Kwa wanyonge njia rahisi ya kusikika mara nyingi huwa ni kuingia barabarani.
Ukifuata sheria ya mazungumzo ya amani hapa nchini utachelewa kufika kwa kuwa watakuweka kapuni na hawajali hata shida ya haraka au utakaa foleni ukome.
Baaada ya migomo kama huu hapo ndipo utaona baraza la chuo watamwita huyo makamu mkuu wa chuo na jopo lake na pia uongozi wa wanafunzi waawelekeze na kushauri cha kufanya.
Inasikitisha kuwa mgomo utokeapo eti ndipo wahusika wanatafuta kuzungumza pande zote.Toeni siasa vyuoni maana hiyo ni taasisi huru haifungamani na chama cha siasa
KUSOMA NI KUELIMIKA
D, teens are tricky, they can corner you easily, ni vizuri kujua kinaga ubaga cha tatizo kabla hujatoa mwongozo. Wenye watoto wanalijua hili. Ni wajibu na haki ya wanafunzi kugoma, hata mie nimeshagoma sana lakini pale tu kunapokuwepo na sababu ya kulazimu mgomo.