Tundu Lissu kuitwa kwenye Kamati ya maadili ya madiwani Singida

Kimsingi, ili wananchi waendelee kuchangia ni lazima pawepo na taarifa za mapato na matumizi yote ya fedha. Wengi wamezoea kuburuza wananchi na kuwalazimisha kulipa kodi. Kama hao madiwani wana ubavu basi walazimishe wananchi kuchangia kama wanavyotaka kulazimisha Mbunge wa wananchi akajieleze kwao. Ni aibu wawakilishi wa watu kushirikiana na chombo (serikali) kukandamiza wananchi badala ya kupanga mipango ya maendeleo pamoja. Ni wajibu wa halmashauri kuweka wazi taarifa zote kwa uwazi ndipo wananchi wachange. Vitisho kwa mbunge halali wa wananchi sio suluhisho la matatizo ya wananchi bali uwajibikaji na utiii wa sheria zilizopo.
 
wananchi hao hawalipi kodi, yaani kuitwa na madiwani wa ccm wasiojua sheria kama lisu ndio unaona kuna jambo singida, kumbuka singida kwa lisu halmashauri inaongozwa na ccm haya yanategemewa huoni kama ni magamba tu haya. Yaani maendeleo yaletwe kwa michango huoni kama haelewani na ccm na si wananchi? Unapocukua take try to be more critical ndio maana hoja hii inaonekana hovyo
Yes Lisu endelea kuwabana. Waeleze matumizi ya kodi za wananchi kabla ya kudai michango. Ng'ombe akiishiwa maziwa hutoa damu na kufa.
 
Maggid , sasa usichoelewa ni nini UNATUBOA na "tafasiri zangu" daily, huna JIPYA jipange
 
Kwanini Wananchi walazimishwe michango? Hapo kinachoonekana wananchi wamechangia tangia uhuru mpaka leo visima hamna sasa iweje miaka 50 hamna visima? Sioni haja kuchangia hizo pesa ni upuuzi mtupu walizochanga tangia uhuru kala nani?
 
Ndugu Mjengwa umekiri yafuatayo :
  • Hakuna sheria inayosema wananchi wachangie shughuli za maendeleo
  • Wananchi waendelee kuchangia hata kama hawajui michango yao inatumika vipi
Kwa mujibu wa ripoti ya CAG, halmashauri ya Singida imekuwa ikirudisha Hazina mabilioni ya fedha zilizokuwa zitumike kwa maendeleo na wakati huo huo wanataka fedha za wananchi. Mim namsifu T. Lissu maana Singida ni moja ya mikoa masikini zaidi Tz, huwezi kuchukua pesa ya mwananchi maskini ukaitumia hovyo wakati ya serikali inarudishwa hazina. Hapa ni ujanja maana wanajua fedha za serikali zinakaguliwa wakati za michango ya wananchi hazikaguliwi. Kama kawaida yako kwa chadema, hii ni tafsiri ya unafiki.
 
Maggid ni CCM gamba gumu .Yeye ni mmoja wa wale walio kuwa na sasa bado wanalamba viatu vya Kikwete .Maggid ni opportunist .Kwanza ana bogu yake kwa nini anatusumbua huyu na uharo wake huu .Uko Sweden huna ujualo ukija TZ unakula kuku na kuendekeza unafiki wako kaka .Yana mwisho haya wewe na CCM yako .Mawazo yako yaache kwenye blogu yako au weke kwenye mitandao ya CCM wenzako mawazo yako mgando haya .
 
Maggid unaujua umasikini wa watt wa Singida? Kuna watu shs 1000 kwao ni mbinde. Lissu alihoji suala la fedha zinazotolewa kwenye budget ya maendeleo ya serikali kuu kwa halmashauri kwa nini zinarudishwa hazina bila ya kufanya yaliyokusudiwa kisha halmashauri hizohizo zinawakamua kwa nguvu maskini miaka nendarudi kwa miradi ileile ambayo fedha zake zimerudishwa hazina? Lissu ana hoja ya msingi.
 
Watoto waliokulia kota shda sana!iyo n tafsiri yako,na Tundu nae ana tafsil yake tena ya kisheria...afu Majid we uwa mnafiki sana!kama miaka miwil ilyopta nikiwa Ughaibuni niliwah kuona umepga picha ktk blog yako..toka Mtera mpka Singda...umaskin,shda na maisha ya watu wa Sngda mjn..ulieleza sana!sasa pale n mjini!je uko bush-country kwa kina Tundu hal ikoje afu watu bado wanachangshwa?Vp hujaskia Pan African Energy wana "TAX HEAVEN" ilyofka 100blion?vp Muuza mkaa kuchangshwa?Tafakari
 
Hiyo ni njema sana pia nawe nikupongeze lakini pia nikukosoe kuwa sio "ujanja" ni "wizi" maana neno ujanja siku hizi linapotoshwa hadi kwa wezi na waujumu uchumi wanaitwa wajanja.
 
Maggid na hii aliyosema Ole Sendeka nayo ni tafsiri yako? "Wajadiliane na wafikie muafaka" Ukasema " Na muafaka hauwezi kuwa wananchi wasichangie michango ya maendeleo yao......"
Mbona unalazimisha huo muafaka? ikiwa watakubaliana wasichangie sio muafaka huo? Hiyo ni tafsiri potofu ya kulazimisha muafaka uweje.
 
Watoto waliokulia kota shda sana!iyo n tafsiri yako,na Tundu nae ana tafsil yake tena ya kisheria...afu Majid we uwa mnafiki sana!kama miaka miwil ilyopta nikiwa Ughaibuni niliwah kuona umepga picha ktk blog yako..toka Mtera mpka Singda...umaskin,shda na maisha ya watu wa Sngda mjn..ulieleza sana!sasa pale n mjini!je uko bush-country kwa kina Tundu hal ikoje afu watu bado wanachangshwa?Vp hujaskia Pan African Energy wana "TAX HEAVEN" ilyofka 100blion?vp Muuza mkaa kuchangshwa?Tafakari

Maggid ni mnafiki tu kapu la mjanja leo anajifanya kusema nini .Anaitetea CCM na JK kama alivyo fanya wakati wa kampeni wote now hasemi hata shida za umeme unamvaa Tundu Lisu .Shame on you mkuu .
 
Sasa mkuu ambacho huelewi ni nini?
Je waendelee kuchangia watu kufanya vikao vya harusi?
Hapa Lissu anatetea wananchi wake wasiendelee kutumika kama mtaji wa kuchangia watu kufuja pesa, au kuchangishwa bila kuambiwa pesa zao zinafanya nini?

I hope wabunge wote wangekuwa kama huyu bwana
 
Watoto waliokulia kota shda sana!iyo n tafsiri yako,na Tundu nae ana tafsil yake tena ya kisheria...afu Majid we uwa mnafiki sana!kama miaka miwil ilyopta nikiwa Ughaibuni niliwah kuona umepga picha ktk blog yako..toka Mtera mpka Singda...umaskin,shda na maisha ya watu wa Sngda mjn..ulieleza sana!sasa pale n mjini!je uko bush-country kwa kina Tundu hal ikoje afu watu bado wanachangshwa?Vp hujaskia Pan African Energy wana "TAX HEAVEN" ilyofka 100blion?vp Muuza mkaa kuchangshwa?Tafakari
Yaani zamani nilikuwa napenda sana kutembelea blog ya huyu jamaa nikijua jamaa ni bonge la mzalendo,kumbe ni tofauti na nilivyokuwa nawaza!Ulichoongea mkuu ni kweli tupu,jamaa alishawahi kupiga mipicha kibao ya kuonyesha umaskini wa Singida afu leo analeta "tafsiri" zake kuhusiana na kauli Lissu.
 
Yaani zamani nilikuwa napenda sana kutembelea blog ya huyu jamaa nikijua jamaa ni bonge la mzalendo,kumbe ni tofauti na nilivyokuwa nawaza!Ulichoongea mkuu ni kweli tupu,jamaa alishawahi kupiga mipicha kibao ya kuonyesha umaskini wa Singida afu leo analeta "tafsiri" zake kuhusiana na kauli Lissu.
Gwamahala ndugu yangu hakuna kitu kibaya kama unafiki na kukosa msimamo....uyu jamaa Mjengwa mnaa sana!sijaelewa mantiki yake,anajiulza swali then anajijbu....na ka-mradi kake ka kumjadili Mwalm na Kambona kwa Fourth hand data!najarbu kuangalia Gallery yangu apa mana zle picha ninazo!Tundu kaza buti...nimeona mapgo yako leo ITV,W e ni kichwa mpaka Nyarandu akamkodi Ole Sendeka?
 
WanaJF hakika ukweli utabaki na utasimama milele. TL amewasilisha hoja makini ya dhuluma kwa wnch vijijini. Amby sasa ni mfumo wa kitaasis tangu skl za mitaa, kuu hadi Magamba. Wananchi wanaishi kwa hofu. Siku hizi madiwani ni dola, wakandarasi bdl ya uwakilishi. TL amefungua milango WJF na WHKT tupaze sauti ya kuondoa dhulums hizi. Mbona waligawa kanga na kofia sasa waendelee
ndelee.
 
Mimi sioni sababu ya kuwepo hiyo michango ya kila siku. Sisi tunashabikia lakini tutambue ya kuwa wananchi wanaumia sana hasa wasiokuwa na kipato. Serikali ingekuwa imeendeleza hizi sehemu kama miji ingekuwa rahisi kukusanya kama kodi na kiasi kiwe kidogo ili kila mtu aweze kulipa hata mia tano kwa mwaka. Lakini serikali haina mpango ni kila mtu anatafuta ulaji tu. Utasikia labda kuna mchango wa kitu fulani kama jengo linahitaji sh milioni 50 lakini watu watachangia hata milioni 25 wakishapata hizo hela hawafanyi kitu chochote labda watafetua matofali 1,000 wanaacha hapo Wanasema watu hawaja toa hela. Tundu Lissu upo sahihi tumechoka kujaza matumbo ya wachache.

USHAURI: Serikali ijitahidi kuwa na kumbukumbu za watanzania hasa wanapo zaliwa na wanapoitwa katika nyumba ya ufalme wa mbinguni yaani kufa.. Hii nikiwa na maana ofisi za madiwani ziwe na compyuta ambazo zitatoa vielelezo hata tanzania nzima zikielezea sehemu hizo na madhari yake. Waelezee ni nguvu ya namna gani inahitajika ili eneo hilo liweze kuendelea. Hapa tunaweza kupunguza kasi ya vijana kukimbilia mijini kutafuta ajira na tunaweza kumaliza hizi tofauti za matajiri na masikini. Mimi ninasema hivyo nikiwa na maana sehemu nilikokuwa ilikuwa chini sana kipindi cha miaka ya 80 lakini walipoanza kupambana na kudhamini wazawa wananchi walipata ajira na walifanya kazi japo walikuwa wanalipwa mishara midogo lakini benki zao zilidhamini yule mzawa anaetoa ajira zaidi ya watu 20 na kuendelea na walifanikiwa na serikali ilifanikiwa kukusanya kodi kutokana na mtandao waliojitengenezea. Sasa hapa tanzania wakiona mtanzania anahela kidogo ndio ugomvi na kuanza kumsingizia vitu vya uongo na kutaka kumfilisi hawajui huyo mtu amepata vipi hizo pesa zake. Serikali ya ccm siipendi kabisa kwa sababu imewafundisha wananchi utapeli, uongo hasa hao mapolisi wao. Polisi imepewa madaraka makubwa sana, inabidi mgambo nao wawe na hadhi na wabadilishiwe mavazi wawe kama polisi, ikiwezekana kuwe na kikundi kingine tena cha tatu kama sungusungu na kila kikosi kiwe na shughuli zake za kufanya. Ninadhani nidhamu ya tz inaweza kurudi. Kwa mfano hawa sungusungu wao wanafuatilia wafanyakazi na wanaoajiri hasa kwenye privaty. Kama kwenye mabar, makampuni ya watu binafsi.

Hayo ni maoni yangu tu.
 
Sijakuelewa, unamaanisha Tundu Lissu achange michango peke yake badala ya wananchi?
Achana na gamba hilo....kwangu mimi naamini hata akiitwa mbele ya baraza la Yesu, Lissu atawatoa knock out mbaya maana sheria za nchi ambayo Lissu anaisim,amia inaeleza kuwa wananchi wanatakiwa wasomewe mapato na matumizi ya michango yao, Lissu anasema atawahamasisha wananchi wachange pale tu watakaposomewa mapato na matumizi. Ccm na madiwani wao wanakwepa
 
Reports mbali mbali za utafiti kwenye sector ya elimu kwa mfano zinaonyesha kuwa pesa zinazotengwa kupelekwa mashuleni kusaidia shule za msingi na Sekondari kununua vitabu na vifaa vya kujifunzia hazifiki kama ilivopangwa. Kwa mfano katika MMES1 kwa miaka mitano ilioyopita serikali ilikuwa imetenga shs 25,000 kwa kila mwanafunzi kwa mwaka ziende shule zote za seko za serikali. Kilichofika kwa wastani ni shs 7600, Je, 17,400 alikula nani?

Kuna masuala muhimu ya kusimamia na Mh. Tundu Lisu anatimiza wajibu wake kuhoji. Wana JF ni watu waelewa ndiyo siagi ya taifa, tusipoelewa hili sisi nani ataelewa. Kwa kweli nimesikitishwa sana na wale wanaomsema Lisu vibaya ka kwamba kafanya kosa. Jamii yetu imetopea sana katika mambo ya wizi, ubabaishaji na rushwa kiasi kwamba ukitaka kutenda wema wewe ndo unaonekana uko nje ya mstari. Ni jamii gani tunayoijenga kwamba hata kama ukweli tunauona tunaubeza au kwa sababu tuko mjini hatuoni adha ya michango hii. Inauma sana!
 
Back
Top Bottom