Uhalisia wa matokeo ya kidato cha nne 2012: Nini kimepelekea kufeli huku?

Wana JF,

Naona wengi wamekereka na matokeo ya F4, na kwa kweli ni aibu ya taifa kuonyesha kwamba karibia wanafunzi wote wamefeli (kwani mimi nasema ukipata Division IV umefeli). Na pia, naona wengi mnatafuta chanzo cha matokeo haya.

Ukitaka kujua kwa nini elimu ya TZ inaendelea kushuka chini, hapa nitakupa jibu kamili: ni kwa sababu serikali ilikuwa na mpango wa kijinga kujenga hovyo hizi shule za kata.

Zamani, watanzania wachache kabisa walikuwa wanamaliza elimu ya sekondari. Lakini wale walioingia sekondari walikuwa na uhakika zaidi kwamba watafundishwa vizuri na walimu ambao ni wataalamu.

Shida ni kwamba baadaye, serikali imeletewa presha kutoka nje kwamba ni lazima watoto wote wasome (hiki kitu kinaitwa Universal Education au Education For All).

Sasa serikali ya nchi hii ilichukua hatua ya kujenga shule kwanza, na kutafuta walimu baadaye. Yule aliyeamua hivyo alifanya kosa kubwa sana, kwa sababu katika elimu KITU CHA MSINGI KABISA NI WALIMU, SIYO MAJENGO.

Bora uwe na mwalimu ambaye anapenda kufundisha na ambaye anajua vizuri sana masomo anayofundisha halafu yule mwalimu awafundishe watoto chini ya mti, kuliko kuwa na majengo ambayo walimu wanaofundisha ndani ni wajinga (au hakuna walimu kabisa).

Nchini huku unaweza kuta shule ya kata ambayo ina wanafunzi 600 na walimu 3. Je, katika shule kama hii wanafunzi watafundishwa nini? Halafu hiyo shule haina maabara, haina maktaba, na haina kompyuta.

Kwa hiyo naomba niwape huu ujumbe kwamba kujenga shule bila kuwa na walimu wa kutosha na wenye vigezo vinavyostahili kunasababisha matokeo kama ya mwaka 2012.
 
Wanafunzi wamejiloga wenyewe mwaka huu na tusilalamike kuwa serikali ndio imesababisha hapana ingetaka ingewafaulisha ili ipate credit ila hayo yote ya nini?
Itakuwa kama form one ambao hawajui kusoma ila wamefaulu
Kwa hapa kila mtu abebe msalaba wake
Mwanafunzi 75%
Wazazi na shule 23%
Serikali 2%
 
Nimetafakari sana kuhusu suala la kufeli kwa wadogo zetu limekua janga kubwa, hivi serikali inamaon gani kuhusiana na swala hili na nini kifanyike ili kupunguza janga hili.
 
Yote yanawezekana kuwa ni tatizo, lakini kuna shule ambazo tunaamini wako makini kwa tabia za wanafunzi na wana walimu wa kutosha na wanafundisha. Angalia matokeo ya Marian, st.Francis nk. Hizi shule zimefanya vizuri kwa mfano st. Francis ndiyo ya kwanza kitaifa lakini tofauti na miaka ya nyuma hawana div 1 ya points7,8,9, wala 10!. Mwenye point 11 yuko mmoja. Je hapo utasema tatizo ni walimu au tatizo ni wanafunzi? Marian girls nao ni vile vile (mwenye point za juu wako wawili wa pts 11); feza boys pts 9 =2, pts 10=1, pts 11=1, ina maana points 7 na 8 hakuna tofauti na miaka mingine.
Mimi naona tatizo liko kwenye mitaala. Inawezekana mitaala iliyotolewa na serikali kufundishia siyo iliyotumika kutungia mitihani.
Hapa naomba wataalamu wa mitaala waangalie mtaala unasema mwanafunzi afundishwe kuishia level (depth) gani na waone kama maswali ya mitihani yalitoka ndani yake.
Kwa kweli sababu za eti walimu, eti simu na tabia za wanafunzi si rahisi kuzihusu shule hata hizo za binafsi nilizotaja hapo juu!
 
Wanastahili hilo hasa hawa wa mjini kwani they are so busy with the social networks charting and talking love stories,they are caring about their modernity especially those resides in town but for those who live in village,they are affected by environmental circumstances.
Am very much sympathized with bad result of those from bush area (vijijini) and am okay to those moderns
 
Watashinda vipi ilihali wanasombwa kwenda kwenye mikutano ya hadhara ya CCM???? Huwa hamuwaoni wanavyotanda na kupndeza mkutano? Wazazi na kamati za shule msikubali watoto wenu kuhudhulia idha kwa kutaka au kulazimishwa na watawala, wakwao mbona hawawagusi? Kwa nini wafanye hivi kwa watoto wa wakulima/ Kayumba (Msingi na Sekondari/yeboyebo) ilin hali watoto wao wakichapa kitabu st.....au majuu??

kaka kwenye ukweli jaribu hata kuukubali...kwa hawa wa mjini ni kweli hawasomi swala la kusombwa kwenye mikutano mnona hli hakipo na kama lipo hyo mikutano inafanyika mara ngap kwa mwez mpaka kuwakosesha kusoma.
 
Hii nayo inachangia na hasa baada ya mfumo wa kileo uliowafanya walimu kuwa washikaji zaid wa wanafunzi,siku hizi unakuta mwalimu anamwambia mwanafunzi wake "mambo,mwanafunzi nae anajibu ,poa" sisi enzi zetu nidhamu ilikuwa kubwa,hakukuwa na huu ushikaji,salaam ni shikamoo mwalimu,leo hii watoto wamerahisisha sana mambo,kila kitu wao ni rahisi,huu utandawazi ndiyo changamoto zake hizi
 
Uko sawa kabisa,yaaani kwa tanzania kama kuna familia ambayo hakuna mtu hata mmoja aliyewahi kuathirika na ukimwi,sasa katika matokeo haya lazima imeguswa kwa namna moja ama nyingine.
Basi kwa ujumla kwa kujali mustakabali wa taifa,tupeane pole na tujipange,serikali iboreshe mitaala na kujali watumishi wa kada hii na vitendea kazi kwa ujumla
 
Hii kauli haina tofauti na ile ya Presidaaa kwamba wanafunzi wa kike wanaopata mimba ni kiherehere chao..! Umetaja Azania mie nimemaliza O level pale na kulikuwa na walimu 85 pamoja na maabara ya kutosha pamoja na madarasa ya arts ya kutosha.. Kwanini nyie mje kukosa walimu..? Haya kama hao unasema facebook na kuzurura.. Hao wa primary jee ambao asilimia kubwa ya waliochaguliwa kwenda sekondary wamepata alama za 40 kwa 250 nao walikuwa wanafesibukua..? Hili ni janga kubwa..
 
wanafunzi wenyewe hawana muamko na elimu.utawakuta wanafunzi wanazurula mlimani city ,posta na coco beach tena mida ya masomo . Ukifanikiwa kusikiliza story zao story za bongo flavor za akina diamond au man united. Dream zao eti nao wanataka kutoka wawe kama lulu ,wema au diamond.

Sijui utafiti wako umefanya vipi? Ina maana wanafunzi waliofeli wote wanakaa Dar es Salaam, maana ndiko kuna Mlimani city, posta na coco beach?

Na kama kweli wamefeli kwa sababu wanatumia muda mwingi kwenye facebook, iweje wale wanaosoma International schools - ambao wana better access na mitandao- wafaulu zaidi kuliko hawa St Kayumba?
 
Facebook, Twitter, zako saaaaana na tokea enzi me mnasoma au hata baba zko Akita anayo a enzi za HI5' Aol, etc..... Na Tanzania kwanza zimechelewa kilikua. Pia wanafunzi weye access na vitu hvyo lbda ni ten percent tu, don't base malls iko yako au research yako kwa maeneo ya mjini unanpigia tu, wame deli hata kijito I Kweli.

What am trying to say hapa ni kwamba kufeli li kwa wanafunzi Kidato Cha nne tusilaumu tu social networks (Kenya, Uganda etc wangefeli),.....

Ukweli ni kwamba...
1. Weza kuwa wanafelishwa
2. Labda Mgomo wa walimu unaendelea
3. Mitaala
4. Maandalizi mabovu
5. Usahihishaji pia etc etc

Hii ni social media na wewe haijakufelisha zaidi na zaidi inakujenga hapa wewe, mimi na mwingine.
 
Wanafunzi wamejiloga wenyewe mwaka huu na tusilalamike kuwa serikali ndio imesababisha hapana ingetaka ingewafaulisha ili ipate credit ila hayo yote ya nini?
Itakuwa kama form one ambao hawajui kusoma ila wamefaulu
Kwa hapa kila mtu abebe msalaba wake
Mwanafunzi 75%
Wazazi na shule 23%
Serikali 2%

true dat bro......nngependa japo mwanafunz mmoja angekuja hapa atuambie mambo ylvyo
 
WanaJF Naamini kwa asilimia 90 wengi wenu ni Critical thinkers, na kwa mtazamo huo huo tukiachilia mbali tofauti za kisiasa na Itikadi za kidini twaweza kuzungumza na kupata ufumbuzi wa hili tatizo ongezeko la wadogo/watoto wetu kufeli mitihani yao ya kidato cha nne!
Hints:
1.Ni nin hasa sababu kuu zinazopelekea hawa watoto kufeli kiasi cha kupata sifuri 60%.
2. Nani hasa awajibike kwa maana ya Mwanafunzi, Mzazi, Serikali.
Sitaki kuamini kwamba asilimia 60 ya wahitimu ni vilaza kiasi cha kukosa daraja la nne (Division four) Mimi binafsi nawasiwasi na Ongezeko kubwa la shule za O'level pasipo kuongeza shule za A'level, hata kama wangefaulu tungewapeleka wapi wakati uwezo wa shule za A'level kwa sasa unakidhi asilimia 15 ya wahitimu wote!
Naomba mchango wako!

i'm sor,Jilanga kama vile nakufahamu,umemaliza cha sita Blb 2012?
 
Zaidi ya 94% ya watoto wetu waliomaliza kidatu cha nne mwaka 2012,wameshindwa au hawajapata alama ambazo zitawezesha kuendelea na masomo ya juu.Hawa ni watoto wa walalahoi ambao hawana uwezo wa kuwapeleka watoto wao kwenye shule za kulipia ada kubwa.Huu ni mkakati uliotengenezwa na wanasisa wetu ndani ya nchi ambao watoto wao ndio waliofaulu.Si mmeona wenyewe shule za binafsi ndio zimefaulisha vizuri.Nani mwenye mtoto kwenye shule za binafsi kama sio Rais au waziri au katibi mkuu wa wizara au kamishna,mkurugenzi,mbunge.Kundi hili la viongozi ndilo lililo linaloratibu elimu kwa watoto wetu,ndilo lililowezesha kuanzishwa shule za kata ambazo hazina walimu wala vitendea kazi vingine.Kundi hili la viongozi linajua kuwa watoto wao hawatasoma kwenye shule hizo bali watasoma kwenye shule za binafsi ambazo zimesheheni walimu na vitendea kazi lukuki.Kundi hili la viongozi kwa makusudi kabisa linawandaa watoto zaidi ya 94% wasipate elimu wanayostahili bali linawandaa watoto wao chini ya 6% wawe kama walivyo wao.Mtoto wa mlalahoi hataweza kushindana kwenye ajira na watoto wa viongozi wetu.

Wanajamii naomba nisaidiwe Kikwete na serikali yake wanaipleleka wapi elimu ya nchi hii?
THIS IS A BIG SHAME ON THE GOVERNMENT..........
 
ccm imeniacha hoi ulivoona matokeo ya mafisadi wanafeli imeamua kutumia namba badala ya jina
Kwa hali mbaya ya matokeo
ya kidato cha nne, naweza sema yamechangiwa sana na uhaba wa walimu
pamoja na maslai duni yaliyowapeleka walimu katika migomo baridi..ni
muda wa serikali sasa kupima na kuona jinsi ya kuokoa kizazi
kilichobakia..hali si nzur
 
Ni jambo la kushangaza, kusikia watu wamepigwa na butwaa na kushangazwa na matokeo mabaya ya From 4, mimi nilifikiri ni kitu ambacho kilipaswa kueleweka!

Kitu ambacho watu wengi hawaelewi ni kwamba hiyo elimu ya mpaka miaka ya tisini wanayoiongelea kwamba ilikuwa bora, haikuwa juhudi zetu, ilikuwa ni masalia ya mfumo ambao Wakoloni waliuacha Tanzania na kama vitu vingine vingi kama Reli, Barabara, Bandari, mipango miji n.k ambavyo vyote tumeviua, na sasa mzunguko umekamilika kwa pia kuua Elimu, na kilichobaki ndio uhalisia wetu wa maisha yetu na hawa watoto ndio kizazi cha kwanza cha matokeo ya mfumo wetu wenyewe bila ya wageni!
 
Back
Top Bottom