Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Serikali ya Kikwete inaonyesha kila dalili za kuibaka demokrasia kwa kutumia nguvu ya dola. Ninayaona haya kutokana na matukio ya hivi karibuni.
Nawashauri pia kuwa tuzilinde kura zetu kwa njia ya kistaarabu ili kuwanyima fursa ya kuweka amri za kijeshi, hivyo kufanikisha zoezi la kuwatoa madarakani bila kumwaga tone la damu.
Aluta Kontinua
- Tamko la jeshi la wananchi (JWTZ) - hii ilikuwa na lengo la kuwachonganisha wapinzani kwa wapiga kura wasiokuwa na uelewa wa kutosha hasa wa vijijini kuwa ni wagomvi na wakipewa nchi wataitumbukiza katika migogoro kama walivyo majirani wetu.
- Tafiti zisizokuwa na kichwa wala mkia - Matokeo ya utafiti yaliyotangazwa na REDET jana yana lengo la kuwakatisha tamaa wale wote wanaunga mkono upinzani kuwa wananchi wengi wa Tanzania bado wana imani na Kikwete na hivyo wao ni wachache sana hivyo kura zao hazitabadili matokeo ya mwisho ili wasipige kura, ama kura zikiibiwa wasishituke sana wajue kuwa waliowengi wanaunga mkono serikali kitu ambacho siyo kweli.
- Taarifa za jeshi kuwa kuna dalili za kutokea machafuko zinaweza kutumika pia kuhalalisha kuwekwa amri ya jeshi kuwakataza watu kukaa jirani na vituo vya kupigia kura, hii itarahisisha wizi wa kura kwa kubadilisha karatasi za kupigia kura na kuwekwa zile wanazozitaka.
Nawashauri pia kuwa tuzilinde kura zetu kwa njia ya kistaarabu ili kuwanyima fursa ya kuweka amri za kijeshi, hivyo kufanikisha zoezi la kuwatoa madarakani bila kumwaga tone la damu.
Aluta Kontinua