Ubinadamu Unahitajika

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Ndugu wana jamii ,napendelea kuuliza na nauliza kama nawauliza wenzangu ambao naamini kabisa sote tumezaliwa na iko siku tutakufa ,kifo hakikimbiliki.
Ninayohitaji ni hii hali inayofanyiwa sehemu moja ya Tanzania kwa hivi sasa nanyo ni Pemba ambayo kila mmoja anaifahamu ipo wapi na kama sikosei haikosi kila mtu amewahi kuwaona au ni rafiki au wameunga udugu na kuchanganya damu.

Mambo ambayo yanapitishwa Pemba kila unapokaribia uchaguzi bila ya shaka wote tunayasikia na wengine yanatugusa kwa karibu kabisa.

Hapa ukumbini tupo aina mbali mbali ya watu ambao kwa upande mmoja inawezekana ni wanachama wa cha kati ya vyama vya upinzani Tanzania.

Sasa tuzungumze kibinadamu tunaionaje hali inayofanywa na Serikali ya au serikali za Chama Tawala ? Katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi mkuu ,tabia ambayo imekuwa inajitokeza kila msimu wa Uchaguzi mkuu unakaribia mpaka kufanyika na hata baada ya kufanyika kuna vitendo huwa vinaendelezwa.

Kwa upande wenu ,labda kwa wale CUF wao msimamo wao unajulikana ,ila kwa Vyama vingine ambavyo kwa sasa vipo upande mmoja wa upinzani na CUF ,naamini wapo wanachama wa vyama hivyo ambao wanaishi huko ,labda watapenda kusikia maoni yenu ,na ilivyokuwa JF wamo viongozi wa juu kabisa wa vyama vya upinzani kwa majina yao na wengize kwa uninja lakini naamini wamo na wanashiriki kikamilifu katika mijadala hapa JF.

Hata kama wapo wanachama wa Chama Tawala ambao nao wanahisia zao kuhusu madhila ambayo yanawanyongesha na kuwatia huzuni wananchi wa Pemba nao pia wasione tabu kwani ujumbe utakaopatikana hapa naamini kabisa unasomwa na watu mbali mbali na mchango wao nao utatazamwa kibinadamu kama michango ya mawazo na fikra za wengine zitakavyothaminiwa na huenda zikavuta hisia za ubinadamu kwa wale wanaopanga mipango isiyokuwa na hulka za kibinadamu.
 
Hivi JF kuna watu ambao wanataka kweli kupata ufumbuzi wa matatizo ya taifa letu au wapo hapa kupinga na kulaumu kila jambo linalo jiri kwenye jamii yetu?

Sidhani kama wapo na kama wapo basi ni wachache mno.
 
huu ni uzandiki na ufisadi wa wazi kabisa
cha msingi ni wananchi wa Pemba wenyewe kuweka msimamo wa wazi pale wanapodhulumiwa, tatizo letu ni kwamba huwa tunatafuta third person wa kutuzungumzia matatizo yetu na kuyatatua
dunia sasa imebadilika, ukiona tatizo linakukabili lizungumzie watu walijue sawa na walizungumzie itasaidia lakini efforts za kulitatua zianze kwa mwathirika mwenyewe ndio hata wale wa nje watakapokuwa na sapoti yenye maana

tuchukue mfano wa Iran hata kama kuna mkono wa Amerika na Ulaya lakini at least wanaonyesha msimamo
 
Mkuu Mwiba,
Tunajuwa fika kwa nini CCM inafanya hila za kuvuruga amani na utulivu visiwani kwa kisingizio cha kulinda uvunjifu wa amani hiyo, inajuulikana kuwa Zanzibar CCM haitakiwi na haina wafuasi hao wa kuiwezesha ibaki madarakani katika uchaguzi huru na haki, hivyo vitisho, kujazwa kwa vikosi vya ulinzi na ujasusi, yote ni kuhakikisha kuwa CCM inabaki madarakani na watu wa visiwani hawatumii haki yao ya kidemokrasi itakayopelekea kushawishi mabadiliko Tanzania nzima, utakumbuka kuwa mwaka 1964 yalitokea Mapinduzi ya serikali halali,iliyochaguliwa na wananchi katika uchaguzi huru na haki kabisa, na mamluki kutoka nje ya Zanzibar wakiongozwa na John Okello wakaipindua na kusabibisha umwagaji mkubwa wa damu visiwani, kumbuka kuwa hali ile ile ilichochea ama kushawishi maasi"mutiny" ya jeshi la Tanganyika, dhidi ya serikali changa ya Nyerere na huyu huyu John Okello alikuwa kama shawishi wa hali ile tete, na ndiyo maana Nyerere aka collaborate na Karume wamfukuze nje ya Afrika ya Mashariki na kweli Okello akawa kitu kilichosahaulika punde tu baadae, kwa hiyo kumbukumbu hizi za mabadiliko ya kisiasa Zanzibar kuweza kushawishi na ya Tanzania bara zinawatisha wakubwa na wanajuwa kuwa once Zanzibar ikiingia mikononi mwa CUF wenzao wa bara hawatakuwa na mawazo mbadala kwa dhana ya "wazanzibari wameweza wana nini na wao (wabara) washindwe wana nini?",kwahiyo kaburi la CCM litakuwa tayari futi sita kwenda chini, wanavyoona kuwa mzizi wa nguvu ya upinzani upo Pemba(haya ni mawazo yao tu) na waanze kuwashughulikia huko huko na Unguja mamluki tu wanatosha, kwa hali ya Pemba nionanyo kuwa waendelee na mapambano ya kuinyima kura CCM na ushawishi ufanywe wa kuziita taasisi za kimataifa na vyombo vya kimataif kuripoti matukio ya uhalifu yanayofanywa na kufadhiliwa na CCM kupitia makundi yao ya kihuni "Janjaweeds", na pili, kutoa tamko rasmi kwa serikali kuwa mara hii dhulma kafara ama wajitayarishe "jino kwa jino" au kupelekwa "The Hague" kujibu mashitaka ya mauwaji na utesaji bila ya sababu.
HAKI SAWA KWA WOTE.
 
Inabidi kazi ianze sasa, si kusubiri wakati wa uchaguzi wa uchaguzi tu. Wao wameshapiga hesabu wakajua kuwa maandalizi ya ushindi yanatakiwa kuanzia hapo, na wengine wanatakliwa kuanza kazi ya kulinda ushindi wao kuanzis hapohapo, wasisubiri hasi siku ya kupiga kura
 
huu ni uzandiki na ufisadi wa wazi kabisa
cha msingi ni wananchi wa Pemba wenyewe kuweka msimamo wa wazi pale wanapodhulumiwa, tatizo letu ni kwamba huwa tunatafuta third person wa kutuzungumzia matatizo yetu na kuyatatua
dunia sasa imebadilika, ukiona tatizo linakukabili lizungumzie watu walijue sawa na walizungumzie itasaidia lakini efforts za kulitatua zianze kwa mwathirika mwenyewe ndio hata wale wa nje watakapokuwa na sapoti yenye maana

tuchukue mfano wa Iran hata kama kuna mkono wa Amerika na Ulaya lakini at least wanaonyesha msimamo
Braza'
Kwani ulikua wapi au ulikua hujazaliwa Jan.26/27 mwaka 2001 wa-Pemba kwa ujumla wana-Cuf walipodai haki yao kwa njia ya amani na wakauliwa kama kuku wengine wakaweka history kwa Tz kua ni wakimbizi wa siasa wa kwanza. Leo hii kwenye Bunge hakuna hata mmoja anaewakumbuka. Imagine ndugu zetu wa ki-Albino wanavyo uliwa kikatili, baadala ya jeshi kupelekwa kuwalinda, linapelekwa Pemba kwenda kufanya tena yale yale ya 2001 na baadae cha Ajabu kua wale waliofanya hivyo wamekua rewarded kupandishwa vyeo. Hi ndiyo Nuksi (kwa msiojua nuksi) Mkosi au doa lililokua haliondoki kwenye nchi yetu na wala sio jambo la kujivunia, na utaona baadhi ya viongozi wa CCM hupanda kwenye majukwaa wakati wa kampeni na ku-refer tokeo hilo kama kua ndio matunda ya chama chao kupatia ushindi. Tutaishi miaka mingapi kwenye dunia hii / Tusisahau twendako kwani hakuna kurudi kuja kurekebisha.
 
Kuiondoa CCM madarakani si kazi ndogo. Hawa jamaa wako kwa lolote, hata mpaka kutumia nguvu ili wabaki madarakani. Kwa hiyo hivi vituko tuvionavyo kuelekea kwa uchaguzi, ndio hivyo hivyo tutaviona wakati wa kupiga kura na hata kutangazwa matokeo. Sijui mwakani Mwafaka utakuja kwa sura gani?. Kwa Zanziba hakuna mjadala kuwa ukiweka uchaguzi huru na wa haki, CCM inaanguka vibaya sana sio Pemba tu, hata Unguja.
 
Back
Top Bottom