Tukio limejirudia tena katika mazingira yaleyale, nikiwa na watu walewale huku tukizungumza maneno yaleyale

Melki Wamatukio

JF-Expert Member
May 3, 2022
5,845
10,070
Msaada wakuu, hii hali imeanza kuwa serious sana. Kwa sasa inanikuta kila mwezi tofauti na awali ilipokuwa inanitokea mara moja kwa mwaka

Inaanza uko maeneo fulani ukiwa na mtu fulani, wakati unamalizia mazungumzo, ndipo unakumbuka kuwa hayo maneno umewahi yatamka kabla. Hata eneo ulilopo ndilo lile lile, pia mtu unayezungumza naye ni yule yule au mtu anayeendana hobies na uliyozungumza naye mwanzoni

Au unapita mahali unakutana na tukio amabalo umewahi kukutana nalo kabla. Hata majibizano ya watu yanayoendelea ni yaleyale ya kipindi hicho. Unapojaribu kufungua mdomo kuzungumza, unajikuta unazungumza yale yale uliyowahi kuzungumza. Unabaki unashangaa tu

Hii hali husababishwa na nini wakuu?
Je, tukio la kwanza kabla, lilikuwa ni ndoto? Au liliwahi tokea kweli? Au ni mawenge tu? Au naumwa malaria? Maake sielewi hata limekuja vipi, yaani from nowhere

Nikijaribu kumuuliza huyo ninayezungumza naye kwamba haoni kama tunafanya marudio?, anaishia kusema nipunguze wenge au kucheka tu

Naombeni ufafanuzi wakuu
N.B: Situmii mihadarati
 
Hyo inaitwa "DEJAVU".

kimsingi sisi binadamu tuna nafsi ambazo zishawahi kuishi kabla hatujapewa hii miili. Kwa hyo mfano ww unaweza kuta mwili wako una nafsi ambayo hapo kabla ishawahi kuishi hayo maeneo unayopitia, then yule alokuwa anamiliki hyo nafsi akafa, then hyo nafsi ikawekwa kwny mwili wako afu ndo ukazaliwa wewe wa saizi.
 
Hyo inaitwa "DEJAVU"
kimsingi sisi binadamu tuna nafsi ambazo zishawahi kuishi kabla hatujapewa hii miili. Kwa hyo mfano ww unaweza kuta mwili wako una nafsi ambayo hapo kabla ishawahi kuishi hayo maeneo unayopitia,, then yule alokuwa anamiliki hyo nafsi akafa, then hyo nafsi ikawekwa kwny mwili wako afu ndo ukazaliwa wewe wa saizi.

Sawa
 
Hii inatokea sana,kuna muda unabaki unashangaa yani kitu kama kimejirudia vile,piq kuna ile unaota upo sehemu fulani,kuna siku ukifika hilo eneo ile ndoto unaikumbuka na eneo husika unaliona live.

Anyway tuishi tu hiizi siri kubwa ambazo ni ngumu kuzijua,hivi ulikua wapi kabla hujazaliwa na unaenda wapi baada ya kufa?
 
Hyo inaitwa "DEJAVU"
kimsingi sisi binadamu tuna nafsi ambazo zishawahi kuishi kabla hatujapewa hii miili. Kwa hyo mfano ww unaweza kuta mwili wako una nafsi ambayo hapo kabla ishawahi kuishi hayo maeneo unayopitia,, then yule alokuwa anamiliki hyo nafsi akafa, then hyo nafsi ikawekwa kwny mwili wako afu ndo ukazaliwa wewe wa saizi.
Umemaliza mkuu ila kuamka sio kwa kila mmoja .
 
NAONA una shida kidogo kwenye muungano wa roho yako na mwili wako, io hali inapelekea mwili wako kupata dodoso za mambo ya Rohoni na haikupaswa iwe hivyo.

Sasa ili kuepukana na tabia hiyo inayofanywa na mwili wako itabidi utafutee mlima mkubwa sana afu utafute kitako chake, ukae hapo chini siku tatu au ila itakuwa vizuri kama ukaingia katikati kabisa ya mlima huo. Kani ya uvutano itaziunganisha vizuri roho n mwili wako.

Asante.
 
Hyo inaitwa "DEJAVU"
kimsingi sisi binadamu tuna nafsi ambazo zishawahi kuishi kabla hatujapewa hii miili. Kwa hyo mfano ww unaweza kuta mwili wako una nafsi ambayo hapo kabla ishawahi kuishi hayo maeneo unayopitia,, then yule alokuwa anamiliki hyo nafsi akafa, then hyo nafsi ikawekwa kwny mwili wako afu ndo ukazaliwa wewe wa saizi.
mkuu hii unayozungmza ni kwel au fikila zk tu
 
Hyo inaitwa "DEJAVU"
kimsingi sisi binadamu tuna nafsi ambazo zishawahi kuishi kabla hatujapewa hii miili. Kwa hyo mfano ww unaweza kuta mwili wako una nafsi ambayo hapo kabla ishawahi kuishi hayo maeneo unayopitia...
Mkuu, kwa maana hiyo, kumbe baada ya binadamu kufa, nafsi zetu haziendi mbinguni wala motoni, badala yake hutunzwa kwa ajili ya binadamu watakaozaliwa?

Maana yake maisha nitakayoyaishi yatafanana na yale ya aliyekuwepo enzi hizo? Hata na kifo alichokufa ndicho ambacho na mimi nitakufa? Hata umri alioishi?
 
Hyo inaitwa "DEJAVU"
kimsingi sisi binadamu tuna nafsi ambazo zishawahi kuishi kabla hatujapewa hii miili. Kwa hyo mfano ww unaweza kuta mwili wako una nafsi ambayo hapo kabla ishawahi kuishi hayo maeneo unayopitia,, then yule alokuwa anamiliki hyo nafsi akafa, then hyo nafsi ikawekwa kwny mwili wako afu ndo ukazaliwa wewe wa saizi.
Kwahyo kisayansi hio ni "Glitch" kwenye system??😂😂
 
Back
Top Bottom