ya Tabora, Kagera na Katavi.

Inatekeleza pia miradi ya ujenzi wa meli kubwa mbili kwa ajili ya abiria na mizigo, inakamilisha ujenzi wa bandari ya Ujiji na Kibirizi, inakamilisha ukarabati wa meli ya kubeba mafuta ya MT Sangara, imeuunganisha mkoa huo na umeme wa Gridi ya Taifa pamoja na uimarishaji mkubwa wa hospitali ya rufaa ya mkoa huo Maweni.

Naye Mzee Ali Msaze wa Buzebazeba anasema tangu awe na akili za kujitambua hujawahi kuona watu wengi Kama hawa," Huyu mama ni mpango wa Mungu "

IMG-20221018-WA0175.jpg


Hakika wanakigoma #Tunaridhika #HakunaKilichosimama #KaziIendelee
 
So what?

Yaani watu wanaacha shughuli za uzalishaji mali, wanakusanyika kusikiliza hotuba!

Halafu mbona wananchi wenyewe ni kama hawana furaha? Wanafaidi migebuka kweli huko? Au inasafirishwa zaidi nje baada ya mipaka kufunguliwa?

Na hii yote ni kumridhisha kiongozi kwa mlengo wa kisiasa. Ila kiuchumi hakuna tija yoyote!
 
So what?
Yaani watu wanaacha shughuli za uzalishaji mali, wanakusanyika kusikiliza hotuba!
Halafu mbona wananchi wenyewe ni kama hawana furaha? Wanafaidi migebuka kweli huko? Au inasafirishwa zaidi nje baada ya mipaka kufunguliwa?

Na hii yote ni kumridhisha kiongozi kwa mlengo wa kisiasa. Ila kiuchumi hakuna tija yoyote!
Kumsikiliza kiongozi mkuu wa nchi ni muhimu mno. Hotuba na maelekezo yake yana mantiki pana mno ktk maisha yako, yangu na ya watu wote. Hata kama hatokani na chama chako as long as ni president unapaswa kumsikiliza. Halazimishwi mtu ila ni muhimu mno.🙏🙏🙏
 
Kumsikiliza kiongozi mkuu wa nchi ni muhimu mno. Hotuba na maelekezo yake yana mantiki pana mno ktk maisha yako, yangu na ya watu wote. Hata kama hatokani na chama chako as long as ni president unapaswa kumsikiliza. Halazimishwi mtu ila ni muhimu mno.🙏🙏🙏

Marufuku ya mikutano ya vyama vya upinzani iondolewe.

Leo CCM mnafurahia jinsi mwenyekiti wenu alivyojaza umati ktk mkutano wa hadhara.

Hivi mnadhani wapinzani sio binadamu, au hawatamani na wao kufanya mikutano na kufurahia kujaza umati?
 
Kwa nchi zinazoendelea wangetakiwa kuwa kazini kama kazi zipo sio kutanga tanga. Pamoja na kumpongeza Raisi Samia wananchi kuacha kufanya kazi kukaa kusikiliza hospitali gani imejegwa wapi wangeweza kusikiliza hata kwenye TV.
 
Naona leo Wazee wa Ujiji walifanya mambo yao, baada ya hotuba ya Zitto yule Mwanamuziki alitaka kuleta kejeli kwa Zitto vyombo vikagoma😆😆

Nafikiri yule Mwanamuziki alitumwa yule.
 
Hayo ndiyo mafanikio pekee ya ccm...kukusanya watu.

Nchi inataka mabadiliko ya kifikra na kiuchumi.
Miaka 60 ya uhuru haiendani na hali halisi ya nchi.
 
Back
Top Bottom