UDSM: Tunaomba msaada wenu JF!

Anti unajipeleka kwenye modomo wa hatari nenda baadaye uje kushuhudia hapa.SHY si mtu wa kusogolea tafadhali kaeni mbali wanafunzi wa UDSM.Lete madai hapa na tuwasaidie SHY yupo kazini .Akisha waweka sawa anapata credit .Kaeni macho si kila mwana JF anaitakia Tanzania mema wengina mafisadi wako sisi na wao wazi hapa.SHY spare those kids achana tafadhali .


LUNYUNGU AND MWAFRIKA WA KIKE MNAWASI WASI WA BURE NA HUYU SHY... MIMI NAMJUA KWA KARIBU SANA NA FAMILIA YAKE YOTE NAIJUA KWA KARIBU SANA HUYU SI WA KUOGOPWA KABSAAA NA SIDHANI KAMA ANAVYOWATAFUTA HAO WANAFUNZI ATAWEZA KUONGEA NAO.......

Asante mkuu.

Mimi sina sababu ya kumpa nafasi yoyote SHY ingawa najua alivyo na anachofanya. The guy ni snitch na hapa marekani watu kama yeye wanatangazwa neighborhood nzima ili waogopwe na kukimbiwa kama ebola!
 
Jana Niliondoka Kwa Shuguli Zingine Ndio Nimerudi Jioni Hii Kuendelea Na Mchakato Mzima

Unajua mkulu Shy, kukubali bila kukubali inawezekana maana naona ndo unashofanya hapa leo, unataka kuwauza watoto wa watu ili kuongeza credit na hupingi kama unataka kuwauza bali unaconfirm kuwa unataka kuwauza, taratibu mzee waonee huruma.
 
Waga
Mimi simuogopi ila nawaonya .Unalojua kwa SHY si ninalo lijua mimi.I dealt with him kwenye issue moja hapa Dar so najua ninacho kisema.Nasema ninawapa onyo Wanafunzi .Msije kusema JF hamkusema.Mie nasema kwa uwazi .Shy ni trairor na namjua sana hata nyumbani kwao na Baba yake .So nazidi kuonya .
 
Kwa Hakika Mimi Sina Nia Mbaya Au Kitu Kibaya Chochote Kwa Vijana Hawa Nashukuru Kuna 6 Wameshanipigia Simu Nimewaomba Basi Waje Meeda Pub Tuongee Vizuri
 
Kwa Hakika Mimi Sina Nia Mbaya Au Kitu Kibaya Chochote Kwa Vijana Hawa Nashukuru Kuna 6 Wameshanipigia Simu Nimewaomba Basi Waje Meeda Pub Tuongee Vizuri

Hakuna aliyekupigia simu wewe na message zinazoingia sasa hivi ni kuwa wale wote wenye kuendesha mambo hapo chuo wamepata picha yako snitch na traitor mkubwa wewe!
 
Mimi Sikai Kwa Baba Wala Mama Na Hao Kina Baba Na Mama Wala Ndugu Zangu Hawajui Ninapoishi Wala Sehemu Ninayofanya Kazi Kwahiyo Hapo Umenoa Babu

Utaishia Huko Huko
 
Mwafrika Wa Kike Na Lunyungu Wanataka Waongee Wao Peke Yao Na Wanataka Wao Tu Ndio Wasikilizwe Wengine Wakiongea Basi Wapelelezi Na Majina Mengine Wanayowataja

Admini Angalia Hawa Wanachama Wako Ni Wanachama Tu Hawa
 
Mwafrika Wa Kike Na Lunyungu Wanataka Waongee Wao Peke Yao Na Wanataka Wao Tu Ndio Wasikilizwe Wengine Wakiongea Basi Wapelelezi Na Majina Mengine Wanayowataja

Admini Angalia Hawa Wanachama Wako Ni Wanachama Tu Hawa

Wangapi hapa wanaongea na hawapewi lebo kama yako. Achana na hao vijana wa mlimani wafanye kazi yao na usitake kuleta upuuzi wako kuwa walikuwa wanarusha mawe!

Kuna msemo kuwa masnitch hawafi na katika hili umethibitisha msemo huu!
 
SHY bwana kapicha kako hako bwana kanafurahisha sana.
kuna wazungu wa wasichana wanilikuta nasoma posts zako walioona picha yako walifurahi sana wakataka kukutana na wewe,mmoja ndio kapagawa kabisa.

Hebu ni PM tuongee vizuri.

Tukirudi ktk maada SHY anawazingua tu wala si mpelezi wala nini,
 
SHY bwana kapicha kako hako bwana kanafurahisha sana.
kuna wazungu wa wasichana wanilikuta nasoma posts zako walioona picha yako walifurahi sana wakataka kukutana na wewe,mmoja ndio kapagawa kabisa.

Hebu ni PM tuongee vizuri.

Tukirudi ktk maada SHY anawazingua tu wala si mpelezi wala nini,

Hakuna aliyesema kuwa SHY ni mpelelezi. SHY ni snitch, wale watu ambao wanajikombakomba polisi na kuwasaliti wenzao kwa kutumia confidential information.

Tatizo la SHY ni kuwa anasaliti wale wasio na hatia! Grrrrrrr
 
UKWELI KUHUSU YA MATUKIO YA VURUGU YA 17 NA 22 FEBRUARI NA 11 APRILI 2008 KATIKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

UTANGULIZI:

Tarehe 15 Aprili 2008 Chuo kikuu cha Dar es Salaam kilitoa taarifa kwa umma juu ya kusimamishwa masomo kwa wanafunzi mbalimbali. Jumla ya wanafunzi 16 wamesimamishwa kwa makosa ya kufanya na kuwa vinara wa vurugu za tarehe 17 na 22 – februari 2008. jumla ya wanafunzi 4 wamesimamishwa kwa kosa la kufanya vurugu tarehe 11 Aprili 2008.

Tukio la 17 na 22, februari 2008.

Mnamo tarehe 17 na 22 – februari – 2008 kulitokea vurugu zilizofanywa na wanafunzi wa Chuo hicho katika Hosteli za Mabibo (17 februari 2008) na Hosteli za Kampasi kuu (22 februari 2008).

A: CHIMBUKO LA VURUGU ZA 17 FEBRUARI 2008, HOSTEL ZA MABIBO.

Kwa muda mrefu wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam wamekuwa wanakabiliwa na matatizo mengi sana kama vile ukosefu wa maji, kukatika kwa umeme kwa muda mrefu, ubovu wa lifti, upungufu wa Hosteli, vyumba vichache vya madarasa, vyoo vibofu hasa vya kukalia, vyumba kuvuja maji, n.k.

Licha ya ubovu huo wanafunzi wa Chui hiki wamekuwa wavumilivu kwa miaka mingi sana. Kuzoea shida na maisha waliyotoka wanaona kuwa ni sehemu ya maisha ya Mtanzania. Wale wachache wanaosimamia kidete na kusema bila woga hupata misukosuko kutoka katika Utawala wa Rwekaza Mkandala.

Tarehe 17 Februari 20008 maji yalikuwa yamekatika katika Hosteli za Mabibo kwa siku nzima. Licha ya viongozi wa Daruso kuwasilisha matatizo hayo kwa USAB Manager na Mawarden ufumbuzi haukupatikana. Hata gari la maji lilileta maji kidogo na kuyamimina katika matenki ya wanafunzi kuchotea maji. Lakini ilikuja kujulikana kuwa kulikuwa na maji ya Dawasco yalikuwa yamejaa hadi juu katika tenki kubwa la kuhifadhia maji katika Hosteli hizo na kuyasambaza katika vyoo, bafu na matenki ya wanafunzi kuchotea maji. Lakini mafundi na mawardeni walisema kuwa pampu na bomba la kusukuma maji katika matenki ya wanafunzi kuchotea ilikuwa imeharibika.

Baadaye tulijiuliza kwa nini magari ya maji yasichukue maji katika hicho kisima na kuyamimina katika matenki ya wanafunzi kuchotea maji badala ya kuyatoa umbali mrefu?

Tuligundua kuwa kumbe mwenye kampuni hiyo ya kuleta maji katika Hosteli hizo wakati wa dharura alikuwa amekula dili na baadhi ya wafanyakazi wa Chuo ili kuweza kutengeneza “udharura” ili alete maji na hivyo kujipatia fedha kwa kuwaumiza wanafunzi. Pia tuligundua kuwa alikuwa akiingia na maji kisha anamimina kidogo kisha anaondoka na kugeuza na kuja kuyaminina tena, hivyo katika msafara mmoja alikuwa anatengeneza misafara miwili. Ufisadi huu wa wazi kabisa uliwakera wanafunzi wakazi wa Hosteli hiyo ya Mabibo.

Majira ya usiku ya tarehe 17 feburari 2008 ndipo fujo zilianza ambapo wanafunzi walianza kuimba nyimbo na kuandamana kuzunguka katika Hosteli hizo, na hatimaye walikwenda katika makazi za Mawadeni na kuyaharibu. Baada ya vurugu hizo tu maji yalianza kutoka kwa wingi sana.

B: TUKIO LA 22 FEBRUARI 2008 – MAIN CAMPUS

Tukio hilo lilianzia katika Hall 2 – Main Campus. Baada ya wanafunzi wakazi wa Hall 2 kukusanyika kusikiliza majibu ya matatizo yao ya kukosekana kwa lifti.

Kwa muda mrefu Chuo kikuu cha Dar kilitoa ahadi ya kufunga lifti na kukarabati Hall 2 kipindi cha likizo. Hata hivyo hadi chuo kinafunguliwa na hadi semesta ya pili kuanza hakuna lifti iliyokuwa imefungwa. Hivyo wanafunzi walikuwa wakipandisha maji kutoka chini hadi ghorofa ya kumi. Hali hii iliwachosha. Hadi hivi sasa lifti bado haijafungwa.

Licha ya uongozi wa Daruso kupitia kwa mwenyekiti wa Hall 2 na waziri wa Malazi kufatilia kero hiyo utawala ulibakia kutoa ahadi za matumaini kwa wakazi hao. Hivyo Daruso ilianza kuonekana kana kwamba wanashirikiana na utawala wa chuo kuwatuliza wanfunzi kwa ahadi hewa za matumaini.

Hivyo wakazi wa Hall 2 waliamua kuunda uongozi wao utakaokwenda kufatilia kero zao kwa Deputy Vice Chancellor – PFA, Porfesa Yunus Mgaya. Walimchagua mwenyekiti wao aliyeitwa Dominick Deogratius wa mwaka wa kwanza. BA Education, FASS.

Waliandika barua mbalimbali ambazo zilikuwa wakijibiwa na Profesa Yunus Mgaya.
Mnamo tarehe 22 februari 2008, ijumaa majira ya saa mbili usiku wakazi wa Hall 2 walikuwa wamekusanyika ili kusikiliza majibu ya mwenyekiti wao kutoka kwa Profesa Yunus Mgaya. Majibu hayo yalisema kuwa lifti itafungwa ndani ya wiki kumi na nne hivyo wawe watulivu.

Ahadi hiyo iliwapa furaha na kuona kuwa kumbe utawala wa Chuo ukitishiwa unatekeleza vitu ndani ya muda maalum, kwani ni siku chache ambapo wanafunzi hao waliazimia kuwa na mgomo wa kulala nje kwa muda wa siku saba.

Pia hali hiyo ilikuwa ni ushindi dhidi ya Daruso kwani wanafunzi waliweza kufanikisha na kutatua matatizo yao pasipo utawala wa serikali ya wanafunzi Daruso.

Hapo ndipo kero ya maji ilipokuwa imewajia akilini mwao, kwani kwa muda wa siku tatu mfululizo maji yalikuwa yamekatika katika Main Campus na hivyo kulikuwa kuna hali mbaya sana, harufu za vyoo zikukuwa kila mahali. Wanafunzi wa kike walisumbuka sana.

Hivyo wanafunzi walianza kuimba kuwa wanataka maji, wanataka maji huku wakipiga makofi, hali ilipelekea kupata wafuasi wengi kutoka Hall 1 na 5 kwani Chuo kizima kilikuwa hakina maji. Lengo lao lilikuwa ni moja.

Hata hivyo kulikuwa kuna sababu zingine ambazo zilisababisha na kutoa tahadhira kwa wanafunzi hao:

1. wanafunzi walijua kuwa Utawala wa Chuo unapotishiwa matatizo yao yanaisha. Walirejea siku chache ambapo wanafunzi walitishia kufunga barabara ya Mandela hadi matuta yawekwe na matuta yaliwekwa katika barabara hiyo kuingilia Hosteli za Mabibo.
2. walijua kuwa wanafunzi wa Mabibo walipogoma na kufanya vurugu sasa hivi wanapata maji mengi sana.
3. Ongezeko la ada kutoka Milioni moja hadi Milioni mbili ziliwafanya wanafunzi waaangalie huduma wanazopata na ada inayotaka kutozwa na Chuo.
4. walikuwa na nia ya kuwaiga wenzao wa Mabibo.

Hivyo vurugu zilianza ambapo hakuna mtu maalumu ambaye alikuwa akiziongoza. Wazo liliotolewa na wazo lililoafikiwa na wengi wanafunzi walilitekeleza. Viongozi wa Daruso walionekana kama wasaliti. Hivyo walibaki kwa nyuma na kujichanganya na wanafunzi. Kazi yao ilikuwa ni kuzuia maafa zaidi yasitokee.

Vurugu zilianza katika Hall2 kupitia Hall one, kisha kwenda katika makazi ya Makamu Mkuu wa Chuo, profesa Rwekaza Mkandala ndipo wanafunzi waliimba nyimbo za kumambia aache ufisadi, na wakavunja geti la makazi yake, kisha walirudi hadi UDASA baada ya kupata fununu kuwa Rwekaza yupo UDASA Club ankunywa, walifika UDASA na kuvunja geti lakini hawakumkuta. Waliondoka hadi katika ofisi za USAB Manager wakavunja vioo, kisha walielekea hadi Hall seven ambapo waliwatoa walokuwa vyumbani na kuhesabika kama wasaliti. Ilikuwa imetimia saa sita ndipo wanafunzi walitoa wazo la kwenda Swimming Pool kuoga kisha waende wakalale kwani waliamini kuwa ujumbe utatakuwa umefika. Kwani maji yalikuwa yalikuwa yamekatika.

Walipofika swmminig walisukuma geti na kufunguka, hapo ndipo mauti yalimkuta mwenyekiti wao wa Hall 2 baada ya kuruka katika kina kirefu cha Swimming Pool ila kuogelea.

TUKIO LA 11 APRILI 2008 LA UCHAGUZI.

Sababu za vurugu za tukio la tarehe 11 Aprili 2008 zilianza baada ya utawala wa chuo hicho kutoa tamko kwa wanafunzi juu ya kuhahirishwa kwa uchaguzi wa Urais wa Serikali ya wanafunzi (DARUSO) kutokana na kuwepo kwa rufaa nyingi na kujiuzulu kwa wajumbe wa Bodi ya Rufaa.

Hali hiyo ya utawala wa Chuo hicho kuingilia uhuru na demokrasia ya Serikali ya wanafunzi (DARUSO) iliamsha hasira kubwa miongoni mwa wanafunzi na hatimaye kuwafanya kukusanyika katika eneo la Revolutonary Square na baadaye katika ukumbi wa Nkrumah.vurugu hizo kama zinavyoitwa zilianza saa nne asubuhi hadi saa saba mchana.

Tarehe 11 Aprili 2008, ijumaa mgombea wa Urais ambaye inasemekana hatakiwi na utawala wa chuo hicho Bw. Odong Silas Kefa Odwar alipewa barua ya kumtaka kudhibitisha uhalali wake wa kuwepo chuoni kwa kuleta vyeti halali. Tarehe 12 Aprili 2008, jumamosi wafuasi watano wa Odong Odwar walipewa barua za kusimamishwa masomo

HALI HALISI:

wengi wa wanafunzi waliosimamishwa na wale wanaokisiwa kuwa ni wafuasi wa vyama vya upinzania hasa Cahdema, na huwa hawana woga katika kutetea maslahi ya wanafunzi wa Chuo hicho.

Ni wazi kuwa Odong Odwar ambaye ni mgombea wa Urais hatakiwi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na anakubalika kwa kuwa na msimamo wa kutetea wanafunzi.

Makamu mkuu wa Chuo Profesa Rwekaza mkandala anafanya kila awezalo kuua demokrasia na uhuru wa kusema. Baada ya Waziri mkuu kuongea kwa uwazi katika Channel Ten tarehe 14 Aprili 2008 kwenye kipindi cha Jenerali Ulimwengu, siku ya Jumatano tarehe 16 Aprili 2008 alisimamishwa masomo na kuunganishwa katika watu kumi na sita waliofanya vurugu za tarehe 17 na 22 februari 2008.

Pia, anajaribu kudanganya umma kwa kuunganisha watu aliowasimamisha kwa kutetea maslahi ya wanafunzi na kuwaunganisha na watu 5 waliokamatwa wanavuta bangi ambao tayari polisi walishasema hawana hatia, pia hawakupewa barua ya kusimamishwa masomo, ili kuwafanya wale waliosimamishwa kwa kutetea maslahi ya wanafunzi waonekane kama wahalifu, wavuta bangi, n.k mbele ya macho ya wanajamii.


Ni wazi kuwa Chuo kilishindwa kutatua matatizo ya wanafunzi kwa wakati mwafaka. Wanafunzi hao wamekuwa wakiishi katika matatizo hayo kwa muda mrefu hadi hivi sasa. Wakati wanafunzi hao wakiona na kushuhudia nchi ikitafunwa na mafisadi wao wanazidi kutaabika na matatizo yanayowapata wanafunzi hao.

Chuo kikuu kinapaswa kuwa kielelezo cha demokrasia ya kweli na siyo kuingilia uchaguzi wa ndani wa Serikali za wanafunzi kwani ni kitendo cha aibu. Wakati vyuo kama Harvard, Capetown zinajenga demokrasia ya kweli Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinaharibu demokrasia na uhuru wa kweli miongoni mwa umma wa wanafunzi.

Pia ijulikane kuwa Kamati ya uchunguzi ilianza kupoteza mwelekeo wake baada ya kuanza kulalamikiwa na wanafunzi kuwa kamati haikuwa huru na wazi kwa mwanafunzi yoyote aliyekuwa na mapendekezo ya kujenga, pia maswali yaliyokuwa wanafunzi yalikuwa ni katika kujua vyama vyao vya kisiasa badala ya maswali ya kuulizwa maswali ya msingi. Pia kamati haikuwa na uwakilishi wa Serikali ya wanafunzi DARUSO.
NINI KIFANYIKE?

1. Utawala wa Chuo hicho kiwarudishe mara moja wanafunzi hao waendelee na masomo na hawapaswi kupelekwa mahakamani. Kwani ni wazi wanahukumiwa kwa kosa ambalo kiini chake ni Utawala wa Chuo.

2. Vilevile kuwasimamisha wanafunzi hao siyo suluhisho la kutatua matatizo, bali yale yote yaliyokuwa madai ya wanafunzi yanapaswa yatatuliwe kwanza.

3. Ripoti ya Kamati ya Uchunguzi ni vyema ikawekwa wazi kwa umma wote wa watanzania na wanafunzi kwa ujumla waweze kufahamu ripoti hiyo imetoa mapendekezo gani, kwani ni wazi kuwa kamati hiyo ilitumia pesa za walipa kodi wa watanzania. Hivyo ni haki ya watanzania kujua yaliyomo katika ripoti hiyo na isibaki kuwa siri kama wanavyofanya Utawala wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam.

4.
 
SHy haukai mbali sana na anapoishi baba yako so dont fake peoples here kuwa hawajui unapoishi.....

au unataka tuseme location yako kabisa ujue kuwa watu wanakufahamu?
 
SHy haukai mbali sana na anapoishi baba yako so dont fake peoples here kuwa hawajui unapoishi.....

au unataka tuseme location yako kabisa ujue kuwa watu wanakufahamu?

No usiseme location yake maana itakuwa ni kinyume na sheria za JF. Nuff with this snitch kwa sasa. Wanafunzi wengi wamepewa picha yake na wanamkimbia kama ugonjwa hatari wa ebola
 
Hakuna aliyesema kuwa SHY ni mpelelezi. SHY ni snitch, wale watu ambao wanajikombakomba polisi na kuwasaliti wenzao kwa kutumia confidential information.

Tatizo la SHY ni kuwa anasaliti wale wasio na hatia! Grrrrrrr

SHY ni nasubiri PM

Mwanamke
wasaliti AKA nyoka hua mara nyingi huwa wapigaji wa mawe yani wengi wanaopiga mawe CCM ndio hao hao nyoka
 
Back
Top Bottom