Tungekuwa wapi leo bila Rais Samia?

Kwakweli bila Rais Samia sijui ata tungekuwa wapi maana duuuh,
Acha Ulevi kipi kizuri alichofanya
Amewapa matumaini
MAFISADI
Amewapa matumaini
MABEBERU
Amewapa matumaini
matapeli wa ccm
Amewapa matumaini wanamtandao

Amewaacha wanyonge wateseke na kuongeza bei za umeme
Amewavunjia mitaji wamachinga wako hoi taabani
Sasa nafuu yake iko wapi sijaiona mie
 
Huelewi maana ya mifano utanipotezea muda tu.
Hata Nigeria kwenye taarifa ya habari ya leo kuna issue ya inflation. Briefly nilitaka nikuambie inflation siyo kigezo cha ubora wa Kiongozi ndiyo maana hata Nchi zilizoendelea zina suffer
wengi humu ni watoto wa Primary wanafungua keshokutwa
hawajawahi kuvaa sandarusi na makatambuga
hawajawahi kupanga foleni ya sukari mgao kilo 1 Duka la kaya mpaka unaweka jiwe kwenye foleni.
leo Mama kaupiga mwingi hawaoni tofauti
awamu iliyopita kila kiongozi haachi Document au Briefcase ni kutumbuliwa au kupotezwa
 
Mkuu acha Viroba kurudi na sio Rombo tu
Bar zote ni 24hrs na Pool table ruksa
Mwendazake na Kolomije walifunga kila kitu eti watu wafanye usafi
mm nina shift za usiku mchana nipo free nikapumzike wapi?
sasa ndio Tanzania niijuayo
Kuhusu kufanya biashara mda wote naunga mkono,ule ulikuwa ujinga,hata siku ya usafi acha watu wafanye biashara na ukaguzi ufanyike atakayebainika hajasafisha mazingira hatua zichukuliwe ila sio kufunga biashara kwa masaa zaidi ya 5..

Mwisho kama kuna vitu vilizuiliwa kwa sababu vinaleta madhara kama viroba sio sawa kuruhusu inamaana hata madawa ya kulevya yatatuhusiwa sasa hii haijakaa sawa kabisa.
 
Kitu cha kwanza kinachonipa furaha katika utawala huu na ambacho kutoweka kwake kulinipa tabu sana na kupelekea kuichukia sana awamu iliyopita, japo najua watanzania sisi ni wasahaulifu na tayari wengi wameshasahau, ni FREEDOM OF SPEECH na ukatili wa wasiojulikana ambao ulitumika kuondoa kabisa hiyo. freedom.

Nafahamu mama ni binadamu na ana makosa yake mengi tu, ila kwa hili, jinsi ninavyoona na kusikia watanzania wengi wakijiachia kwa uhuru kabisa kuukosoa na kuutusi utawala wa awamu hii bila hofu, nasamehe hayo makosa mengine yote. Namuombea asije kubadilika kabisa.

Katika awamu iliyopita ilikuwa ni kuchunga kila kauli, tulielekea mahala hata ukitaka kukohoa unaangalia pande zote kama hufuatiliwi! Ilikuwa ni unakihofia hata kivuli chako, hukiamini! Watu tulichukua kadi za ccm bila kupenda! Yaani nikisikia mtu anasifia ile awamu na kuiponda hii huwa nasikitika sana!

Sikupenda kifo cha Magu, ila utawala wake niliuondoa kabisa kichwani mwangu na nikaacha kuuombea (kama alivyotuomba) tangu 7/9/2017.
Ndugai alitumia uhuru wake kwa kutoa maoni waziwazi, nini kilimkuta? Usiegemee upande mmoja tu wa shilingi mkuu.
 
Sema kama sio Mungu Kwa sababu Mwenyezi Mungu ndio kamtoa Samia kama zawadi Kwa watanzania..

Samia mbele kwa mbele
Hakuna kitu kama hiki, unajipendekeza tu ndugu. Wewe toa maoni yako, ni wapi parekebishwe ili maisha ya watanzania yawe bora
 
Mkuu Mwananchi Huru usijali.. kama siyo SSH angetokea mwingine ambaye angefanya maajabu zaidi yake tu..
Jina la Kiongozi lisikupe taabu.. kuna ambaye angefanya maajabu usinge amini basi tu hakupata nafasi..
 
Mkuu Mwananchi Huru usijali.. kama siyo SSH angetokea mwingine ambaye angefanya maajabu zaidi yake tu..
Jina la Kiongozi lisikupe taabu.. kuna ambaye angefanya maajabu usinge amini basi tu hakupata nafasi..
Naomba nikujibu Mimi hivi,

"Ndio maana kibali kikawa kwa Samia coz Mungu anawajua wote ila akampenda zaidi Mama Samia, Tumuunge mkono"
 
Toka ndani ya mioyo yetu tutafakari haya kwa pamoja huku tukimshirikisha Mungu wetu:

1. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu,Je watu wasiojulikana wangekuwa wamepoteza wenzetu wengine wangapi mpaka leo,Wewe unayempinga Rais Samia leo Je umewahi kujiuliza kama ungekuwa hai mpaka leo kama sio huyu Rais Samia unayempinga na kumbeza kila leo?

2. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu tungefanyaje kumaliza upungufu wa madarasa wa miaka mingi yanayofikia elfu 15 sawa na wastani wa madarasa matatu katika kila Shule ya Sekondari ya Serikali nchi nzima na mengine zaidi ya elfu 3 kwa shule za msingi Shikizi najua mnajua kabla tulisema Tanzania hatuna maambukizi ya Covid 19 hivyo tusingeweza kupata mkopo ule usio na riba,

3. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nilini tungekusanya kodi inayofikia Shilingi trilioni 2.51 kwa mwezi mmoja tena bila kunyanyasa wala kukimbiza walipakodi wetu,Kwani simnakumbuka Mzee Jakaya yeye alikusanya wastani wa trilioni 10 kwa mwaka mzima pesa tunayoweza kuikusanya kwa miezi minne tu sasa!!

4. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angeweza kuongeza mzunguko wa fedha kwenye nchi ( M3 ) kwa mara mbili zaidi kutoka asilimia 6.5 hadi asilimia 12.7 tena kwa miezi tisa tu,

5. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angeufikisha Uchumi wetu kwenye ukuaji wa Pato la Taifa wa asilimia 5.4 kutoka mdororo wa asilimia 2.1 wakati wa mtangulizi wake,

6. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu ni lini tungeifikia sera yetu ya 50/50 kwenye nyadhifa mbalimbali za Kivyama, kiserikali na taasisi nyingine mbalimbali kwani kupitia yeye Tanzania na dunia vimejifunza kuwa ni kweli kuwa " A Woman Can Lead anywhere at any Post "

7. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angeinusuru miradi hii mikubwa ya kimkakati ya SGR na SG iliyokuwa ikijengwa kwa mikopo ya masharti ya kibiashara,Je umewahi kuwaza nini ingekuwa hatma ya Tanzania na Watoto wa Watanzani kwa madeni haya hatari ya kibiashara?

8. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angewaachilia huru Mashekhe wetu wa uamsho waliosota gerezani kwa miaka zaidi ya 10 bila kosa au Nani angewaachia Wana-CHADEMA waliokuwa wametapakaa karibu kila gereza hapa Tanzania?

9. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angeifungua Tanzania kimataifa baada ya kuchafuliwa vibaya na kwa muda mrefu na akina Tundu Lissu na wenzake kiasi cha kunyimwa misaada na mikopo ya masharti|riba nafuu kulikotulazimu kama Taifa kuanza kuiingiza nchi yetu kwenye mikopo ya kibiashara wakati nchi haifanyi biashara ila inatoa huduma tu hili lilikuwa ni bomu kwa nchi,

10. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angewaongezea mishahara na madaraja makubwa makubwa watumishi wetu wa Serikali waliosota miaka mitano mfululizo bila kuona senti ya Serikali?

11. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angewaondolea Wasomi wetu VRF ya asilimia 6 toka makato ya asilimia 15 toka HESLB kwani leo wanakatwa asilimia 9 tu tena mpaka upate kazi ndio uanze kukatwa,

12. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angekivusha Chama Changu cha Mapinduzi Salama mwaka wa Uchaguzi 2024|25 ikiwa ni baada ya Rais Samia kurudisha Ushawishi wa Chama kwa jamii|Umma kutokana na matendo mema na mazuri ya Chama Chake na Serikali yake,

#Kama Sio katazo la Katiba kwa kudra za mwenyezi Mungu huyu Mama alitakiwa apewe miaka 20 ila katiba iheshimiwe twende na Mama mpaka 2030 itatufaa sana,Wewe unasemaje?

Kwakweli bila Samia sijui ata tungekuwa wapi leo Watanzania, Kila nikiwaza naona giza, Mungu amlinde Mama huyu
 
wengi humu ni watoto wa Primary wanafungua keshokutwa
hawajawahi kuvaa sandarusi na makatambuga
hawajawahi kupanga foleni ya sukari mgao kilo 1 Duka la kaya mpaka unaweka jiwe kwenye foleni.
leo Mama kaupiga mwingi hawaoni tofauti
awamu iliyopita kila kiongozi haachi Document au Briefcase ni kutumbuliwa au kupotezwa
Ni kweli maamuzi anayoyafanya Rais kisera kwa sasa, matunda yake tutayaona miaka 3-4 ijayo.

Ila wajinga wanataka waone leo
 
Back
Top Bottom