Wapendwa Watanzania, hasa Wataalamu wa sekta ya Ardhi: Town Planners, Surveyors, Land Officers, Valuers, Estate Agents. Mbona tumekaa kimya wakati Ardhi Yetu Tanzania inaumia na kuumizwa?
Ardhi inaumia na watu wake wanaumia. Madaktari (wataalamu tumekaa kimya!) Tuanzishe sasa Hospitali ya Ardhi. Tutibu maradhi na tuwasaidie wagonjwa wa ardhi ambao ni wengi mno. Watu wanapigana, wanakufa kwa shinikizo la damu, wanahamishwa, wanapewa fidia isiyo halali. Viongozi wa serikali wanadanganywa na wanapewa ushauri wa kitaalamu usio sahihi!
Wengine wakikaa kimya sasa nani ataongelea Ardhi Yetu Tanzania.. Tujadiliane na turekebishe hali ilivyo sasa. Kwa kweli hali ni Mbaya Sana. Vikao na Makongamano hayajatoa msaada wa kutosha. Wewe wasemaje? Tuzungumze.
Ardhi inaumia na watu wake wanaumia. Madaktari (wataalamu tumekaa kimya!) Tuanzishe sasa Hospitali ya Ardhi. Tutibu maradhi na tuwasaidie wagonjwa wa ardhi ambao ni wengi mno. Watu wanapigana, wanakufa kwa shinikizo la damu, wanahamishwa, wanapewa fidia isiyo halali. Viongozi wa serikali wanadanganywa na wanapewa ushauri wa kitaalamu usio sahihi!
Wengine wakikaa kimya sasa nani ataongelea Ardhi Yetu Tanzania.. Tujadiliane na turekebishe hali ilivyo sasa. Kwa kweli hali ni Mbaya Sana. Vikao na Makongamano hayajatoa msaada wa kutosha. Wewe wasemaje? Tuzungumze.