Ubaguzi wazidi kuiangamiza CHADEMA

CDM wanaweza kujifunza mambo mengi katika sakata hili na hvyo kurekebisha tofauti zilizopo.
Yote yanawezekana.


Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Mkuu, CDM imeshajifunza sana kutoka CCM, NCCR, na CUF. Mwaka 1995 CDM hawakusimamisha mgombea, mwaka 2000 CDM waliwaunga mkono CUF na Prof Lipumba, hawakusimamisha mgombea Urais na kulikuwa na makubaliano ya kutosimamisha mgombea wa Ubunge pale ambapo chama komojawapo kitaweka mgombea kwa kuzungatia nguvu ya chama mojawapo ktk jimbo husika. Matokeo yake CUF wakaweka wagombea hata pale CDM ilipokuwa na nguvu! Kama hiyo haitoshi, baada ya uchaguzi wa 2010, CUF wakaingia 'collabo' na CCM kule Zanzibar bila kuhusisha wapinzani wengine.

Sasa unataka CDM wawaamini vyama vya aina hiyo?
 
Sikutukani ila kwa asiyekuwa na akili timamu kama zako atafikiri uliyoandika ya namaana maana binadamu yoyote anaruhusiwa kuzungumza hata kama anachozungumza hakina maana sijaona uchunguzi.
sijaelewa ulichotaka kuongelea hivi mtu akitaka sheria ifuatwe hapo anakuwa mbaguzi???hayo yote uliyoyasema mbona hayana mashiko mfano hili la Arusha ninavyofahamu mimi sijasikia kuwa baada ya uchaguzi wanaenda kumngoa meya zaidi nilisikia sasa Arusha itakuwa shwari kwakuwa hakuna moja yakijinga itapitishwa bila kupigia kura kama ilivyo kwenye bunge wanapitisha hoja za kipumbavu alafu wakija kwa wananchi wanajitoa ufahamu mfano hoja ya 1000 kwenye line za simu leo CCM nawao wanaishangaa wakati wakiwa bungeni walipiga kelele ndiooooooooo
 
sasa wewe unategemea hao waliberali cuf wangeweza tena kuwa wapinzani? walishaungana na ccm zanzibar sasa unagemea wawe wapinzani kwenye serikali yao tena?tumieni akili kuandika mambo mengine, chadema waliona mbali sana, cuf walishinda zanzibar ila kwa upumbvu wao wakakubali kuunda serikali ya pamoja na ccm, kwa maana hiyo chadema walikuwa sahihi kuwakatalia, nao tlp na nccr nao ni wale wale hamna kitu mule. mwisho wa siku kitaeleweka tu nyie subirini muone uchaguzi ujao.
 
sasa wewe unategemea hao waliberali cuf wangeweza tena kuwa wapinzani? walishaungana na ccm zanzibar sasa unagemea wawe wapinzani kwenye serikali yao tena?tumieni akili kuandika mambo mengine, chadema waliona mbali sana, cuf walishinda zanzibar ila kwa upumbvu wao wakakubali kuunda serikali ya pamoja na ccm, kwa maana hiyo chadema walikuwa sahihi kuwakatalia, nao tlp na nccr nao ni wale wale hamna kitu mule. mwisho wa siku kitaeleweka tu nyie subirini muone uchaguzi ujao.

UBAGUZI baina ya vyama vya upinzani uliopata nguvu bungeni wakati wa kuanzisha Kambi Rasmi ya Upinzani chini ya CHADEMA, umeanza kutafuna chama hicho chenye ushawishi mkubwa kuliko vyama vingine vya upinzani Tanzania Bara.


Uundwaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, ulitokana na msimamo wa CHADEMA yenye wabunge wengi bungeni, kukataa kushirikisha vyama vingine vya upinzani, ikiwamo CUF ambayo ilikuwa na idadi ya wabunge wanaotosheleza kuunda Kambi ya Upinzani, lakini imezidiwa kiidadi na CHADEMA.

CHADEMA pia ilikataa kushirikiana na NCCR- Mageuzi, TLP, UDP na kuamua kuunda kambi ya wabunge wa CHADEMA pekee, ambapo kwa busara kwa kuwa CUF pia ingeweza kuunda Kambi ya Upinzani, kambi hiyo ya CHADEMA ikapewa jina la Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni.

Athari za ubaguzi huo zilijitokeza Arusha hivi karibuni, ambapo chama hicho kilionekana kutaka kuongoza halmashauri ya jiji hilo, lakini kikashindwa baada ya kukosa kura mbili tu za TLP, na jana imejidhihirisha wakati wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma.

Katika siasa za Arusha, baada ya CHADEMA kutetea viti vyake vinne vya udiwani katika uchaguzi mdogo na uliokuwa muhimu kwa siasa za CHADEMA, ilifikisha viti 15 kwenye Baraza la Madiwani la Arusha, huku CCM ikibakiwa na viti 12 na TLP viti sita.

Pia CHADEMA mbali na kuwa na viti hivyo 15, inayo nafasi ya kuongeza kiti zaidi, kwani kuna nafasi moja ya viti maalumu iliyokuwa ikishikiliwa na Rehema Mohamed, aliyetimuliwa mwaka 2011.

Hata hivyo, pamoja na CHADEMA kuongoza kwa kuwa na viti vingi vya udiwani Arusha, haikuwa na uwezo wa kumweka Meya, kwa kuwa idadi ya madiwani wake ni 16 na kingehitaji zaidi ya kura 17 katika baraza, ili kupata nafasi ya kuongoza halmashauri hiyo.

Hivyo CHADEMA ilihitaji kushirikiana na TLP, ili kupata zaidi ya nusu ya kura inayohitajika kikanuni kumuweka Meya madarakani.

Uvinza Baada ya CHADEMA kusema haina uroho wa madaraka katika umeya wa jiji la Arusha, chama hicho kimejikuta katika mazingira kama ya Arusha, mkoani Kigoma.

Mkoa wa Kigoma, katika halmashauri mpya ya Uvinza, CHADEMA ikishindwa kuishawishi NCCR-Mageuzi kuwaunga mkono, itakuwa katika mazingira ya kukosa nafasi ya kuongoza halmashauri hiyo mpya.


Katika halmashauri hiyo, CCM ina madiwani wanane, CHADEMA madiwani saba na NCCR-Mageuzi inayo madiwani watano na Mbunge mmoja, ambaye anaingia katika Baraza la Madiwani na anaruhusiwa kupiga kura na hivyo chama hicho kuwa madiwani sita.

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA) alinukuliwa akiwataka madiwani wa CHADEMA na NCCR- Mageuzi, kuunganisha nguvu ili CCM iunde Kambi ya Upinzani katika halmashauri hiyo.


“CHADEMA na NCCR-Mageuzi tuna madiwani 13 katika Halmashauri ya Wilaya Uvinza…CCM ina madiwani wanane tu, hivyo tuna kura nyingi upinzani. CHADEMA ina madiwani saba, NCCR-Mageuzi watano na Mbunge mmoja,” alinukuliwa Zitto akishawishi huku akisema wakishindwa kuungana, CCM itapita katikati.

Umoja wavunjika Tofauti na matazamio ya Zitto, kwamba vyama hivyo vingeweka mgombea mmoja dhidi ya mgombea wa CCM, Hamisi Mkwafi, NCCRMageuzi pamoja na kuwa na madiwani sita tu, ilisimamisha mgombea wake, Fidelis Kumbo, na CHADEMA ikaamua kuweka mgombea wake, Cassiano Mabondo.

Katika mazingira yaliyoonesha kuwa vyama hivyo vya upinzani, ikiwemo CHADEMA vilikuwa na uroho wa nafasi ya Mwenyekiti, havikusimamisha mgombea katika nafasi ya Makamu Mwenyekiti, ambayo CCM ilijikuta ikiwa haina mpinzani baada ya kumsimamisha Diwani wa Kalya, Lucas Kanoni.

Awamu ya kwanza ya uchaguzi huo uliokuwa ukisimamiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza, Nicolous Kombe na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, ulishindwa kupata mshindi baada ya kila chama kupata kura saba.

Matokeo hayo yaliamsha mjadala wa muda mrefu na mwishowe walikubaliana uchaguzi huo urudiwe, ambapo matokeo yake yalionesha kuwa wajumbe walipigia kura wagombea wa vyama vyao kwani mgombea wa CCM, aliongoza kwa kupata kura nane na kufuatiwa na mgombea wa CHADEMA aliyepata kura saba na wa NCCR -Mageuzi aliambulia kura sita.

Utata Baada ya matokeo ya uchaguzi wa raundi ya pili, mjadala uliibuka tena kuhusu matakwa ya kikanuni, kwamba mshindi anapaswa kupata zaidi ya nusu ya kura za wajumbe waliopiga kura, ambazo ni 11, jambo ambalo hakuna mgombea hata mmoja aliyefikisha.

Msimamizi wa Uchaguzi, Kombe alilazimika kusitisha mjadala huo kwa muda, ili wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi wapate ufafanuzi wa kisheria, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Baada ya zaidi ya saa moja ya kusubiri, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kigoma, Miriam Mbaga, alisema majibu waliyopata yanaeleza kuwa aliyeshinda kwa kura nyingi, mgombea wa CCM Mkwafi, anapaswa kutangazwa mshindi.

Majibu hayo ya Mkurugenzi yalizua tafrani ambapo baadhi ya madiwani walimtaka Mkurugenzi huyo kufuta kauli hiyo, kwa madai kwamba si kauli rasmi.


Mkurugenzi huyo alilazimika kufuta kauli hiyo, na baadaye Msimamizi wa Uchaguzi, Kombe aliahirisha uchaguzi huo hadi utakapoitishwa upya.

Baada ya kuahirishwa kwa uchaguzi wa Mwenyekiti, wajumbe walikataa kupiga kura kumchagua Makamu Mwenyekiti, ambayo ilikuwa na mgombea mmoja, Kanoni (CCM).

UBAGUZI WAZIDI KUIANGAMIZA CHADEMA - MPEKUZI HURU
 
watu wa kilimanjaro na kaskazini kwa ujumla wamezidi kwa ukabila na ujambazi pia wanaangaliana wao tu.

J4.
Ukisema watu wa Kaskazini wamezidi kwa ukabila unamaanisha sehemu zingine za Tanzania hakuna makabila isipokuwa kaskazin tu??
Ukifikri kama Kaskazini kuna Wachaga tu unakuwa unakosea, Kaskazini kuna Wamasai,Wairaq,Wameru,Wapare,Wachaga,Wasambaa nakadhalika, sasa huo ukabila wa kaskazini upo wapi??
Kama unataarifa za ujambazi wa watu wa kaskazini kwanini usipeleke polisi ili hatua stahiki zichukuliwe juu yao??

TAHADHARI.
Ukiona watu wanajibidisha na kazi usiwachukie, nenda kajifunze kutoka kwao.
 
kunavitu vingi tu viko wazi na tunaviona lakini hatutaki kukubali kuwa viko wazi,nisawa nakujua kasoro yako nakuto ikubali kama ni kasoro..Tunajaribu kurekebisha pasipo hitaji marekebisho..!!nadhani bado wengi hatujui maana ya mabadiliko tunayo hitaji hayo tunayo ita yakifikra,ikwa sisi wenyewe hatuhijaji hayo mabadiliko katika mioyo yetu
 
Je, wewe ukiambiwa ukaungane na fisi utakubali? Rudi shule ukasome uelimike!



UBAGUZI baina ya vyama vya upinzani uliopata nguvu bungeni wakati wa kuanzisha Kambi Rasmi ya Upinzani chini ya CHADEMA, umeanza kutafuna chama hicho chenye ushawishi mkubwa kuliko vyama vingine vya upinzani Tanzania Bara.


Uundwaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, ulitokana na msimamo wa CHADEMA yenye wabunge wengi bungeni, kukataa kushirikisha vyama vingine vya upinzani, ikiwamo CUF ambayo ilikuwa na idadi ya wabunge wanaotosheleza kuunda Kambi ya Upinzani, lakini imezidiwa kiidadi na CHADEMA.

CHADEMA pia ilikataa kushirikiana na NCCR- Mageuzi, TLP, UDP na kuamua kuunda kambi ya wabunge wa CHADEMA pekee, ambapo kwa busara kwa kuwa CUF pia ingeweza kuunda Kambi ya Upinzani, kambi hiyo ya CHADEMA ikapewa jina la Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni.

Athari za ubaguzi huo zilijitokeza Arusha hivi karibuni, ambapo chama hicho kilionekana kutaka kuongoza halmashauri ya jiji hilo, lakini kikashindwa baada ya kukosa kura mbili tu za TLP, na jana imejidhihirisha wakati wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma.

Katika siasa za Arusha, baada ya CHADEMA kutetea viti vyake vinne vya udiwani katika uchaguzi mdogo na uliokuwa muhimu kwa siasa za CHADEMA, ilifikisha viti 15 kwenye Baraza la Madiwani la Arusha, huku CCM ikibakiwa na viti 12 na TLP viti sita.

Pia CHADEMA mbali na kuwa na viti hivyo 15, inayo nafasi ya kuongeza kiti zaidi, kwani kuna nafasi moja ya viti maalumu iliyokuwa ikishikiliwa na Rehema Mohamed, aliyetimuliwa mwaka 2011.

Hata hivyo, pamoja na CHADEMA kuongoza kwa kuwa na viti vingi vya udiwani Arusha, haikuwa na uwezo wa kumweka Meya, kwa kuwa idadi ya madiwani wake ni 16 na kingehitaji zaidi ya kura 17 katika baraza, ili kupata nafasi ya kuongoza halmashauri hiyo.

Hivyo CHADEMA ilihitaji kushirikiana na TLP, ili kupata zaidi ya nusu ya kura inayohitajika kikanuni kumuweka Meya madarakani.

Uvinza Baada ya CHADEMA kusema haina uroho wa madaraka katika umeya wa jiji la Arusha, chama hicho kimejikuta katika mazingira kama ya Arusha, mkoani Kigoma.

Mkoa wa Kigoma, katika halmashauri mpya ya Uvinza, CHADEMA ikishindwa kuishawishi NCCR-Mageuzi kuwaunga mkono, itakuwa katika mazingira ya kukosa nafasi ya kuongoza halmashauri hiyo mpya.


Katika halmashauri hiyo, CCM ina madiwani wanane, CHADEMA madiwani saba na NCCR-Mageuzi inayo madiwani watano na Mbunge mmoja, ambaye anaingia katika Baraza la Madiwani na anaruhusiwa kupiga kura na hivyo chama hicho kuwa madiwani sita.

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA) alinukuliwa akiwataka madiwani wa CHADEMA na NCCR- Mageuzi, kuunganisha nguvu ili CCM iunde Kambi ya Upinzani katika halmashauri hiyo.


“CHADEMA na NCCR-Mageuzi tuna madiwani 13 katika Halmashauri ya Wilaya Uvinza…CCM ina madiwani wanane tu, hivyo tuna kura nyingi upinzani. CHADEMA ina madiwani saba, NCCR-Mageuzi watano na Mbunge mmoja,” alinukuliwa Zitto akishawishi huku akisema wakishindwa kuungana, CCM itapita katikati.

Umoja wavunjika Tofauti na matazamio ya Zitto, kwamba vyama hivyo vingeweka mgombea mmoja dhidi ya mgombea wa CCM, Hamisi Mkwafi, NCCRMageuzi pamoja na kuwa na madiwani sita tu, ilisimamisha mgombea wake, Fidelis Kumbo, na CHADEMA ikaamua kuweka mgombea wake, Cassiano Mabondo.

Katika mazingira yaliyoonesha kuwa vyama hivyo vya upinzani, ikiwemo CHADEMA vilikuwa na uroho wa nafasi ya Mwenyekiti, havikusimamisha mgombea katika nafasi ya Makamu Mwenyekiti, ambayo CCM ilijikuta ikiwa haina mpinzani baada ya kumsimamisha Diwani wa Kalya, Lucas Kanoni.

Awamu ya kwanza ya uchaguzi huo uliokuwa ukisimamiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza, Nicolous Kombe na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, ulishindwa kupata mshindi baada ya kila chama kupata kura saba.

Matokeo hayo yaliamsha mjadala wa muda mrefu na mwishowe walikubaliana uchaguzi huo urudiwe, ambapo matokeo yake yalionesha kuwa wajumbe walipigia kura wagombea wa vyama vyao kwani mgombea wa CCM, aliongoza kwa kupata kura nane na kufuatiwa na mgombea wa CHADEMA aliyepata kura saba na wa NCCR -Mageuzi aliambulia kura sita.

Utata Baada ya matokeo ya uchaguzi wa raundi ya pili, mjadala uliibuka tena kuhusu matakwa ya kikanuni, kwamba mshindi anapaswa kupata zaidi ya nusu ya kura za wajumbe waliopiga kura, ambazo ni 11, jambo ambalo hakuna mgombea hata mmoja aliyefikisha.

Msimamizi wa Uchaguzi, Kombe alilazimika kusitisha mjadala huo kwa muda, ili wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi wapate ufafanuzi wa kisheria, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Baada ya zaidi ya saa moja ya kusubiri, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kigoma, Miriam Mbaga, alisema majibu waliyopata yanaeleza kuwa aliyeshinda kwa kura nyingi, mgombea wa CCM Mkwafi, anapaswa kutangazwa mshindi.

Majibu hayo ya Mkurugenzi yalizua tafrani ambapo baadhi ya madiwani walimtaka Mkurugenzi huyo kufuta kauli hiyo, kwa madai kwamba si kauli rasmi.


Mkurugenzi huyo alilazimika kufuta kauli hiyo, na baadaye Msimamizi wa Uchaguzi, Kombe aliahirisha uchaguzi huo hadi utakapoitishwa upya.

Baada ya kuahirishwa kwa uchaguzi wa Mwenyekiti, wajumbe walikataa kupiga kura kumchagua Makamu Mwenyekiti, ambayo ilikuwa na mgombea mmoja, Kanoni (CCM).

UBAGUZI WAZIDI KUIANGAMIZA CHADEMA - MPEKUZI HURU
 
Haijawahi kuwezekana kuwa na chama au kikundi chenyewe kikawa na sifa ya UDINI na UKABILA kwa pamoja..... inawezekana tu ktk ufikiri wa wanaCCM na washirika wao vinginevyo ni ngumu Mno ... kwa mwanazuoni yeyote hata kuthubutu kufikiria uwezekano wake...!

Unapoita chama fulani ni cha kidini tayari umeisha jumuiasha makabila kadhaa wa kadhaa...! Unapoita chama fulani ni cha kikabila tayari umeisha kivua udini wake manake dini Ina makabila mengi.....lakini CDM kimeitwa ni Chama cha Kidini na Kikabila na ikawezekana kuaminika hivyo.... !

My Take;

Kama CDM kimeweza kuwa na uwezo wakuwa chama cha Kidini na Kikabila basi kina uwezo wa kuwa chochote Tanzania na Duniani!

Nimependa sana akili zako...natamani wangekuwepo watu .10 wenye akili kama zako katika ngazi za juu serikalini
 
Hivi kwa nini watu wanachuki na watu wa Kilimanjaro na Kaskazini??,

Muulize Nasari alisema nini? sasa unataka watu wanaotaka kuigawa hii nchi tuwapende? isitoshe, amani ya Tanzania imetoweka kwa ajili ya hawa watu, sifa zote mbaya wanazo wao. Halafu tuwape nchi?
 
MziziMkavu nakushauri uendelee na thread zako za kishirikina na tiba za kusadikika kule JF DOCTOR, Unalazimisha siasa lakini siasa haikutaki.

Sintoshangaa kesho ndio ukija na thread ya Chadema yashinda kata zote 4 Arusha, kama unaishi North Korea nakushauri hapa JF ubakie tu kuwa msomaji, wengi unatuchukiza kila siku kutupachikia habari za juzi wakati kila mtu anaitegemea JF kama be the fist to know, kama unatumika tafuta namna bora ya kutumika na si style ya condom.
Mkuu.@FaizaFoxy njoo upesi umjibu huyu.cc.@Matola anazungumza kam mtu aliyekunywa maji ya choooni au mlevi mbwa njoo umjibu maneno yake machafu anazungumza maneno ya Pumba huyu Matola.
 
Muulize Nasari alisema nini? sasa unataka watu wanaotaka kuigawa hii nchi tuwapende? isitoshe, amani ya Tanzania imetoweka kwa ajili ya hawa watu, sifa zote mbaya wanazo wao. Halafu tuwape nchi?

FaizaFoxy unakosea sana.
Amani ya nchi inatoweka kwa sababu ya kutotenda haki na udhaifu wa serikali, kama hutoi haki watu wataidai KWA NGUVU.
Serikali itoe haki ya kila mtu bila kumbagua kwa itikadi yake,dini yake,kabila lake au anakotoka alafu serikali iwe madhubuti kukamata mkorofi basi amani ingekuwepo.
Mbona hao watu wa Kaskazini walikuwepo tangia enzi na enzi na pailkuwa na amani?? iweje leo???
Alafu kama unasema CHADEMA mbona ipo nchi nzima siku hizi??? je unamaanisha nini kwa WaCHADEMA wanaotoka maeneo mengine ya Tanzania ??? watu wa Kaskazini amabao ni CCM wao sio wabaguzi??

Usichukie watu kwa ajili ya asili yao usije nawe ukachukiwa kwa ajili ya asili yako
 
Back
Top Bottom