Tate Mkuu
JF-Expert Member
- Jan 24, 2019
- 28,958
- 83,868
Kama siyo Rais Samia Suluhu Hassan kulijaza tumbo lako kiasi cha kukaribia kuvimbiwa! Ungepata wapi nguvu na ujasiri wa kuleta uzi uliojaaa kila aina ya unafiki na kujipendekeza kama huu?Toka ndani ya mioyo yetu tutafakari haya kwa pamoja huku tukimshirikisha Mungu wetu:
1. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu,Je watu wasiojulikana wangekuwa wamepoteza wenzetu wengine wangapi mpaka leo,Wewe unayempinga Rais Samia leo Je umewahi kujiuliza kama ungekuwa hai mpaka leo kama sio huyu Rais Samia unayempinga na kumbeza kila leo?
2. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu tungefanyaje kumaliza upungufu wa madarasa wa miaka mingi yanayofikia elfu 15 sawa na wastani wa madarasa matatu katika kila Shule ya Sekondari ya Serikali nchi nzima na mengine zaidi ya elfu 3 kwa shule za msingi Shikizi najua mnajua kabla tulisema Tanzania hatuna maambukizi ya Covid 19 hivyo tusingeweza kupata mkopo ule usio na riba,
3. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nilini tungekusanya kodi inayofikia Shilingi trilioni 2.51 kwa mwezi mmoja tena bila kunyanyasa wala kukimbiza walipakodi wetu,Kwani simnakumbuka Mzee Jakaya yeye alikusanya wastani wa trilioni 10 kwa mwaka mzima pesa tunayoweza kuikusanya kwa miezi minne tu sasa!!
4. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angeweza kuongeza mzunguko wa fedha kwenye nchi ( M3 ) kwa mara mbili zaidi kutoka asilimia 6.5 hadi asilimia 12.7 tena kwa miezi tisa tu,
5. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angeufikisha Uchumi wetu kwenye ukuaji wa Pato la Taifa wa asilimia 5.4 kutoka mdororo wa asilimia 2.1 wakati wa mtangulizi wake,
6. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu ni lini tungeifikia sera yetu ya 50/50 kwenye nyadhifa mbalimbali za Kivyama, kiserikali na taasisi nyingine mbalimbali kwani kupitia yeye Tanzania na dunia vimejifunza kuwa ni kweli kuwa " A Woman Can Lead anywhere at any Post "
7. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angeinusuru miradi hii mikubwa ya kimkakati ya SGR na SG iliyokuwa ikijengwa kwa mikopo ya masharti ya kibiashara,Je umewahi kuwaza nini ingekuwa hatma ya Tanzania na Watoto wa Watanzani kwa madeni haya hatari ya kibiashara?
8. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angewaachilia huru Mashekhe wetu wa uamsho waliosota gerezani kwa miaka zaidi ya 10 bila kosa au Nani angewaachia Wana-CHADEMA waliokuwa wametapakaa karibu kila gereza hapa Tanzania?
9. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angeifungua Tanzania kimataifa baada ya kuchafuliwa vibaya na kwa muda mrefu na akina Tundu Lissu na wenzake kiasi cha kunyimwa misaada na mikopo ya masharti|riba nafuu kulikotulazimu kama Taifa kuanza kuiingiza nchi yetu kwenye mikopo ya kibiashara wakati nchi haifanyi biashara ila inatoa huduma tu hili lilikuwa ni bomu kwa nchi,
10. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angewaongezea mishahara na madaraja makubwa makubwa watumishi wetu wa Serikali waliosota miaka mitano mfululizo bila kuona senti ya Serikali?
11. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angewaondolea Wasomi wetu VRF ya asilimia 6 toka makato ya asilimia 15 toka HESLB kwani leo wanakatwa asilimia 9 tu tena mpaka upate kazi ndio uanze kukatwa,
12. Kama sio Rais Samia Suluhu Hassan kupewa kibali na Mungu nani angekivusha Chama Changu cha Mapinduzi Salama mwaka wa Uchaguzi 2024|25 ikiwa ni baada ya Rais Samia kurudisha Ushawishi wa Chama kwa jamii|Umma kutokana na matendo mema na mazuri ya Chama Chake na Serikali yake,
#Kama Sio katazo la Katiba kwa kudra za mwenyezi Mungu huyu Mama alitakiwa apewe miaka 20 ila katiba iheshimiwe twende na Mama mpaka 2030 itatufaa sana,Wewe unasemaje?