Tukiwa tunaelekea Uchaguzi mkuu, sasa hivi kila Mbunge anajifanya kuiponda Serikali

Mhaya

JF-Expert Member
Aug 20, 2023
1,658
4,866
Siku ya jana na Leo Bunge limekuwa la moto kweli, kila mbunge akiishambulia serikali na mawaziri wake. Kwa sisi wenye uelewa tunajua hizi ni mbio za sakafuni tu.

Sasa hivi wabunge wanajua Muda wa kukaa bungeni umeisha, kila mbunge anajinadi sasa na kuishtumu serikali juu ya ubadhirifu wa fedha na ufisadi wote uliofanywa na serikali. Kwa sababu wanajua wamebaki mwaka mmoja tu wa kuendelea kubaki madarakani na mwaka huu umeshaisha ndio kwamba tuko Novemba, na mwaka 2025 hasa hasa ni wa kampeni na uchaguzi, hivyo mwaka pekee uliobaki kuwashawishi wananchi tuone wanafanya kazi ni mwaka 2024.

Wanajua kabisa Wananchi hawakubali mtaani, kwanza walipitisha DP World, pili Ufisadi, tatu Upigaji umerudi, rushwa na kadharika. Wabunge walikuwa wanapiga makofi tu bungeni, na kupitisha mikataba bila kusoma.

Sasa mtaani wanajua kurudi bungeni ni mtiti, wanafanya juu chini sasa hivi kutukana serikali, kwani mwanzo kipindi wananchi tunalalamika mlikuwa wapi wakati nyinyi ndio sauti zetu bungeni. CCM mnatuletea unafiki, mmeshapiga hela sasa hivi mnatuektia.

Mimi kura yangu ya wabunge na madiwani naipeleka vyama Pinzani, Kwenye Urais bado nasikilizia upepo, akitokea rais wa maana nampatia kura yangu.
 
Siku ya jana na Leo Bunge limekuwa la moto kweli, kila mbunge akiishambulia serikali na mawaziri wake. Kwa sisi wenye uelewa tunajua hizi ni mbio za sakafuni tu.

Sasa hivi wabunge wanajua Muda wa kukaa bungeni umeisha, kila mbunge anajinadi sasa na kuishtumu serikali juu ya ubadhirifu wa fedha na ufisadi wote uliofanywa na serikali. Kwa sababu wanajua wamebaki mwaka mmoja tu wa kuendelea kubaki madarakani na mwaka huu umeshaisha ndio kwamba tuko Novemba, na mwaka 2025 hasa hasa ni wa kampeni na uchaguzi, hivyo mwaka pekee uliobaki kuwashawishi wananchi tuone wanafanya kazi ni mwaka 2024.

Wanajua kabisa Wananchi hawakubali mtaani, kwanza walipitisha DP World, pili Ufisadi, tatu Upigaji umerudi, rushwa na kadharika. Wabunge walikuwa wanapiga makofi tu bungeni, na kupitisha mikataba bila kusoma.

Sasa mtaani wanajua kurudi bungeni ni mtiti, wanafanya juu chini sasa hivi kutukana serikali, kwani mwanzo kipindi wananchi tunalalamika mlikuwa wapi wakati nyinyi ndio sauti zetu bungeni. CCM mnatuletea unafiki, mmeshapiga hela sasa hivi mnatuektia.

Mimi kura yangu ya wabunge na madiwani naipeleka vyama Pinzani, Kwenye Urais bado nasikilizia upepo, akitokea rais wa maana nampatia kura yangu.
Inafikirisha Sana kiukwelli
 
Hawa watu ni washenzi mno,ni waigizaji wazuri tu,kuweni makini nao sana
 
Hawa watu ni washenzi mno,ni waigizaji wazuri tu,kuweni makini nao sana
Ubaya watanzania wengi hawaelewi hizi drama za viongozi... Miaka ya mwanzoni wakiingia bungeni wanajifanya kuwa wamoja, hawaipondi serikali, hawafichui maovu, sasa hivi tunaelekea Uchaguzi wanatafuta namna ya kupata kura, wanaanza kusontana, na kujifanya wanafichua ufisadi, wakati mwanzo walikuwa wanapiga makofi tu
 
Sisi ni Wahuni wakubwa sana
Ila kura yako haisaidii kitu
Lazima tuendelee kulamba asali kila mtu apambane na hali yake
 
Sisi ni Wahuni wakubwa sana
Ila kura yako haisaidii kitu
Lazima tuendelee kulamba asali kila mtu apambane na hali yake
Sawa kura yangu inaweza kuwa aina msaada, lakini kura zetu zikiwa nyingi, au tukisala... Mnaondoka madarakani
 
wakati wa kupitisha ile tozo walikua wanajadili katika namna ambayo wanatuchamba sisi raia kina mwigulu walitoa matamko mabaya ila muda utaaamua
 
Washazoea kuwapiga fix wabongo

Wanawaona watanzania mafal.....

Sahv kuna wabunge watapiga magoti na kutambaaaa

Ova
 
wakati wa kupitisha ile tozo walikua wanajadili katika namna ambayo wanatuchamba sisi raia kina mwigulu walitoa matamko mabaya ila muda utaaamua
Walitutuka sana wananchi kipindi cha Tozo na DP World... Sasa hivi wanajifanya kututetea, wanaonesha kuwa wanauchungu juu ya ufisadi
 
Back
Top Bottom