Elections 2010 Tupigeni kura, wakichukua uongozi kwa nguvu ya dola hatutajuta

Ntemi Kazwile

JF-Expert Member
May 14, 2010
2,182
307
Serikali ya Kikwete inaonyesha kila dalili za kuibaka demokrasia kwa kutumia nguvu ya dola. Ninayaona haya kutokana na matukio ya hivi karibuni.
  • Tamko la jeshi la wananchi (JWTZ) - hii ilikuwa na lengo la kuwachonganisha wapinzani kwa wapiga kura wasiokuwa na uelewa wa kutosha hasa wa vijijini kuwa ni wagomvi na wakipewa nchi wataitumbukiza katika migogoro kama walivyo majirani wetu.
  • Tafiti zisizokuwa na kichwa wala mkia - Matokeo ya utafiti yaliyotangazwa na REDET jana yana lengo la kuwakatisha tamaa wale wote wanaunga mkono upinzani kuwa wananchi wengi wa Tanzania bado wana imani na Kikwete na hivyo wao ni wachache sana hivyo kura zao hazitabadili matokeo ya mwisho ili wasipige kura, ama kura zikiibiwa wasishituke sana wajue kuwa waliowengi wanaunga mkono serikali kitu ambacho siyo kweli.
  • Taarifa za jeshi kuwa kuna dalili za kutokea machafuko zinaweza kutumika pia kuhalalisha kuwekwa amri ya jeshi kuwakataza watu kukaa jirani na vituo vya kupigia kura, hii itarahisisha wizi wa kura kwa kubadilisha karatasi za kupigia kura na kuwekwa zile wanazozitaka.
Hata hivyo nawashauri wapiga kura wenzangu kuwa tupige kura kwa wengi wetu na tuwapelekee salamu kuwa hatuwataki, hata wakiiba nafsi zao zitawasuta kama ambavyo zimewasuta Zanzibar na kuanzisha serikali ya umoja wa kitaifa.

Nawashauri pia kuwa tuzilinde kura zetu kwa njia ya kistaarabu ili kuwanyima fursa ya kuweka amri za kijeshi, hivyo kufanikisha zoezi la kuwatoa madarakani bila kumwaga tone la damu.

Aluta Kontinua
 
CCM hawawezi kushinda uchaguzi kwa njia yoyote ile. Hii ni taarifa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Soma PSALMS 15:21 These things you have done, I kept silent, you thought I was altogether like you, I will rebuke you and set them in order before your eyes."

Soma DEUTORONOMY 32:35 Vengeance is Mine, and recompense, their foot will slip in due time, for the day of their calamity is at hand and the things to come hasten upon them


Soma hizo karama takatifu na kuzirudia siku ya uchaguzi halafu tuone CCM inatokea wapi mbele ya Mwenyezi Mungu.
 
CCM hawawezi kushinda uchaguzi kwa njia yoyote ile. Hii ni taarifa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.






Soma hizo karama takatifu na kuzirudia siku ya uchaguzi halafu tuone CCM inatokea wapi mbele ya Mwenyezi Mungu.

Mkuu mbona Plsalms inamistari 5 pekee, naomba uangalia na uundike upya mkuu
 
Serikali ya Kikwete inaonyesha kila dalili za kuibaka demokrasia kwa kutumia nguvu ya dola. Ninayaona haya kutokana na matukio ya hivi karibuni.

  • Tamko la jeshi la wananchi (JWTZ) - hii ilikuwa na lengo la kuwachonganisha wapinzani kwa wapiga kura wasiokuwa na uelewa wa kutosha hasa wa vijijini kuwa ni wagomvi na wakipewa nchi wataitumbukiza katika migogoro kama walivyo majirani wetu.
  • Tafiti zisizokuwa na kichwa wala mkia - Matokeo ya utafiti yaliyotangazwa na REDET jana yana lengo la kuwakatisha tamaa wale wote wanaunga mkono upinzani kuwa wananchi wengi wa Tanzania bado wana imani na Kikwete na hivyo wao ni wachache sana hivyo kura zao hazitabadili matokeo ya mwisho ili wasipige kura, ama kura zikiibiwa wasishituke sana wajue kuwa waliowengi wanaunga mkono serikali kitu ambacho siyo kweli.
  • Taarifa za jeshi kuwa kuna dalili za kutokea machafuko zinaweza kutumika pia kuhalalisha kuwekwa amri ya jeshi kuwakataza watu kukaa jirani na vituo vya kupigia kura, hii itarahisisha wizi wa kura kwa kubadilisha karatasi za kupigia kura na kuwekwa zile wanazozitaka.
Hata hivyo nawashauri wapiga kura wenzangu kuwa tupige kura kwa wengi wetu na tuwapelekee salamu kuwa hatuwataki, hata wakiiba nafsi zao zitawasuta kama ambavyo zimewasuta Zanzibar na kuanzisha serikali ya umoja wa kitaifa.

Nawashauri pia kuwa tuzilinde kura zetu kwa njia ya kistaarabu ili kuwanyima fursa ya kuweka amri za kijeshi, hivyo kufanikisha zoezi la kuwatoa madarakani bila kumwaga tone la damu.

Aluta Kontinua

I wish kila mmoja angekuwa na moyo kama huu
 
Back
Top Bottom