UDOM kuajiri wahadhiri 50 toka India?

lugamba2001

Member
Aug 18, 2009
12
0
Habari za uhakika toka kwa raia wa India, aliyepata mkataba wa Kufundisha Sociology UDOM, zinasema kuwa raia wa India wapatao 50, wamepata mkataba wa kufundisha katika Chuo kikuu cha Dodoma, ambapo watalipwa dola za Kimarekani 3,000/ kwa mwezi. Mwandishi wa habari hii, alikutana na jamaa huyo katika chuo kikuu kimojawapo kilichopo, katika jiji la Hyderabad, India. Jamaa huyo aliyepata ajira Bongo, alionyesha hamu kubwa ya kutaka kuongea na mwandishi wa habari hii, baada kugundua ugumu wa nywele katika kichwa chake, kwa kuwa hapa India weusi si kigezo, Maana weusi hapa ni wengi kama vile Kariakoo. Alitaka kujua mwandishi, anatoka nchi gani. Baada ya kuambiwa anatoka Tanzania, alianza kutaka kujua mambo mengi, ikiwa ni pamoja na kuzungumzia ajira yake mpya UDOM. Alieleza kuwa, Interview ya kuwapata ilifanyika jijini Delhi, mwezi wa September, hivyo anajiandaa na safari ya kwenda Tanzania baada ya kufaulu interview hiyo. Baada ya kuona maswali yanakuwa mengi, akashtuka kidogo na kuanza kujidai ana haraka. Akawa hajatoa habari kamili ni lini atatua Bongo, na Mikataba waliyopata ni ya miaka mingapi! Hakuna aliyepatikana toka Serikali ya Tanzania wala UDOM kuthibitisha habari hii. Pateni uhakika toka UDOM au serikali ya Bongo, maana inaamini sana EE (External Expertriatism)
 
Kuna mada iliwahi kujadiliwa humu JF na mimi nilionya tu kwamba serikali ijihadhari na hawa wahindi kwa sababu wengi wana tabia ya kuficha utaalamu wao, na wengine siyo qualified wana vyeti vya kupikwa.

Ukweli ni kwamba interview ya kwanza ilifanyika june, na ya pili ilifanyika mwishoni mwa August. Kweli kuna fani nyingi hatuna wataalamu lakini ni ajabu kwamba wanaajiri mtu wa fani ambazo tunao watu wa kutosha.

Shida yetu kubwa ni science & Technology nadhani huku ndo tunapo hitaji expertiates lakini siyo sociology na english, wahindi wenyewe kingereza ni mgogoro.
 
Tatizo ni uanzishwaji wa vyuo kabla ya kuwa na resources za kutosha. Hivi kweli chuo kiwe na wahindi 50???? Kelele zao madarasani humo sipati picha, itakuaje? Huko ni kufulia kielimu bana! Tafuteni na kwingineko, hata Africa ya Kusini hapo kuna walimu wengi sana na wako fit vibaya mno. Ila hii nchi pia inashangaza: Wakati walimu wazawa wanaenda kufundisha nje sisi tunaenda nje kuleta wageni. Tunao walimu wetu lukuki wametimkia hapo kwa majirani zetu(Rwanda) Prof. Kaijage,Prof.Mshana, to name but a few. Wapo wengine wengi ktk IT na Computer science huko wanapiga job. Kama hatuwezi kumotivate resource zetu wenyewe kila mara zoezi la kutafuta walimu wabahatishaji halitaisha. Tunapoteza vichwa vingi sana wakati nchi inavihitaji hasa kwa kipindi hiki na kijacho. Ikiwezekana nchi iwe na mpango mkakati wa kuwafanya walimu wazawa wabaki na kuwarudisha wale walioenda nje. Kwani Rwanda wanatushinda kitu gani bana? Rwanda imejiwekea mpango wake wa muda mfupi wa kuvuta walimu wazuri toka nchi zote zinazowazunguka mpaka hapo watakapokua na walimu wao wenyewe. Meanwhile inaandaa walimu wao wazawa kwa kasi ya ajabu, wanawapeleka masomoni ndani na nje ya nchi. Sisi tunashindwa nini mpaka tunachukua option ambazo ktk africa hii ndio itakua ya aina yake....wahindi 50???? You can't be serious!
 
Tatizo ni uanzishwaji wa vyuo kabla ya kuwa na resources za kutosha. Hivi kweli chuo kiwe na wahindi 50???? Kelele zao madarasani humo sipati picha, itakuaje? Huko ni kufulia kielimu bana! Tafuteni na kwingineko, hata Africa ya Kusini hapo kuna walimu wengi sana na wako fit vibaya mno. Ila hii nchi pia inashangaza: Wakati walimu wazawa wanaenda kufundisha nje sisi tunaenda nje kuleta wageni. Tunao walimu wetu lukuki wametimkia hapo kwa majirani zetu(Rwanda) Prof. Kaijage,Prof.Mshana, to name but a few. Wapo wengine wengi ktk IT na Computer science huko wanapiga job. Kama hatuwezi kumotivate resource zetu wenyewe kila mara zoezi la kutafuta walimu wabahatishaji halitaisha. Tunapoteza vichwa vingi sana wakati nchi inavihitaji hasa kwa kipindi hiki na kijacho. Ikiwezekana nchi iwe na mpango mkakati wa kuwafanya walimu wazawa wabaki na kuwarudisha wale walioenda nje. Kwani Rwanda wanatushinda kitu gani bana? Rwanda imejiwekea mpango wake wa muda mfupi wa kuvuta walimu wazuri toka nchi zote zinazowazunguka mpaka hapo watakapokua na walimu wao wenyewe. Meanwhile inaandaa walimu wao wazawa kwa kasi ya ajabu, wanawapeleka masomoni ndani na nje ya nchi. Sisi tunashindwa nini mpaka tunachukua option ambazo ktk africa hii ndio itakua ya aina yake....wahindi 50???? You can't be serious!

Rwanda pia ina waalimu kutoa India. Kama anapatikana mhindi mwenye taalum mwacheni apige mzigo huko.
 
Outsourcing human resources? Ila huo mshahara! Ni fedha za walipa kodi au kutoka kwa wajomba?
 
Kitaaluma wahindi wamepiga hatua na wako na elimu nzuri ijapokuwa kuna pia wa street. Kupata walimu kutoka India ni jambo zuri na la kupongezwa na USD 3,000 ni rahisi kwa lecturer kutoka nje angekuwa wa marekani tusingeweza kumlipa.

Kuliko kupeleka vijana wetu India kusoma ni bora kuleta walimu ili watu wengi zaidi wanufaike. Binafsi nilibahatika kukaa Delhi institutional area na NOIDA sector 21 kwa miezi kadhaa na kutembelea vyuo kibao jamaa wamepiga hatua katika taaluma, tubadili mitazamo yetu ili tuende mbele manake mitazamo mingi ni chanzo cha umaskini wetu.
 
Kwa ufupi ni kuwa hiyo misaada mnayosikia ndio inakuja kwa njia hiyo, utakuta labda serikali ya India inaaahidi kutoa msaada wa Elimu Tanzania, hivyo inamleta huyo mtu wao na hiyo hela inahesabiwa kama msaada
 
Tatizo ni uanzishwaji wa vyuo kabla ya kuwa na resources za kutosha. Hivi kweli chuo kiwe na wahindi 50???? Kelele zao madarasani humo sipati picha, itakuaje? Huko ni kufulia kielimu bana! Tafuteni na kwingineko, hata Africa ya Kusini hapo kuna walimu wengi sana na wako fit vibaya mno. Ila hii nchi pia inashangaza: Wakati walimu wazawa wanaenda kufundisha nje sisi tunaenda nje kuleta wageni. Tunao walimu wetu lukuki wametimkia hapo kwa majirani zetu(Rwanda) Prof. Kaijage,Prof.Mshana, to name but a few. Wapo wengine wengi ktk IT na Computer science huko wanapiga job. Kama hatuwezi kumotivate resource zetu wenyewe kila mara zoezi la kutafuta walimu wabahatishaji halitaisha. Tunapoteza vichwa vingi sana wakati nchi inavihitaji hasa kwa kipindi hiki na kijacho. Ikiwezekana nchi iwe na mpango mkakati wa kuwafanya walimu wazawa wabaki na kuwarudisha wale walioenda nje. Kwani Rwanda wanatushinda kitu gani bana? Rwanda imejiwekea mpango wake wa muda mfupi wa kuvuta walimu wazuri toka nchi zote zinazowazunguka mpaka hapo watakapokua na walimu wao wenyewe. Meanwhile inaandaa walimu wao wazawa kwa kasi ya ajabu, wanawapeleka masomoni ndani na nje ya nchi. Sisi tunashindwa nini mpaka tunachukua option ambazo ktk africa hii ndio itakua ya aina yake....wahindi 50???? You can't be serious!
Na kitu kibaya kabisa ni utaratibu mbovu wa kutoa scholarship tunazopewa kwa walimu wanaotaka masters na PHD. Kuna scholarship nyingine huwa mpaka muda wa kutuma upite ndio wanazipeleka vyuoni. Kwa vyovyote vile, bila kuwaandaa walimu wa kutosha wa engineering/science&technology we will suffer. Most of those that go to USA an Europe these days never come back. Kimbilio letu limekuwa wahindi!!! Nakubaliana nawe kwenye kelele sijui itakuwaje..na madust bin kujaa tambuu!! Kazi kweli kweli.
Yule Prof Mshana alikuwa ni mwalimu Pekee wa solid mechanics baada ya Warioba na Selekwa kutorudi TZ walipomaliza PHD zao. Hilo somo muhimu litakosa walimu wa kueleweka trend ikiendelea hivi ilivyo
 
Viongozi wa Tanzania ni watu wa ajabu sana

Bwana mdogo wangu alikuwa anasoma India, anasema Mkurugenzi wa wizara akiwa huko, wlimuuliza swali hili "Serikali ina mpango gani na sisi" aakajibu "Serikali haina mpango wowote na ninyi,mipango jitengenezeeni wenyewe,ukitaka kubaki huku baki,popote nenda tuu".

Nikamwambia dogo maliza uje tutafute kazi, amemaliza yupo hapa anatafuta kazi.
 
Viongozi wa Tanzania ni watu wa ajabu sana

Bwana mdogo wangu alikuwa anasoma India, anasema Mkurugenzi wa wizara akiwa huko, wlimuuliza swali hili "Serikali ina mpango gani na sisi" aakajibu "Serikali haina mpango wowote na ninyi,mipango jitengenezeeni wenyewe,ukitaka kubaki huku baki,popote nenda tuu".

Nikamwambia dogo maliza uje tutafute kazi, amemaliza yupo hapa anatafuta kazi.

Kwanza kitendo cha wao kwenda huko India tu ni deal hilo. Wanasign perdiem za kufa mtu hapo. Unasikia wanaendesha interview ya kwanza halafu wanarudi bongo kula bata. Then wanaenda tena kuendesha ya pili halafu wanarudi bongo kula bata. Then wanaenda ya tatu kufinalize. Then wanawafuata walimu ili waje nao bongo. sie walipa kodi hatujafulia tu hapo?
 
wasije wakawa makanjanja. lakini mshahara huo mbona ni zaidi ya lecturer mweusi (mtz)? NCHi hii mbona mnashindwa kuwajali raia wetu wanaotoil kujenga nchi hii ya tanzania.weupe wanakuja kila siku maskini wanaondoka matajiri weusi wanachakaa tu kujenga nchi. wakati wenzetu wanawajali kwanza wajenga nchi sisi tunajifanya wakalimu sana kwa wageni.
 
nadhani suala hapa ni kupata watu wazuri sana hasa ktk science & Technology. Kweli serikali ya TZ haijali wataalamu wake, professor mtanzania analipwa mshahara milioni 2.5 lakini analetwa mhindi PhD holder analipwa dola 3000 za marekani (3.6 million Tshs) sasa hapo unashangaa kulikoni.

Lakini kama hawa wahindi ni qualified mimi sina tatizo kwani hata nchi nyingine zina outsource wataalamu, japokuwa sisi tuna outsource hata vitu ambavyo hatukutakiwa ku-outsource.
 
Tanzania ni nchi ya ajabu kidogo, labda ndiyo uchanga wenyewe! Ina viongozi ambao mara wafikapo ofisini, hutafuta nini kiwape umaarufu wa haraka haraka, japo wa muda mfupi tu. Hawajali, wala kuzingatia mipango ya maendeleo iliyofanyiwa utafiti na vitengo vya mipango (Planning) vilivyojaza wasomi na mabingwa katika fani husika.

Hali huwa mbaya zaidi uchaguzi unapokaribia, takwimu zitapikwa, zitatengenezwa na ile miradi yoote iliyoanzishwa kwa kufanyiwa utafiti wa kutosha na makini, hufa na miradi ya dharura huanzishwa! Matokeo yake nchi inapoteza mwelekeo, kila anapoingia kiongozi mpya anakuja na lake na kila uchaguzi ukikaribia basi litaanzishwa jipya ilimradi tu kuwazuga wapiga kula. Ushahidi wa haya kila mtu ano! MKUKUTA na MKURABITA, na ile mipango ya 2010 na 2020 imefika wapi!

UDOM hamna jipya, ni yaleyale ya wasomi vipofu au wenye macho lakini wakajidai hawaoni! Kweli kinachotafutwa hapo ni takwimu tu, ili bwana mkubwa apate 'justification' mwaka ujao! Hakuna lolote la maana kwa taifa! Jiulize, wangetoa hizo pesa, wakapeleka Watanzani kusoma! Miezi kumi nane tu wamerudi na wameiva! Sasa huo ulazima wa leoleo unatoka wapi kwa planners? Je ni kweli sasa tatizo la wahadhiri litaisha kwa sababu hiyo? Kufanya mambo kwa zima moto kama vile wakati tunaanzisha chuo hatukuliona hilo ni aibu kwa maprofessa wetu. Taifa halina mpango wa kuendeleza watu wake, au kama upo hautekelezwi kwa sababu hauleti takwimu za haraka za kudanganyia! Kuhusu, taaluma! Mimi nipo India kimasomo na wengine wote waliosoma haku waseme, hiyo tofauti ya kitaaluma iliyopo kati ya India na Tanzania ni ipi? Kiasi cha kuamini tumepata wakombozi!
 
Kuna Jamaa fulani hivi anaitwa Lugalla Yupo America katika chuo cha New Hemiphere huko anafundisha Sociology hiivyo Kama kweli Serikali inataka basi kuna haja ya kuwarudisha Watanzania wengi sana wanafundisha vyuo mbalimbali kuja UDOM na kufundisha huko Kulipwa pesa nyingi katika Elimu basi haina noma kama wana vigezo vyote
 
Kuna Jamaa fulani hivi anaitwa Lugalla Yupo America katika chuo cha New Hemiphere huko anafundisha Sociology hiivyo Kama kweli Serikali inataka basi kuna haja ya kuwarudisha Watanzania wengi sana wanafundisha vyuo mbalimbali kuja UDOM na kufundisha huko Kulipwa pesa nyingi katika Elimu basi haina noma kama wana vigezo vyote

Josh
Harudi mtu kwa mauza uza ya Tanzania. Tanzania inatawaliwa na genge la wahuni na wezi wachache wanaokutana kila kukucha kupanga mabaya kwa wanyonge. Sio kwamba mtu hana uzalendo, ila umeshinda.
 
Kuna Jamaa fulani hivi anaitwa Lugalla Yupo America katika chuo cha New Hemiphere huko anafundisha Sociology hiivyo Kama kweli Serikali inataka basi kuna haja ya kuwarudisha Watanzania wengi sana wanafundisha vyuo mbalimbali kuja UDOM na kufundisha huko Kulipwa pesa nyingi katika Elimu basi haina noma kama wana vigezo vyote

Kuwarudisha wale waliokwishatimka ni ndoto mkuu. Hatuna utamaduni wa kuwajali wasomi nchi hii. Cha msingi hapo ni kuhakikisha kua waliopo nao hawatimki. Maana tusipoangalia tutakuta walimu wote wameshaingia mitini tumebakiwa na wageni tu ambao hata mifano yao haieleweki wanapokua wanashusha nondo zao.
 
It is dream? I should join hand with the follow jamiiforums here on the issue of recruiting lecturers from India. that will not be the contraceptive. I think we are lossing a track. There is a problem between planners and implementers. A good suggestion have been given on how to solve the problem of lecturers in Tanzania but no one is implementing it those findings. Good number of Tanzanian with good educaton are stranded in the streets, no one is ready to pay for their studies. I am in University of Turku,Finland, no one is paing for my studies, I struggle here and there until I get sponsor, our government is not doing so. Where are we heading to?
 
Na kitu kibaya kabisa ni utaratibu mbovu wa kutoa scholarship tunazopewa kwa walimu wanaotaka masters na PHD. Kuna scholarship nyingine huwa mpaka muda wa kutuma upite ndio wanazipeleka vyuoni. Kwa vyovyote vile, bila kuwaandaa walimu wa kutosha wa engineering/science&technology we will suffer. Most of those that go to USA an Europe these days never come back. Kimbilio letu limekuwa wahindi!!! Nakubaliana nawe kwenye kelele sijui itakuwaje..na madust bin kujaa tambuu!! Kazi kweli kweli.
Yule Prof Mshana alikuwa ni mwalimu Pekee wa solid mechanics baada ya Warioba na Selekwa kutorudi TZ walipomaliza PHD zao. Hilo somo muhimu litakosa walimu wa kueleweka trend ikiendelea hivi ilivyo

Kinachoturudisha Nyuma Tanzania ni Ombwe ya uongozi. Wanasiasa wetu Tanzania kila kitu wanakichukulia kwa mtanzamo wa political benefit kwanza kwake binafsi. Tanzania tuna wataalam wengi sana nje ya nchi. Kama wanasiasa wetu wangekuwa serious katika kuendeleza nchi, basi wangeangalia umuhimu wa kuwalipa vizuri hawa watu walionoa bongo zao.

Lakini wapi maslahi na mishahara mizuri wanalipwa akina Chitalilo (vihiyo) na wabunge ambao hawana productivity yoyote katika kuendeleza Taifa zaidi ya kulala bungeni na kuongea kwa kujipendekeza kwa wakubwa wao ili wasitupwe nje uchaguzi ujao.

Hii ndiyo inafanya wataalam wengi wajitumbukize kwenye siasa kama kina Mwandosya, Msekela, Sarungi, Mwakyembe et al. Na wale wanaoona hawawezi kuingia kwenye siasa kwa ajili ya majungu na ushirikina unaoendekwa na wanasiasa, wanaamua kwenda kwenye nchi zinazojali taaluma na kuwalipa ipasavyo kama akina Prof Mshana et al .

Hao wahindi unaosema wanaletwa tayari ni deal la kifisadi la wanasiasa hilo, japo watalipwa $3,000 si ajabu kwenye vitabu zikarekodiwa $6,000 kumzuga Uttouh na timu yake.
 
Matatizo ya wahadhri bongo ni mengi pamoja na mshahara mdogo, uchache wa wahadhiri, uhaba wa ofisi na vitendea kazi vingine, kipao mbele duni cha serikali kuhusu tafiti, na mkururo wa mambo mengi yanayowafanya wahadhiri wetu wakose morali ya kufanya kazi na wengine waamue kutimkia nje.
 
Matatizo ya wahadhri bongo ni mengi pamoja na mshahara mdogo, uchache wa wahadhiri, uhaba wa ofisi na vitendea kazi vingine, kipao mbele duni cha serikali kuhusu tafiti, na mkururo wa mambo mengi yanayowafanya wahadhiri wetu wakose morali ya kufanya kazi na wengine waamue kutimkia nje.

Kweli watatimka karibu wote,sio utani mkuu!
 
Back
Top Bottom