Uhasama wa Tanzania bara na Zanzibar unazidi kukua na utaleta madhara makubwa kama yanayosemwa hayatashughulikiwa

Muungano uboreshwe hapo tunaongea lugha moja. Na ndiyo maana kuna Wizara inayoshughulikia kero za Muungano chini ya Makamu wa Rais. Halafu kuna Tume ya Fedha ya pamoja ndani ya Wizara ya Fedha ya JMT.
Swali limeulizwa hapa mara kadhaa, kwa nini wanaoona kero za muungano iwe ni Zanzibar peke yake? Kuna uratatibu gani wa kukusanya kero za muungano za Watanzania bara ili nazo zishughulikiwe, au haiwezekani kwa sababu bara hawana serikali?

Na pia, kwa nini utatuzi wa hizo kero 18 zilizoshughulikiwa hauwekwi wazi - je ni hofu ya kwamba hizo kero zimeshughulikiwa kwa namna ambayo watu wa bara wakijua kilichofanyika watachukia na kuona kuna upendeleo zaidi unafanywa kwa Zanzibar, au kwamba kero zimetatuliwa kwa namna ambayo inazidi kudhoofisha muungano? Na watu wanauliza, kwa nini kero za muungano zimeshughulikiwa nyingi na kwa kasi katika kipindi cha Raisi Samia, na huko nyuma marais toka bara walisita kuwakubalia Zanzibar juu ya kuondoa kile wanachoita kero za muungano?

Kwa mfano kero moja ya muungano upande wa bara - ni kitendo cha watu wa bara kutozwa umeme kwa bei ambayo inalenga kufidia hasara wanayopata Tanesco kwa sababu Zanzibar siku zote hawataki kulipia umeme. Lini hili litaisha? Kwa nini nilipishwe umeme kwa bei ya kuwabeba Zanzibar?
 
Juzi juzi hapa nilimsikia waziri tena dokta mzima akisema kero za muungano zimetatuliwa kutoka 15 Sasa zimebaki tatu tu😝
Kilichonidhi hakuzitaja kero zilizo tatuliwa na kero zilizobaki. Ni vizuri Sasa tuziweke kero zote hapa ili waziri amalizie home work yake.
Tusisubiri mpaka wanaokerwa na hizi kero wakawa wengi kuliko wasiokerwa.
Mkuu kero nne za Jumbe alipokuwa raisi kwenye barua yake kwenda kwa Mzee wa Butiama hata moja hawajatatua...
Hapo bado hatujakumbushiia kikao cha AAK na mawaziri wake walipofunga safari kwenda Daslam kumuona mzee wa Butiama.....
Bado kero ya komandoo Amour ilipigwa tarehe hadi Leo......kero ni mingi aisee.
 
Sheria iliyounda Senagambia, had provisions za kuuvunja. Ule ulikuwa ni mkataba, the same to UK kujitoa EU.

Huu Muungano wetu adimu na adhimu ni Muungano wa dhima ya Muungano wa milele, zile Articles of the Union, sio mkataba, ni makubaliano ya milele, hakuna provision ya kuuvunja Muungano, tumeunganisha nchi mbili kwa kuchanganya udongo, na kuumwaga bara na Zanzibar, ili kuuvunja, lazima tuutafute ule udogo, tuupembue, punje za udongo wa Tanganyika, zirejeshwe Tanganyika na punje za Zanzibar zirejeshwe Zanzibar.

Kikemikali, muungano wetu ni compound na sio mixture!. Kikemikali, Ukichanganya vitu viwili na kuwa mixture, vitu hivyo vinakuwa havijaungana kikemikali, mfano kuchanhanya pombe na maji, kwa kutumia fractional distillation inawezekana kuitenganisha pombe na.maji. Vitu kama maji, H2Ounaweza kutenganisha hydrogen na oxygen, chumvi, unaweza hydrogen na.chlorine etc.

Lakini vitu viwili vinapoungana kwa chemical reaction, vitu viwili vile hufa na kuzaliwa kitu kipya kinachoitwa compound, huwezi tena kuvirejesha kwenye hali ya awali kama kuyeyusha sabuni ya unga kwenye maji, kunatokea chemical reaction, huwezi kutenganisha.

Huu Muungano wetu adimu na adhimu, ume undergo chemical reaction kwa mataifa mawili Tanganyika na Zanzibar kuungana, kupoteza utaifa wake.na kuunda taifa jipya la Tanzania ambalo ni compound, halivunjiki tena!.

Muungano tutaulinda kwa gharama yoyote.
P
kama ndi hivyo mambo ya compound. Imekuwaje sasa zanzibar imegoma ku dissolve completely under so called chemical reaction ya huu muungano?
 
kama ndi hivyo mambo ya compound. Imekuwaje sasa zanzibar imegoma ku dissolve completely under so called chemical reaction ya huu muungano?
Kumbe chemistry unaipata mkuu! Pascal hana jibu hapo, maana kwenye compound reaction huwezi hata kujua components zilikuwaje kabla hazija react pamoja na kutoa kitu kimoja kipya na homogeneous!
 
Serikali 3 ni kurudi nyuma na madhara yatakuwa makubwa kwa raia. Bora kwenda mbele kwenye serikali moja.
Madhara ya erikali moja ni baadhi ya wanasiasa kukosa vyeo na madaraka.
Usisahau tulianza na vyama vingi, tukaenda chama kimoja, tukarudi kwenye vyama vingi. Tulianza pia na uchumi huria, tukaingia ujamaa, tumerudi uchumi huria, na sasa tuko uchumi wa serikali ya kifisadi.

Tuko flexible sana, gari letu lina reverse gear.
 
Tuna vyama vingi lakini hatuna katiba ya vyama vingi. Iliyopo ni ya kuhakikisha chama tawala kinabaki madarakani. Hata Bashiru alisema chama kilichopo kwenye madaraka kuondolewa ni uzembe.
 
Nahisi siwezi kulumbana na wewe haya mambo. Hatutafikia muafaka kwa sababu tuko level tofauti katika ufahamu. Labda wewe umenizidi sana, au mimi nimekuzidi sana.

Kukuaga, soma hapa chini;

Nigeria
Oil was discovered in Nigeria in 1956 at Oloibiri in the Niger Delta after half a century of exploration. The discovery was made by Shell-BP, at the time the sole concessionaire. Nigeria joined the ranks of oil producers in 1958 when its first oil field came on stream producing 5,100 bpd.

UAE
In the early 1930s the first oil company teams conducted geological surveys in the UAE. Thirty years later, in 1962, the first cargo of crude oil was exported from Abu Dhabi.
Kuhusu UAE uko sahihi,mawazo yangu nilidhani mwaka huo 1930 ndio walianza oil extraction,kumbe huo mwaka ulikua wa research.
Ahsante kwa kunisahihisha ila kuhusu Zanzibar tusiipe umuhimu usiostahili.
 
Mnaunga mkono Muungano wa Afrika Mashariki wakati huo huo mnakomaa kuvunja Muungano wa Tanganyika na Zanzibar sio! 😆
 
Nadhani hujaelewa hili somo, kwa nini tumefikia hpa tulipo na tumefikia hapa tulipo leo na sio huko nyuma. Nataka nikueleze jambo moja very serious, ujue kuna mengi sana nyuma ya pazia. Makubwa ni matatu;
  1. Zanzibar kuna potential kubwa ya mafuta, na yakipatikana Zanzibar itakuwa kama Kuwait; kimapato, ukitumia GDP, the richest country in the world. Tangu ijulikane kuwa Zanzibar ina uwezekano mkubwa wa kuwa na mafuta, suala la nishati (mafuta na gesi) kuwa katika muungamo likawa ni kero ya muungano kwa upande wa Zanzibar, jambo la kuondolewa
  2. Zanzibar ni kisiwa cha kimkakati (strategic island) kiuchumi. Kuna mataifa kama Oman, UAR, Saudi Arabia nk, wako tayari kuingia makubaliano nao ili kiwe katika himaya zao na kuwaahidi Zanzibar mabilioni ya dola, kwamba wakikubali wataishi kama wako peoponi tayari na hakutakuwa na Mzaznibar masikini au asiye na nyumba ya kifahari, matibabu bire kwa wote, na kila mkazi atajengewa nyumba ya kisasa nk. Zanzibar hawawezi kuingia makubaliano kama hayo wakiwa sehemu ya Tanzania, na wakilazimisha basi itabidi JWTZ wachukulie ni uvamizi.
  3. Zanzibar ni kisiwa cha kimkakati (strategic island) kijeshi. Kuna mataifa kama USA, China, Russia nk, wako tayari kuingia makubaliano nao ili kiwe kituo chao cha kijeshi, na kuwaahidi Zanzibar mabilioni ya dola. Tanzania (bara) hawako tayari kuruhusu hili, kwa gharama yeyote ya kulinda muungano, hata kama ni kuwalea huku wanakukojolea kila siku.
Kwa hiyo basi, hizo ndio sababu za msingi zinafanya Zanzibar waone muungano kwa sasa unawazuia kuingia peponi, kulingana na ahadi wanazopewa kama wakiuvunja. Wanafanya kila njia ili kuwakera Tanzania bara kwa visababu vingi vidogovidogo lakini haya ndio mambo yaliyoko nyuma ya pazia.

Hawatasema sababu za kutaka kuvunja muungano, na haya mengine unayosikia ni kelele tu. Na aliethubutu kujaribu hili la kuiondoa Zanzibar katika muungano alikuwa ni Aboud Jumbe, ndio maana akaishia kutengwa kama mtu mwenye ukoma. In fact, ilitakiwa afungwe kwa uhaini. Aliyevujisha taarifa za kile Aboud Jumbe alitaka kufanya alikuwa ni Maalim Seif Sharif, hadi akazawadiwa Uwaziri Kiongozi. Lakini waliambiwa wazi, mtu mwingine yeyote akithubutu, JWTZ itaingia, na wakumbuke hatutahitaji kuweka boots on the ground in Zanzibar wakifanya uasi. Tunaweza kuwapiga tukiwa Bagamoyo.

Sasa, theory nyingine ya kutisha iliyopo ni kwamba hata Raisi Samia huenda anatumika kama kichocheo cha kuvunja muungano, akitumia nafasi yake kuwaudhi watu wa bara ili wafikie hatua kusema hawataki tena muungano. Watu wana theorize kwamba anafanya makusudi kuingia mikataba kama ya bandari, kuleta Wa-Zanzibar waajiriwe bara nk, kwa lengo la kuchochea hasira upande wa bara, hasira ambayo mwisho wake ni kuvunja muungano.

Angalia kwamba theory ya Raisi Samia kutumika kama kichocheo cha kuvunja muungano inakuwa na logic fulani kwa jinsi alivyong'ang'ania mkataba wa bandari. Ilikuwa ni kama ugomvi wa watu wa bara na Samia, na hakujali kuendelea kuwaudhi watu, hata viongozi wa dini, na wazee wa busara, kwa sababu hilo ndio lilikuwa lengo; wakasirike, waseme sasa muungano basi. Katika hali ya kawaida ya siasa, zile kelele zilipaswa kumfanya aseme basi tunaacha tumewasikia wananchi. Lakini akakaza uzi tu, japo upinzani wa juu sana aliokabiliana nao. Theory ni kwamba kulikuwa na sababu ya yeye kushika ule msimamo, na hiyo sababu haikuwa ya kiuchumi.

Na kuna vitu vingine vingi vinavyohusu kuwafungulia waarabu fursa upande wa bara, pamoja na mambo ya mbuga za wanyama nk. Haya yote yalionekana kuwa ni strategy, kwamba hata kama muungano utavunjika, uwepo wa hawa waarabu upande wa bara, waarabu wanaoonwa kuwa wajomba wa Samia na watu wa Zanzibar, kutakuwa na manufaa kwa Zanzibar. Na hata kuna watu wanasema haya mambo yanafanyika kwa coordination ya Zanzibar na Uarabuni.

Kuna mengi sana nyuma ya pazia. Suala ni kwamba, ni thory tu au yana ukweli ndani yake? Nilitaka kupost hili jambo kama thread inayojitegemea, lakini wewe sasa ndio umefanya niliseme. Haya ni baadhi ya mambo Nyerere alijua, na akawa na msimamo muungano usivunjwe kwa gharama yeyote ile. Hofu yake ilikuwa ni ya kuisalama. Lakini suala la Samia kuwa Raisi wa Tanzania limepeleka hili jambo katika level nyingine kabisa.
Issue kubwa ni kuwa Border ya Tanganyika to the East side of the country isn't clear. Please tuwekee hapa map of Tanganyika
 
Jinsi masuala ya muungano yanavyoshughulikiwa na kwa sasa, ni mtu kipofu wa akili tu ndio hataona kwamba kadiri siku zinavyopita mbegu za uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar inazidi kuota mizizi, majani ya chuki yakizidi kuchanua. Ni kiongozi mjinga tu asieweza kuona kwamba jinsi haya mambo ya muungano yanakoenda, yanaweza kusababisha mgongano (confrontation) mkubwa sana kati ya wakazi wa Zanzibar walioko bara na wakazi wa bara walioko Zanzibar.

Badala ya kujibu hoja zinazowekwa mezani, viongozi wameamua kwa makusudi kuwashambulia wale wanaozitoa, bila kuona kuwa kwa kufanya hivyo wanazidi kuchochea uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Kwa kumfurahisha nani?

Kama Tanzania bara wanaona kwamba kwao kero kubwa ya muungano ni kutokuwa na serikali ya Tanganyika, kwa nini hawasikilizwi? Wakati wa Nyerere huenda kulikuwa na sababu za msingi kuwa na serikali mbili, lakini ni wazi hilo halikubaliki kwa sasa, na huwezi kulilazimisha likaendelea kuwapo bila kuleta madhara.

Muungano tunaweza kulazimishwa uendelee kuwapo kwa kutumia nguvu ya dola, lakini haitazuia watu kuanza violence (kupigana) uhasama unaojitokea ukizidi kukua. Amini nawaambieni, huu muungano mnaodai uko imara unaweza kuvunjwa kwa nguvu na kuleta hali ya machafuko bara na visiwani. Watanzania bara walioko visiwani wataondolewa kule kwa nguvu, na wa-Zanzibar walikoko bara wataondolewa huku kwa nguvu, na hata kupoteza mali au uhai wao. Ndilo tunalosubiri? Au tunadhani haliwezi kutokea Tanzania, vitu kama hivyo vinatokea Rwanda tu?

Muungano ulifanyika zaidi ili Zanzibar kusiwe na counter-revolution ya Waarabu (wajomba) walipopinduliwa na kuchinjwa, na kwa Tanganyika kulinda usalama wake katika kuwa kitovu cha kupigania uhuru wa Afrika. Sasa hizi sababu sio hoja tena. Kama imefikia mahali Watanzania hawautaki muungano, basi ni bora uvunjwe kwa utaratibu na kuelewana, watu waulizwe je ungependa kubaki bara au kurudi visiwani, au ungependa kubaki visiwani au kurudi bara nk. Labda tuanze na "Referendum", wananchi ndio tuamue kidemokrasia kama tunataka au hatutaki muungano, sio serikali ituamulie kwa maslahi yake, au maslahi ya serikali ya Mapinduzi Zanzibar, au maslahi ya CCM.

Tusione aibu kukaa chini na kutafakari kuuvunja muungano, kama kuwa na serikali moja au tatu haiwezekani, kwa sababu mfumo wa muungano uliopo sasa hivi unazidi kukuza uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Mwaka 1982 Senegal na Gambia waliungana na kuwa nchi moja ya Senegambia. Iliposhindikana, waliuvunja muungano, mwaka 1989. Juzi hapa Uingereza imejitoa kwenye muungano wa Ulaya. Kwa hiyo Tanzania haitakuwa ya kwanza kuvunja muungano. Muungano ni mkataba.
Wakati wabunge 55 au G55 walipotoa hoja yakutaka uwepo wa serikali ya Tanganyika Nyerere aliwazuia kwa hoja wale ni wabunge waliotokana na Chama Cha mapinduzi hivyo hoja yao ilitakiwa ianzie ndani ya chama.
Jaji Warioba akizungumzia rasimu ya mabadiliko ya time ya katiba alisema ni heri uwape watanganyika serikali yao kabla hawajaidai.
Siku watanzania,aidi ya milioni 60 watakapoingiabarabarani kudai serikki yao hakuna atakayewazuia.
 
Nadhani hujaelewa hili somo, kwa nini tumefikia hpa tulipo na tumefikia hapa tulipo leo na sio huko nyuma. Nataka nikueleze jambo moja very serious, ujue kuna mengi sana nyuma ya pazia. Makubwa ni matatu;
  1. Zanzibar kuna potential kubwa ya mafuta, na yakipatikana Zanzibar itakuwa kama Kuwait; kimapato, ukitumia GDP, the richest country in the world. Tangu ijulikane kuwa Zanzibar ina uwezekano mkubwa wa kuwa na mafuta, suala la nishati (mafuta na gesi) kuwa katika muungamo likawa ni kero ya muungano kwa upande wa Zanzibar, jambo la kuondolewa
  2. Zanzibar ni kisiwa cha kimkakati (strategic island) kiuchumi. Kuna mataifa kama Oman, UAR, Saudi Arabia nk, wako tayari kuingia makubaliano nao ili kiwe katika himaya zao na kuwaahidi Zanzibar mabilioni ya dola, kwamba wakikubali wataishi kama wako peoponi tayari na hakutakuwa na Mzaznibar masikini au asiye na nyumba ya kifahari, matibabu bire kwa wote, na kila mkazi atajengewa nyumba ya kisasa nk. Zanzibar hawawezi kuingia makubaliano kama hayo wakiwa sehemu ya Tanzania, na wakilazimisha basi itabidi JWTZ wachukulie ni uvamizi.
  3. Zanzibar ni kisiwa cha kimkakati (strategic island) kijeshi. Kuna mataifa kama USA, China, Russia nk, wako tayari kuingia makubaliano nao ili kiwe kituo chao cha kijeshi, na kuwaahidi Zanzibar mabilioni ya dola. Tanzania (bara) hawako tayari kuruhusu hili, kwa gharama yeyote ya kulinda muungano, hata kama ni kuwalea huku wanakukojolea kila siku.
Kwa hiyo basi, hizo ndio sababu za msingi zinafanya Zanzibar waone muungano kwa sasa unawazuia kuingia peponi, kulingana na ahadi wanazopewa kama wakiuvunja. Wanafanya kila njia ili kuwakera Tanzania bara kwa visababu vingi vidogovidogo lakini haya ndio mambo yaliyoko nyuma ya pazia.

Hawatasema sababu za kutaka kuvunja muungano, na haya mengine unayosikia ni kelele tu. Na aliethubutu kujaribu hili la kuiondoa Zanzibar katika muungano alikuwa ni Aboud Jumbe, ndio maana akaishia kutengwa kama mtu mwenye ukoma. In fact, ilitakiwa afungwe kwa uhaini. Aliyevujisha taarifa za kile Aboud Jumbe alitaka kufanya alikuwa ni Maalim Seif Sharif, hadi akazawadiwa Uwaziri Kiongozi. Lakini waliambiwa wazi, mtu mwingine yeyote akithubutu, JWTZ itaingia, na wakumbuke hatutahitaji kuweka boots on the ground in Zanzibar wakifanya uasi. Tunaweza kuwapiga tukiwa Bagamoyo.

Sasa, theory nyingine ya kutisha iliyopo ni kwamba hata Raisi Samia huenda anatumika kama kichocheo cha kuvunja muungano, akitumia nafasi yake kuwaudhi watu wa bara ili wafikie hatua kusema hawataki tena muungano. Watu wana theorize kwamba anafanya makusudi kuingia mikataba kama ya bandari, kuleta Wa-Zanzibar waajiriwe bara nk, kwa lengo la kuchochea hasira upande wa bara, hasira ambayo mwisho wake ni kuvunja muungano.

Angalia kwamba theory ya Raisi Samia kutumika kama kichocheo cha kuvunja muungano inakuwa na logic fulani kwa jinsi alivyong'ang'ania mkataba wa bandari. Ilikuwa ni kama ugomvi wa watu wa bara na Samia, na hakujali kuendelea kuwaudhi watu, hata viongozi wa dini, na wazee wa busara, kwa sababu hilo ndio lilikuwa lengo; wakasirike, waseme sasa muungano basi. Katika hali ya kawaida ya siasa, zile kelele zilipaswa kumfanya aseme basi tunaacha tumewasikia wananchi. Lakini akakaza uzi tu, japo upinzani wa juu sana aliokabiliana nao. Theory ni kwamba kulikuwa na sababu ya yeye kushika ule msimamo, na hiyo sababu haikuwa ya kiuchumi.

Na kuna vitu vingine vingi vinavyohusu kuwafungulia waarabu fursa upande wa bara, pamoja na mambo ya mbuga za wanyama nk. Haya yote yalionekana kuwa ni strategy, kwamba hata kama muungano utavunjika, uwepo wa hawa waarabu upande wa bara, waarabu wanaoonwa kuwa wajomba wa Samia na watu wa Zanzibar, kutakuwa na manufaa kwa Zanzibar. Na hata kuna watu wanasema haya mambo yanafanyika kwa coordination ya Zanzibar na Uarabuni.

Kuna mengi sana nyuma ya pazia. Suala ni kwamba, ni thory tu au yana ukweli ndani yake? Nilitaka kupost hili jambo kama thread inayojitegemea, lakini wewe sasa ndio umefanya niliseme. Haya ni baadhi ya mambo Nyerere alijua, na akawa na msimamo muungano usivunjwe kwa gharama yeyote ile. Hofu yake ilikuwa ni ya kuisalama. Lakini suala la Samia kuwa Raisi wa Tanzania limepeleka hili jambo katika level nyingine kabisa.
Rais Samia haingii mikataba Kwa lengo la kuwaudhi Watanganyika, Kwa sababu maudhi siyo economic and social benefit.
Bali Rais anafanya hivyo kufaidi tundu la udhaifu wa katiba ya Tanganyika kuhusu ulinzi wa raslimali zake ikiwa Rais atatokea Zanzibar kutawala Tanzania yote.
Sasa hapo bado yu ana haki kuendelea kuingia uwekezaji wa kubinafsisha hata KINAPA, Kwa kuwa bado havunji katiba.

Katiba Mpya haiwahusu wanaoipinga, tuendelee Kwa uelewa uliopo. Uzuri Ni kuwa Watanganyika wa ukanda wa pwani huwa Sisi tunajisikia kama ni Wazanzibari.

Kuhusu uchumi, Ni mwendo fikra za Yericko Nyerere tu!
 
Sheria iliyounda Senagambia, had provisions za kuuvunja. Ule ulikuwa ni mkataba, the same to UK kujitoa EU.

Huu Muungano wetu adimu na adhimu ni Muungano wa dhima ya Muungano wa milele, zile Articles of the Union, sio mkataba, ni makubaliano ya milele, hakuna provision ya kuuvunja Muungano, tumeunganisha nchi mbili kwa kuchanganya udongo, na kuumwaga bara na Zanzibar, ili kuuvunja, lazima tuutafute ule udogo, tuupembue, punje za udongo wa Tanganyika, zirejeshwe Tanganyika na punje za Zanzibar zirejeshwe Zanzibar.

Kikemikali, muungano wetu ni compound na sio mixture!. Kikemikali, Ukichanganya vitu viwili na kuwa mixture, vitu hivyo vinakuwa havijaungana kikemikali, mfano kuchanhanya pombe na maji, kwa kutumia fractional distillation inawezekana kuitenganisha pombe na.maji. Vitu kama maji, H2Ounaweza kutenganisha hydrogen na oxygen, chumvi, unaweza hydrogen na.chlorine etc.

Lakini vitu viwili vinapoungana kwa chemical reaction, vitu viwili vile hufa na kuzaliwa kitu kipya kinachoitwa compound, huwezi tena kuvirejesha kwenye hali ya awali kama kuyeyusha sabuni ya unga kwenye maji, kunatokea chemical reaction, huwezi kutenganisha.

Huu Muungano wetu adimu na adhimu, ume undergo chemical reaction kwa mataifa mawili Tanganyika na Zanzibar kuungana, kupoteza utaifa wake.na kuunda taifa jipya la Tanzania ambalo ni compound, halivunjiki tena!.

Muungano tutaulinda kwa gharama yoyote.
P

Makubaliano ya milele kama yale ya DP na Bandari yetu, Kwahiyo unataka kutwambia na DP nao watakaa milele?
 
Duh!
Leo nimekuwa jasiri wa kukusoma hadi kwenye hiyo aya niliyonyanyua na kuibandika hapa.
mimi ni mpenzi wa kusoma na kuandika, hivyo nasoma kila chenye interest yangu na nasoma hadi mwisho, asante kwa ujasiri wa kunisoma。
Umeeleza vyema huko juu, lakini ukaja kujichanganya kwenye hizi kemikali, ambazo ni dhahiri huna ujuzi nazo.
ni kweli sina ujuzi na kemia kivile,O-level nimepiga A ya siasa na B ya history halafu mathe,physics,chemistry,biology, geography kiswahili nimepiga makarai, nika opt for HGL, ila combi zote zilikubali!.
Ukizungumzia hydrogen na chlorine kutengeneza compound, ambayo ni HCl, au maji, ukanyambua hydrogen na Oksijen, tayari unazungumzia kompound, huwezi tena kuzifanannisha na pombe na maji, ambazo ni compound mbili zilizochanganywa tu kwa pamoja na zinaweza kutenganishwa kirahisi, kwa distillation kama ulivyoeleza hapo na kubaki na pyuwa compond ya maji, na ya pili ikiwa compound ya pombe.
Asante
Maelezo yako ya aina ya muungano wetu inashawishi kukubalika, lakini elewa kwamba hata hizi 'elements ulizozitaja kwenye mifano yako kiuhalisia zinaweza kunyambuliwa. Hydrogen atoms zake mbili zinatenganishwa na kuwa mbalimbali, na teknologia hiyo ndiyo inayofanya mambo mengi siku hizi. Kwa hiyo hakuna kinacho shindikana.
Ni kweli
hata huu muungano imebaki swala la muda tu. kama hakutatokea kiongozi mwenye ushawishi wa kutosha kuujenga upya na kuwashirikisha wananchi wake katika kazi hiyo, hatuna muda mwingi sana nao huu muungano.
Duh!, hakuna any provisions popote za kuuvunja muungano, huko kuuvunja kutaanzia wapi?.
Tanganyika inaweza kulazimisha muungano uendelee kwa nguvu au kwa kutoa rushwa kwa waZanzibari kama inavyofanyika sasa? Muungano wa kutumia nguvu ni shida tupu. Kuna mifano duniani ya miungano ya kutumia mabavu iliyodumu? Sina mfano usiokuwa na mashaka. Labda Marekani, zile Confederate states na hizi nyingine walizokuwa wakipambana nazo. Huu mfano tunaweza kuutumia hapa? Sina jibu ya hilo, ingawa naelekea kulikubali.
Hata mimi sina jibu
Wakati mwingine manufaa ya muungano yasiyoonekana sasa, huko baadae ukishaleta neema watu wanasahau magumu waliyoyapitia. Confederate leo ukiwaambia wajitenge sidhani kuwa utawapata wengi.
Hii inaitwa positivism, positive attitude, this is affirmative, huu ndio uzalendo wa kweli
Leo nimekusoma mkuu P, na nimeona mantiki ndani ya andiko lako refu kiasi.
Asante, huu ni mwanzo mzuri, ukipata nafasi, nisome Mwananchi kila Jumatano, na Nipashe kila Jumapili, na Jumapili usiku, angalia KMT on Channel Ten. J Mnyika, Aunguruma Channel TEN, Athibitisha maridhiano yameisaidia Sana CHADEMA, Sasa Inayatambua Matokeo, Inalitambua Bunge na Kumtambua Mbunge Wake
P
 
Duh!, hakuna any provisions popote za kuuvunja muungano, huko kuuvunja kutaanzia wapi?.
Soviet Union, ilikuwa na 'provisions' za kuvunja muungano wao?
Ngoja nikurudishe tena kwenye ile mifano yako ya kemikali. Usisahau 'new knowledge' inatengenezwa kila siku, ndiyo sababu akina Hydrogen ambao zamani zzziiiile alionekana hawezi kuwa mbali na mshirika wake Oksijeni katika tone la maji; sasa hivi ni tone hilo linalotumika kuzalisha Hydrogen, ambayo sasa inatumika kama 'Green Hydrogen' kuzalisha nishati.
Kwa hiyo hizo 'provisions' unazodhani wewe kwamba zimefunga kila kitu, fikiri tena.
 
Asante, huu ni mwanzo mzuri,
Hapana.
Labda nikusome kwenye maswala kama haya ya Muungano. Inapokuja kwenye vyama vya siasa, UCCM wako huondoa hamu ya kutaka nikusome.
Na naomba unielewe, sijajitangaza hapa mimi kuwa ndani ya CHADEMA, au chama kingine chochote cha kisiasa.
Chama changu pekee, nisichoweza kukivua, ni maslahi ya hii nchi inayoitwa Tanzania. Wakiuvunja huo muungano, basi nitaifia Tanganyika yetu.
 
Jinsi masuala ya muungano yanavyoshughulikiwa na kwa sasa, ni mtu kipofu wa akili tu ndio hataona kwamba kadiri siku zinavyopita mbegu za uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar inazidi kuota mizizi, majani ya chuki yakizidi kuchanua. Ni kiongozi mjinga tu asieweza kuona kwamba jinsi haya mambo ya muungano yanakoenda, yanaweza kusababisha mgongano (confrontation) mkubwa sana kati ya wakazi wa Zanzibar walioko bara na wakazi wa bara walioko Zanzibar.

Badala ya kujibu hoja zinazowekwa mezani, viongozi wameamua kwa makusudi kuwashambulia wale wanaozitoa, bila kuona kuwa kwa kufanya hivyo wanazidi kuchochea uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Kwa kumfurahisha nani?

Kama Tanzania bara wanaona kwamba kwao kero kubwa ya muungano ni kutokuwa na serikali ya Tanganyika, kwa nini hawasikilizwi? Wakati wa Nyerere huenda kulikuwa na sababu za msingi kuwa na serikali mbili, lakini ni wazi hilo halikubaliki kwa sasa, na huwezi kulilazimisha likaendelea kuwapo bila kuleta madhara.

Muungano tunaweza kulazimishwa uendelee kuwapo kwa kutumia nguvu ya dola, lakini haitazuia watu kuanza violence (kupigana) uhasama unaojitokea ukizidi kukua. Amini nawaambieni, huu muungano mnaodai uko imara unaweza kuvunjwa kwa nguvu na kuleta hali ya machafuko bara na visiwani. Watanzania bara walioko visiwani wataondolewa kule kwa nguvu, na wa-Zanzibar walikoko bara wataondolewa huku kwa nguvu, na hata kupoteza mali au uhai wao. Ndilo tunalosubiri? Au tunadhani haliwezi kutokea Tanzania, vitu kama hivyo vinatokea Rwanda tu?

Muungano ulifanyika zaidi ili Zanzibar kusiwe na counter-revolution ya Waarabu (wajomba) walipopinduliwa na kuchinjwa, na kwa Tanganyika kulinda usalama wake katika kuwa kitovu cha kupigania uhuru wa Afrika. Sasa hizi sababu sio hoja tena. Kama imefikia mahali Watanzania hawautaki muungano, basi ni bora uvunjwe kwa utaratibu na kuelewana, watu waulizwe je ungependa kubaki bara au kurudi visiwani, au ungependa kubaki visiwani au kurudi bara nk. Labda tuanze na "Referendum", wananchi ndio tuamue kidemokrasia kama tunataka au hatutaki muungano, sio serikali ituamulie kwa maslahi yake, au maslahi ya serikali ya Mapinduzi Zanzibar, au maslahi ya CCM.

Tusione aibu kukaa chini na kutafakari kuuvunja muungano, kama kuwa na serikali moja au tatu haiwezekani, kwa sababu mfumo wa muungano uliopo sasa hivi unazidi kukuza uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Mwaka 1982 Senegal na Gambia waliungana na kuwa nchi moja ya Senegambia. Iliposhindikana, waliuvunja muungano, mwaka 1989. Juzi hapa Uingereza imejitoa kwenye muungano wa Ulaya. Kwa hiyo Tanzania haitakuwa ya kwanza kuvunja muungano. Muungano ni mkataba.
Bongo nguvu ya umma ina safari ya karne kadhaa sio leo!! Muungano hauvunjiki kwa kizazi hiki cha kunguru, ni bora ungetumia muda vizuri kuwaza urithi wa wanao siasa za bongo hakuna azijuae zaidi ya Nyerere peke yake
 
Back
Top Bottom