Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Mdomo haumkatai bwana wake.
Ndugu yangu unaweza ukauamuru mdomo wako kuropoka chochote kile na utakutii.

Hebu soma haya hapa chini kisha fananisha na Alfu Lela Ulela:

''...kabla hajafariki dunia Abdulwahid alifanya mazungumzo na Nyerere. Mazungumzo haya baina ya Abdulwahid na Nyerere yalifanyika katika miezi ya mwisho ya mwaka 1968 wakati mashekhe na Waislam mashuhuri wanasombwa na kutupwa gerezani.

Abdulwahid na Nyerere walikuwa wametoka mbali. Watu hawa walikuwa marafiki wa zamani. Huenda kama isingelikuwa kwa msaada wa Abdulwahid historia ya TANU na ya Nyerere mwenyewe zingechukua mkondo tofauti.

Mazungumzo haya yalikuwa muhimu kwa Abdulwahid kwa sababu kwa kiasi fulani alihisi anahusika na yale yaliyokuwa yakiwasibu Waislam, wale kutoka Dar es Salaam. Taarifa za Waislam kukamatwa usiku na kuwekwa kizuizini zilikuwa zikimfikia karibu kila siku.

Abdulwahid hakuweza kujifanya kuwa haathiriki na matokeo yale.

Baadhi ya watu ambao Nyerere alikuwa anawatupa gerezani walikuwa watu ambao yeye Abdulwahid binafsi walimuunga mkono wakati anaanza siasa na watu ambao aliwashawishi wamuunge mkono Nyerere wakati wa kuunda TANU.
..''

Bado akili yako inakueleza kuwa unasoma riwaya na si matokeo ya kweli?
Hivi ndivyo wazee wangu walivyoagana na Nyerere.

Huu ulikuwa mwaka wa 1968.

I dare say 'you are serving the purpose best known to you and your like Mohamed Said' huna uchungu na sio Tanzania wala Zanzibar bali umeamua kutumia mgongo wa dini kutekeleza matakwa yako
 
Last edited by a moderator:
Mohamed Said

Hivi huwa huchoki na hizi hadithi zako za wazee wa kariakoo?
Mimi na wrngi wetu zimeshatuchosha sana.
 
Kwanza nikupongeze mkuu, na nikupe pole kwani mjadala wewe unachukua karibu wiki ya tatu sasa,

Nimeamua kuuleta hapa peupe kwakuwa kule mjadala huu ulijificha chini ya Tamko la maaskofu, lakini hapa tunapata uwanja mpana wakujadiliana kwa hoja kile ukiitacho historia upande wa pili na kile nikiitacho mimi kuwa ni uchochezi na uhaini.

Nikirudi kwenye majibu ya maswali yangu, Jibu lako la kwanza tu linakutoa kwenye maana ya ulichoandika!

Mfano: Unasema,

"Nimeathirika kwa kuona wazee wangu hawamo katika historia kwa hiyo hawatakuwamo katika kumbukumbu kama mashujaa wazalendo waliopigana kuung'oa ukoloni Tanganyika".

Hii inakupa nguvu ya kusema ni historia ya uhuru upande wapili?

Unataka kukiambia kizazi hiki kuwa kila aliyesikia au kuhisi mzazi wake alishiriki katika uhuru wa nchi hii na hayumo kwenye historia aje na kitabu na kukiita historia mpya ya UHURU na kubeza vingine kikiwemo chako?

Katika majibu yako unajichanganya sana, mara useme ni historia ya uhuru upande wa pili, mara histori ya waislamu na sasa unasema ni historia ya wazee wako, Je sisi tusimamie wapi?

Weka sawa kwenye jibu la kwanza tu hapo ili twende mbele mkuu!

Ikiwa utajituliza tutakwenda vizuri katika mjadala huu wetu.
Bahati mbaya kuna watu wanakuunga mkono lakini wanatukana.

Ni shida mie kujibu matusi hivyo sisemi kitu kwao.

Nimegundua kitu kimoja kwako nacho ni ufahamu wa Kiswahili.
Kiswahili kama lugha inakwenda na utamaduni.

Mimi sina lugha nyingine isipokuwa Kiswahili. Sina lugha ya kikabila.

Naona huko nyuma nimesema sitakufanyia jambo fulani nikasema ''nisamehe.''

Nadhani wewe kwa kuwa huna utamaduni wa lugha sawa na mie ukachukua ile
samahani kuwa nimeomba radhi na ukafanya hicho kuwa jambo kubwa kwako.

Ukweli ni kuwa katika utamaduni wa watu wa pwani huo ni msemo wa kiungwana
baina ya watu wawili wenye kustahiana.

Sikukuomba radhi.

Sikulaumu hukuwa unajua.

Kwa hakika mimi sijichanganyi labda ukisoma huelewi kama nilivyoonyesha hapa juu.
Ningekuwa mimi ni mtu wa kujichanganya nyote nyie mngekuwa mshachoka kunisoma.

Sasa tuje tena kwenye lugha.

Nikisema ''upande wa pili,'' ''ya Waislam'' na mfano kama huo kwa lugha kama tunavyoongea watu wa pwani
maana ni ile ile kuwa nakusudia historia ya wazee wangu dhidi ya historia rasmi.

Usikejeli kwa kutia hoja zisizokuwa na maana.
Mie si wa kutaka kuwa kila mtu aandike kitabu.

Napenda kukuasa na hii ni kwa faida yako.
Naamini wewe ni kijana na una miaka mingi ya kuishi Insha Allah.

Watu wengi wanatusoma humu.
Jitokeze kama msomi makini na mtu alofunzwa na wazazi wake.

Maandishi yako yatoe nuru ya akhlak (tabia) yako.
Jiepushe na lugha za kibri...za kuamrisha.

Fanya hivi, fanya vile...jibu kwanza...
Lugha hizi hazifai.

Mimi ni mtu mzima na mzee khasa sawa pengine na baba yako naweza kukuzaa.
 
Hivi huwa huchoki na hizi hadithi zako za wazee wa kariakoo?
Mimi na wrngi wetu zimeshatuchosha sana.

Ikiwa ukumbi utaona nijitoe katika mjadala mimi sitalazimisha kuwemo.
Nitajitoa na hamtasoma tena ''hadithi.''

Washauri wana ukumbi mkifikia makubaliano niarifu.
 
Mwita Maranya bana, unatamaani niwe president? Nitalifikiria ombi lako kwa sasa tunamwambia Yericko aache kutugawa kwa misingi ya kidini yeye ni mtu muhimu sana kwa CHADEMA.

Katika mada hii ukisoma kwa kina utagundua kuwa siwagawi watanzania bali nazuia kwa nguvu harakati za kuwagawa zinazofanywa na akina Mohamed Said
 
Ikiwa utajituliza tutakwenda vizuri katika mjadala huu wetu.
Bahati mbaya kuna watu wanakuunga mkono lakini wanatukana.

Ni shida mie kujibu matusi hivyo sisemi kitu kwao.

Nimegundua kitu kimoja kwako nacho ni ufahamu wa Kiswahili.
Kiswahili kama lugha inakwenda na utamaduni.

Mimi sina lugha nyingine isipokuwa Kiswahili. Sina lugha ya kikabila.

Naona huko nyuma nimesema sitakufanyia jambo fulani nikasema ''nisamehe.''

Nadhani wewe kwa kuwa huna utamaduni wa lugha sawa na mie ukachukua ile
samahani kuwa nimeomba radhi na ukafanya hicho kuwa jambo kubwa kwako.

Ukweli ni kuwa katika utamaduni wa watu wa pwani huo ni msemo wa kiungwana
baina ya watu wawili wenye kustahiana.

Sikukuomba radhi.

Sikulaumu hukuwa unajua.

Kwa hakika mimi sijichanganyi labda ukisoma huelewi kama nilivyoonyesha hapa juu.
Ningekuwa mimi ni mtu wa kujichanganya nyote nyie mngekuwa mshachoka kunisoma.

Sasa tuje tena kwenye lugha.

Nikisema ''upande wa pili,'' ''ya Waislam'' na mfano kama huo kwa lugha kama tunavyoongea watu wa pwani
maana ni ile ile kuwa nakusudia historia ya wazee wangu dhidi ya historia rasmi.

Usikejeli kwa kutia hoja zisizokuwa na maana.
Mie si wa kutaka kuwa kila mtu aandike kitabu.

Napenda kukuasa na hii ni kwa faida yako.
Naamini wewe ni kijana na una miaka mingi ya kuishi Insha Allah.

Watu wengi wanatusoma humu.
Jitokeze kama msomi makini na mtu alofunzwa na wazazi wake.

Maandishi yako yatoe nuru ya akhlak (tabia) yako.
Jiepushe na lugha za kibri...za kuamrisha.

Fanya hivi, fanya vile...jibu kwanza...
Lugha hizi hazifai.

Mimi ni mtu mzima na mzee khasa sawa pengine na baba yako naweza kukuzaa.

Falsafa yako yakuamini ni sahihi kile ukiaminicho si tu inafifisha mjadala na kudharirisha weledi wako, bali inanifedhehesha hata mimi ninaejadiliana nawe hapa.

Mkuu Mohamed Said, mimi ni MSWAHILI asilia na wakimachipuko, na nimelelewa katika maadili ya ustarabu wa kiafrika na ninaamini katika jando la taifa!

Si muamini wa utwana na si muamini wa maisha ya kiimla.

Turudi kwenye mjadala mkuu, ninakuomba ujibu swali langu kama lilivyo ili tusonge mbele kwa faida ya watanzania,

Mengine ya utwana hayawasaidii watanzania hawa unaowapotosha kwa maandiko yako uyaitayo ni historia sahihi ya uhuru wa Tanganyika!
 
I dare say 'you are serving the purpose best known to you and your like Mohamed Said' huna uchungu na sio Tanzania wala Zanzibar bali umeamua kutumia mgongo wa dini kutekeleza matakwa yako

Hii ndiyo historia yetu.
Haya mambo yalitokea na kwetu na kizazi chetu ni muhimu yakijulikana ili tujikinge yasitokee tena.
 
Katika mada hii ukisoma kwa kina utagundua kuwa siwagawi watanzania bali nazuia kwa nguvu harakati za kuwagawa zinazofanywa na akina Mohamed Said

Vipi kuhusu wale 'activists' kwenye ile doc aliyopost Mzee Mwanakijiji wanaodai kuwa rais Kikwete anapendelea waislamu unawaunga mkono?
 
Falsafa yako yakuamini ni sahihi kile ukiaminicho si tu inafifisha mjadala na kudharirisha weledi wako, bali inanifedhehesha hata mimi ninaejadiliana nawe hapa.

Mkuu Mohamed Said, mimi ni MSWAHILI asilia na wakimachipuko, na nimelelewa katika maadili ya ustarabu wa kiafrika na ninaamini katika jando la taifa!

Si muamini wa utwana na si muamini wa maisha ya kiimla.

Turudi kwenye mjadala mkuu, ninakuomba ujibu swali langu kama lilivyo ili tusonge mbele kwa faida ya watanzania,

Mengine ya utwana hayawasaidii watanzania hawa unaowapotosha kwa maandiko yako uyaitayo ni historia sahihi ya uhuru wa Tanganyika!

Huwa silazimishwi kufanya jambo.
Wala simlazimishi mtu kuamini niliyoandika.
 
Mwandishi wa uzi huu udini na kutojua historia ya zanzibar ndio ulokupelekea kuandika pumba zako soma kitabu kinachoitwa uhasidi wa marekani kwa mapinduzi ya zanzibar. Kilichotungwa na giorgio galinoshadjivayansi na abdulrahman babu ndio utajua ukweli wote otherwise u havo no right to question any thng about zanzibar
Nadhani wewe ndiye uliyekurupuka na nina hakika hujasoma uzi wote. Malizia kahawa na kashata kwanza halafu soma tena uzi wote then changia. Unaweza ukaokotaokota kitu cha maana cha kuchangia tofauti na ulivyofanya sasa.
 
Yeriko, achana na watu wenye ubishi wa kijiweni. hawa wanajua kukariri na kumeza hivyo ilivyo. Unapoleta hoja zinazohitaji fikra na uchambuzi, utawachosha!

Soma hapa chini na mtafute nani mchochezi:

Jan P van Bergen katika kitabu chake, Development and Religion in Tanzania,(1981) [1] ametoboa siri kuhusu uadui aliokuwa nao Rais Mstaafu, Nyerere dhidi ya Uislam na Waislam.

Kitabu kinaeleza kwa ufasaha jinsi Nyerere wakati alipokuwa madarakani alivyokuwa akifanya mikutano ya siri na viongozi wa Kanisa kuweka mikakati ya kuupa nguvu Ukristo. Katika mikutano hiyo Nyerere aliwahakikishia viongozi wa Kanisa kuwa anaaunga mkono Ukristo.

Kitabu hicho kinaeleza jinsi Nyerere alivyotimiza ahadi yake hiyo kwa Kanisa kwa kuhakikisha kuwa anawapa Wakristo nafasi za juu katika serikali na chama.

Kitabu hiki kilikuwa kinauzwa Catholic Bookshop, Dar es Salaam. Lakini ilipokuja kudhihirikia Kanisa kuwa kitabu hiki kilikuwa kinatoa habari nyeti na siri za Kanisa kuhusu njama dhidi ya Waislam, kwa haraka sana kikaacha kuuzwa. [1]

Hadi hivi sasa kitabu hicho ni marufuku kuletwa tena Tanzania.


Kitabu cha pili ni cha Dr John C. Sivalon, Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania Bara 1953 Hadi 1985 (1992). [1] Kitabu hiki kinaeleza njama ndani ya serikali kuuhujumu Uislam. Sivalon anafichua kuwa kuanzia mwaka 1961 baada ya Tanganyika kupata uhuru, Kanisa lilikuwa na hofu mbili. Hofu ya kwanza ilikuwa umoja wa madhehebu za Kiislam kati ya Sunni, Bohora, Ismailia na Ithnasheri. Hofu ya pili ilikuwa kuhamishwa kwa makao makuu ya EAMWS kutoka Mombasa kuja Dar es Salaam.

Kanisa lilikuwa linahofu kuwa mali walizokuwanazo Waasia Waislam zikitiwa katika harakati za Waislam ambao walikuwa na nguvu kubwa katika uwanja wa siasa zitaathiri maslahi ya Ukristo katika Afrika ya Mashariki. Kwa ajili hii Kanisa likatanganza kuwa Uislam ni adui wake na ikaanza mikakati ya hujma dhidi ya Uislam ili kuudhoofisha. [1]
 
Huwa silazimishwi kufanya jambo.
Wala simlazimishi mtu kuamini niliyoandika.

Hahaaha sasa mkuu Mohamed, ili tuendelee na mjadala huu unapenda/unapendekeza mimi niwe nakufuata utakacho?

Ikiwa hujibu hoja zenye sura ya mantiki ya mjadala, jamii uliyodai hapa kuwa inatuangalia itatuelewa vipi mkuu?

Tuliza murkali mzee, kaa kwenye hoja tusonge membele,

Mjadala mkuu ni upotoshaji wako uliokatika maandishi uliyoyaita Historia ya Uhuru uande wa pili! Tetea hoja zinazochomoza kutokana na kitabu chako mkuu!
 
Mohamed Said,
Tunakushukuru sana umewafumbua macho watanzania wengi Mungu akuzidishie usichoke kutoa darsa.

Najua utakutana na vikwazo vingi kejeli, matusi, dhiaka, lakini hizo ni changamoto.

Tunakuombea dua...
 
Last edited by a moderator:
Mohamed Said,
Tunakushukuru sana umewafumbua macho watanzania wengi Mungu akuzidishie usichoke kutoa darsa.

Najua utakutana na vikwazo vingi kejeli, matusi, dhiaka, lakini hizo ni changamoto.

Tunakuombea dua...
Na majini nayo yatamwombea aishi maisha marefu ili aendelee kusanifu historia zingine ma kuupotosha umma.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu zangu,

kwa mtindo huu wa kulaumu mambo yaliyo pita, Ujerumani na Japan zisinge inuka kiuchumi na kimiundo mbinu baada ya kuteketezwa ( Obliteration ) ya vita kuu ya pili (WWII).


There are a lot of challenges we all face as a nation irrespective of our denominations. Let us solve them instead of Blaming the past.
 
Hahaaha sasa mkuu Mohamed, ili tuendelee na mjadala huu unapenda/unapendekeza mimi niwe nakufuata utakacho?

Ikiwa hujibu hoja zenye sura ya mantiki ya mjadala, jamii uliyodai hapa kuwa inatuangalia itatuelewa vipi mkuu?

Tuliza murkali mzee, kaa kwenye hoja tusonge membele,

Mjadala mkuu ni upotoshaji wako uliokatika maandishi uliyoyaita Historia ya Uhuru uande wa pili! Tetea hoja zinazochomoza kutokana na kitabu chako mkuu!

Mkuu Yericko Nyerere hapo ndipo pagumu sana unapofanya mjadala na ustaadh Mohamed Said. Hana uwezo wa kujenga hoja kutetea hoja zake. Mara nyingi ni mtu wa kutaka kukulisha sumu tuuu ukimbana kwenye kona hachelewi kukimbia.

Sisi wengine tulishajaribu kujadiliana nae kila tukimtupia maswali ya maana kuhusu tenzi zake na masimulizi ya mababu/wazee wake anaishia kupepesa macho. Kwahiyo usimshangae ndivyo alivyo na ndivyo anavytaka kila mtu akubaliane nae, anasahau kwamba hapa ni JF na sio redio imani ambako haulizwi maswali ya kumchallenge!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom