Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Chadema wanatupeleka ile sehemu ambayo kila Mtanzania atakuwa anajua anaelewa kuna nini ndani ya nchi yake na kinachotaka kifanywe ni kitu gani ,ujumbe ambao Chadema wameufikisha si mdogo ni mkubwa sana ,naamini kabisa kuwa hivi sasa Ndani ya Taifa hili na pia nje ya mipaka yake watu wanauelewa mkubwa juu ya mabadiliko na mwamko wa kisiasa walionao WaTanzania.
Chadema kwa kutumia mitego na njia ambazo Chama tawala CCM na Serikali yake wanashindwa kuitambua ,CCM na Serikali yake wamenasa katika mtego wa Chadema ambao umegharimu maisha ya WaTanzania ,faida iliyopatikana ni kubwa sana na ndio chimbuko ya mambo ambayo yatakuja mbeleni kwa urahisi kabisa,tayari imeshajulikana kuwa utawala uliopo hauendeshi nchi kibinadamu ni unyama unyama tu ,hiyo ni faida kwa WaTanzania wapenda maendeleo na nchi yao ,walio ndani na wale waliopo nje.
Njia kama hizi ambazo Chadema imeanza kutumia ni njia za kubeba majukumu na viongozi nilazima wajue hivyo na ni lazima wawe wakiwaeleza wananchi kuwa panapopiganiwa haki na usawa ni lazima kutatokea patashika kwani sio rahisi kumpokonya mtu tonge inayoelekea mdomoni ,ni mapambano hivyo katika mapambano hayo maisha ya watu pia yanaweza kupotea na isichukuliwe kuwa Chama kinapendelea hivyo ila ni njia ambayo ni lazima tuipite ili kuiweka sawa Taifa hili la Tanzania, na pia watawala waliopo madarakani hawapo tayari kuachia utawala kwa wengine kwa njia za uadilifu hivyo njia za kupita ili kukabiliana nao zitacost even life kama nilivyosema.
Tukubalianeni tu kuwa njia ambazo Chadema inatupitisha ni njia zisizokuwa na tatizo katika kulikomboa Taifa hili na mkoloni mweusi.
Chadema kwa kutumia mitego na njia ambazo Chama tawala CCM na Serikali yake wanashindwa kuitambua ,CCM na Serikali yake wamenasa katika mtego wa Chadema ambao umegharimu maisha ya WaTanzania ,faida iliyopatikana ni kubwa sana na ndio chimbuko ya mambo ambayo yatakuja mbeleni kwa urahisi kabisa,tayari imeshajulikana kuwa utawala uliopo hauendeshi nchi kibinadamu ni unyama unyama tu ,hiyo ni faida kwa WaTanzania wapenda maendeleo na nchi yao ,walio ndani na wale waliopo nje.
Njia kama hizi ambazo Chadema imeanza kutumia ni njia za kubeba majukumu na viongozi nilazima wajue hivyo na ni lazima wawe wakiwaeleza wananchi kuwa panapopiganiwa haki na usawa ni lazima kutatokea patashika kwani sio rahisi kumpokonya mtu tonge inayoelekea mdomoni ,ni mapambano hivyo katika mapambano hayo maisha ya watu pia yanaweza kupotea na isichukuliwe kuwa Chama kinapendelea hivyo ila ni njia ambayo ni lazima tuipite ili kuiweka sawa Taifa hili la Tanzania, na pia watawala waliopo madarakani hawapo tayari kuachia utawala kwa wengine kwa njia za uadilifu hivyo njia za kupita ili kukabiliana nao zitacost even life kama nilivyosema.
Tukubalianeni tu kuwa njia ambazo Chadema inatupitisha ni njia zisizokuwa na tatizo katika kulikomboa Taifa hili na mkoloni mweusi.