Ubinafsi huu utaiua CCM na kuiacha nchi ikiwa taabani

fikirikwanza

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
7,452
3,065
Ukiangalia kwa kina unagundua ni ubinafsi mkubwa ambao unafanyika bila kujali maslahi ya taifa. Maslahi ya taifa ni kitu chochote ambacho kinakuja kwanza ama kabla ya maslahi ya mtu, kikundi au chama.

Ukimuuliza mwana CCM kama Nape na wengine wengi nyuma yake, utasikia hawako tayari kuona CCM inakufa, hata kuona inaachia ngazi kiserikali. Hapa unapata mawazo mengi sana, kuwa nani aliwaambia na kuwasadikisha kuwa CCM lazima iwepo na lazima ishike dola kila uchaguzi??? kuna ubaya gani CCM after 50years ya kuongoza tanzania ikasema inaachia ngazi, ukiangalia hali ya uchumi wa nchi hii, ukaangalia mihimili ya uchumi kuwa ni siasa safi, watu, uongozi bora na ardhi, unagundua kuwa watu makini ndani ya CCM wangeomba CCM iachie serikali ili kupata fursa ya kujifunza wapi walikosea na wapi walifanya vizuri. ni suala la akili na hekima tu hapa, kila mtz analalamika uchumi na maisha duni sasa kama kiongozi unajitathmini harafu unachuka hatua za kuachia ngazi.

ukitoa ubinafsi wa viongozi na viongozi nyemelezi, utauona ukweli kuwa CCM kwa hali ilivyo sasa inapaswa kwa heshima kubwa kujiweka pembeni ili watu wengine na mawazo mengine yaweze kufanyiwa kazi. Ubinafsi wa kutaka kutawala milele, ubinafsi wa kufanya nchi kama aina fulani ya biashara. Viongozi wakubwa wanataka wawalisishe wadogo tena mbaya zaidi wenye uhusiano wa damu madaraka ya nchi ambayo hapo awali tuliwapa wao madaraka kwa jitihada zao sio za watoto na familia zao kwa ujumla.

Leo hii watoto wa vigogo wa zamani ndo viongozi wetu katika serikali, chama na mashirika ya umma. orodha ni ndefu na inajulikana kwa kila mtu.

Ubinafisi huu utaiua CCM kifo kibaya sana, kuna watu wanaamini kuwa kuna mgogoro mkubwa ndani ya CCM kugombea madaraka, nami pia naamini hivyo; Kuna kambi ya Lowassa, Membe, Sitta etc. Hawa watu hawawezi kukubaliana kutokana na faida binafsi na ubinafsi. Chama kimepoteza mvuto kwa raia wa tz hata wanawake ambao ndo walikibeba sana kwenye chaguzi za hivi karibuni, chama kimepoteza mvuto kwa wazee (suala la mafao yao) na wakulima (bei za mazao ya biashara kama pamba etc) ambao pia walikuwa nyuma yake kwa miaka nenda rudi.

Hali hii ya kutokubaliana na ukweli kuwa kivumacho hakidumu, hakuna mwenye hati miliki ya ikulu ya dar es salaam, hakuna mwenye hati miliki ya jimbo lolote TZ au halmshauri yoyote ndo itapelekea CCM kufa na pengine kuacha nchi ktk hali ya mmomonyoko mkali. Tukubali hali ya kutokukubali kuacha madaraka ilianza na ipo ndani ya CCM kwa muda mrefu. fikiria utitili wa majimbo ya uchaguzi hata kama hakuna tija kwa wananchi kwa lengo moja tu la kupatiana sehemu ya madaraka ili kila mwanaCCM mafia apate jimbo. Tumeshuhudia majimbo yakigawanywa bila sababu halisi (real reasons) japo sababu nzuri (good reasons) juu ya jambo hilo hutolewa. ubinafsi na uroho wa madaraka umefanya wilaya kuongezeka hata kama hatuna fedha za kuhudumia wilaya na mikoa hiyo.

Wakati technolojia inapanda na uwezo wa mtu mmoja kuhudumia sehemu kubwa zaidi kwa njia ya teknolojia unakuwa mkubwa, ambapo tulipaswa kupunguza hata wilaya na mikoa yetu, sisi tunaongeza kwa faida ya wachache. kwa hili ndo kodi zinaongezeka hata bila kujali vipato vya watanzania, kwa hili nani alaumiwe??? sio ubinafsi huu???

Ubinafsi huu utaiua CCM na kuiacha nchi ikiwa taabani.

Nawasilisha
 
Ukiangalia kwa kina unagundua ni ubinafsi mkubwa ambao unafanyika bila kujali maslahi ya taifa. Maslahi ya taifa ni kitu chochote ambacho kinakuja kwanza ama kabla ya maslahi ya mtu, kikundi au chama.

Ukimuuliza mwana CCM kama Nape na wengine wengi nyuma yake, utasikia hawako tayari kuona CCM inakufa, hata kuona inaachia ngazi kiserikali. Hapa unapata mawazo mengi sana, kuwa nani aliwaambia na kuwasadikisha kuwa CCM lazima iwepo na lazima ishike dola kila uchaguzi??? kuna ubaya gani CCM after 50years ya kuongoza tanzania ikasema inaachia ngazi, ukiangalia hali ya uchumi wa nchi hii, ukaangalia mihimili ya uchumi kuwa ni siasa safi, watu, uongozi bora na ardhi, unagundua kuwa watu makini ndani ya CCM wangeomba CCM iachie serikali ili kupata fursa ya kujifunza wapi walikosea na wapi walifanya vizuri. ni suala la akili na hekima tu hapa, kila mtz analalamika uchumi na maisha duni sasa kama kiongozi unajitathmini harafu unachuka hatua za kuachia ngazi.

ukitoa ubinafsi wa viongozi na viongozi nyemelezi, utauona ukweli kuwa CCM kwa hali ilivyo sasa inapaswa kwa heshima kubwa kujiweka pembeni ili watu wengine na mawazo mengine yaweze kufanyiwa kazi. Ubinafsi wa kutaka kutawala milele, ubinafsi wa kufanya nchi kama aina fulani ya biashara. Viongozi wakubwa wanataka wawalisihe wadogo tena mbaya zaidi wenye uhusiano wa damu madaraka ya nchi ambayo hapo awali tuliwapa wao madaraka kwa jitihada zao sio za watoto na familia zao kwa ujumla.

Leo hii watoto wa vigogo wa zamani ndo viongozi wetu katika serikali, chama na mashirika ya umma. orodha ni ndefu na inajulikana kwa kila mtu.

Ubinafisi huu utaiua CCM kifo kibaya sana, kuna watu wanaamini kuwa kuna mgogoro mkubwa ndani ya CCM kugombea madaraka, nami pia naamini hivyo; Kuna kambi ya Lowassa, Membe, Sitta etc. Hawa watu hawawezi kukubaliana kutokana na faida binafsi na ubinafsi. Chama kimepoteza mvuto kwa raia wa tz hata wanawake ambao ndo walikibeba sana kwenye chaguzi za hivi karibuni, chama kimepoteza mvuto kwa wazee (suala la mafao yao) na wakulima (bei za mazao ya biashara kama pamba etc) ambao pia walikuwa nyuma yake kwa miaka nenda rudi.

Hali hii ya kutokubaliana na ukweli kuwa kivumacho hakidumu, hakuna mwenye hati miliki ya ikulu ya dar es salaam, hakuna mwenye hati miliki ya jimbo lolote TZ au halmshauri yoyote ndo itapelekea CCM kufa na pengine kuacha nchi ktk hali ya mmomonyoko mkali. Tukubali hali ya kutokukubali kuacha madaraka ilianza na ipo ndani ya CCM kwa muda mrefu. fikiria utitili wa majimbo ya uchaguzi hata kama hakuna tija kwa wananchi kwa lengo moja tu la kupatiana sehemu ya madaraka ili kila mwanaCCM mafia apate jimbo. Tumeshuhudia majimbo yakigawanywa bila sababu halisi (real reasons) japo sababu nzuri (good reasons) juu ya jambo hilo hutolewa. ubinafsi na uroho wa madaraka umefanya wilaya kuongezeka hata kama hatuna fedha za kuhudumia wilaya na mikoa hiyo.

Wakati technolojia inapanda na uwezo wa mtu mmoja kuhudumia sehemu kubwa zaidi kwa njia ya teknolojia unakuwa mkubwa, ambapo tulipaswa kupunguza hata wilaya na mikoa yetu, sisi tunaongeza kwa faida ya wachache. kwa hili ndo kodi zinaongezeka hata bila kujali vipato vya watanzania, kwa hili nani alaumiwe??? sio ubinafsi huu???

Ubinafsi huu utaiua CCM na kuiacha nchi ikiwa taabani.

Nawasilisha

Nini unataka kusema? CCM ikae pembeni au unaelezea migogoro ndani ya CCM? mbona hali hiyo ni zaidi ndani ya Vyama vingine? Umeshasikia CCM wakimfukuza Mwanachama? nenda ukatazame migogoro ndani ya CDM, CUF, NCCR-mAGEUZI n.k huko kunafuka moshi, watu wanatafutana kwa ndumba, ukabila na itikadi za kidini, usiwaone wakijificha katika kichaka cha kushambulia Serikali na chama tawala, subiri 2015 utajua uozo ulioko huko.
 
nataka kusema CCM sasa basi, tumetosha tuweke mikono chini tupumzike. Migogoro ndani ya CCM ni hatari sana kwa taifa; kimsingi inatusababisha tunapata viongozi wabovu. Nchi inakwisha kiuchumi na itatugarimu sana tukimaliza raslimali zetu huku hakuna maendeleo; TZ inaanzisha vita wapi ipate mafuta, au madini fulani ikiwa hoji bin taabani??? fikria mbele na mbali mkuu.
 
Yaani Ufisadi, Uongozi mbovu, Rushwa, Kurithishana madaraka, Kuhisiwa inaiba kura, maisha mabaya kwa watanzania yote ni CCM. Mbona zamani tulikuwa tunajua kabisa CCM inashinda jimbo hili na lile, leo unataka kusema hatujui kama CCM inashindwa jimbo hili na lile??? TUNAJUA ndo maana wananchi wanalalamika juu ya mambo kama haya.

Ni busara kama za mwl kuachia ngazi, tukiwaachisha itakuwaje??? mnataka fujo kwenye nchi ya utulivu kama yetu???
 
Nini unataka kusema? CCM ikae pembeni au unaelezea migogoro ndani ya CCM? mbona hali hiyo ni zaidi ndani ya Vyama vingine? Umeshasikia CCM wakimfukuza Mwanachama? nenda ukatazame migogoro ndani ya CDM, CUF, NCCR-mAGEUZI n.k huko kunafuka moshi, watu wanatafutana kwa ndumba, ukabila na itikadi za kidini, usiwaone wakijificha katika kichaka cha kushambulia Serikali na chama tawala, subiri 2015 utajua uozo ulioko huko.
Na tatizo moja wapo la ccm ni kushindwa kuchukuwa maamuzi magamu hata wanachama wake wanapokoseya hawana ubavu wa kuwafukuza.angalia akina chenge ni watuhumiwa wa ufisadi kwenye rada lkn amelindwa.walipotaka kumwondoa lowasa walishindwa baada ya lowasa kuwambia kuwa hayuko tayari kuondoka kwenye chama mpaka atangulie kwanza mwenyekiti kwani hakuna alicho kifanya pasipo kuelekezwa na mwenyekiti.ccm walipoona kumbe na dingi nae anatakiwa kuondoka waliahirisha ile kauli yao ya kujivuwa gamba hivyo kuendelea kuwa chama pekee kinacho endelea kuwalinda wahalifu.
 
Inashindikana kuchukua maamuzi magumu kwa vile wote wanahusika, ndo maana ni vema chema kife harafu wajiunde upya wakati serikali iko mikononi mwa CDM au CUF.
 
Nini unataka kusema? CCM ikae pembeni au unaelezea migogoro ndani ya CCM? mbona hali hiyo ni zaidi ndani ya Vyama vingine? Umeshasikia CCM wakimfukuza Mwanachama? nenda ukatazame migogoro ndani ya CDM, CUF, NCCR-mAGEUZI n.k huko kunafuka moshi, watu wanatafutana kwa ndumba, ukabila na itikadi za kidini, usiwaone wakijificha katika kichaka cha kushambulia Serikali na chama tawala, subiri 2015 utajua uozo ulioko huko.

ccm haiwezi kufukuza wanachama kwa sababu kila mwanachama wale wa juu wote wana nguvu(power) kwenye chama. Si tuliambiwa magamba yatavuliwa? (i.e akina lowasa na wengineo) mpaka sasa bado wapo na wataendelea kuwapo mpaka kufa kwao. hapo penye blue unataka kusema ccm hakufuki moshi? waulize akina mwakyembe walitaka kulishwa sumu, waulize akina mukama,nape,membe kama ccm hawatafutani. Vyama vya upinzani vinaonyesha hakuna mtu mkubwa zaidi ya chama mwanachama akifanya kosa anasimamishwa au kufukuzwa hiyo ndio demokrasia...ccm hawana huo ubavu
 
Udhaifu wa CCM unadhani ni sifa, kama hawafukuzani unataka kusema hakuna watu wanafanya ovyo ndani ya CCM??? haiwezekani wanachama 5milioni wasifanye fyongo, ni uimara na ushujaa wa wapinzani kama wanafukuzana na udhaifu wa CCM kushindwa hata kukamata wezi ambao mwenyekiti wao anawajua, unabisha EPA Je??? rais aliomba warudishe fedha na alipohojiwa akasema baadhi wamerudisha, alipotakiwa kusema ni kina nani KIMYAAAAAAAAAAAAAAAAAAA
 
Back
Top Bottom