Tuanzishe utaratibu huu

NGUVUMOJA

JF-Expert Member
Jul 1, 2011
1,347
325
Watanzania wenzangu, nashauri tuanzishe utaratibu wa form za kiapo kwa wagombea woote, hasa wagombea wa nafasi ya urais na ubunge.
Ahadi zote watakozozitoa majukwaani tunasema "OK FINE BUT PUT IN WRITING" Jaza ahadi zako zooote kwenye fomu ya kiapo tena mbele ya mashahidi, kisha fomu zote zinahifadhiwa Polisi.
Baada ya miaka mitano fomu zinatolewa na kuzipitia ahadi mojamoja.
Enhee, ulituahidi 1, 2 .....3. Je ulitimiza? kama hakutimiza FUNGA JELA MIAKA 30 NA KAZI NGUMU.
Nadhani hapatakuwa na wagombea uchwara tena katika nchi yetu.
Nawasilisha......
 
Kwa kweli hiyo iache iwe ndoto kwako hata nchi zinazoongoza duniani viongozi wao huwa wanakumbwa na mengi na wanashindwa tekeleza mengine kwa sababu... In short siasa hii

SASA UNGESEMA WAJIELEZE PESA WAMETUMIAJE ZA WANANCHI KAMA HUWA WANAPEWA KUFANYA HILI NA LILE AU PESA WANAOMBA KUSAIDIA MAJIMBO YAO AU ETC NDIO WAJIELEZE WAMETUMIAJE HAPO SAWA NITAKUELEWA AS HUO NI WIZI WA PESA ZA PUBLIC
 
Hilo lilitumika enzi za ukomunisti lakini karne ya sasa halina tija. Hili namna nzuri ya kulifanyia kazi ni kupitia mchakato wa katiba mpya ambapo tunatakiwa tusiache mwanya wowote kutowajibika kwa viongozi tunaowachagua. Hii ndiyo njia mwafaka ambayo ni ya kidemokrasia. Kwa hiyo tuchangie mawazo yetu tutakapoanza huo mchakato bila kukiuka haki za binadamu.
 
Wewe waache wajisahau adhabu yao ni kuwanyima kura kipindi kijacho. Miaka mitano sio mingi. Waulize wa iringa walimfanya nini Mama Mbega baada ya kujisahau?
 
Wewe waache wajisahau adhabu yao ni kuwanyima kura kipindi kijacho. Miaka mitano sio mingi. Waulize wa iringa walimfanya nini Mama Mbega baada ya kujisahau?<BR>
 
Back
Top Bottom