GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,277
- 6,673
Licha ya kwamba watanzania wana matatizo mengi hasa ya kiuchumi na kisiasa bado tatizo la mapenzi, mahusiano na urafiki ni changamoto yao ya kila siku. Utashangaa nikikwambia kuwa MMU (Mapenzi, mahusiano na urafiki) ni kimbilio la walio wengi. Binafsi naweza kusema kuwa hili ni jukwaa bora likishika nafasi ya pili kwa pamoja na jukwaa la uchumi, Tech & gadgets Majukwaa haya matatu nayapa nafasi sawa kutokana na umuhimu wake. Jukwaa ambalo nalipa namba moja kwa umuhimu ni JF DOCTOR.
Lengo lak kuanzisha Thread hii ni kutaka kutoa pendekezo langu kwa wapenzi na washabiki wa jukwaa hili.
Kama utafuatilia vizuri post zinazokuja hapa utagundua haya yafuatayo.
Mwisho napenda kushauri kuwa tuache Lugha kali kwani kuna jukwaa maalum la mambo kama hayo.
NAWASILISHA.
Lengo lak kuanzisha Thread hii ni kutaka kutoa pendekezo langu kwa wapenzi na washabiki wa jukwaa hili.
Kama utafuatilia vizuri post zinazokuja hapa utagundua haya yafuatayo.
- Baadhi ya post zinazoletwa hapa jamvini si tu za kitoto bali pia zimeletwa na watoto hasa. Kama utafuatilia kiundani utakuta ni post za wanafunzi ambao bado wako shuleni na hawana haki na mambo wanayoyazungumzia.
- Wengi hunufaika kwa mawazo mbalimbali wanayoyapata hapa MMU ingawa wanapouliza hawaweki wazi kuwa hizo shida ni za kwao, utaona mtu akiandika kuwa hicho anachotaka msaada kimemkuta rafiki yake au jirani yake wakati ukweli yeye mwenyewe ndio muhusika, Hili sio baya ni maamuzi ya mtu kulinda P yake.
- Hili ni jukwaa ambalo linapunguza machungu mbalimbali ya kitaifa yanayotukabili.
- Hili ni jukwaa ambalo tofauti na SIASA ambako mara nyingi ni malalamiko ambayo hayapatikani ufumbuzi wake, huku ufumbuzi unaupata moja kwa moja licha ya utani na mbwembwe za hapa na pale ambazo muhusika hujua wazi kwamba kitu hiki ni utani.
- Kwenye siasa kuna watu wanakuwa wameshika mpini wakati sisi huku jukwaani tumeshika makali lakini MMU Mpini na makali vyote vipo kwako
Mwisho napenda kushauri kuwa tuache Lugha kali kwani kuna jukwaa maalum la mambo kama hayo.
NAWASILISHA.