Tumsaidie JK kupanga baraza jipya la mawaziri na "kusafisha UVUNDO"

Umutwale

Mbona linatajwa jina moja tu Wilson? ina maana ndiyo huyuhuyu masarafu?


No no no no! Soma vizuri kwenye highlight ya Blue and Bold. Kisha tafuta jina la huyo MB wa BK mjini, alafu uliza hapa Geneva nini kilimkimbiza mpaa kuacha familia? Unanitega wewe....!
 
Na John Daniel, Dodoma

WABUNGE wamemwomba Rais Jakaya Kikwete, kutomrejesha katika Baraza jipya la Mawaziri mtu yeyote aliyetajwa katika tuhuma za ufisadi zikiwamo zinazoendelea kuchunguzwa na kuhakikisha pia anapunguza ukubwa wa Baraza hilo.

Wabunge hao wamesema, Baraza lililopita lilikuwa mzigo kwa wananchi kwa kuwa lilikuwa kubwa kuliko uwezo wa nchi, hivyo kumtaka alipunguze.

Pia walimpongeza Rais Kikwete kwa uamuzi wake wa kukubali kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa, na kuonya kuwa iwapo angekataa kufanya hivyo, wao na wananchi wasingemwelewa.

"Kwa kweli Rais amefanya vizuri kukubali kujiuzulu kwa Waziri Mkuu, kama asingekubali tusingemwelewa na hata Wananchi wasingemwelewa," alisema Bw. Mgana Msindai, Mbunge wa Iramba Mashariki.

Naye Mbunge wa CCM aliyeomba jina lake kutotajwa kwa maslahi ya kisiasa, alisema: "Maoni yangu kwa Rais ni kutothubutu kumrejesha mtu aliyetajwa katika tuhuma yoyote hata ambayo bado yanachunguzwa, akifanya hivyo, asije kutulaumu," alionya Mbunge huyo na kuongeza:

Jana asubuhi Spika, Bw. Samwel Sitta, alitangaza rasmi kwamba Rais Kikwete alimjulisha rasmi kukubali kujiuzulu kwa Bw. Lowassa na kuvunja Baraza la Mawaziri, hivyo kumlazimu asitishe shughuli za Bunge baada ya uwakilishi wa Serikali kukosekana bungeni.
 
Nakubaliana nawe Idimi kuhusu Mwakyusa hakujiuzulu wakati ule. Lakini bado namuona ni mtu asiye na kashfa na siyo mpenda ubilionea among the rest tulionao. ni suala la yeye kubadilika sasa na kuwajibika ipasavyo.

Nashauri pia JK aache ule utaratibu aliotumia wakati ule wa kuchomoa mawaziri kutoka kila mkoa. utaratibu huu haukuwa na manufaa yoyote kwa taifa zaidi ya kuingiza Mafisadi wengi serikalini. hatuitaji political balance, tunataka maendeleo that's all

Nashukuru kwa kukubaliana nami kuhusu Mwakyusa. Kwa kukuunga mkono, hili la kuchukua mtu kila mkoa kwa ajili ua waziri naona pia linatuangusha sana, ni bora kuangalia utaratibu mwingine, (kama upo), kwani tumeona jinsi mawaziri wengi wasivyo waadilifu.



Mie naona Pombe bado anatufaa kuwepo katika Baraza.Suala la nyumba kwa kweli alivuruga lakini tusisahau alikuwa chini Rais mwizi BMK. Inawezekana maagizo yalitoka kwa BMK au alitekeleza yeye Mwenyewe. Hapo alikosea lakini tunajua wazi hakuchukua pesa au kujiridhisha yeye.Tumsamehe kafanya mengi mazuri kuliko mabaya.

Huu mtindo wa mbunge kuwa waziri unapunguza sana uwigo wa kupata Mawaziri wachapakazi na waaminifu.Wengi wanaokuwa wabunge ndani ya CCM ni watu walele na ndo wanaotuibia na kutumia pesa kwa ajili ya kuchaguliwa kuwa wabunge then wapate nafasi ya uwaziri.Ni vizuri Serikali ikaacha kiburi, na kuruhusu marekebisho ya katiba.Kama ambavyo JK ameona kuwa haifai kuwa mfanya biashara na ukawa kiongozi wa serikari ndo hivyo hivyo haifai kuwa mbunge na kuwa waziri.Huwezi kuserve masters wawili kwa wakati mmoja.

Nyangumi,
Nakuunga mkono kuhusu kuangalia namna bora ya kuteua mawaziri. Ni uharamia kuteua mawaziri kutoka miongoni mwa wabunge, kwani hata wao wabunge wameilalamikia sana tabia hii. Kwanza, kwa sababu unapomteua mbunge kuwa waziri, anakoma kuwa msemaji na mtetezi wa wananchi wa jimbo lake bungeni, anabaki kuwa msemaji wa sirikali kupitia wizara yake. Kwa mantiki hii, anakuwa mbunge wa Watanzania wote, sio wa jimbo lake. Pili, kwa kuwa mawaziri wanakuwa na access na rasilimali za sirikali wakiwa wizarani kwao, wengi wamehusika na kupeleka rasilimali nyingi majimboni kwao ili kufagia njia ya kuchaguliwa tena katika chaguzi nyingine. Kumbuka kwamba huyu huyu Pombe alipitisha barabara ya lami jimboni kwake Chato (akiwa waziri wa ujenzi) kwa makusudi haya haya niliyotaja hapo juu, huku majimbo mengine mkoani Kagera yakiwa hayana hata barabara za kokoto.


Ningependa wafuatao wabakishwe kwenye wizara zao wamalizie visions zao:

1. Magufuli
2. Kawambwa
3. Tyson
4. Makongoro (awe waziri kamili)
5. Mama Sitta
6. Membe
7. Mary Nagu
8. Mwakyusa
9. Mwinyi
10. Maghembe

Maana kubadilisha badilisha within a short time nayo ina madhara ya mtu kushindwa ku achieve long run goals alizojiwekea.

* Msolwa na Mwandosya wanatakiwa wabadilishane wizara.

Chochonde JK mikorokocho ifuatayo ikaa bench pamoja na
" mabangusilo":

!. Chenge
2. Mramba
3. Mungai
4. Mwapachu

Wafuatao wapewe wizara:

1. Mwakyembe---Ushirikiano wa Africa Mashariki
2. Jenista Mhagama...Wanawake na Watoto
3. Ole Sendeka...Usalama wa Raia

Panga panga na wengine wenye uwezo wasio na harufu ya ufisadi

Orodha yako ya kwanza imetulia, ila sijaridhika na uwepo wa Pombe barazani. Huyu kauza nyumba zetu, bado tunamdai chenji. Tuanajua kwamba alikuwa anatumiwa tu kuuza zile nyumba, kwamba halikuwa wazo lake, lakini alipaswa kutokubaliana na wakubwa wake kwa kujiuzulu. huyu bado ana mawaa.
Orodha yako ya pili naiunga mkono kwa 100%, umenikosha sana na Mwalimu Jenista Mhagama. Ikumbukwe kwamba mama huyu amewahi kukaimu madaraka ya unaibu spika (enzi za Msekwa) na alikuwa anaendesha mambo vyema tu. Ole Sendeka naye sina mashaka naye.



Sura Mpya aingie
Zitto , Lunyungu ,Kitila , Mwanakijiji, Mzee Es, Mwafike Jike , utaendeleza

Kwi kwi kwi.
Wakiingia barazani hawa nadhani watakuwa wasenaji wa sirikali badala ya wananchi, kama ilivyo sasa. Ni wazalendo sana, hawafai barazani kwa sababu watahamishia uzalendo huo kuitetea sirikali.


Sijui Katiba ya Tanzania inasemaje, maana sijawahi hata iona...Naomba Msaada raisi anaruhusiwa kuchagua wabunge wapinzani kuingia kwenye baraza la mawaziri ? ama ni lazima watoke chama anachotoka raisi? Nilikuwa natamani Slaa achukue uwaziri wa Usalama wa Raia apambane na mafisadi na Zito achukue nafasi ya mama Zakia...


Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina rangi ya kahawia na inapatikana kwa Kiingereza na Kiswahili. Tumejaribu kuijadili wiki mbili zilizopita, hapa JF na thread hiyo inapatikana hapa,
http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=9086.
Katiba haijasema lolote kwamba waziri atoke katika chama gani, ila possibly kutoka chama chenye wabunge wengi, unless tuwe tunaongela serikali ya mseto.


Jaribuni kubalance kwani inaonekana mnaipeleka nchi kwenye udini,uwiano uwepo ili kuondoa migongano ya kidini ,ni bora kama Waziri Mkuu Mkiristo ,Naibu awe muislamu hivyo hivyo kama Waziri Muislamu naibu awe Mkiristo ,kiasi kuweka kitu kinachoonesha uwiano flani ,Wakiristu wapo na waislamu wapo wanaoweza kushika nyadhifa hizo.Pia ikiwezekana wachukuliwe wasomi ambao wanathamini kazi za usomi wao kwa kile walichosomea na wameridhika na hali ya maisha waliyonayo naweza kusema wameridhika na umasikini wa nchi yao na hivyo hawatatumia vyeo vyao kujitajirisha binafsi zaidi watakuwa wafanyakazi wenye kufanya kazi kwa ajili ya kujenga Taifa lao na kuinua hali ya kipato cha wananchi ambao wanajumlisha wafanyakazi wakulima na waviwanda.
Nionavyo kumrudisha yeyote yule hata mdudu ambae wizara yake imekumbwa skendo basi kutamrudsha Mh.Kikwete katika ukurasa ule ule kwani wengine wamewekwa hapo na fadhila za hao walioondoka hivyo ulipaji wa fadhila utaivamia serikali ya Kikwete kwa rangi nyengine na kuwapa kazi wapinzani kup[iga mayowe.

Mwiba,
Suala la kuweka dini mbele katika serikali halifai kwa nyakati hizi. Tutakuwa hatuwatendei haki wale wasiokuwa wakristo ama Waislamu, kwani nao tunawahitaji serikalini kutokana na utendaji wao.
 
Mimi naona mwisho wa Tanzania yangu ni kama Kenya.. badala ya chanzo kuwa Makabila kuna hatari itakuwa dini maanake madai mengi ynayoyaona ni sawa na yale ya Wajaluo!

Hupaswi kuwa na hofu, mambo yote yataenda vizuri tu. Naamini tutaaendelea kuelimishana kwa hoja hadi tufikie mwafaka.
 
Hupaswi kuwa na hofu, mambo yote yataenda vizuri tu. Naamini tutaaendelea kuelimishana kwa hoja hadi tufikie mwafaka.
Ni balance tu maana nikiangalia hapo kwenye mapendekezo sioni mabaniani wala masingasinga inafaa awepo Waziri wa Jamii ambae atakuwa ni mhusika wa wale wasio na dini au wenye hoja za kidini na kikabila ili zipate uwakilishi bungeni na kujadiliwa na wanataaluma mbalimbali.
Waziri huyu awe anahusika na matatizo ya kikabila na kidini na bora atokee ule upande wa akina Kingunge.Ili asifungamane na upande wowote.Badala ya matatizo ya aina hii kuwakilishwa na mbunge ambae atakuwa anatokea katika dini au kabila ,hivyo wabunge hawatakuwa na nguvu au awausiki kabisa na vita vya mashamba na wafugaji.Waziri wa mambo ya ndani hayupo hapa,yeye yake mengine.
 
Angalia uzalendo wa mtu siyo madigrii yake; Professor Malima alikuwa na Ph.D. bila uzalendo. Sokoine alikuwa na uzalendo bila Ph.D. Je, ni nani kato yao alitufaa zaidi?

Kichuguu

unachuki mbaya na Professor Malima. huyu bwana kafa masikini ana nyumba moja tu Tanzania iko karibu na hospital ya mikocheni.

familia yake kaicha iko hoi? jee uzalendo gani unautaka? wa Mramba kula kila kitu anamiliki shirika la ndege lenye wachaga wengi unalijua, au unataka Uzalendo wa Diallo anamiliki Community airline na star TV, au magufuri ambaye kaiba nyuma nyingi sana, mungai,Sumaye? katika mawaziri walioshika nafasi kubwa na kuondoka bila kitu ni huyu Malima.

mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni. unaweza kumchukia kwa dini yake ila uzalendo alikuwa nao.

mambo ya haki za raia wenye imani tofauti hata Archbishop wa Canterbury dr. roman William wa UK kasema waislam wapewe haki za ndoa na miradhi kwa sheria zao.ingekuwa kwetu tayari vurugu.
 
Timu mpya ya JK iwe ya yeye kushinda 2010 vinginevyo hata mwakani ni matatizo kufika. Matatizo ya Kenya yamesaidia EL kutoweka bila longolongo maana wananchi wenye nchi wamechoka na MAFISADI.
 
What if baada ya kuunda baraza, na Bunge linaunda kamati nyingine ya kuchunguza Benki Kuu halafu wanakuja na ripoiti ya kuwa implicate mawaziri wapya, nao wakajiuzulu.. tutaendelea hivyo hadi lini?

Hapo ndipo haja ya kubadili pia sheria ili mawaziri siyo lazima wawe wabunge wa kuchaguliwa au kuteuliwa. Hivi kama Rais akiangalia nje ya Bunge anaweza kuwapata watu wazuri kumsaidia kazi?
 
1)Freeze Mali za Mkapa,Sumaye,Lowassa,Msabaha na Karamagi.
2)wafunguliwe mashtaka
3)Punguza balaza la mawaziri
Ministry of Housing,Urban Development & Agriculture
Ministry of of Health & Human Services
Ministry of the Treasury
Ministry of Transportation
Ministry of Energy
Ministry of Foreign affairs
Ministry of Education
Ministry of Labor
Ministry of Defense
Ministry of Justice
Ministry of Commerce
Ministry of Interior
Ministry of Sports na utamaduni
Team under PM office

Kila wizara kuwa na Waziri mmoja na Naibu waziri Mmoja..PERIOD

Kuwa hakikishia atakaye fanya ulaji,atanyag'anywa mali zake na kufungwa..Hakuna Mchezo..

Watu wachapa kazi na adabu itakuwepo.
 
Logically hii kitu ya Kusema dini sii muhimu tusahau- mimi siafikiani nayo!

Kwa nini JK Hakuchagua Mwislamu??? Haingewezeka Rais, Mwakamu, na PM kuwa Waislamu!

Hata akipanga baraza la Mawaziri- dini pia anaconsier- haiwezekani eti mawaziri wote wawe Wakristo kwa kuwa tuu mradi tuwe na mtu mchapa kazi!

Tuyaongelee tu -wala tusifumbe macho- all the time maraisi ktk kuunda Cabineti tangu 1961 wamekuwa wanabalace kwa misingi ya mikoa, dini, jinsia na kadhalika!

Mzaendo halisi.

Nyerere alikuwa akibagua watu kwa dini zao aliwapendelea sana wakristu soma hata kitabu cha the mwembechai killings.na ikulu aweka ndugu zake kama mzee Apiyo kuwa katibu mkuu wa Ikulu.

halikadhalika MKAPA aliweka waziri mkuu mkristu huku rais akiwa yeye mkristu makatibu wakuu wengi wakristu na wizara nyeti zote aliweka mawaziri wakristu.

kwenye chama chake yeye alikuwa Mwenyekiti-mkristu, katibu mkuu mangula-mkristu, makamu mwenyekiti John Malecela-mkristu,katibu mwenezi -Jackson Msome -mkristu, kulikuwa na kina Chizi , barongo wote wakristu. makatibu wa mikoa na wenyeviti wengi wakristu. hakuona aibu kuendeleza udini.
 
Msabaha Hana Kitu Ametumiwa Tu Mnofu Kala El.
Hapo Ongeza Mramba Na Diallo Na Yona Daniel Huko Benki Kuu Utasikia Kivumbi Watu Wanaomba Balali Afe Ili Wao Wasitajwe.
 
Mauaji ya Mwembechai yametokea lini?... Mbona Sheikh Kassim bin JUmaa na baraza lake la waislaam walikuwa wanted wakati wa Mwinyi?..Nyerere yuko wapi hapa ikiwa muda wote wa Utawala wake hatukuwa na matatizo pamoja na kwamba mijadala ilikuwa ruksa!.
Nakuuliza tena JK ni muislaam anawasaidia nini waislaam?...
Huyo Mkapa, Lowassa na Sumaye waliokuwa wakristu waliwasaidia nini wakristu hata baada ya kuiba mabillioni?..
Jamani tume na upeo zaidi ya vitu hivi kwani JF ni uwanja mpana zaidi ya kufikiria ndani ya sanduku la udini.
 
udini wa nini tena hapa!!!na sie wapagani ni wazalendo kama nyie wenzetu wakristu na waislam
 
Mauaji ya Mwembechai yametokea lini?... Mbona Sheikh Kassim bin JUmaa na baraza lake la waislaam walikuwa wanted wakati wa Mwinyi?..Nyerere yuko wapi hapa ikiwa muda wote wa Utawala wake hatukuwa na matatizo pamoja na kwamba mijadala ilikuwa ruksa!.
Nakuuliza tena JK ni muislaam anawasaidia nini waislaam?...
Huyo Mkapa, Lowassa na Sumaye waliokuwa wakristu waliwasaidia nini wakristu hata baada ya kuiba mabillioni?..
Jamani tume na upeo zaidi ya vitu hivi kwani JF ni uwanja mpana zaidi ya kufikiria ndani ya sanduku la udini.

Lowasa, mkapa na sumaye wamefanya mengi kwa wakristu soma hicho kitabu na kingine Muslim in Tanzania.
 
sihitaji kusoma kitabu hicho (nimeshakisoma) na nilishazungumza na mtunzi Dr. Njozi.. nenda kwenye KLH News utayaona mahojiano yangu ya 2006 .. you should know that.
 
Back
Top Bottom