Picha za Sheikh Suleiman Takadir Wakati wa Anapigania Uhuru wa Tanganyika (1954 - 1958)

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,264
Picha za Sheikh Suleiman Takadir Wakati Anapigania Uhuru wa Tanganyika (1954 - 1958)

1697775002545.jpeg

Kulia: Bibi Titi Mohamed, Clement Mohamed Mtamila, Sheikh Suleiman Takadir, Julius Nyerere katika moja ya mikutano ya TANU ya mwanzoni 1954/55
1697775056061.jpeg

Kushoto: Sheikh Suleiman Takadir, John Rupia na Julkius Nyerere na nyuma waliosimama na silaha za jadi ni Bantu Group wahamasishaji umma na walinzi wa chama cha TANU.
1697775141854.jpeg

Waliochutama wa pili kulia ni Sheikh Suleiman Takadir
1697775246913.jpeg

Sheikh Suleiman Takadir kulia wa tatu waliochutama
Wazee mashuhuri waliomuunga mkono Julius Nyerere walikuwa Sheikh Suleiman Takadir mwanachuoni wa Kiislamu aliyeelimika sana, akijulikana zaidi kwa jina la utani ''Makarios,'' Jumbe Tambaza, mzee aliyekuwa akihodhi ardhi kubwa; Mshume Kiyate, mzee muuza samaki aliyekuwa na kipato kizuri; Mwinyijuma Mwinyikambi, mzee aliyekuwa na viunga vya minazi na miembe; Rajabu Diwani, seremala hohe hahe lakini aliyejaaliwa ufasaha mkubwa wa kuzungumza; Max Mbwana, kiongozi wa Wazaramo mjini Dar es Salaam; Sheikh Haidari Mwinyimvua, fundi cherehani na mtu mwadilifu; Iddi Faizi Mafungo na Idd Tosiri ndugu wawili Wamanyema na binamu wa Sheikh Mohamed Ramia wa Bagamoyo, Khalifa wa tariqa ya Qadiriya.

Iddi Faizi akiwa Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na Iddi Tosiri mwanachama shupavu; Iddi Tulio, mzee mwenye heshima zake, Mashado Ramadhani Plantan, mhariri na mmiliki wa gazeti la Zuhura na kaka yake Schneider Abdillah Plantan, watoto wa Affande Plantan.

Julius Nyerere aliungwa mkono na wazee wengine wengi wa mjini.
Hiki kilikuwa kipindi muhimu katika historia ya Tanganyika.
(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes)
Haiwezekani hata kidogo historia hii ikafutwa katika maisha ya Julius Nyerere katika historia ya uhuru wa Tanganyika na katika historia ya chama cha TANU na Tanganyika ikawa na historia ya kweli ya ukombozi wake.
 
Huyu Suleiman Takadir,alitaka kupinga mfumo kristo Mwaka 1958. Nyerere akamfukuza Tanu,na waislam wenzake wakamtenga. Wakampachika jina kuwa Suleiman mtakadini🤣🤣🤣🤣🤣🤣💺
 
Hakika JKN alikua mjuzi wa mambo,bila yeye hata mzee side asinge weza kuuona uhuru wa tanganyika mana Waislamu waliukataa wakitaka mpaka waelimike,kitu ambacho kingechelewesha uhuru, hivyo kwa maono na uwezo wa JKN alipambana uhuru ukapatikana na kutaifisha shule zote za makanisa na za taasisi mbalimbali ili ziwe za umma ili kila mtanganyika apate elimu bila ubaguzi wowote.

Hakina JKN alikua mjuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii.

Naliomba kanisa RC liharakishe mchakato wa kumtangaza kama mwenye heri hatimaye kuwa Mtakatifu mana watanzania tunajivunia neema ya baba wa taifa JKN.
 
Hakika JKN alikua mjuzi wa mambo,bila yeye hata mzee side asinge weza kuuona uhuru wa tanganyika mana waislamu waliukataa wakitaka mpaka waelimike,kitu ambacho kingechelewesha uhuru,hivyo kwa maono na uwezo wa JKN alipambana uhuru ukapatikana na kutaifisha shule zote za makanisa na za taasisi mbalimbali ili ziwe za umma ili kila mtanganyika apate elimu bila ubaguzi wowote.

Hakina JKN alikua mjuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii.

Naliomba kanisa RC liharakishe mchakato wa kumtangaza kama mwenye heri hatimaye kuwa Mtakatifu mana watanzania tunajivunia neema ya baba wa taifa JKN.
Jiwe...
Nimeeleza hapa kuwa AMNUT hakikuwa chama cha Waislam kwa maana ya TANU kilivyokuwa chama cha Waislam.

Waislam chama chao kwa hakika kilikuwa TANU.

Kweli AMNUT kilianzishwa Waislam: Abdallah Mohamed, Khamis Hunde, Ramadhani Mashado Plantan, Abdulwahid Abdulkarim lakini mwisho wake ni hapo tu.

Waislam kwa ujumla wao walikipiga vita waziwazi na AMNUT ikabakia jina hakina watu.

Nimeweka hapa pia barua waliyoandika kwenda Trusteeship Council mwaka wa 1960 kueleza kuwa wamefuta msimamo wao wa kuchelewesha uhuru.

Rejea nyuma usome upya ikiwa haya yalikupita.
 
Back
Top Bottom