ha ha ha ha!Usinikumbushe hii zahama, mana siku moja niliandika kurasa tatu. Mesenja wangu akagoma kuipeleka kwasababu sikumpa posho. Nikaona haijalishi, nikamtafuta demu hadi nikambana kwenye kona ya darasa, acha nianze kumsomea barua niliyomwandikia kurasa hadi kurasa, yaani kama risala mbele ya mgeni rasmi, nilipomaliza..."wasalamu mimi......." demu alikuwa kashayayuka kitamboo, kumbe alimwona mwalimu na akatoweka, mwalimu kumbe kaja kimya kimya na kuchukuwa nafasi ya demu na akawa ndio msikilizaji wa ile barua. Kuinua kichwa namwona mwalimu mbele yangu....sikujuwa kama nilikuwa na-jamba au na-koj-oa au nilishikwa na degedege. Mwalimu kaniambia nimpe barua na niwahi darasani, gafla nikasikia ofisi mzima ya walimu inarindima kwa vicheko...teacher alikwenda kuwasomea ile barua. Kibaya mimi ndio nilikuwa kaka mkuu na demu ni dada mkuu, yakawa makubwa!!! Barua ikawa imebandikwa kwenye ofisi ya walimu...utadhani ni thesis.
hahhaaaaa... mkuu umenivunja mbavuUsinikumbushe hii zahama, mana siku moja niliandika kurasa tatu. Mesenja wangu akagoma kuipeleka kwasababu sikumpa posho. Nikaona haijalishi, nikamtafuta demu hadi nikambana kwenye kona ya darasa, acha nianze kumsomea barua niliyomwandikia kurasa hadi kurasa, yaani kama risala mbele ya mgeni rasmi, nilipomaliza..."wasalamu mimi......." demu alikuwa kashayayuka kitamboo, kumbe alimwona mwalimu na akatoweka, mwalimu kumbe kaja kimya kimya na kuchukuwa nafasi ya demu na akawa ndio msikilizaji wa ile barua. Kuinua kichwa namwona mwalimu mbele yangu....sikujuwa kama nilikuwa na-jamba au na-koj-oa au nilishikwa na degedege. Mwalimu kaniambia nimpe barua na niwahi darasani, gafla nikasikia ofisi mzima ya walimu inarindima kwa vicheko...teacher alikwenda kuwasomea ile barua. Kibaya mimi ndio nilikuwa kaka mkuu na demu ni dada mkuu, yakawa makubwa!!! Barua ikawa imebandikwa kwenye ofisi ya walimu...utadhani ni thesis.
HAHAHAHAHAAHAHA...!
YANI HIZI SIMU ZIMETUHARIBIA SAAAAANA..! unakuta barua ilitumwa kama mwezi uliopita ndo unaipata ukiwa boarding skul.
basi unaanza kumsifia demu mbele ya marafiki, kumbe demu mwenyewe kiporiii...! yani kuku wa kienyeji :becky::becky::becky: