CHASHA FARMING
JF-Expert Member
- Jun 4, 2011
- 7,789
- 8,917
Kama una mayai 1000 kuna ulazima wa kuyatibu mkubwa
Mkuu kwani hayo madawa yanauzwa Tsh ngapi? na yanapatikana Tanzania? au nayenyewe ni lazima uyanunue kutoka Nje?
Kama una mayai 1000 kuna ulazima wa kuyatibu mkubwa
Mkuu kwani hayo madawa yanauzwa Tsh ngapi? na yanapatikana Tanzania? au nayenyewe ni lazima uyanunue kutoka Nje?
Kwahiyo KM kama nimekuelewa vema, nikishawapata hao Rhode Island kwa mfano, waka-cross na hawa wa kienyeji nliokuwa nao, mayai yatakayokua yanatoka hayana shida kuku hawa wa kienyeji wakilalia ili watotoe? Nauliza hivi kwa sababu nimeshawahi kuuziwa mayai kutoka kwa mtu mwenye hawa machotara nikawawekea hawa wangu wa kienyeji walalie lakini outcome yao nimeshindwa kufaidika nayo. Namimi naomba uni pm namba yako tafadhali.
Madawa yote yanapatikana hapahapa Tanzania.Kwa mfano formaldehyde 40% inauzwa tsh 16500/= ujazo wa lita moja na potassium permanganate ujazo wa gram 500 inauzwa tsh 65000/=
Nakushukuru ndugu Dafo kwa swali lako.Kifupi dalili ya vifaranga kuvimba macho inaweza ikawa ni magonjwa mawili ambayo yote yanakuwa na hizi dalili.Ugonjwa wa kwanza ni upungufu wa Vitamin A.Kifaranga mwenye ugonjwa huu huvimba macho na kutoa uchafu mzito kama sabuni ya kipande iliyolowana.Kuku wenye huu ugonjwa mara nyingi huwa hawaponi,wanakufa.
Ugonjwa huu kwa kawaida hujitokeza baada ya kpindi kirefu cha kiangazi.Kinga ni kuwapa kuku mchicha au majani mabichi mara kwa mara.Pia kuku wote wapewe dawa ya vitamin mfano vitalyte,antistress,amin'total,multivitamin,supervit etc.ili kuzuia kujitokeza kwa ugonjwa.
Ugonjwa mwingine unaonyesha dalili za kuvumba macho ni ugonjwa wa mafua ambayo ni haya kawaida sio yale mafua makali ya ndege.Dalili za mafua (Infectious coryza) ni pamoja kuvimba macho,kuziba macho,huanza jicho moja na badae jicho la pili.Pia kama utapata nafasi ya kuwasikiliza vizuri hasa wakati wa usiku utasikia wanakoroma.Pia kutokwa kamasi puani na kupiga chafya.Ugonjwa huu unatibiwa na dawa moja inaitwa Coridix au tylosine 75%
Kuhusu antistress unaruhusiwa kutumia madala ya vitalyte kweni nayo ipo kwenye kundi la dawa za vitamin.
Tujuze kuhusu kupata parent stock ya layersKama unahitaji parent stock,nipigie nitakupa mwongozo mzuri.Kwa kifupi,kuku wazazi huingizwa nchini toka wakiwa vifaranga,nawe utawakuza mpaka watakapoanza kutaga kisha mayai yataokotwa na kuwekwa tayari kwa kutototoreshwa kwenye machine.Mayai ya parent hayaruhusiwi kuingizwa nchini.
RIKA | CHICKS | GROWERS WANAOKUWA | LAYERS WANAOTAGA |
UMRI KTK WIKI | 0-6 | 7-20 | 20-80 |
KUKU/ENEO LA M[SUP]2 [/SUP]MOJA ZA MRABA | 12 | 9 | 6 |
M[SUP]2 [/SUP]ZINAZOHITAJIKA /KUKU 1000 | 83.7M[SUP]2[/SUP] | 111.2M[SUP]2[/SUP] | 166.6M[SUP]2[/SUP] |
Tujuze kuhusu kupata parent stock ya layers
Asante mkuu nimekuelewa vyema.katika kipindi cha wiki mbili za mwanzo za uleaji wa vifaranga nadhani pia uwezekano wa maambukizi unakua mkubwa, je kusubiri hadi siku ya 16 ndio uanze kuwapatia antibiotic haiwezi kuleta athari? na pia hapo katikati kabla ya siku ya 16 wakiugua wanaweza pewa hiyo otc plus?pia umeshauri ctc20% ni kwa ajili ya kuku wakubwa ningependa kufahamu mkuu ni kuku wa kuanzia umri gani wanastahili kutumia hiyo dawa.asante
mkuu
Mkuu hicho kitabu ni soft copy au?
Mkuu hicho kitabu ni soft copy au?
Ndugu yangu, hawaleti mazara yoyote,kwani kuanzia siku 2-6 vifaranga wanakuwa ndani ya dozi,siku saba vifaranga wanapewa chanjo ya mdondo baada ya hapo kuku wapewe chakula na maji safi yasiyochanganywa dawa hadi siku ya kumi 14 ambapo watapewa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Gumboro.Siku ya kumi 15 wapewe chakula na maji safi yasiyochanganywa na dawa na siku ya kumi 16-20 warudiwe kupewa dawa kwa ajili ya ugonjwa wa kuhara damu.Na siku ya 21 irudiwe chanjo ya Mdondo.Kama utaona kuku wanasinziasinzia na kuzubaa kabla ya siku ya 14 unaruhusiwa kuwapa trisulmysine plus dawa yoyote ya vitamin.
Dawa Ctc 20% kwa kuku wanaokaribia kutaga na wanaotaga inawafaa sana na pia kuna namna ukitumia inatumika kama eggs promoter na kuwafanya kuku watage zaidi.
Kuna mwongozo kwa wafugaji wa kuku,una kila ambacho mfugaji angehitaji.Kifupi unajibu maswali mengi ya wafugaji.Niliuandaa kutokana uzoefu wangu kwenye mambo ya kuku,matatizo mbalimbali niliyokutana nayo ambayo yanawakabili wafugaji nk.Huo mwongozo umeeleza nini cha kufanya toka kifaranga ana siku moja hadi unamuuza kama ni wa nyama na wa mayai mpaka anachoka kutaga.Nimeeleza pia magonjwa mbalimbali hatari ya kuku na namna ya kuyatibu au kuyazuia.Namna ya uanzishwaji wa hatchary kwa ajili ya utotoreshaji wa vifaranga na mengine mengi.Huu mwongozo nauuza kwa tshs 60,000/=Kwa mfugaji halisi ambaye angependa kufuga kwa faida na kuepuka vifo,tuwasiliane.
Mkuu kuna ukweli kwamba majani ndo hufanya kuku watage mayai yenye kiini cha njano?