Tusiokuwa na mazoea ya kuhesabu pesa benki tunapopewa na mateller wa hizi benki tuwe makini, wamenipiga leo

Witmak255

JF-Expert Member
Feb 5, 2019
3,264
5,403
Sijawahi kuwa na mashaka na huduma za kibenki wakati ninapoenda kutoa pesa, ukiachana na kutoa kwa njia ya ATM ambayo iko limited kwa kiasi Cha pesa unachotoa kwa siku.., ni Mara nyingi natoa pesa dirishani ( kwa mateller), hasa pale kiwango ninachohitaji siwezi kukitoa kwa njia ya ATM.

Leo hawa mateller wameniibia, wameniibia kwa sababu nimefika bank ya CRDB lumumba asubuhi na nikajaza fomu ya kutoa pesa taslimu million 9 ( 9,000,000/=), nikaipeleka wakaiverify sehemu ya huduma kwa wateja ikiambana na kitambulisho changu baadae nikampelekea teller akaendelea na taratibu zake za kunitolea pesa alipomaliza akazitoa nje ya dirisha pamoja na bahasha, nikaziweka ndani ya bahasha then kwenye begi tayari kuondoka.

Kipindi chote hiki nilikuwa mwenyewe, na Wala sikuwa na mashaka ya kuihesabu ile pesa maana Sio Mara ya kwanza kutoa na zinakuwa sawa, nimetoka nje nimefungua gari yangu naingia nikiwa mwenyewe begi lenye pesa nikaliweka siti ya mbele maana sikuwa na mtu, na kwa vile hii pesa tayari nilishaipangia matumizi niliigawanya moja kwa kwa matumizi husika.

Baada ya kuanza kuzitumia kwa matumizi nilikoyaelekeza, na kote huku nilikokuwa natoa hizi pesa nilikuwa nazihesabau ( kuverify Kama kiasi Cha pesa ninachotoa ni sahihi).

Baada ya kutoa mill7 nikajua kabisa nimebakiwa na million2 kwenye bahasha, ikabidi nizihesabu ili nizitoe kwenye bahasha niziweke kwenye pochi, nimetoa rubber band kwenye burungutu la kwanza kuzihesabu ziko million Moja, la pili iko laki nane na nusu, laki na nusu haipo (150,000/=).

Hamna namna zaidi ya Kusema nimeangusha hizi pesa, zingeanguka zote au burungutu moja. Huyu mhudumu kanipiga, na tayari nimeshatoka masaa kama matatu toka nihudumiwe na sikuzihakikisha palepale hata nikimfuata anaweza kuniruka lakini ukweli Hawa jamaa wameanza mchezo mchafu kuweni makini mnaoenda kuchukua pesa dirishani hakikisheni mnazihesabu kabla ya kuondoka.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daaaa mkuu pole sana lkn pia shukrani kwa kutupa tahadhari.
Hawa mateller baadhi yao sio waaminifu sana hasa unapotoa kiasi kikubwa cha pesa wanajua huwezi hakikisha maana ni mzigo mkubwa.
Lkn kwa kifupi tuwe makini sana.
Mimi mwenyewe nilitoa hela kwenye atm crdb haohao na ninafahamu salio lililobaki lkn narudi siku ya pili 170k haipo.
Nawauliza wananiambia nilitoa mwenyewe na ile bank statement wamenipa.
Kuna wizi wa kitaalam pia tunafanyiwa.
Sasa nikutoa pesa zote mshahara ukiingia na kuweka ndani hayo ndio maamuzi yangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daaaa mkuu pole sana lkn pia shukrani kwa kutupa tahadhari.
Hawa mateller baadhi yao sio waaminifu sana hasa unapotoa kiasi kikubwa cha pesa wanajua huwezi hakikisha maana ni mzigo mkubwa.
Lkn kwa kifupi tuwe makini sana.
Mimi mwenyewe nilitoa hela kwenye atm crdb haohao na ninafahamu salio lililobaki lkn narudi siku ya pili 170k haipo.
Nawauliza wananiambia nilitoa mwenyewe na ile bank statement wamenipa.
Kuna wizi wa kitaalam pia tunafanyiwa.
Sasa nikutoa pesa zote mshahara ukiingia na kuweka ndani hayo ndio maamuzi yangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kumbe ni kawaida hii mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daaaa mkuu pole sana lkn pia shukrani kwa kutupa tahadhari.
Hawa mateller baadhi yao sio waaminifu sana hasa unapotoa kiasi kikubwa cha pesa wanajua huwezi hakikisha maana ni mzigo mkubwa.
Lkn kwa kifupi tuwe makini sana.
Mimi mwenyewe nilitoa hela kwenye atm crdb haohao na ninafahamu salio lililobaki lkn narudi siku ya pili 170k haipo.
Nawauliza wananiambia nilitoa mwenyewe na ile bank statement wamenipa.
Kuna wizi wa kitaalam pia tunafanyiwa.
Sasa nikutoa pesa zote mshahara ukiingia na kuweka ndani hayo ndio maamuzi yangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Na haya ndio maamuzi bora kabisaaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijawahi kuwa na mashaka na huduma za kibenki wakati ninapoenda kutoa pesa, ukiachana na kutoa kwa njia ya ATM ambayo iko limited kwa kiasi Cha pesa unachotoa kwa siku.., ni Mara nyingi natoa pesa dirishani ( kwa mateller), hasa pale kiwango ninachohitaji siwezi kukitoa kwa njia ya ATM.

Leo hawa mateller wameniibia, wameniibia kwa sababu nimefika bank ya CRDB lumumba asubuhi na nikajaza fomu ya kutoa pesa taslimu million 9 ( 9,000,000/=), nikaipeleka wakaiverify sehemu ya huduma kwa wateja ikiambana na kitambulisho changu baadae nikampelekea teller akaendelea na taratibu zake za kunitolea pesa alipomaliza akazitoa nje ya dirisha pamoja na bahasha, nikaziweka ndani ya bahasha then kwenye begi tayari kuondoka.

Kipindi chote hiki nilikuwa mwenyewe, na Wala sikuwa na mashaka ya kuihesabu ile pesa maana Sio Mara ya kwanza kutoa na zinakuwa sawa, nimetoka nje nimefungua gari yangu naingia nikiwa mwenyewe begi lenye pesa nikaliweka siti ya mbele maana sikuwa na mtu, na kwa vile hii pesa tayari nilishaipangia matumizi niliigawanya moja kwa kwa matumizi husika.

Baada ya kuanza kuzitumia kwa matumizi nilikoyaelekeza, na kote huku nilikokuwa natoa hizi pesa nilikuwa nazihesabau ( kuverify Kama kiasi Cha pesa ninachotoa ni sahihi).

Baada ya kutoa mill7 nikajua kabisa nimebakiwa na million2 kwenye bahasha, ikabidi nizihesabu ili nizitoe kwenye bahasha niziweke kwenye pochi, nimetoa rubber band kwenye burungutu la kwanza kuzihesabu ziko million Moja, la pili iko laki nane na nusu, laki na nusu haipo (150,000/=).

Hamna namna zaidi ya Kusema nimeangusha hizi pesa, zingeanguka zote au burungutu moja. Huyu mhudumu kanipiga, na tayari nimeshatoka masaa kama matatu toka nihudumiwe na sikuzihakikisha palepale hata nikimfuata anaweza kuniruka lakini ukweli Hawa jamaa wameanza mchezo mchafu kuweni makini mnaoenda kuchukua pesa dirishani hakikisheni mnazihesabu kabla ya kuondoka.



Sent using Jamii Forums mobile app
Daah, kiutaratibu wa benki ya CRDB ni kwamba kila burungutu ilipaswa alifungue na kulipitisha kwenye mashine na mashine aigeuze uone inavyohesabu, tena china ya uangalizi wa CCTV camera, je, hakuzipisha kwenye mashine huku ukiona?
 
Hahaha aisee mimi niko radhi nionekane mshamba lakini lazima nihakikishe hata kwa kukaa chini kabisaa,.maana kuna watu wanajidai mashine hazikosei wakati hizo mashine zimeundwa na binadam ambaye nayeye anakosea vilevile,.sembuse mashine,.lol

Kuna mwaka nilienda W.U posta kuchukua pesa flan hazikuwa millions nyingi lakini baada ya kupewa nikamuomba yule mrembo wa dirishani nikae nizihesabu tena hahaha ilibidi acheke kidogo,.nilivyohesabu ikawa imepungua kama sh.450 hivi hahaha ilibidi nisepe tuu nikajiambia dola itakuwa ilikosa chenji😅na wala sikumuuliza yule mdada,.niliwaaga tuu kwa tabasam😊
 
Daah, kiutaratibu wa benki ya CRDB ni kwamba kila burungutu ilipaswa alifungue na kulipitisha kwenye mashine na mashine aigeuze uone inavyohesabu, tena china ya uangalizi wa CCTV camera, je, hakuzipisha kwenye mashine huku ukiona?
Mkuu pamoja na kwamba naendaga kutoa huduma pale Mara kwa Mara but huu utaratibu sikuwahi kuufahamu
 
Back
Top Bottom