Uislamu na Ukristo ndiyo vimeleta ubaguzi wa kijinsia, Afrika haikuwabagua wanawake

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,240
12,762
Katika historia ya Tanzania kuna mtu aliyeitwa Kisabengo. Kisabengo alikuwa ni mtumwa wakati ambapo Sultani wa Zanzibar anatawala Zanzibar na pwani ya Afrika mashariki. Alikuwa ni mtu mwenye nguvu sana. Baada ya muda akatoroka atumwa akiwa na watumwa wengine akiwa kiongozi wao.

Baada ya kutoroka akaanza kuwa mbabe wa kivita, akivamia na kupora maeneo ambayo leo ni mikoa ya Pwani na Morogoro. Kokote lilikosikika jina Kisabengo watu waliingiwa na hofu kuu. Baadaye akaanzisha mji. Aliuita mji huo Simbamwenni/Simbamwene. Mji aliojenga leo ndiyo Moro Town. Ulikuwa mji wa maana sana. Ulikuwa na Kuta za mawe. Minara miine ya ulinzi iliyojengwa kwa mawe na ulilindwa na maaskari wenye magobole. ulijengwa kando ya mto na ulikuwa na milango minne ya mpingo kila pande, milango yake ilipambwa vizuri sana. Mji ulikuwa moja ya vituo muhimu ya misafara kutoka bagamoyo kwenda Ujiji kituo.

Huyu Kisabengo alikuwa na binti yake ambaye alimwita Simbamweni. Alimpenda sana binti yake. Hata alipokufa alimuachia usultani wa mji ule. Kipindi H. M Stanley anapita kwenda unyanyembe aliweka kambi Simbamwene. Alistaajabu uzuri wa mji ule uliokuwa ukiongozwa na mwanamke. Askari wakakamavu wenye silaha wakimtii.

Stori hii inaonyesha jinsi Waafrika hatukua na habari za ubaguzi wa kinjinsia wala kuwadharau wanawake. Ushahidi mwingine ni lugha. Lugha yetu haina habari za She/He/Her/Him. Haibagui jinsia.

Ushahidi mwingine ni uwepo wa Matrineal Societies. Huko mikoa ya kusini urithi ulikuwa unapita kwa mwanamke, hata jamii nyingine kama wanyakyusa utakuta ni semi -matrineal. Na hii habari ya matrineal ipo sehemu nyingi africa.

Sasa zikaja dini za kutoka Mashariki ya kati na utamaduni wa watu wa eneo hilo kudogosha na kudharau mwanamke. Wakatulisha maneno kibao kibao na kutufanya hata sisi tuanze kufikiri kama wao. Hizi dini za middle east ndiyo zimefanya muafrica aanze kudharau mwanamke.
 
Ungetueleza basi enzi hizo kabla ya hizi dini kuja wanawake wa kiafrika walikuwa wanafanya nini na nini ambayo sasa hawawezi kufanya kutokana na mitazamo ya dini kuhusu wanawake iliyokuja kutuathiri?
Walikuwa hadi masultani. Soma hiyo habari ya Binti Kisabengo.
 
Wengi wa Wakurya na wasukuma hawana dini na ndio wanyanyasaji wa kijinsia wakubwa.
Huwapiga wake zao, wengine huenda mbali zaidi kwa kuwakata kisimbusi kinachowapa hisia za tendo la ndoa wanawake.
Hio Jamii bila ubabe hawaendi.
 
hujasikia shehe anasema mwanamke hafai kuwa Rais.
Sasa tuangalie Sheikh anavyosema au tuangalie marais wanawake waliyopo pamoja na nafasi zengine za uongozi ambazo wanawake wanazo hivi sasa?

Ukiacha hilo tukio la mwanamke kuwa Sultan je kuna una mifano mengine ya kuonesha kwamba waafrika hatukuwa tukiwabagua wanawake?
 
Kabla ya hizi dini kuja kulikuwepo na jamii zilizokuwa zinawachukulia wanawake kama watu wa daraja la pili na pia kulikuwa na jamii ambazo wanawake walionekana ni daraja na wanaume
 
Hivi chuki zenu kwa dini za Ukristo na Uislam zitawaisha lini ?!!!

Hamuwezi kuzifuta dini hizo......

Siyo dini tu mkuu huyo ana lenga mbali. Macho yote kwa beberu. Anamlaumu beberu kwa lolote. Mark my words - lolote.
 
Wengi wa Wakurya na wasukuma hawana dini na ndio wanyanyasaji wa kijinsia wakubwa.
Huwapiga wake zao, wengine huenda mbali zaidi kwa kuwakata kisimbusi kinachowapa hisia za tendo la ndoa wanawake.

Labda hao si waafrika mkuu
 
Wengi wa Wakurya na wasukuma hawana dini na ndio wanyanyasaji wa kijinsia wakubwa.
Huwapiga wake zao, wengine huenda mbali zaidi kwa kuwakata kisimbusi kinachowapa hisia za tendo la ndoa wanawake.
Umesahu na waarab, wao wanatahiri wanawake wao pia
 
Ila ni kweli tusipoangalia hizi dini za kuletewa zisizo na mantiki kwetu zitazidi kututenganisha huku wenyewe waarab na wazungu wakitucheka. Utamuanije Mungu asiye fanana na wewe? Inasemwa kuwa Mungu aliumba mwanadamu kwa mfano wake na sisi waafrika ndiye binadamu wa kwanza hapa ulimwenguni, kwanini tunawaamini waarab na wazungu? Afrika amkeni, tumechezewa akili sana mpaka hatujielewi.
 
Sasa tuangalie Sheikh anavyosema au tuangalie marais wanawake waliyopo pamoja na nafasi zengine za uongozi ambazo wanawake wanazo hivi sasa?

Ukiacha hilo tukio la mwanamke kuwa Sultan je kuna una mifano mengine ya kuonesha kwamba waafrika hatukuwa tukiwabagua wanawake?
Ukisoma title ukaelewa utaona kwanini nomezungumza mfano wa Shehe.

Na ukisoma mada hadi mwisho utaona mifano mingine inayoonyesha kwanini nasema hatukuwa tunabagua wanawake.
 
Back
Top Bottom