ChaMtuMavi
JF-Expert Member
- Oct 15, 2008
- 330
- 8
Leo ninakerwa na uchafu unaoimarishwa na viongozi wetu ambao unaathiri afya za wananchi.
Kuna hii issue ya viongozi wetu (wanasiasa) Kuanzisha shule zao binafsi (private schools). Tunawashukuru kwa jitihada zao; LAKINI.
Viongozi wanajenga shule bila kuweka system za kukusanya na ku-treat maji taka toka vyooni (sewage). Hii inasikitisha sana.
1. Kuna shule ya Mbunge wa Songea Mh.John Komba, ipo kule Mbweni Mpiji. Shule ni ya bweni, imezungushiwa wigo wa senyenge. Ina wanafunzi zaidi ya 1000. Maji ya vyooni yanayozalishwa na wanafunzi yamechimbiwa ka-mfereji (open & shallow) nje ya fence ya shule. Maji hayo yanatiririka kuelekea kwenye barabara kuu na kwenye property za wengine jirani, yananuka sana. Wananchi wanalalamika lakini hakuna hatua zinazochukuliwa kisa eti shule ni ya mheshimiwa, ameshafikishiwa malalamiko lakini hakuna kilichofanyika.
Kwa hali hii Watanzania tutaondokana na uchafu????
2. Shule nyingine ni ya mam ANNA MKAPA ipo karibu na shule ya Mh. Komba kule Mbweni Mpigi. Yenyewe ipo kwenye mwinuko na imezungushiwa vizuri sana, lakini nayo inatema untreated maji taka nje ya fence, yakielekewa katika makazi ya wananchi.
Jamani huyu mwananchi atajikomboaje na hali hiii? Ni MJINGA, MASIKINI, pia manamletea MARADHI mpaka kwenye mmakazi yake???? HUU NI UUNGWANA KWELI???
Viongozi tunawachagua wajipatie pesa na kuanzisha miradi inayowaua wananchi?? Halafu leo utamkemea mwekezaji huko Geita anauwa wananchi kwa taka za sumu majini???
Vipindupindu, mazalio ya mbu na malaria vitaishaje??
Sisi wananchi wa eneo hili tumekerwa sana, tumeona tulilete humu ili wanaJamii Forum watusaidie kuchambua hilo. Mji wetu ni mpya, planned na tungependa tuuweke katika hali inayokubalika ki-mazingira lakini viongozi wetu wanatuangusha na kutukatisha tamaa.
Kuna hii issue ya viongozi wetu (wanasiasa) Kuanzisha shule zao binafsi (private schools). Tunawashukuru kwa jitihada zao; LAKINI.
Viongozi wanajenga shule bila kuweka system za kukusanya na ku-treat maji taka toka vyooni (sewage). Hii inasikitisha sana.
1. Kuna shule ya Mbunge wa Songea Mh.John Komba, ipo kule Mbweni Mpiji. Shule ni ya bweni, imezungushiwa wigo wa senyenge. Ina wanafunzi zaidi ya 1000. Maji ya vyooni yanayozalishwa na wanafunzi yamechimbiwa ka-mfereji (open & shallow) nje ya fence ya shule. Maji hayo yanatiririka kuelekea kwenye barabara kuu na kwenye property za wengine jirani, yananuka sana. Wananchi wanalalamika lakini hakuna hatua zinazochukuliwa kisa eti shule ni ya mheshimiwa, ameshafikishiwa malalamiko lakini hakuna kilichofanyika.
Kwa hali hii Watanzania tutaondokana na uchafu????
2. Shule nyingine ni ya mam ANNA MKAPA ipo karibu na shule ya Mh. Komba kule Mbweni Mpigi. Yenyewe ipo kwenye mwinuko na imezungushiwa vizuri sana, lakini nayo inatema untreated maji taka nje ya fence, yakielekewa katika makazi ya wananchi.
Jamani huyu mwananchi atajikomboaje na hali hiii? Ni MJINGA, MASIKINI, pia manamletea MARADHI mpaka kwenye mmakazi yake???? HUU NI UUNGWANA KWELI???
Viongozi tunawachagua wajipatie pesa na kuanzisha miradi inayowaua wananchi?? Halafu leo utamkemea mwekezaji huko Geita anauwa wananchi kwa taka za sumu majini???
Vipindupindu, mazalio ya mbu na malaria vitaishaje??
Sisi wananchi wa eneo hili tumekerwa sana, tumeona tulilete humu ili wanaJamii Forum watusaidie kuchambua hilo. Mji wetu ni mpya, planned na tungependa tuuweke katika hali inayokubalika ki-mazingira lakini viongozi wetu wanatuangusha na kutukatisha tamaa.