Uchaguzi 2020 TUJADILI: Je, hotuba za mgombea Urais - CHADEMA ndugu Tundu Lissu katika kampeni huwa anamtukana Mgombea Urais - CCM na Rais wa JMT ndugu Magufuli?

The Palm Tree

JF-Expert Member
Apr 13, 2013
7,951
12,535
Nimeanzisha mjadala huu baada ya tukio la jana huko Chato la msafara wa Mgombea Urais - CHADEMA ndugu Tundu Lissu kushambuliwa kwa mawe na wafuasi wa CCM mara baada ya kumaliza kuzungumza na wananchi katika mkutano wake wa kampeni.

Kabla ya tukio hilo la Jana tulimwona yule ajiitaye "mwanaharakati huru" wa kumtetea Bw. John Pombe Magufuli, Cyprian Musiba akionya kuwa Lissu asiende Chato na kumtukana Rais Magufuli kwa sababu atakiona cha mtema kuni!

Baada ya tukio hilo baadhi ya posts ktk mitandao ya kijamii zikaunga mkono uhalifu huo eti ni kwa sababu anamtukana sana Rais Magufuli na kuidhalilisha serikali badala amwage Sera..!!

Honestly, hoja hii mimi huwa siielewi, hainingii kwenye akili yangu na naiona ni ya watu wasio na ufahamu wa kutosha wa maarifa.

KWANZA;

Inaeleweka kuwa, kwa mujibu ya sheria za Tanzania "MATUSI" ama "KUTOA LUGHA YA MATUSI" ni kosa la jinai kwa yeyote dhidi ya mtu aliyetukanwa..!

PILI;

Ni nani amewahi kumlalamikia Tundu Lissu kuwa amemtukana? John Pombe Magufuli amewahi kufanya hivyo? Jibu ni: HAPANA. Kwanini? Haijulikani...!

Kama hakuna ambaye amewahi kumshtaki Tundu Lissu kwa madai ya "kutukanwa" akiwemo Magufuli mwenyewe, haya madai ya kuwa Tundu Lissu anamtukana Rais Magufuli na kuidhalilisha serikali yanatoka wapi? Msingi wake ni nini?

Kwa mtazamo wangu nadhani hizi ni sababu wanazozitumia kuficha udhaifu na mapungufu ya bwana Mkubwa huyu anayedaiwa kutukanwa;

1. Tundu Lissu amevunja MWIKO (taboo) na MAZOEA/UTAMADUNI mbaya (bad tradition) uliokuwa uanajaribiwa kujengwa miongoni mwa wanajamii kudhani kuwa "ni mwiko kumkosoa mfalme - Rais". Hili limewashitua na kwao wanaona haya ni MATUSI makubwa sana kuusema wazi udhaifu na mapungufu ya kiutendaji ya mfalme - Rais...

Lakini hakuna sheria inayounga mkono dai lao. Kwa sababu, hakuna matusi ktk hotuba za Lissu..!

2. Kingine kinachowasumbua ni umahiri na style ya mgombea Urais wa CHADEMA ndg Tundu Lissu kuuelezea udhaifu na mapungufu ya mgombea Urais wa CCM ndg John Pombe Magufuli katika lugha yenye kueleweka kwa urahisi kwa wananchi.

Wakati mwingine Tundu Lissu hutumia lugha kali kidogo yenye msisitizo wa nguvu ktk jambo analotaka kulikazia ili watu waelewe. Hili pia huwa ni tatizo kwa wahafidhina hawa..!

Hili ni baya mno kwao wana CCM na wafuasi wao. Ni MATUSI makubwa mno kwao. Hii inafunua upande wa pili wa shilingi wa John Pombe Magufuli ambao wananchi hawa walikuwa hawajui. Na kwa kweli wanashangaa na kupigwa na butwaa kuliko kawaida hata kusema;

"... ala, kumbe huyu mtu ndivyo alivyo? Kumbe tumekuwa tukidanganywa miaka yote hii huku ukweli ukiwa tofauti ..?"

Hili ndilo tatizo lao kwa Tundu Lissu...!!

3. Haya MAZOEA na utamaduni mbaya ndiyo uliokuwa katika majaribio ya kujengwa katika miaka hii mitano ya Rais Magufuli.

Na kiuhalisia yeye binafsi na wafuasi wake baadhi wachache, walishaamini kabisa kuwa wamefanikiwa na wanaweza kukaa kwenye viti vyao vya enzi milele kwa raha mustarehe.!

Kujitokeza ghafla kwa mtu mmoja jasiri wa kuanza kubomoa MAZOEA na UTAMADUNI huu mbaya kabisa kumewashitua. Kunawafanya wahahe, wawe desperate kujiokoa. Chochote kilichopo mbele yao cha kujiokoa, watakitumia. Iwe uongo au hata kumwaga damu ya mtu/watu..!!

Namna pekee ya kujitetea na kujaribu kuulinda au kuu - restore ni kubuni njia ya kunzuia. Kifo ndiyo ilikuwa option ya mwisho. Bahati mbaya kwao option hiyo ika - fail spectacularly!!

4. Kufeli kwa options zote ikiwemo ya kifo, ikawaweka katika "desperation state" watu hawa ktk namna ambayo pengine hawakurajia kabisa,kabisa..

Sasa kinachofanyika ni kutengeneza propaganda, wanazihalalisha kisha wanazitumia kama sababu za kuamuru vyombo vya mabavu hususani polisi kutumia nguvu zenye kusababisha maafa na uharibifu na maumivu makubwa kwa wafuasi wa mgombea huyu wanaomfuata kumsikiliza..!

Karibu kwa maoni na mtazamo wako wewe. Na wana CCM mnakaribishwa zaidi ya wengine kushiriki mjadala huu...
 
..Mzee Shibuda aliwahi kusema wanasiasa wana lugha zao za kwenye majukwaa.

..wanapokuwa majukwaani hurusha VIJEMBE, sasa mtu asiyejua siasa anaweza kusema ni matusi au kuhatarisha amani.

..CCM wanaposema watawachinja wapinzani hawamaanishi kwamba wananoa majambia tayari kuwakata vichwa.
 
Kurudisha FAO la kujitoa iko kwenye Ilani ya CHADEMA.

Je unadhani wafanyakazi sekta binafsi mikataba yao kuisha na kunyimwa Pesa zao Ni Haki?

Kwanini Magufuli alifuta FAO la kujitoa?

Kikwete na Mkapa hawakuondoa, ni wajinga?

Pesa za mafao ni za wafanyakazi au ni za Serikali?
 
Jamii ndo inaliki lugha na tafsiri yake, na kila kitu dunia huwa kina pande mbili, wa kushoto na kulia, hii ina maana kwamba neno lilelile linaweza kuwa tafsiri tofauti kuliangana na aliyeongea alikuwa katika mazingira gani? Anaongea na nani? na Uhusiano kati yake na anayeongea pia huyo mtu ni nani?

Kwa hiyo inawezekana Ndg Lissu anamtukana Dr. Magufuli au hamtukani .Pia Mgombea wa urais kwa tiketi ya CDM Ndg Tundu antipas Lissu anamtukana au hamtukani mgombea urais kwa tiketi ya CCM Dr John Joseph Pombe Magufuli
 
Moja ya tamadun amabyo inatakiwa ikataliwe hapa Tanzania kwa nguvu zote, kuanzia ngazi ya familia mpaka uongozi ni kuchukulia umetukanwa ukikosolewa. Hii sio President tu, ipo toka ngza ya famalia zetu kabisa, ukimbishia mkubwa au ukamshinda kwa hoja ili akugandamize utasikia kanitukana, basi baada ya hapo familia nzima hua upande ule.

Hata shuleni, mwalimu ukimbishia kitu kwa facts, utasikia amenitukana, basi huko staff ni viboko tu, unaulizwa kwa nini umemtukana mwalimu. Nako kweny jamii zetu, hasa vijijini ukimjibu mzee tofauti na zile itaikadi zao, utasikia huyu mtoto ana matusi sana.

Kwa hiyo hili swala sio Magufuli pekee yake, tuanze kujifunza toka ngazi ya familia, kwan huku ndiko hutuzalishia akina Magufuli ambao hawataki kuguswa utafikir wanaongoza familia zao, kumbe ni nchi yenye watu 60million. Swaini kabisa
 
Moja ya tamadun amabyo inatakiwa ikataliwe hapa Tanzania kwa nguvu zote, kuanzia ngazi ya familia mpaka uongozi ni kuchukulia umetukanwa ukikosolewa. Hii sio President tu, ipo toka ngza ya famalia zetu kabisa, ukimbishia mkubwa au ukamshinda kwa hoja ili akugandamize utasikia kanitukana, basi baada ya hapo familia nzima hua upande ule. Hata shuleni, mwalimu ukimbishia kitu kwa facts, utasikia amenitukana, basi huko staff ni viboko tu, unaulizwa kwa nini umemtukana mwalimu. Nako kweny jamii zetu, hasa vijijini ukimjibu mzee tofauti na zile itaikadi zao, utasikia huyu mtoto ana matusi sana. Kwa hiyo hili swala sio Magufuli pekee yake, tuanze kujifunza toka ngazi ya familia, kwan huku ndiko hutuzalishia akina Magufuli ambao hawataki kuguswa utafikir wanaongoza familia zao, kumbe ni nchi yenye watu 60million. Swaini kabisa
Unatambua kuwa Rais na mpiga debe Wana hadhi tofauti??

Toka Tanzania, Nenda duniani kwanini haya maneno hutumika kwa watu special:
His/her majesty.

Mhesimiwa N.k

Ndipo utatambua unapo mkosoa mpiga debe ni tofauti unavyo mkosoa Rais.(For public purpose).
 
Lisu ni jeuri na ana kejeli sana!

Hotuba zake nyingi hajisikii raha kama hajamkejeli rais Magufuli personal!

Huyu mimi naunga mkono kupopolewa na mawe maana hakajielewi haka kawakala ka beberu
 
Lisu ni jeuri na ana kejeli sana!

Hotuba zake nyingi hajisikii raha kama hajamkejeli rais Magufuli personal!

Huyu mimi naunga mkono kupopolewa na mawe maana hakajielewi haka kawakala ka beberu
Mabeberu wanakusalimia
SmartSelect_20201014-094838_Twitter.jpg
 
Lisu ni jeuri na ana kejeli sana!

Hotuba zake nyingi hajisikii raha kama hajamkejeli rais Magufuli personal!

Huyu mimi naunga mkono kupopolewa na mawe maana hakajielewi haka kawakala ka beberu
Wapopoaji waliotumwa....haya wanayaweza CCM tu. Yalitokea Hai. Hizi ni dalili za kushenzika tu yaani kukosa ustarabu.
 
Nimeanzisha mjadala huu baada ya tukio la jana huko Chato la msafara wa Mgombea Urais - CHADEMA ndugu Tundu Lissu kushambuliwa kwa mawe na wafuasi wa CCM mara baada ya kumaliza kuzungumza na wananchi katika mkutano wake wa kampeni.

Kabla ya tukio hilo la Jana tulimwona yule ajiitaye "mwanaharakati huru" wa kumtetea Bw. John Pombe Magufuli, Cyprian Musiba akionya kuwa Lissu asiende Chato na kumtukana Rais Magufuli kwa sababu atakiona cha mtema kuni!

Baada ya tukio hilo baadhi ya posts ktk mitandao ya kijamii zilizokuwa zinaunga mkono uhalifu huo eti ni kwa sababu anamtukana sana Rais Magufuli na kuidhalilisha serikali!!

Honestly, hoja hii mimi huwa siielewi, hainingii kwenye akili yangu na naiona ni ya watu wasio na ufahamu wa kutosha wa maarifa.

KWANZA;

Inaeleweka kuwa, kwa mujibu ya sheria za Tanzania "MATUSI" ama "KUTOA LUGHA YA MATUSI" ni kosa la jinai kwa yeyote dhidi ya mtu aliyetukanwa..!

PILI;

Ni nani amewahi kumlalamikia Tundu Lissu kuwa amemtukana? John Pombe Magufuli amewahi kufanya hivyo? Jibu ni: HAPANA. Kwanini? Haijulikani...!

Kama hakuna ambaye amewahi kumshtaki Tundu Lissu kwa madai ya "kutukanwa" akiwemo Magufuli mwenyewe, haya madai ya kuwa Tundu Lissu anamtukana Rais Magufuli na kuidhalilisha serikali yanatoka wapi? Msingi wake ni nini?

Kwa mtazamo wangu nadhani hizi ni sababu wanazozitumia kuficha udhaifu na mapungufu ya bwana Mkubwa huyu anayedaiwa kutukanwa;

1. Tundu Lissu amevunja MWIKO (taboo) na MAZOEA/UTAMADUNI mbaya (bad tradition) uliokuwa uanajaribiwa kujengwa miongoni mwa wanajamii kudhani kuwa "ni mwiko kumkosoa mfalme - Rais". Hili limewashitua na kwao wanaona haya ni MATUSI makubwa sana kuusema wazi udhaifu na mapungufu ya kiutendaji ya mfalme - Rais...

Lakini hakuna sheria inayounga mkono dai lao. Kwa sababu, hakuna matusi ktk hotuba za Lissu..!

2. Kingine kinachowasumbua ni umahiri na style ya mgombea Urais wa CHADEMA ndg Tundu Lissu kuuelezea udhaifu na mapungufu ya mgombea Urais wa CCM ndg John Pombe Magufuli katika lugha yenye kueleweka kwa urahisi kwa wananchi.

Wakati mwingine Tundu Lissu hutumia lugha kali kidogo yenye msisitizo wa nguvu ktk jambo analotaka kulikazia ili watu waelewe. Hili pia huwa ni tatizo kwa wahafidhina hawa..!

Hili ni baya mno kwao wana CCM na wafuasi wao. Ni MATUSI makubwa mno kwao. Hii inafunua upande wa pili wa shilingi wa John Pombe Magufuli ambao wananchi hawa walikuwa hawajui. Na kwa kweli wanashangaa na kupigwa na butwaa kuliko kawaida hata kusema;

"... ala, kumbe huyu mtu ndivyo alivyo? Kumbe tumekuwa tukidanganywa miaka yote hii huku ukweli ukiwa tofauti ..?"

Hili ndilo tatizo lao kwa Tundu Lissu...!!

3. Haya MAZOEA na utamaduni mbaya ndiyo uliokuwa katika majaribio ya kujengwa katika miaka hii mitano ya Rais Magufuli.

Na kiuhalisia yeye binafsi na wafuasi wake baadhi wachache, walishaamini kabisa kuwa wamefanikiwa na wanaweza kukaa kwenye viti vyao vya enzi milele kwa raha mustarehe.!

Kujitokeza ghafla kwa mtu mmoja jasiri wa kuanza kubomoa MAZOEA na UTAMADUNI huu mbaya kabisa kumewashitua. Kunawafanya wahahe, wawe desperate kujiokoa. Chochote kilichopo mbele yao cha kujiokoa, watakitumia. Iwe uongo au hata kumwaga damu ya mtu/watu..!!

Namna pekee ya kujitetea na kujaribu kuulinda au kuu - restore ni kubuni njia ya kunzuia. Kifo ndiyo ilikuwa option ya mwisho. Bahati mbaya kwao option hiyo ika - fail spectacularly!!

4. Kufeli kwa options zote ikiwemo ya kifo, ikawaweka katika "desperation state" watu hawa ktk namna ambayo pengine hawakurajia kabisa,kabisa..

Sasa kinachofanyika ni kutengeneza propaganda, wanazihalalisha kisha wanazitumia kama sababu za kuamuru vyombo vya mabavu hususani polisi kutumia nguvu zenye kusababisha maafa na uharibifu na maumivu makubwa kwa wafuasi wa mgombea huyu wanaomfuata kumsikiliza..!

Karibu kwa maoni na mtazamo wako wewe. Na wana CCM mnakaribishwa zaidi ya wengine kushiriki mjadala huu...
Lissu ni shujaa wa vita.
 
Sio hapa kwetu tu, nakumbuka hata akina Nabukadrezza walilazimisha watu wawaabudu ndipo walipokataa akaamuru watupwe kwenye tanuru la moto.

Madaraka yanalevya sana na watawala wengi shetani huwatumia sana na Magufuli yuko kwenye mkumbo huo.

Inaonekana kimoyo moyo haamini kama kuna Mungu, anaamini yeye ndio anapaswa kusujudiwa sasa akipatikana mtu kama Lissu asiye tayari kuabudu sanamu basi anatangaziwa "Fatwa"....!!!
 
Jamii ndo inaliki lugha na tafsiri yake, na kila kitu dunia huwa kina pande mbili, wa kushoto na kulia, hii ina maana kwamba neno lilelile linaweza kuwa tafsiri tofauti kuliangana na aliyeongea alikuwa katika mazingira gani? Anaongea na nani? na Uhusiano kati yake na anayeongea pia huyo mtu ni nani?
Kwa hiyo inawezekana Ndg Lissu anamtukana Dr. Magufuli au hamtukani .Pia Mgombea wa urais kwa tiketi ya CDM Ndg Tundu antipas Lissu anamtukana au hamtukani mgombea urais kwa tiketi ya CCM Dr John Joseph Pombe Magufuli

Asante sana...

Wewe umejikita kwenye tafsiri, kwamba, tafsiri ya tusi anayo anayesikiliza/soma

Mfano jamii nyingine, wakisikia neno "panua", kwao ni tusi kubwa kwelikweli wakati jamii zingine itaelewa kuwa ni kuongeza ukubwa wa eneo au kuongeza mpaka au kuongeza wigo...

Asante sana..
 
Nimeanzisha mjadala huu baada ya tukio la jana huko Chato la msafara wa Mgombea Urais - CHADEMA ndugu Tundu Lissu kushambuliwa kwa mawe na wafuasi wa CCM mara baada ya kumaliza kuzungumza na wananchi katika mkutano wake wa kampeni.

Kabla ya tukio hilo la Jana tulimwona yule ajiitaye "mwanaharakati huru" wa kumtetea Bw. John Pombe Magufuli, Cyprian Musiba akionya kuwa Lissu asiende Chato na kumtukana Rais Magufuli kwa sababu atakiona cha mtema kuni!

Baada ya tukio hilo baadhi ya posts ktk mitandao ya kijamii zikaunga mkono uhalifu huo eti ni kwa sababu anamtukana sana Rais Magufuli na kuidhalilisha serikali badala amwage Sera..!!

Honestly, hoja hii mimi huwa siielewi, hainingii kwenye akili yangu na naiona ni ya watu wasio na ufahamu wa kutosha wa maarifa.

KWANZA;

Inaeleweka kuwa, kwa mujibu ya sheria za Tanzania "MATUSI" ama "KUTOA LUGHA YA MATUSI" ni kosa la jinai kwa yeyote dhidi ya mtu aliyetukanwa..!

PILI;

Ni nani amewahi kumlalamikia Tundu Lissu kuwa amemtukana? John Pombe Magufuli amewahi kufanya hivyo? Jibu ni: HAPANA. Kwanini? Haijulikani...!

Kama hakuna ambaye amewahi kumshtaki Tundu Lissu kwa madai ya "kutukanwa" akiwemo Magufuli mwenyewe, haya madai ya kuwa Tundu Lissu anamtukana Rais Magufuli na kuidhalilisha serikali yanatoka wapi? Msingi wake ni nini?

Kwa mtazamo wangu nadhani hizi ni sababu wanazozitumia kuficha udhaifu na mapungufu ya bwana Mkubwa huyu anayedaiwa kutukanwa;

1. Tundu Lissu amevunja MWIKO (taboo) na MAZOEA/UTAMADUNI mbaya (bad tradition) uliokuwa uanajaribiwa kujengwa miongoni mwa wanajamii kudhani kuwa "ni mwiko kumkosoa mfalme - Rais". Hili limewashitua na kwao wanaona haya ni MATUSI makubwa sana kuusema wazi udhaifu na mapungufu ya kiutendaji ya mfalme - Rais...

Lakini hakuna sheria inayounga mkono dai lao. Kwa sababu, hakuna matusi ktk hotuba za Lissu..!

2. Kingine kinachowasumbua ni umahiri na style ya mgombea Urais wa CHADEMA ndg Tundu Lissu kuuelezea udhaifu na mapungufu ya mgombea Urais wa CCM ndg John Pombe Magufuli katika lugha yenye kueleweka kwa urahisi kwa wananchi.

Wakati mwingine Tundu Lissu hutumia lugha kali kidogo yenye msisitizo wa nguvu ktk jambo analotaka kulikazia ili watu waelewe. Hili pia huwa ni tatizo kwa wahafidhina hawa..!

Hili ni baya mno kwao wana CCM na wafuasi wao. Ni MATUSI makubwa mno kwao. Hii inafunua upande wa pili wa shilingi wa John Pombe Magufuli ambao wananchi hawa walikuwa hawajui. Na kwa kweli wanashangaa na kupigwa na butwaa kuliko kawaida hata kusema;

"... ala, kumbe huyu mtu ndivyo alivyo? Kumbe tumekuwa tukidanganywa miaka yote hii huku ukweli ukiwa tofauti ..?"

Hili ndilo tatizo lao kwa Tundu Lissu...!!

3. Haya MAZOEA na utamaduni mbaya ndiyo uliokuwa katika majaribio ya kujengwa katika miaka hii mitano ya Rais Magufuli.

Na kiuhalisia yeye binafsi na wafuasi wake baadhi wachache, walishaamini kabisa kuwa wamefanikiwa na wanaweza kukaa kwenye viti vyao vya enzi milele kwa raha mustarehe.!

Kujitokeza ghafla kwa mtu mmoja jasiri wa kuanza kubomoa MAZOEA na UTAMADUNI huu mbaya kabisa kumewashitua. Kunawafanya wahahe, wawe desperate kujiokoa. Chochote kilichopo mbele yao cha kujiokoa, watakitumia. Iwe uongo au hata kumwaga damu ya mtu/watu..!!

Namna pekee ya kujitetea na kujaribu kuulinda au kuu - restore ni kubuni njia ya kunzuia. Kifo ndiyo ilikuwa option ya mwisho. Bahati mbaya kwao option hiyo ika - fail spectacularly!!

4. Kufeli kwa options zote ikiwemo ya kifo, ikawaweka katika "desperation state" watu hawa ktk namna ambayo pengine hawakurajia kabisa,kabisa..

Sasa kinachofanyika ni kutengeneza propaganda, wanazihalalisha kisha wanazitumia kama sababu za kuamuru vyombo vya mabavu hususani polisi kutumia nguvu zenye kusababisha maafa na uharibifu na maumivu makubwa kwa wafuasi wa mgombea huyu wanaomfuata kumsikiliza..!

Karibu kwa maoni na mtazamo wako wewe. Na wana CCM mnakaribishwa zaidi ya wengine kushiriki mjadala huu...
Mkuu CCM imefanikiwa kuongoza na kuwatawala watanzania kwa kuwa 70% ya watanzania ni wajinga Mtaji wa watawala ni elimu mbovu inayozuia mtu kujitambua, kutambua umuhimu wa siasa, uhuru na haki kuwa ndio tunu za taifa lenye maendeleo watanzana huona siasa ni kama ushabiki Simba na Yanga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom