Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,115
Kesi ya inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake itaendelea katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, ambapo Ushahidi unaendelea kutolewa. Shahidi wa kwanza kwa upande wa Jamhuri ACP Kingai atamalizia Ushahidi wake.
========
Mawakili upande wa utetezi wapo katika chumba cha Mahakama
Watuhumiwa wote wamekwisha wasili katika ukumbi wa mahakama asubuhi hii
Jaji ameingia
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Imetajwa
Wakili wa Serikali: Ikupendeze Mh Jaji Naitwa Robert Kidando nimeongozana na
1. Chriss ........
2. Abdallah Chavula
3. Jenitreza akitali
4. Ester Martin Ignas
5. Mwinuka Tulimanywa Majige
Kibatala: ikukupendeza Mheshimiwa Jaji naitwa Peter Kibatala nipo pamoja na
; 1. Alex Massaba
2. Seleman Matauka
3. Sisty Aloyce
4. Dickson Matata
5. Michael Mwangasa
6. Jonathan Mndeme
7. Hadija Aron
8. Evaresta Kisanga
9. Maria Mushi
10. Idd Msawanga
11. John Malya
JAJI: upande wa Jamhuri
Wakili wa Serikali: Shauri limekuja kwa ajili ya Re examination kwa Shahidi wa Kwanza, Yupo na tupo tayari kuendelea.
Jaji: Upande wa Utetezi..?
Kibatala: Na sisi tupo tayari Mheshimiwa Jaji
Jaji: Umesema kwa niaba ya Wenzio Siyo.?
Kibatala: Ndiyo
Jaji: Mshitakiwa namba 1,2,3, na 4 Wanainuka Kila Mmoja Ishara kwamba wapo Mhakamani
Jaji: Shahidi Jana ulihojiwa Maswali ya Dodoso na Upande wa Utetezi, Leo tukasema utakuja kwa ajili ya Re examination, Nakukumbusha bado upo chini ya kiapo.
Wakili wa Serikali: Jana Mtobesya alikuuliza wakati gani Jalada la Uchunguzi Lilifunguliwa na wakati gani Jalada la Kesi lilifunguliwa
Shahidi: Jalada la Uchunguzi tulikuwa tumefungia Baada ya Kukutana na Luteni Denis Urio katak Ofisi ya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai.
Wakili wa Serikali: Na Jalada la Kesi
Shahidi: Nilifungua baada ya Mimi Kupata Taarifa kuwa Vijana walipokuwa wanatafutwa na Luteni Urio kwa Amri ya Mbowe ndipo tulifungua Jalada.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kuhusiana kama Ulikuwa na Taarifa ya kabla ya Kumchukua Maelezo Mshitakiwa wa Pili, Elezea ni taarifa gani.
Kibatala: OBJECTION swali lilikuwa kwamba Swala la Kumtafuta Moses Lijenje, Je Ulimuhoji Mshitakiwa wa Pili,"
Jaji: Wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa sijauliza alichofanya Cross examination yeye, nipo kwa Mtobesya
JAJI: Uliza tena
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu Kuwa na Taarifa za Moses Lijenje wakati unamuhoji Mshitakiwa wa Pili, Je ulijua Taarifa hizo kabla au Baada?
JAJI: Kibatala Umesikia Swali?
Kibatala: Nimesikia lakini kaniondoa Mimi, Sasa ni Eneo la Mtobesya
Shahidi: Nilipata Taarifa kuwa Freeman Mbowe alikuwa anatafuta Kundi la Waalifu
Kibatala: Wakili Mtobesya Hakufika huko, it's something New alisema alikuwa anatafuta Vijana
JAJI: Ndiyo namimi nimesikia hivyo Jana ulisema Alikuwa anatafuta Vijana siyo Kundi la Wahalifu
Shahidi: Ndiyo nilipata Taarifa kuwa Freeman Mbowe Alikuwa anatafuta Kundi la Vijana walioachishwa kazi Jeshini, Kwa dhumuni la Kudhuru Viongozi wa Serikali na Pia Mpango wa maandamano ya kushinikiza Viongozi ya siyo kuwa na Kikomo na Kwamba Lengo la Kufanya hivyo Nchi ........isitawalike na ionekane imefeli kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa hapa Jana Kwamba wakati Mshitakiwa Wa pili Kama Ulikuwa Umempa Onyo, kuhusiana na Ukamataji, wewe Ukasema ulikuwa umeshampa Haki zake. Haki zake zipi?
Shahidi: Haki zake ni Pamoja na Kumfahamisha Kosa alilokuwa anashitakiwa nalo na Kwamba....... halazimishwi Kusema lolote ila Jambo analozungumza linaweza Kutumika kama Ushahidi Dhidi yake Mahakamani.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kwamba Matukio ya Kula Njama Yalifanyika kati ya 01 May 2020 na tarehe 05 August 2020 lakini katika Ushahidi wako ulisema Kula Njama huku kulifanyika tarehe 25 July 2020 hadi tarehe 01 August 2020 huko Aishi Hotel. Unasemeje Juu ya Ushahidi .......wako Kupinga na Hati ya Mashitaka?
Shahidi: Naomba Kuona hiyo Hati ya Mashitaka
Jaji: Utetezi Mapingamizi Juu ya Hilo
MTOBESYA: Hapana apewe tu
Shahidi: Miye naona Hakuna utofauti bado, ipo kati ya (in between) bado
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali Kuhusiana Maelezo ya mshitakiwa wa Kwanza kwamba yaliandikwa Chang'ombe ukasema ndiyo Ni kweli Na Maelezo Mshitakiwa wa pili na watatu yalichukuliwa Central Dar es Salaam Eleza kwanini uliamuru Maelezo ya Mtuhumiwa wa Kwanza .......yachukuliwe Chang'ombe?
Shahidi: Kwanza Chang'ombe ni Dar es Salaam, Pili uwezi kufananisha na Moshi, Alafu pia na angalia Masaa Manne.
Utetezi: OBJECTION Mheshimiwa Jaji wamuelekeze Shahidi wao Vizuri hatutaki kila Saa Kusimama Simama.
Jaji: Jamhuri
Wakili wa Serikali: Shahidi Eleza sababu tu kwanini uliamuru Maelezo ya Mshitakiwa wa 01 yachukuliwe Chang'ombe?
Shahidi: Baada ya Mshitakiwa kudanganya kuhusu Makazi yake.
Utetezi: OBJECTION Mheshimiwa Jaji hayo ya Kudanganya ni Mapya Sheria ya Ushahidi ipo wazi haupaswi Kuongea Mambo Mapya
Jaji: Nafikiri shida ipo kwenye Neno Kudanganywa hata Mimi sikusikia Neno "Kudanganywa" ondoa hilo Neno uendelee
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kwamba Mshitakiwa wa Pili uliomuonya kuhusu Kula Njama ya kutenda Matendo ya ugaidi, kwanini hukumuonya na Makosa mengine
Kibatala: OBJECTION hayo niliuliza Mimi sikumuuliza kwanini Hukumuonya kila Shitaka, Nilikuwa nauliza kwa kila Kosa........Kama Mnataka twende hivyo tutaomba kumuhoji tena.
Jaji: Unasemaje wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: Nitarudia swali Mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali kuhusiana na Kuamini na Kutoamini hasa kwenye sababu ya Wakili.
Shahidi: Nilikuwa siamini kwamba Mkuu wa Wilaya anaweza Kushusha Bendera lakini pia ndiyo iwe sababu ya Kumdhuru Kiongozi wa Serikali. Lakini statement niliiamini sababu alitoa yeye.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Kupatiwa Kielelezo P1
Wakili wa Serikali: Shahidi chukua Karatasi hii Nitakuuliza maeneo ambayo ulihojiwa na Mawakili wa Utetezi
Wakili wa Serikali: Tafuta eneo ulikohojiwa kuhusiana Kumfikisha Mheshimiwa Mikocheni, ukipata nitakuuliza swali
Mahakama Bado Ipo Kimya Shahidi anatafuta
Wakili wa Serikali: Baada ya Kufika Dar es Salaam na Kumfikisha Mheshimiwa Mikocheni, hujaona
Jaji: Labda uchukue Kwanza wewe Usome halafu umuonyeshe.
Wakili wa Serikali: Kama hawatokuwa na pingamizi
Kibatala: Hatuna Mheshimiwa Jaji
Wakili wa Serikali: Soma hapa
Shahidi: Baada ya Kufika Dar es Salaam na Kumfikisha Mheshimiwa Mikocheni Mimi na Mohammed tulipewa Laki mbili mbili baada ya Kesho yake kuwa anakuja Lissu na hakumpokea.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuwa huyo Mheshimiwa ni nani ukasema sasa ieleze Mahakama Huyo Mheshimiwa ni nani?
Mtobesya: OBJECTION Mheshimiwa Jaji Kifungu cha 61 Cha Sheria ya Ushahidi Inasema Nyaraka Isitafsiriwe Bali Nyaraka ijieleze yenyewe, hapo Shahidi anaulizwa tafsiri.
Wakili wa Serikali: Naona hiyo Objection haina Mashiko sababu tutakuwa hatuna Cha Kufanya.
JAJI: Nafikiri Mtobesya Hoja yako inahusu Thamani ya Nyaraka, Sasa Mahakama itaangalia hicho anachokisema Kipo kwenye Nyaraka.?
MTOBESYA: Sawa Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Ni Mheshimiwa Mbowe, Kwa sababu Mheshimiwa aliyetajwa kwenye Statement hii ni Mheshimiwa Mbowe na Mbowe Mwenyewe anaishi Mikocheni
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia kuhusiana na Kupewa Laki mbili na Mohammed, huyu Mohamed med ni nani?
Shahidi: Ni Ling'wenya kwa sababu huko Juu tulikuwa tunazungumzia Mohamed Ling'wenya na statement hii alikuwa anatoa Mwenyewe.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali Kama kwenye Statement hiyo, kama alivyoelezea yeye kama Mshitakiwa Wa pili Kama alimfuatilia Sabaya katika Maeneo aliyokuwa akienda Arusha Uliulizwa swali wewe Ukasema Hapana, Sasa nitakupeleka kwenye Statement halafu utafafanua.
Kibatala: OBJECTION samahani Mheshimiwa Jaji labda kwa Maelekezo yako nitakubali Maelekezo ya Mahakama, anachoulizwa Shahidi Alisha Jibu kuwa Hakuwa Arusha anaulizwaje Jambo hilo hilo tena.
JAJI: Nafikiri Ngoja tusubiri swali lake.
Wakili wa Serikali: Kwa Utaratibu wa Mahakama Kibatala anapaswa aongee kwa Ushahidi Kama Kuna kitu kweli Umekiona Kitolee Ushahidi, Siyo kuja na Neno Una suspect, Nani kafanya na Kitu gani Kimefanywa
Jaji: Kibatala ulikusudia Nimuonye, na Tunachukulia una Taarifa za ......kiintelijensia kwamba tumuonye shahidi kwa Intelijensia yako. Kibatala: Mimi nimesema Mahakama imuangalie.
Jaji: Basi kwa sababu Mimi sijaona naomba Upande wa jamhuri waendelee Kuuliza Maswali
Shahidi: Katika Kufuatilia Nyendo za Sabaya tulienda Club Kokoriko lakini hatukumpata Mheshimiwa Sabaya Siku hiyo.
Wakili wa Serikali: Eleza sasa Kwenye Statement hii Kama Mshitakiwa alifika Club Kokoriko.
Shahidi: Alifika
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia swali kuhusiana kama Kuna sehemu yoyote kama Mshitakiwa Wa Pili amechukuliwa finger print katika Statement hii, NI kwanini katika Statement hii hakuna Maelezo ya Kuchukuliwa finger Print
Shahidi: Mimi kama Mchunguzi nilishaona Hakuna haja.....Ya kuchukua Finger prints
Shahidi: Hitaji la Kuchukua Finger Prints lilikuwa baada ya Kumpekua Mshitakiwa Namba Moja na baada kukuta Kijitabu ikabidi sasa Kuchukua Finger Prints. Wakati nachukua Maelekezo Mshitakiwa wa pili ilikuwa tarehe 07 August 2020 kabla ya Kupata Kijitabu hicho.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kama Ulichukua Sampuli za Finger Prints za Pistol inavyodaiwa kukutwa na Mshitakiwa wa Pili. Sasa wewe Kama Mchunguzi ni kwanini hukuchukua Finger Prints na Sampuli za DNA.
Shahidi: Mimi sikuona haja ya kuchukua Finger Prints kwa sababu.......Mshitakiwa tulikuwa naye, Tunafanya Finger prints kama Mshitakiwa amevunja na hayupo Sisi Hatukuwa na hitaji hilo kama alivyo uliza wakili.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kuwa Kwa kipindi Chote baada ya Kupata nia ya Uhalifu, kama ulimtaarifu Kiongozi aliyelengwa Ole Sabaya, kama ulimpatia taarifa. Ukasema hukumpati na wala Kamati ya Ulinzi ya mkoa wa Kilimanjaro, ni kwanini sasa.
Shahidi: Tulikuwa kuwa na....Uhakika wa Taarifa zetu, hatukuona sababu za kuwaambia Watu wengine kwa kuwa tunge Create Pressure.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Wakati Mtuhumiwa wa kwanza anakamatwa palikuwa na Askari Jeshi na Ukasema Hakukuwa na Askari Jeshi
Shahidi: Hapakuwa na Askari Jeshi kwa sababu Mimi Ndiyo nilikuwa Arresting Officer na Nikisaidiwa na Inspector Mahita pamoja na ASP Mahita
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusiana na Maandamano Ukasema ni Sheria Inaruhusu lakini kwa Kufuata taratibu eleza Unamaana gani?
Shahidi: Ni kweli Sheria Inaruhusu Maandamano lakini kuna Sheria zingine pia zinaweka taratibu kuwa kabla ya Kufanya Maandamano awe amepata kibali
Wakili wa Serikali: Kibali gani
Shahidi: Cha Polisi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali Kuhusiana na Mtu wa Pili katika Maelezo yake kuwa Mtu Mmoja anaitwa Kakobe, Ukasema ukabaini Kuwa Mtu huyo anayeitwa Kakobe ndiyo Moses Lijenje, eleza ni wakati gani ulibaini
Shahidi: Wakati tunawakamata Watuhumiwa walikuwa wawili......lakini tulikuwa tuna Taarifa wapo watatu, Tukiwauliza Yupo wapi Mwenzetu Wakasema anaitwa Kakobe ambaye ndiyo Lijenje.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali kuhusiana na Sheria ya Ushahidi Wakati wa Onyo Kuwa section one na Two hukuweka, Ukasema hiyo ni Curable, Ulikuwa unamaanisha nini.
Shahidi: Haiwezi Kuathiri Maelezo ya Kuonywa
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji tunaomba Tukomee hapa.
Jaji: anaandika Kidogo
JAJI: Upande wa Utetezi
Kibatala: Mheshimiwa Tumekubaliana kuwa hatuna Pingamizi lolote
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji tuna Shahidi Mwingine lakini Kabla ya Kuendelea naye tunaomba ahirisho fupi, Ikiwezekana tuweze Ku resume Saa 5:30.
Jaji: Maombi yanakubaliwa, tutarudi Mahakamani saa Tano na Nusu.
Jaji: Kama tumekukwaza Kwa niaba ya Mahakama naomba Radhi, Naomba Radhi kwa niaba ya Utetezi na Ninakushukuru Kwa Ushahidi wako.
Jaji anatoka Mahakamani
---------
JAJI anaingia
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021
Wakili wa Serikali Kidando: Wapo tayari Kuendelea na Mashahidi
Jaji: Upande wa Utetezi Mpo tayari
Kibatala: Tupo tayari kwa ruhusa yako Mheshimiwa
Jaji: Shahidi wa Pili
Wakili wa Serikali: Shahidi amefuatwa
Mahakama ipo kimya ina subiri shahidi aingie
Shahidi amefika
JAJI: Majina shahidi: JUSTINE ELIYA
Jaji: Umri wako
Shahidi: Umri 31, Kabila Mmeru, Dini Mkrito, Shughuli Mkulima
Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama hii kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa ni kweli, kweli tupu Eenheeeee Mwenye Mungu nisaidie
Wakili wa Serikali: Ataongozwa na Wakili wa Serikali Abdallah Chavula
Jaji: Karibu
Wakili wa Serikali: Nitakuwa nakuhoji Maswali utakuwa unajibu kwa Kuelekea kwa Mheshimiwa Jaji
Wakili wa Serikali: Majina yako yapi:
Shahidi: Justine Eliya Kaaya
Wakili wa Serikali: Bw Kaaya Kwa sasa Shughuli zako ni Zipi?
Shahidi: Kilimo na Biashara
Wakili wa Serikali: Kilimo cha aina gani
Shahidi: Cha Mboga Mboga na Nafaka
Wakili wa Serikali: Unamaanisha nini
Shahidi: Mboga Mboga Nyanya, Vitunguu na Karoti na Nafaka, namaanisha Mahindi na Maharage
Wakili wa Serikali: Shughuli hizi unazifanyia wapi
Shahidi: Arumeru Mkoani Arusha
Wakili wa Serikali: Wateja wako hasa ni wanunuzi wa hayo mazao ni akina nani?
Shahidi: Ni watu tofauti Watanzania na Wageni wanaokuja Mkoa wa Arusha
Wakili wa Serikali: Unazifanyia wapi
Shahidi: Mkoani Arusha, wilaya ya Arumeru, Longido na Wilaya ya Arusha Mjini.
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Mwaka 2017 wewe Maskani yako yaliku a ni wapi?
Shahidi: Nilikuwa naishi Longido
Wakili wa Serikali: Wilaya ya Longido ipo Mkoa gani
Shahidi: Arusha
Wakili wa Serikali: Hapo Wilaya ya Longido ulikuwa unajishughulisha na Shughuli zipi?
Shahidi: Kupiga Picha na Kilimo katika Wilaya ya Arumeru
Wakili wa Serikali: Mwaka 2017 ulikuwa unajishughulisha na Kilimo cha aina gani
Shahidi: Nilikuwa nalima Karoti
Wakili wa Serikali: Wateja wako walikuwa ni akina nani?
Shahidi: Waliotoka Sokoni na baadhi ya watu pale Arusha
Wakili wa Serikali: Tueleze sasa hii Shughuli ya Kupiga Picha nayo, Ni Shughuli gani?
Shahidi: Picha za Mnato kwa kutumia Camera na Simu
Wakili wa Serikali: Ulikuwa ukiwapiga akina nani
Shahidi: Viongozi wa Serikali na Viongozi wa Kisiasa
Wakili wa Serikali: Unaweza ukatuambia ni akina nani hasa
Shahidi: Dr. Steven Kemomo Kiruswa Mbunge wa Longido
Wakili wa Serikali: Mwingine
Shahidi: Mrisho Gambo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Gabriel Daqaro aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Na wengine wengi
Wakili wa Serikali: Hao umewataja wa Ki-serikali, Je wa kisiasa
Shahidi: Lengai Ole Sabaya
Wakili wa Serikali: Huyu Lengai Ole Sabaya ulikutana naye wapi mara ya kwanza?
Shahidi: Mwaka 2017 Uchaguzi Mdogo wa Marudio Jimbo la Longido, Akanitaka nikamsaidie Kupiga Picha katika Shughuli zake zingine Mbalimbali
Wakili wa Serikali: Nini Kilijiri wakati huo baina yako wewe na yeye?
Shahidi: Alikuwa Diwani wa Kata ya Kisambasha, Wilaya ya Arumeru alivutiwa na Upigaji wangu wa picha
Wakili wa Serikali: Alikutaka ukamsaidie Wapi?
Shahidi: Katika kata yake ya kisambasha, Wilayani Arumeru
Wakili wa Serikali: Ulipokea Vipi Ombi hilo
Shahidi: Nilimkubalia kwa kuwa ilikuwa ni fursa kwangu
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama baada kukubali lile Ombi Utaratibu wa Ufanyaji kazi wenu ulikuwaje
Shahidi: Longido ni Mbali, hivyo ilinipasa kuhama Longido na Kuhamia Arusha, Nyumbani Kwa Lengai Ole Sabaya, Sehemu Inaitwa Kibanda Maziwa SAKINA
Wakili wa Serikali: Ulifanya kazi na Ole Sabaya na kuishi kwenye Nyumba yake kwa muda gani?
Shahidi: Mwaka 2017 Mpaka Mwaka 2018 July Alipoteuliwa Kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai
Wakili wa Serikali: Wewe ulienda kuishi wapi baada ya Kuteuliwa?
Shahidi: Nilienda Kuishi naye Hai Mkoani Kilimanjaro katika Makazi ya Mkuu wa Wilaya
Wakili wa Serikali: Kwenye hiyo Nyumba ya Ole Sabaya ulikuwa ukiishi na nani?
Shahidi: Yeye Mwenyewe Sabaya na Mke wake Jesca
Wakili wa Serikali: Ulipokuwa ukiishi naye wewe hasa ulikuwa Ukifanya Shughuli zipi
Shahidi: Kufanya Shughuli zake ndogo Ndogo ikiwemo Kumpelekea Nguo zake Dry Cleaner, Ikiwemo Kumpelekea Chai na Chakula Ofisini Kila Siku.
Wakili wa Serikali: Katika hiyo Nyumba ya Mkuu wa Wilaya Hai, Lengai Ole Sabaya Ulikuwa ukiishi na nani?
Shahidi: Nilikuwa nikiishi naye, yeye Mwenyewe na Mke wake.
Wakili wa Serikali: Umeishi Pale kwa Muda gani?
Shahidi: Kutoka July 2018 Mpaka Mwezi wa 10, 2018
Wakili wa Serikali: Nini kilitokea?
Shahidi: Niliamua Kurudi Longido Kuendelea na Shughuli zangu Nyingine sababu nikiacha Mchumba na Kutaka Kusimamia Shughuli zangu zingine za Kilimo.
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama sasa Mwaka 2018 uliporudi Longido unaweza Kukumbuka watu gani katika Medani za Kisiasa Ulianza Kufanya nao Mawasiliano
Utetezi: OBJECTION, Quite Leading kwa Kutaka Kuuliza ni watu gani wa Kisiasa Ulifanya Mawasiliano nao.
Wakili wa Serikali: Shahidi hebu tuambie Ulifanya Mawasiliano na Watu Gani?
Shahidi: Siku Moja nikiwa nyumbani nilipigiwa simu kwenye simu yangu Airtel 0693006700 kutoka kwenye namba ya Airtel 0784779944 na Mtu aliyejitambulisha Kuwa ni Freeman Mbowe
Wakili wa Serikali: Akakwambia kitu gani?
Shahidi: Nilishtuka sana akaniuliza Ujambo?. Nikamwambia sijambo akasema anashida ya Kuniona
Wakili wa Serikali: Ukafanyeje?
Shahidi: Nikamuuliza Upo wapi, Akajibu yupo Arusha
Wakili wa Serikali: Ukajibu Kitu gani,
Shahidi: Nikamwambia Nipo Longido kwa sasa Siwezi Kuja kwa sababu ya Changamoto ya Usafiri
Wakili wa Serikali: Nini Kikatokea?
Shahidi: Akaniambia Chukua Gari Noah Gharama Nitakuja Kulipa Ukifika Arusha. Kwa sababu ya Ile hofu nikamwambia siwezi Kuja
Wakili wa Serikali: Hofu ya Nini?
Shahidi: Kwanza Nikiongozi Mkubwa lakini Pia sina Ukaribu na Yeye
Wakili wa Serikali: Baada ya Kumueleza hayo nini Kilitokea
Shahidi: Aliniambia Subiri nakupigia, akakata simu.
Shahidi: Baada ya Muda akaniambia nipo Njiani nakufuata Longido.
Wakili wa Serikali: Muitikio wako ulikuwaje?
Shahidi: Kwa kuwa alisema yupo Njiani nakuja nikasema wacha nisubiri nisingeweza Kumzuia
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama nini kilitokea
Shahidi: Baada ya Dakika 40 alinipigia Simu kuwa Njoo hapa Uwanja wa Mpira
Wakili wa Serikali: Uwanja wa Mpira wa wapi?
Shahidi: Ndani ya mji Mdogo wa Longido
Wakili wa Serikali: Baada ya Kumueleza hayo Ulichukua hatua zipi?
Shahidi: Nilichukua Bodaboda na Kwenda
Wakili wa Serikali: Tuambie yaliyojiri
Shahidi: Akunichukua Bodaboda Nikaenda mpaka Uwanjani, na Kukuta Gari inaunguruma
Wakili wa Serikali: Ilikuwa ni Majira ya Muda gani
Shahidi: Saa 3 Usiku
Wakili wa Serikali: Baada ya kukuta gari,
Shahidi: Akaniambia Sogea hapa kwenye Gari Kwa namba ile ile ya 0784779944, Akaniambia ingia Kwenye gari Chief acha Kuogopa
Wakili wa Serikali: Kwenye Gari kulikuwa Kuna watu wangapi?
Shahidi: Nilimkuta yeye na Dereva na Nyuma ya upande wa Dereva palikuwa na Mwanamke
Wakili wa Serikali: Alikwambia Dhumuni lake lilikuwa na Ujumbe gani?
Shahidi: Akaniambia kuwa Lengai anamsumbua Sana
Wakili wa Serikali: Lengai ni nani..?
Shahidi: Mkuu wa Wilaya ya Hai
Wakili wa Serikali: Endelea
Shahidi: Akataka nimpatie Taarifa na Shughuli anazofanya pamoja na Watu anaofanya nao kazi pale Hai
Shahidi: Nikamwambia haitowezekana, kwa sababu mimi Sipo tena kwa Sabaya
Wakili wa Serikali: Ulipomueleza haya, yeye alifanya nini?
Shahidi: Akaniambia yeye Kiongozi Mkuu wa Chama Cha Upinzani Kwenye Nchi hii, Hivyo atafanya Vyovyote vile anavyoweza ili nirudi kwa Sabaya Kuendelea na Kazi
Wakili wa Serikali: Muitikio wako Ulikuwa ni Upi?
Shahidi: Nikamwambia haitowezekana kwa sababu nimechagua Kufanya Shughuli zangu Binafsi
Wakili wa Serikali: Nini Kilitokea?
Shahidi: Akaniambia samahani kwa Usumbufu wa Kunisumbua na akanipa TSh Laki 3
Wakili wa Serikali: Nini kikaendelea?
Shahidi: Akaniambia ni za Usumbufu, Tutawasiliana
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea
Shahidi: Tuliagana na aliondoka
Wakili wa Serikali: Baada ya Yeye Kuondoka wewe Ulielekea wapi
Shahidi: Baada ya kushuka kwenye Gari nilimpigia Ole Sabaya simu lakini hakupokea simu
Wakili wa Serikali: Wewe Ulienda wapi sasa
Shahidi: Nilibakia pale pale kwenye Uwanja na Kumpigia Dr Steven Kiruswa na Kumueleza kilichotokea?
Wakili wa Serikali: Wewe sasa Ulienda wapi?
Shahidi: nilirudi Nyumbani Kwangu
Wakili wa Serikali: Ulirudi Vipi Nyumbani kwako
Shahidi: Niliita Bodaboda nikarudi Nyumbani Kwangu
Wakili wa Serikali: Ni wakati gani tena Ulikuja kuwasiliana na Mtu uliye mtaja kuwa ni Freeman Mbowe pale uwanjani?
Shahidi: Mwaka 2020 Mwanzoni alinipigia Simu kupitia Whatsap
Wakili wa Serikali: Kwa namba ipi?
Shahidi: Kwa namba ile ile ya 0784779944
Wakili wa Serikali: Alikuwa na ujumbe gani
Shahidi: Akasema tumepotezana sana Chief
Wakili wa Serikali: Alikupa ujumbe gani?
Shahidi: Akasema anataka tuonane
Wakili wa Serikali: Wapi?
Shahidi: Moshi, wakati huo nilikuwa Arusha
Wakili wa Serikali: We Ukasemaje?
Shahidi: Ngoja nimalizie Kumwagilizia Shambani huku nikishamaliza nitakuja
Wakili wa Serikali: Nini kilitokea Kutokana na ahadi yenu?
Shahidi: Baada ya Kumalizia Shughuli zangu nilipanda Costa na Kumpigia Simu Kwamba naenda
Wakili wa Serikali: Ulipanda Costa Kuelekea wapi?
Shahidi: Moshi Kilimanjaro
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama ukifika hadi wapi?
Shahidi: Baada ya Kumpa Taarifa kuwa Nipo kwenye gari akasema nishuke Machame road.
Wakili wa Serikali: Kwa namba ipi?
Shahidi: ile ile ya 0784779944
Wakili wa Serikali: Ulipomueleza akakupa Maelekezo yepi?
Shahidi: Akaniambia nishuke Machame Road
Wakili wa Serikali: Ipo wapi?
Shahidi: Ipo Wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro
Wakili wa Serikali: Tueleze sasa baada ya Kupewa Maelekezo hayo nini kilitokea?
Shahidi: Nilishuka kwenye Gari nikapiga tena simu
Wakili wa Serikali: Simu ipi?
Shahidi: Namba yake ile ile ya 0784779944
Wakili wa Serikali: Ulipompigia simu nini kilitokea?
Shahidi: Akaniambia ni subiri hapo nakuja
Wakili wa Serikali: Nini kilijiri?
Shahidi: Baada ya Muda akinipigia simu kuniambia, Umefika, umekaa Upande upi, Akaniambia Vuka kaa Upande wa Kulia.
Wakili wa Serikali: We Ulikutana na nini?
Shahidi: Palikuwa na Barabara ya kwenda Machame na Nyingine kwenda Arusha na Nyingine Moshi
Wakili wa Serikali: Nini kikatokea?
Shahidi: Ilikuja Gari aina ya Land cruiser V8 Yenye Mlingoti na Bendera ya Bunge ikiwa na Plate Namba zilizoandikwa KUB
Wakili wa Serikali: Nini kilitokea?
Shahidi: Ilisimama Upande wangu, ikashusha Kioo Upande wa Abiria, nikamuona Mwenyekiti akaniambia Panda
Wakili wa Serikali: Baada ya Kuambiwa Upande nini kili tokea?
Shahidi: Alishuka Mtu kutoka Siti ya Nyuma akaniambia pita nikaingia kwenye Gari
Wakili wa Serikali: Enheeeee
Shahidi: Ile gari ilienda Muelekeo wa Kwenda Machame, Baadae tukaingia sehemu ambayo nilikuja Kugundua Hotel ya Aishi
Wakili wa Serikali: Palikuwa na watu gani kwenye Gari?
Shahidi: Palikuwa na Dereva na huyo Mlinzi wake aliyenipisha nikaingia kwenye Gari
Wakili wa Serikali: Mahusiano yenu ya Dereva na huyo Mlinzi kabla ya Siku hiyo yalikuwaje?
Shahidi: Tulikuwa hatufahamiani
Wakili wa Serikali: Ulijuaje aliyekupisha kuwa ni Mlinzi wake
Shahidi: Baada ya Yeye Kunitambulisha kuwa ni Mlinzi lakini pia ni Diwani wa Kata ya kiboriloni
Wakili wa Serikali: Baada ya Dakika 08 Mlifika wapi Vile?
Shahidi: Hotel ya Aishi Machame Wakili wa Serikali: Wewe ulitambuaje
Shahidi: Sababu ya Kibao Kilichoandikwa Aishi Hotel
Wakili wa Serikali: Tueleze sasa yaliyotokea
Shahidi: Baadae tulishuka kwenye Gari Mimi, yeye na Yule Mlinzi wake
Wakili wa serikali: Mlivyoshuka nini Kiliendelea?
Shahidi: Tulielekea Upande wa Mgahawa
Wakili wa Serikali: Umekuwa ukielezea Yeye na Mlinzi wake. Mlinzi wake na Yeye nani?
Shahidi: Freeman Mbowe
Wakili wa Serikali: Baada ya kushuka kwenye Mgahawa
Shahidi: Akasema tuongee kidogo sababu anamikutano kwenye jimbo lake akaniambia niagize Chakula
Wakili wa Serikali: Muda huo ilikuwa saa ngapi?
Shahidi: Saa Saba Mchana
Wakili wa Serikali: Wakati anakutaka Mkutane Moshi ilikuwa ni Saa Ngapi?
Shahidi: Saa Mbili Asubuhi
Wakili wa Serikali: Wewe Safari yako Kuelekea Moshi ulianza Saa ngapi?
Shahidi: Saa Tano kasoro
Wakili wa Serikali: Ulianzia wapi hiyo saa Tano kasoro
Shahidi: Sehemu inaitwa Kilala Wilaya ya Arumeru
Wakili wa Serikali: Alikwambia nini sasa?
Shahidi: Akauliza Mnampango gani Juu ya Mkutano inayoendelea Jimboni
Wakili wa Serikali: Jambo gani lingine alikwambia
Shahidi: Akaomba nimtajie wale wasaidizi wa Sabaya alipokuwa anatembea nao
Wakili wa Serikali: Wewe ulimwambia nini
Shahidi: Nilimwambia sina Taarifa yoyote ya kumwambia kwa wakati ule
Wakili wa Serikali: Nataka kuhusu hayo Majina
Shahidi: Nikimtajia Majina na Yule Diwani akawa anaandika kwenye Kikaratasi
1.Japhet Rwendela
2.Vedastus sibula
3.Mtoto wa Mkulima
4.Sylvester Nyegu
5.Binti wa kichaga
6.Mwalimu Doreen
7.Watson Malimumgu
JAJI: Mtoto wa Mkulima na Binti wa Kichaga ni Majina?
Shahidi: Ndiyo Majina nilivyokuwa nayafahamu wanayatumia kwenye Mitandao
Wakili wa Serikali: Kipi Kingine alikueleza
Shahidi: Nilitoa hizo namba kwenye simu niliwatajia Wakaziandika
Wakili wa Serikali: Lipi lingine alikueleza
Shahidi: Akasema atashughulika nao tutawasiliana na Wewe na Mimi baadae
Wakili wa Serikali: Nini kilitokea Baina yako wewe na yeye?
Shahidi: Akaniaga kasema atanitumia Chochote jioni
Wakili wa Serikali: Ulisema Chochote umaanisha nini?
Shahidi: Gharama zangu za Nauli
Wakili wa Serikali: Ilikuwaje baada ya hiyo ahadi
Shahidi: Hakutimiza hiyo ahadi na pia hakunitafuta baada ya pale
Wakili wa Serikali: Baada ya Makutano yenu pale Aishi Hotel wewe ukielekea wapi?
Shahidi: Nilirudi Arusha
Wakili wa Serikali: Ni wakati gani Mwingine uliwasiliana na Mbowe?
Shahidi: Mwezi 07 Mwaka 2020
Wakili wa Serikali: Tarehe ngapi?
Shahidi: Sikumbuki tarehe
Wakili wa Serikali: alikutafuta kwa namna gani
Shahidi: Alinipigia kwa Njia ya Mtandao wa Whatsap
Wakili wa Serikali: Kwa namba ipi
Shahidi: 0784779944
Wakili wa Serikali: ujumbe wake ulikuwa nini
Shahidi: Nipo Dar es Salaam nakuja Moshi, Naomba tuonane Nina Jambo la Kuzungumza na wewe
Wakili wa Serikali: Wakati huo wewe ulikuwa wapi
Shahidi: Shambani Kwangu Maji ya Chai
Wakili wa Serikali: Majira ya Saa ngapi
Shahidi: Mchana wa Saa Nane
Wakili wa Serikali: Ulichukua hatua zipi baada ya Ujumbe huo
Shahidi: Nikafanya Shughuli zangu, nikaanza Safari ya kwenda Moshi
Wakili wa Serikali: na ulienda Moshi kwa aina gani ya Usafiri
Shahidi: nikipanda Basi la Kilimanjaro Kutokea singida
Wakili wa Serikali: ahadi ilikuwa Mkutane Majira gani
Shahidi: alisema Saa 1 atakuwa amefika Moshi
Wakili wa Serikali: baada ya Kupanda Basi la Kilimanjaro ulifikia wapi
Shahidi: Moshi stendi
Wakili wa Serikali: wakati unashuka ilikuwa Majira gani
Shahidi: Saa 1 Usiku
Wakili wa Serikali: ikawaje
Shahidi: nilimpigia Simu Freeman Mbowe kuwa nimefika
Wakili wa Serikali: Kwa namba gani
Shahidi: 0784779944
Wakili wa Serikali: akasemaje
Shahidi: nichukie Pikipiki nimfuate Keys Hotel
Wakili wa Serikali: Baada ya Maelekezo hayo nini kilitokea
Shahidi: Niliita Bodaboda Nikaenda Hadi Keys Hotel na baada ya Kufika Keys Hotel nikampigia Freeman Mbowe kwamba Nimefika
Wakili wa Serikali: Kwa namba ipi
Shahidi: 0784 779944, Nikamwambia nimefika, Akasema namtuma Msaidizi wangu anifuate
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo nini kilitokea
Shahidi: alikuja Dereva wake ambaye namtambua kwa Jina Moja la Willy
Wakili wa Serikali: Nini hasa kilikufanya Umtambue
Shahidi: Siku nakutana naye kwa Mara ya Kwanza Machame ndiye aliyekuwa anamuendesha na Alinitambulisha
Wakili wa Serikali: Kule Nyuma ya Hotel Ulipoenda, Nyuma ya swimming ukikutana na Jambo gani
Shahidi: waliniambia Mheshimiwa Yupo Kwenye Kikao, Tukae hapa tukiwa tunasubiria amalizie Kikao
Wakili wa Serikali: ukiacha wewe na Dereva nani Mwingine Mlikaa naye
Shahidi: tulikaa na Mlinzi wake alikuwa baunsa baunsa Kidogo
Wakili wa Serikali: Ulifahamu Vipi huyo Baunsa baunsa ni Mlinzi wake
Shahidi: Willy aliniambia, huyo ni Mlinzi wa Mheshimiwa usiwe na wasi wasi
Wakili wa Serikali: nini kiliendelea hapo Mlipokuwa mmekaa
Shahidi: tulikula baada ya kula Mlinzi wake akaenda Kule alipokuwa Mwenyekiti Freeman Mbowe, na baada ya muda alirudi na Kusema tunaondoka
Wakili wa Serikali: Wewe SHAHIDI ulijuaje Kuwa Kule alipo Mwenyekiti ndipo alikuwa Mwenyekiti
Shahidi: Ilikuwa ni sehemu ya wazi tulikuwa tumetengenishwa na Swimming Pool
Wakili wa Serikali: tueleze wakati hayo yanatokea ilikuwa ni Majira ya saa ngapi
Shahidi: Saa tatu kasoro Usiku
Wakili wa Serikali: aliporudi na kuwaambia sasa mnaomdoka, nini kilitokea
Shahidi: Tulinyanyuka wote na kuelekea Kule alipo Freeman Mbowe
Wakili wa Serikali: tueleze wakati hayo yanatokea ilikuwa ni Majira ya saa ngapi
Shahidi: Saa tatu kasoro Usiku
Wakili wa Serikali: aliporudi na kuwaambia sasa mnaomdoka, nini kilitokea
Shahidi: Tulinyanyuka wote na kuelekea Kule alipo Freeman Mbowe
Wakili wa Serikali: Mlipoelekea huko alipokwepo Mwenyekiti nini Kilitokea
Shahidi: akatuambia pole sana kwa kutuweka, Baada ya muda Mlinzi wake akatufungulia Mlango wa Gari, Naye Mwenyekiti akaingia kwenye gari na nyuma ya Dereva akaingia aliyekuwa mlinzi wa Chadema Joyce Mukya
Mimi NikaKaa Katikati na Nyuma akakata Mlinzi wake
Wakili wa Serikali: Mlielekea wapi
Shahidi: tukitoka keys Hotel tukaelekea Mwelekeo wa Arusha
Wakili wa Serikali: iliwafikisha wapi
Shahidi: Aishi Hotel
Wakili wa Serikali: We Ulijuaje Kuwa Mmefika Aishi Hotel
Shahidi: nilishafika pale, haikuwa mara ya kwanza
Wakili wa Serikali: nini Kilitokea
Shahidi: aliwaambia watangulie ndani sisi tuna Kikao kifupi
Wakili wa Serikali: Kikao Kifupi mlifanya nani na nani
Shahidi: Freeman Mbowe, Mlinzi wake. Dereva alipotaka Kujumuika akamwambia hiki Kikao ni Cha watu watatu
Wakili wa Serikali: Hebu tuambie sasa, Mahusiano yako na Huyu Mtu unayesema ni Mlinzi, kabla yakikuwaje
Shahidi: nilikuwa sifahamiani naye
Wakili wa Serikali: Kwenye hicho Kikao mliongea Maswala gani
Shahidi: alinitambulisha kwanza kuwa Huyu ni Mlinzi wake anaitwa Khalfani Bwire na Msiri wake na hivyo niwe huru Kuzungumza naye
Wakili wa Serikali: yeye Mlinzi alikuwa wapi
Shahidi: tulikuwa tumekaa naye Upande wa kushoto
Wakili wa Serikali: Kikao chenu Mlizungumza Mambo yepi
Shahidi: alikuwa ananiambia nitaje tena Majina ya wale Vijana na Namba zao za simu na kazi wanazozifanya kwa Sabaya
Wakili wa Serikali: Wewe baada ya kukutaka Ufanye hivyo Ulichukua hatua gani
Shahidi: Kabla ya kuanza kuwataja nikamtaka Mlinzi wake akachukue kalamu na Karatasi ilituweze kuandika
Wakili wa Serikali: Baada ya hayo Maelekezo ikawaje
Shahidi: alirudi na kalamu na Karatasi Nikaanza Kuziandika
Wakili wa Serikali: Wewe Majina na namba za Simu za hao watu wewe ulizitoa wapi
Shahidi: nilikuwa nawafahamu tangu nafanya kazi kwa Sabaya
Wakili wa Serikali: hizo namba za Simu ulizitoa wapi wewe
Shahidi: nilizitoa kwenye simu
Wakili wa Serikali: Majina ya akina nani shahidi:
1. Japhet Rwendela
2. Vedastus sibula
3. Mtoto wa Mkulima
4. Sylvester Nyegu
5. Binti wa kichaga
6. Mwalimu Doreen
7. Watson Malimumgu
8. Enock kirigiti
Baada ya pale aliniambia nimtajie sehemu anazopenda kutembelea Mheshimiwa Sabaya
Wakili wa Serikali: Ulimtajia Sehemu gani
Shahidi:
1. Cocoriko Annex iliyopo Arusha
2. Cocoriko ya kijenge
3. The Don, Ipo karibu na Tanzania Breweries
4. Milestone Park iliyopo Sakina
Na hotel anazolala Sabaya
1. SG resort Iliyopo Sakina Arusha
2. Golden Crest Hotel ipo Arusha
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama baada ya kuwa wewe Umetoa Taarifa hizi ulifanya nini
Shahidi: Nilimuuliza mwenyekiti haya Majina na hizi sehemu unataka za Nini?
Akaniambia hilo niachie Mimi kazi yako hapa Imeisha.
Wakili wa Serikali: Lingine nini lilijitokeza baada ya mazungumzo yake
Shahidi: akaniambia nimkabidhi Khalfani Bwire Yake majina, Khalfani BWIRE akasema huyu Sabaya ni Mtu Mdogo sana Nitamchezesha. Baada ya pale Mwenyekiti akaniambia kazi Ndiyo inaanza rasmi kuanzia sasa hivi nitakuwa na Kulipa Mshahara
Wakili wa Serikali: ilikuwa ni Majira ya saa ngapi
Shahidi: Takribani saa 4 usiku
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama wewe baada ya yale Mazungumzo Ulielekea wapi
Shahidi: alisema wewe utapewa Chumba utalala hapa baada ya muda kuwa Umekwenda
Wakili wa Serikali: kingine
Shahidi: ilibidi nilale kwa sababu nisingepata Usafiri wa Kwenda Arusha
Wakili wa Serikali: nini kilifuatia
Shahidi: Kesho yake Asubuhi alinipatia TSh Laki Mbili kwenye namba yangu ya 0754916666 kutoka Airtel Money yenye namba 0784 779944.
Wakili wa Serikali: baada ya hapo Ulielekea wapi
Shahidi: Nilirudi Arusha kuendelea na Kazi zangu za Shambani
Wakili wa Serikali: Ni wakati Mwingine upi tena Ulikuja kuwasiliana tena na Mwenyekiti
Shahidi: hatukuwasiliana tena kwa sababu tarehe 25 August 2020 nilikamatwa na Askari wa Jeshi la Polisi
Wakili wa Serikali: Ulikamatiwa wapi
Shahidi: Makumira, Wilaya ya Arumeru nikiwa napanda CRDB, USA RIVER
Wakili wa Serikali: ulikuwa unapelekea CRDB pesa za Nini?
Shahidi: Nimetoka Kuuza Mazao Shambani
Wakili wa Serikali: Mazao gani
Shahidi: Karoti
Wakili wa Serikali: Ulikuwa umewauzia watu gani
Shahidi: Watu wa Mount Meru, wao walikuwa wanapeleka Game site huko Ngorongoro
Wakili wa Serikali: ulikuwa na Kiasi gani
Shahidi: Dollar za Kimarekani 1100 na TSh Millioni Moja Laki Moja na Kumi na Saba Pamoja na Euro 240
Wakili wa Serikali: baada ya Kumatwa nini Kilifuata
Shahidi: Nilikamatwa nikapakizwa Kwenye gari ni kapeleka Kituo Kikuu cha Arusha
Baada ya Lisa Moja Nilienda Kupekuliwa Nyumbani kwangu
Na Baadae Kusafirisha Kuletwa Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama zile pesa zako zilikuwa wapi
Shahidi: zilikuwa Mikono Mwa Askari pamoja na Simu zangu
Wakili wa Serikali: ilikuwaje hizo fedha
Shahidi: walinipekua kutoka katika mifuko yangu wakasema ni Noti bandia
Wakili wa Serikali: walipokukamata walikueleza wanakukamata kwa Makosa gani
Shahidi: Kwamba Nina tuhuma za kujihusisha Kula njama za kufanya Vitendo Vya ugaidi
Wakili wa Serikali: tueleze sasa Ulipofikishwa Dar es Salaam nini kilikusibu
Shahidi: Baada ya kufikishwa kituo cha polisi Dar es Salaam nilifanyiwa mahojiano na afande Mahita
Wakili wa Serikali: baada ya Mahojiano
Shahidi: Niliweka lockup Mpaka nilipofikishwa Mahakamani Kisutu
Wakili wa Serikali: Mahakamani Kisutu Ulipofikishwa ulifikishwa kwa sababu zipo
Shahidi: nilifungukiwa mashitaka Mbalimbali ikiwemo Kushiriki Vikao Vyakutenda Mambo ya kigaidi, Kula Njama za kutenda ugaidi, Kesi ya Utakatishaji wa Fedha
Wakili wa Serikali: Eleza Mahakama sasa Kwa kuanza na Khalfani Bwire we ulikutana naye wapi kabla ya Kuunganishwa naye
Shahidi: Nilikutana naye akiwa Keys Hotel na Aishi Hotel akiwa na Freeman Mbowe
Wakili wa Serikali: VIPI kuhusiana na Mohammed Ling'wenya
Shahidi: huyo sifahamu nilikutana naye Mara ya Kwanza Gerezani
Wakili wa Serikali: VIPI kuhusiana na Adam kasekwa
Shahidi: huyo simfahamu pia
Wakili wa Serikali: baada ya kuwa umeunganishwa kwenye kesi hiyo Mahakama ya kisutu ulipeleka wapi
Shahidi: Nilipelekwa Gereza la Ukonga
Wakili wa Serikali: ulikuwa na akina nani
Shahidi: kila mtu alikuwa na wing yake, Nilikuwa na Khalfani Bwire na baadae kaongezeaka Mtu anaitwa a Khalid Athuman na Baadae akaongezeka Mohamed Ling'wenya akitokea Segerea
Wakili wa Serikali: Umekuwa kwenye kesi ile kwa muda gani
Shahidi: Kwa Miezi 11
Wakili wa Serikali: Nini kilitokea Shahidi: aliletwa Mheshimiwa Mbowe Siku ya 26 July 2021 alitukuta tukiwa na Khalfani Bwire, akasema Poleni sana Nimekuja kuwatoa.
Wakili wa Serikali: Baada ya Kauli hiyo nini Kilitokea
Shahidi: Asubuhi watu wa Magereza walikuja Kusema tujiandae tunaenda Mahakamani Kesho yake 27 July 2021 tulipelekwa Kisutu Mbele ya Hakimu Mzee Simba Mimi, Khalid Athuman (Mshitakiwa 05) na Gabriel Muhina (Mshitakiwa wa 6)
Mwanasheria akasema bada ya Upelelezi, Sisi hatuhusiki kwa hiyo tumefutiwa mashitaka kwa kifungu kidogo Baada ya pale niliondoka kutoka Mahakamani kwenda kwa Mdogo wake Kitunda Kesho yake nikarudi Mahakamani Kwa Mwendesha Mashitaka Kuuliza Vitu vyangu
JAJI: ni sehemu ya Ushahidi wenu kwamba alienda Mdogo
Wakili wa Serikali: Hapana Mheshimiwa
Shahidi: Kesho yake nilipoenda Kisutu Kuuliza Utaratibu wa fedha zangu wakanielekeza niende Central Police Dar es Salaam Nikaenda Kuonana na Inspector Swila akaniandika Maelezo baada ya Kuniandika a maelezo akanipa Vitu Vyangu
Wakili wa Serikali: Umemtaja Mtu anaitwa Freeman Mbowe, Khalfani Bwire, Mohamed Ling'wenya, Just unaweza Kuwatambua
Shahidi: Ndiyo, wapo hapa mahakamani
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba sasa awatambue Hapa Mahakamani
JAJI: Utetezi
Kibatala: Hatuna Pingamizi
SHAHIDI anatembea anaenda Kumtaja Kila Mmoja kwa Jina Lake
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji siye ni hayo tu
JAJI: upande wa Utetezi
Jaji: mkizingatia ni Muda wa Mapumziko
Kibatala: tunaweza za Kushauriana nao?
Jaji: sawa Kibatala" tunapendekezo kwamba tukuombe Tu-break Kwa Dakika 30
Jaji: Saa 8:25 tutarudi tena Kuendelea
Jaji anatoka.
Jaji amerudi
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021, inatajwa
Jamhuri Kolamu yao ipo Vile vile
Upande wa Utetezi Kolamu yao Ipo Vile vile
Utetezi: wanaomba wanamtambulishe na wamjumuishe Wakili Nashon Nkungu Kwa sababu alikuwa Mahakama Kuu kwenye kesi Nyingine Asubuhi ya Leo.
Jaji: Sasa tulikuwa tumebakiza Upande wa Cross examination na ningependa Kuanza na wakili wa Mshitakiwa namba Moja
MTOBESYA: Nitakuwa sahihi nikisema kwamba katika Ushahidi wako hukutoa uthibitisho Wako wako kwamba Ulikuwa Ukifanya kazi kwa Ole Sabaya
Shahidi: Siyo sahihi
Mtobesya: Mwambie sasa Mheshimiwa Jaji ni uthibitisho upi Umetoa Mbele ya Mahakama hii
Shahidi: Muulize Mheshimiwa Mbowe ndiyo atakwambia kama nilikuwa nafanya kazi.
Jaji: Mbowe siyo shahidi
Jaji: labda Wakili urudie swali
Mtobesya: Ni sahihi Kwamba umesema ulikuwa unafanya kazi na Ole sabaya
Shahidi: sahihi
MTOBESYA: ni sahihi sasa kwamba Hukutoa chochote Mahakamani Kuthibitisha
Shahidi: Ndiyo sikutoa
Mtobesya: Umesema katika Ushahidi Wako kuwa ulikuwa unasafikiri Kutoka Longido kuja Moshi na kutoka Arusha Kuja Moshi ulikuwa unatumia Usafiri gani
Shahidi: Usafiri wa Umma
MTOBESYA: Ni matumaini yangu kuwa Ulipanda Basi la Umma unapewa Ticket
Shahidi: inategemea na hilo Basi
MTOBESYA: Mwambie Sasa Mheshimiwa Jaji kwamba wewe hukutoa Ticket
Shahidi: Si kutoa Ticket kwa sababu nilipandia Njiani.
MTOBESYA: kwa hiyo nipo sahihi kwamba huku safiri kwa sababu hukutoa Ticket wala Uthibitisho Wako wowote hapa Mahakamani
Shahidi: Siyo sahihi, Siyo lazima uwe na Ticket kuthibitisha.
Mtobesya: Okey Tunashukuru
Mtobesya: Tangu Ukutane na Mbowe Mpaka Unakutana na Inspector Swila ni Muda umepita
Shahidi: Umeuliza Swali siyo Sahihi
JAJI: ukuliza na Mawakili wa Serikali Wamenyamaza na Mahakama haijaingilia Ujue hilo swali ni sahihi, utatakiwa ujibu. kama hufahamu Shahidi Jibu sifahamu.
Mtobesya: Tangu huyo unayemuita Mbowe Mkutane ni Muda gani umepita
Shahidi: Mwaka moja na Nusu
Mtobesya: Kuna lolote alikuachia afande Swila baada ya kukuandika Maelezo
Shahidi: Hakuna aliloniachia baada ya Kuandika Maelezo akanipa Vitu vyangu nikaondoka
Mtobesya: kwa hiyo swila hakukwambia kwamba Siku Moja Maelezo yako anayoandika yatatumika kama Ushahidi
Shahidi: Hakuniambia
Mtobesya: alichokiandika Alikupa ukakisoma
Shahidi: Ndiyo alinipa nikasoma
Mtobesya: Ukajiridhisha Kwamba ulichokisema ni sahihi
Shahidi: ni sahihi, Ndiyo
Mtobesya: Hakuna Wakati alikwambia kuwa Umpatie kila kitu, umwambie unakijua
Shahidi: Hapana
Mtobesya: Unauhakika ulichoandika ndicho Ulichosema Leo Mahakamani
Shahidi: Ndiyo hichohicho
Mtobesya: Kwa Bahati nzuri sisi Mawakili wa Utetezi tuna nafasi ya Kupewa Nyaraka za Maelezo mliyoandika Mheshimiwa Jaji naomba nipewe Original Document ya hii, Na Msingi wangu wa Kuomba Ni Kifungu cha 164 cha Sheria ya Ushahidi
Mawakili wa Serikali Hatuna Pingamizi Mheshimiwa Mtobesya anatembea Kumfuata Shahidi alipo
Mtobesya: pitia Nyaraka hii Kama ndiyo Swila aliyoyaandika na Kama Ulikubali kuwa sahihi
Shahidi: Haya Ndiyo Maelezo yangu ya Kwanza
Mtobesya: Unaweza Kusoma?
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Soma tarehe kisha soma Mtu aliyeandika ni nani
Shahidi: Ndiyo haya
MTOBESYA: naomba Nikuulize kuhusu hii Statement yako dhidi ya Ulichokisema Leo 1. Nionyeshe kwenye hiyo Statement sehemu ilivyoandikwa kwamba huyo uliyemuita Mheshimiwa Mbowe kuwa yule alikuwa Mlinzi wake na Msiri wake
Wakili wa Serikali: OBJECTION Kwa Mujibu wa Kifungu cha 154 anatakiwa a Muonyeshe Shahidi hicho analichokisoma, yeye amefanya Vice versa
Mtobesya: Sijapata Msingi wa Objection ya Ndugu yangu Robert Kidando Nilianza Kutengeneza Msingi kwa Kuuliza Je alichokisema hapa ndiyo kilichopo kwenye Statement, Sasa Kama anataka twende hivyo tutaenda
Jaji: Hapana tuwasaidie Wateja wetu
Wakili wa Serikali: Provisory Mstari wa Nne ndiyo inakataza
JAJI: tueleze Nyie Mmelewa nini
Wakili wa Serikali: Maamuzi ya Kifungu Hichi Yametolewa Uamuzi na Mahakama ya Rufaa katika kesi ya Lilian Otesi Vs Jamuhuri, namba 77 katika Rufaa ya Jinai ya Mwaka 251 Mwaka 2008 katika Mahakama Ya Rufaa. Katika kesi hii Ukurasa wa 25 Mahakama ilisema yafuatayo; Kinachozungumzwa pale ni sawa na Kifungu namba 154 cha Sheria ya Ushahidi Kama Kilivyo gawanyika Maeneo Mawili Eneo la kwanza, Shahidi anaweza Kudodoswa kupitia Maelezo yake aliyoyaandika Nyuma Eneo la Pili anaweza Kuhojiwa kuhusu Maswala yake hayo hayo bila Kumuonyesha Maelezo yake Lakini kama anadhamiriwa kumpima Mkanganyiko wake shahidi, Kuna Utaratibu unaotakiwa Kufuatwa. Na hivyo kabla ya a kuthibitisha amuelekeze kwanza, Tofauti na Yeye kaenda na Kumfuata
Mtobesya: Rafiki yangu anarejea Vifungu viwili Tofauti Walitaka hayo ningefika huko kwa sababu hata a kesi ya Alberto Mendez imejadili hayo na Mimi nilikuwa ni sehemu ya Ile kesi. Kwa hiyo nafahamu ninachofanya.
Wakili wa Serikali: kifungu 164 hakisimami Pele yake, Kusimama kwake kunatemegea Kifungu cha 154 Na huo ndiyo Msimamo wa Mahakama
Mtobesya: Tusaidiane Mheshimiwa Jaji dhumuni la Kifungu cha 164 ni Kumchanganya (contradict) Shahidi
Wakili wa serikali: Mimi nilikuwa nimeanza Kwenye kifungu cha 154,Sikuwa nimefika huko
Jaji: wao wanasema Wana hukumu ambayo wanaweza Kutu Supply, nafikiri ni Vyema basi tuweze Kuona tu
Mtobesya: hili swala linaweza Kuibuka tena Mbeleni tunaomba Liwe Cleared kabisa na Mahakama
Wakili wa Serikali: tunaomba Dakika 15
Jaji: sawa tunaahirisha Kwa Dakika 15
Unaachiwa huru kwa masharti ya kuja kutoa ushahidi wa uongo Tangu lini Machame ikawa Wilaya ya Moshi.
Jaji bado hajarejea mpaka sasa
Jaji Kaingia
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 imetajwa
Robert Kidando: Kolamu yao Ipo Vile vile na anasema wapo tayari Kupokea Maelekezo ya Mahakama
Jaji: Muda Mfupi wakati wa Dodoso na Upande wa Utetezi, Upande wa Utetezi waliomba Mahakama iruhusu itoe Maelezo yaweze Kutumika kwa Nakala halisi p4 Baada ya Mawakili wa Utetezi Kusimama Upande wa Serikali Walisimama na Kusema Utaratibu haukufuatwa
Jaji: Baada ya hapo pande zote zilisema kuna Maamuzi nikaomba Maamuzi hayo
1. Nyaraka inatakiwa itolewe, hilo limeshafanyika
2. Nyaraka hiyo inapaswa Isomwe Katika Maeneo anayotaka Kumuuliza Maswali Ili Kumcontradict
Jaji: Mahakama hii inasema Kwakuwa huo ndiyo Utaratibu basi Unatakiwa Ufuatwe na Kuendelea na Shughuli Wakili wote wanasimama na Kushukuru ishara ya Kukubaliana Maamuzi ya Jaji.
Mtobesya: Anarudi kwa Shahidi na anaomba Mahakama Impatie tena Nyaraka anaweza kuisoma Shahidi anaanza Kusoma Alishawahi KUWA Msaidizi wa Katibu wa CCM Longido Amesomea Hotel Management Alishawahi Kufanya kazi na Sabaya kama Msaidizi wake Na aliacha kazi kwa Sabaya kwasababu alitaka Kurudi Longido na alienda kwa ajili ya Kumfuata Mchumba wake Anarudia kuwa alipigiwa simu na Freeman Mbowe, Kwamba alifuatwa Longido. "Freeman aliniambia kuwa nilitumia Elfu 50 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Hai Mama Helga na kumtomgoza
Shahidianaendelea kusoma: Nilishangaa Sana Kwamba alijuaje kwa sababu ilikuwa ni kweli nilimtomgoza Alinipigia Simu Tukutane Moshi Alinipigia niende Keys Hotel Na Siku Nyingine tulienda Aishi Hotel
Mtobesya: Soma eneo linalosema Mimi nilikwenda Kwa Kutumia Nauli yangu. Umeona?
Shahidi: anapekua
Shahidi: Mimi nilikwenda Kwa Kutumia Nauli yangu, na Nilipofika alikuja Kunichukua
Mtobesya: Eleza Mahakama Kwamba huyo Mlinzi alikuwa Diwani wa Kiboriloni
Shahidi: Nilisema
MTOBESYA: elezea Sasa hapo Katika Maandishi yako humo kuna Mlinzi anaitwa Bwire
Shahidi: Mheshimiwa Jaji MI Leo nilikuwa nafafanua.
Mtobesya: hakuna mahala Kwenye Statement inaonyesha kuna Mlinzi anaitwa Bwire
Shahidi: Statement Haionyeshi
Mtobesya: kwenye Statement yako kuna sehemu inasema Baada ya Kukutana Mara ya Pili, kwamba Ulimtajia Majina huyo Mbowe watu wanaotembea na Sabaya?
Shahidi: Majina hayajaandikwa hapa kwenye Statement
Mtobesya: Ulipokutana Mara ya Tatu ulisema Ulimtajia pia Majina, hayo Majina yapo kwenye Maelezo Yapo?
Shahidi: Hayapo
Mtobesya: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali na huyo uliyemuita Mbowe ulimpigia Sabaya na Baadae Mbunge uliyemjulisha, Je hayo yapo kwenye Statement Yako?
Shahidi: hayapo
Mtobesya: pia wakati wakili wa Serikali anakuongoza nilisikia Majina ya Hotel na Club ulizotaja kwa Majina yake, Hizo Taarifa zipo humo kwenye Statement Yako?
Shahidi: Hazipo
Mtobesya: Wakati wakili wa Serikali anakuongoza Huyo uliyesema ni Bwire alitamka Sabaya ni Mtoto Mdogo atamchezesha, Je yapo kwenye Statement?
Shahidi: Hayapo
Mtobesya: Wakati wakili wa Serikali anakuongoza a umesema wewe unajishughulisha na Kilimo na Ukasema unavyofanya Kilimo, Je yapo hapo kwenye Statement..?
Shahidi: Hayapo
Mtobesya: Soma kwa Sauti Kuanzia Sehemu unayosema kuwa Ulikuwa Msaidizi wa Katibu wa CCM Shahidi anasoma Kuwa alikuwa Msaidizi wa Katibu wa CCM na mwanaharakati wa CCM.
Mtobesya: Wakati wakili wa Serikali anakuongoza ulisema kuwa wewe Ulishawahi kuwa Msaidizi wa CCM.
Shahidi: Hapana
Mtobesya: Je ungependa Maelezo uliyoyaongea Leo yaingie kwenye Ushahidi wako?
Shahidi: Ndiyo kwa sababu nimeongea Chini ya Kiapo ningependa yaingie kama Ushahidi
Jaji: Upande wa Serikali
wakili wa Serikali: Hatuna Pingamizi
Mheshimiwa Jaji anaandika Mahakama ipo Kimya
MTOBESYA amerudi kukaa katika Eneo lake
Jaji: kwa sababu imeombwa na Shahidi Kuwa Maelezo hayo hayajapingwa Na Mahakama, na haijapingwa na Upande wa Mashitaka basi Mahakama Imepokea Maelezo hayo Kama Kielelezo namba 1.
Mtobesya: naomba Kuendelea Mheshimiwa
MTOBESYA: Nitakuwa sahihi nikisema Kwa kipindi hicho Mpaka Unaandika Statement ulikuwa unajishughulisha na siasa
Shahidi: Siyo sahihi Kwa sababu Mimi ni Mwandishi ninayepiga Picha Siyo Mwanasiasa
Mtobesya: Kwa hiyo wewe siyo Mwanachama
Shahidi: Siyo Mwanachama Wa Chama Chochote
Mtobesya: Ni lini Uliacha kuwa Mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi
Shahidi: Sijawahi Kuwa Mwanachama wa Chama chochote Kile
Mtobesya: Hujawahi Kuwa Karibu na Viongozi wa Kisiasa
Shahidi: Nimesema kuwa nimekua karibu na Viongozi wa Serikali na Siasa
Mtobesya: Unaweza Kumtajia Mheshimiwa Jaji ni akina nani uliwahi Kuwa nao karibu
Shahidi: Mrisho Gambo, Daqaro, na Sabaya
MTOBESYA: hujawahi Kuandika Barua ukiwa Gerezani Kwa Viongozi wa Kisiasa wakusaidia kwenye kesi iliyokuweka Jela?
Shahidi: Sijawahi
Mtobesya: hujawahi Kutembelewa na Viongozi wa Kisiasa Ukiwa Gerezani?
Shahidi: sijawahi
Mtobesya: Ulikutana na Mheshimiwa Mbowe Gerezani tarehe ngapi
Shahidi: Tarehe 26 07 2021
MTOBESYA: Maelezo yako umeandika Lini
Shahidi: Siku Mbili baada ya Kutoka Gerezani
Mtobesya: na Umesema wakati Umefika Mahakamani Kisutu Siku hiyo, mlielekezwa nini Siku hiyo
Shahidi: Baada ya Upelelezi Kukamilika tumeonekana hatuna hatia tena
Mtobesya: Unakumbuka Namba ya Kesi Uliyokuwa umeshitakiwa nayo
Shahidi: sikumbuki Mtobesya: Naweza Kusema Kesi namba 63 ya Mwaka 2020
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Unakumbuka Mashitaka uliyoshitakiwa nayo wewe Binafsi
Shahidi: Kushiriki Vikao Kula Njama za kutenda Vitendo Vya ugaidi na Utakatishaji
Mtobesya: Kwa Niaba ya Mshitakiwa wa Kwanza naomba tuishie hapa
Mheshimiwa Jaji naitwa John Mallya
Mallya: shahidi Nina Mswali Machache, Jibu kwa Sauti
Mallya: Diwani analipwa TSh ngapi
Shahidi: sifahamu
Mallya: Diwani analipwa posho TSh Ngapi
Shahidi: sifahamu
Mallya: Kwa ufahamu wako wewe Sabaya alikuwa anakulipa Kutoka Mfuko gani
Shahidi: sifahamu
Mallya: Kwa hiyo wewe hukutaka kabisa Kujua kama anaiba au anatoa wapi
Shahidi: sikujua Mallya: alikuwa anakulipa TSh ngapi
Shahidi: Laki tatu
Mallya: Kwa Picha au Kwa Mwezi
Shahidi: Kwa Mwezi
Mallya: Mheshimiwa naomba Kielelezo namba D1
Mallya: Soma Hapo Mwanzoni Shahidi: nilianza Harakati za Kisiasa na Kuwa Msaidizi wa Katibu wa CCM
Mallya: Umemtaja Mrisho Gambo alikuwa Chama Gani
Shahidi: CCM
Mallya: Sabaya alikuwa Chama gani
Shahidi: CCM
Mallya: Daqaro Mkuu wa Wilaya Alikuwa Chama gani
Shahidi: Mkuu wa Wilaya hana Chama
Mallya: Unasema Sabaya alikuwa Diwani wa Chama gani
Shahidi: CCM
Mallya: halafu Magufuli akamteua kuwa Mkuu wa wilaya
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa mKuu wa Wilaya hana Chama ila Magufuli alimteua Sabaya wa CCM
Shahidi: Ndiyo alimteua akiwa CCM
Mallya: hapa karibu Umesikia kabla ya Sabaya kufungwa Miaka 30 aliomba Mahakama impungzuie Adhabu sababu anamchumba, Wewe Umesema Sabaya alikuwa na Mke
Shahidi: Mimi najua Sabaya alikuwa na Mke
Mallya: Kwa hiyo Kule Kadanganya Mahakama
Shahidi: sijui yeye sasa
Mallya: nimesikia Ulimtajia Mheshimiwa Freeman Mbowe, Sylvester Nyegu
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Umesikia Kuwa Mahakama Imemfunga Kwa Makosa ya Ujambazi Arusha
Shahidi: Ndiyo nimesikia
Mallya: Soma Statement yako hapo Mlipokuwa Mwishoni Mwa Mwaka 2017
Shahidi anasoma
Mallya: Kwa hiyo Hapa ulisema Mwishoni Mwa 2018, Mahakama ichukue lipi
Shahidi: Aliye andika atakuwa amekosea
Mallya: Soma Hapo Juu
Shahidi: Mimi nathibitisha kuwa Maelezo haya ni Sahihi
Mallya: Sasa wakati gani tujue upo sahihi hapo Umethibitisha Upo sahihi na Leo unasema tuchukue ya leo Kwamba Uliacha kazi kwa Sabaya 2017 na Leo unasema uliacha kazi 2018, Hapo Chini Maelezo uliyosaini yana maana gani
Shahidi: Yana maana ya Uthibitisho
Mallya: Mkuu wa Wilaya analipwa TSh ngapi
Shahidi: Sifahamu
Malya: Sabaya alikuwa anakulipa TSh ngapi
Shahidi: Laki tatu
Mallya: alikuwa anatoa wapi
Shahidi: sifahamu
Mallya: umesema Sabaya alikuwa anaongozana na Watu 7 au 8, Je walikuwa wanalipwa na nani
Shahidi: sifahamu, Walikuwa ni MARAFIKI zake
Mallya: wakati Unatoa Majina Mwaka 2017 na Ukaja kuyatoa tena Mwaka 2018 kwanini ulikuwa nayo.
Shahidi: walikuwa MARAFIKI zangu
Mallya: ulipokamatwa Arusha alikuhoji Afande Mahita
Shahidi: Ndiyo
Mallya: hayo aliyokuhoji umeyatoa hapa Mahakamani?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: je umeshawahi kuyatoa hayo Maelezo kwa Maana Karatasi kwa Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Siyo kazi yangu
Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba ajibu swali langu
Jaji: Je aliyatoa lakini
Mallya: nataka iingie kwenye Rekodi ya Mahakama
Mallya: Ulipokutana na Mbowe Gerezani alikwambia Nimekuja kuwatoa na Kesho yake ukatoka kweli
Shahidi: Ni sahihi nilitoka
Mallya: baada ya Kufutiwa kesi ulienda Central Kufuata Vitu vyako
Shahidi: Ni sahihi, Nilienda Central kwa Inspector Swila nikatoa Maelezo, ndiyo Nikapewa vitu Vyangu
Mallya: Kwa hiyo Mahakama irekodi kuwa ulipewa Vitu Vyako baada ya Kuandika Maelezo
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Ni hayo tuh Mheshimiwa Jaji
JAJI: hujamuuliza kama alipotoka Gerezani alienda kwa MChumba wake
Mahakama KICHEKO
JAJI: Kesho tunaweza kumaliza Mapema Je tunaweza Kupata Shahidi Mwingine
Wakili wa Serikali: Bado hatuna Uhakika tulikuwa tunahangaika kumpata
Jaji: basi Jitahidini Msijiandae Kumkosa
Jaji: basi nahairisha Mpaka kesho ambapo Upande wa utetezi watamalizia Kuuliza Maswali ya Dodoso Kisha Upande wa Mashitaka watarudi kwaajili ya Re examination
Jaji: naahirisha Mpaka Kesho saa 3 kamili
========
Mawakili upande wa utetezi wapo katika chumba cha Mahakama
Watuhumiwa wote wamekwisha wasili katika ukumbi wa mahakama asubuhi hii
Jaji ameingia
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Imetajwa
Wakili wa Serikali: Ikupendeze Mh Jaji Naitwa Robert Kidando nimeongozana na
1. Chriss ........
2. Abdallah Chavula
3. Jenitreza akitali
4. Ester Martin Ignas
5. Mwinuka Tulimanywa Majige
Kibatala: ikukupendeza Mheshimiwa Jaji naitwa Peter Kibatala nipo pamoja na
; 1. Alex Massaba
2. Seleman Matauka
3. Sisty Aloyce
4. Dickson Matata
5. Michael Mwangasa
6. Jonathan Mndeme
7. Hadija Aron
8. Evaresta Kisanga
9. Maria Mushi
10. Idd Msawanga
11. John Malya
JAJI: upande wa Jamhuri
Wakili wa Serikali: Shauri limekuja kwa ajili ya Re examination kwa Shahidi wa Kwanza, Yupo na tupo tayari kuendelea.
Jaji: Upande wa Utetezi..?
Kibatala: Na sisi tupo tayari Mheshimiwa Jaji
Jaji: Umesema kwa niaba ya Wenzio Siyo.?
Kibatala: Ndiyo
Jaji: Mshitakiwa namba 1,2,3, na 4 Wanainuka Kila Mmoja Ishara kwamba wapo Mhakamani
Jaji: Shahidi Jana ulihojiwa Maswali ya Dodoso na Upande wa Utetezi, Leo tukasema utakuja kwa ajili ya Re examination, Nakukumbusha bado upo chini ya kiapo.
Wakili wa Serikali: Jana Mtobesya alikuuliza wakati gani Jalada la Uchunguzi Lilifunguliwa na wakati gani Jalada la Kesi lilifunguliwa
Shahidi: Jalada la Uchunguzi tulikuwa tumefungia Baada ya Kukutana na Luteni Denis Urio katak Ofisi ya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai.
Wakili wa Serikali: Na Jalada la Kesi
Shahidi: Nilifungua baada ya Mimi Kupata Taarifa kuwa Vijana walipokuwa wanatafutwa na Luteni Urio kwa Amri ya Mbowe ndipo tulifungua Jalada.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kuhusiana kama Ulikuwa na Taarifa ya kabla ya Kumchukua Maelezo Mshitakiwa wa Pili, Elezea ni taarifa gani.
Kibatala: OBJECTION swali lilikuwa kwamba Swala la Kumtafuta Moses Lijenje, Je Ulimuhoji Mshitakiwa wa Pili,"
Jaji: Wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa sijauliza alichofanya Cross examination yeye, nipo kwa Mtobesya
JAJI: Uliza tena
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu Kuwa na Taarifa za Moses Lijenje wakati unamuhoji Mshitakiwa wa Pili, Je ulijua Taarifa hizo kabla au Baada?
JAJI: Kibatala Umesikia Swali?
Kibatala: Nimesikia lakini kaniondoa Mimi, Sasa ni Eneo la Mtobesya
Shahidi: Nilipata Taarifa kuwa Freeman Mbowe alikuwa anatafuta Kundi la Waalifu
Kibatala: Wakili Mtobesya Hakufika huko, it's something New alisema alikuwa anatafuta Vijana
JAJI: Ndiyo namimi nimesikia hivyo Jana ulisema Alikuwa anatafuta Vijana siyo Kundi la Wahalifu
Shahidi: Ndiyo nilipata Taarifa kuwa Freeman Mbowe Alikuwa anatafuta Kundi la Vijana walioachishwa kazi Jeshini, Kwa dhumuni la Kudhuru Viongozi wa Serikali na Pia Mpango wa maandamano ya kushinikiza Viongozi ya siyo kuwa na Kikomo na Kwamba Lengo la Kufanya hivyo Nchi ........isitawalike na ionekane imefeli kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa hapa Jana Kwamba wakati Mshitakiwa Wa pili Kama Ulikuwa Umempa Onyo, kuhusiana na Ukamataji, wewe Ukasema ulikuwa umeshampa Haki zake. Haki zake zipi?
Shahidi: Haki zake ni Pamoja na Kumfahamisha Kosa alilokuwa anashitakiwa nalo na Kwamba....... halazimishwi Kusema lolote ila Jambo analozungumza linaweza Kutumika kama Ushahidi Dhidi yake Mahakamani.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kwamba Matukio ya Kula Njama Yalifanyika kati ya 01 May 2020 na tarehe 05 August 2020 lakini katika Ushahidi wako ulisema Kula Njama huku kulifanyika tarehe 25 July 2020 hadi tarehe 01 August 2020 huko Aishi Hotel. Unasemeje Juu ya Ushahidi .......wako Kupinga na Hati ya Mashitaka?
Shahidi: Naomba Kuona hiyo Hati ya Mashitaka
Jaji: Utetezi Mapingamizi Juu ya Hilo
MTOBESYA: Hapana apewe tu
Shahidi: Miye naona Hakuna utofauti bado, ipo kati ya (in between) bado
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali Kuhusiana Maelezo ya mshitakiwa wa Kwanza kwamba yaliandikwa Chang'ombe ukasema ndiyo Ni kweli Na Maelezo Mshitakiwa wa pili na watatu yalichukuliwa Central Dar es Salaam Eleza kwanini uliamuru Maelezo ya Mtuhumiwa wa Kwanza .......yachukuliwe Chang'ombe?
Shahidi: Kwanza Chang'ombe ni Dar es Salaam, Pili uwezi kufananisha na Moshi, Alafu pia na angalia Masaa Manne.
Utetezi: OBJECTION Mheshimiwa Jaji wamuelekeze Shahidi wao Vizuri hatutaki kila Saa Kusimama Simama.
Jaji: Jamhuri
Wakili wa Serikali: Shahidi Eleza sababu tu kwanini uliamuru Maelezo ya Mshitakiwa wa 01 yachukuliwe Chang'ombe?
Shahidi: Baada ya Mshitakiwa kudanganya kuhusu Makazi yake.
Utetezi: OBJECTION Mheshimiwa Jaji hayo ya Kudanganya ni Mapya Sheria ya Ushahidi ipo wazi haupaswi Kuongea Mambo Mapya
Jaji: Nafikiri shida ipo kwenye Neno Kudanganywa hata Mimi sikusikia Neno "Kudanganywa" ondoa hilo Neno uendelee
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kwamba Mshitakiwa wa Pili uliomuonya kuhusu Kula Njama ya kutenda Matendo ya ugaidi, kwanini hukumuonya na Makosa mengine
Kibatala: OBJECTION hayo niliuliza Mimi sikumuuliza kwanini Hukumuonya kila Shitaka, Nilikuwa nauliza kwa kila Kosa........Kama Mnataka twende hivyo tutaomba kumuhoji tena.
Jaji: Unasemaje wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: Nitarudia swali Mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali kuhusiana na Kuamini na Kutoamini hasa kwenye sababu ya Wakili.
Shahidi: Nilikuwa siamini kwamba Mkuu wa Wilaya anaweza Kushusha Bendera lakini pia ndiyo iwe sababu ya Kumdhuru Kiongozi wa Serikali. Lakini statement niliiamini sababu alitoa yeye.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Kupatiwa Kielelezo P1
Wakili wa Serikali: Shahidi chukua Karatasi hii Nitakuuliza maeneo ambayo ulihojiwa na Mawakili wa Utetezi
Wakili wa Serikali: Tafuta eneo ulikohojiwa kuhusiana Kumfikisha Mheshimiwa Mikocheni, ukipata nitakuuliza swali
Mahakama Bado Ipo Kimya Shahidi anatafuta
Wakili wa Serikali: Baada ya Kufika Dar es Salaam na Kumfikisha Mheshimiwa Mikocheni, hujaona
Jaji: Labda uchukue Kwanza wewe Usome halafu umuonyeshe.
Wakili wa Serikali: Kama hawatokuwa na pingamizi
Kibatala: Hatuna Mheshimiwa Jaji
Wakili wa Serikali: Soma hapa
Shahidi: Baada ya Kufika Dar es Salaam na Kumfikisha Mheshimiwa Mikocheni Mimi na Mohammed tulipewa Laki mbili mbili baada ya Kesho yake kuwa anakuja Lissu na hakumpokea.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuwa huyo Mheshimiwa ni nani ukasema sasa ieleze Mahakama Huyo Mheshimiwa ni nani?
Mtobesya: OBJECTION Mheshimiwa Jaji Kifungu cha 61 Cha Sheria ya Ushahidi Inasema Nyaraka Isitafsiriwe Bali Nyaraka ijieleze yenyewe, hapo Shahidi anaulizwa tafsiri.
Wakili wa Serikali: Naona hiyo Objection haina Mashiko sababu tutakuwa hatuna Cha Kufanya.
JAJI: Nafikiri Mtobesya Hoja yako inahusu Thamani ya Nyaraka, Sasa Mahakama itaangalia hicho anachokisema Kipo kwenye Nyaraka.?
MTOBESYA: Sawa Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Ni Mheshimiwa Mbowe, Kwa sababu Mheshimiwa aliyetajwa kwenye Statement hii ni Mheshimiwa Mbowe na Mbowe Mwenyewe anaishi Mikocheni
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia kuhusiana na Kupewa Laki mbili na Mohammed, huyu Mohamed med ni nani?
Shahidi: Ni Ling'wenya kwa sababu huko Juu tulikuwa tunazungumzia Mohamed Ling'wenya na statement hii alikuwa anatoa Mwenyewe.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali Kama kwenye Statement hiyo, kama alivyoelezea yeye kama Mshitakiwa Wa pili Kama alimfuatilia Sabaya katika Maeneo aliyokuwa akienda Arusha Uliulizwa swali wewe Ukasema Hapana, Sasa nitakupeleka kwenye Statement halafu utafafanua.
Kibatala: OBJECTION samahani Mheshimiwa Jaji labda kwa Maelekezo yako nitakubali Maelekezo ya Mahakama, anachoulizwa Shahidi Alisha Jibu kuwa Hakuwa Arusha anaulizwaje Jambo hilo hilo tena.
JAJI: Nafikiri Ngoja tusubiri swali lake.
Wakili wa Serikali: Kwa Utaratibu wa Mahakama Kibatala anapaswa aongee kwa Ushahidi Kama Kuna kitu kweli Umekiona Kitolee Ushahidi, Siyo kuja na Neno Una suspect, Nani kafanya na Kitu gani Kimefanywa
Jaji: Kibatala ulikusudia Nimuonye, na Tunachukulia una Taarifa za ......kiintelijensia kwamba tumuonye shahidi kwa Intelijensia yako. Kibatala: Mimi nimesema Mahakama imuangalie.
Jaji: Basi kwa sababu Mimi sijaona naomba Upande wa jamhuri waendelee Kuuliza Maswali
Shahidi: Katika Kufuatilia Nyendo za Sabaya tulienda Club Kokoriko lakini hatukumpata Mheshimiwa Sabaya Siku hiyo.
Wakili wa Serikali: Eleza sasa Kwenye Statement hii Kama Mshitakiwa alifika Club Kokoriko.
Shahidi: Alifika
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia swali kuhusiana kama Kuna sehemu yoyote kama Mshitakiwa Wa Pili amechukuliwa finger print katika Statement hii, NI kwanini katika Statement hii hakuna Maelezo ya Kuchukuliwa finger Print
Shahidi: Mimi kama Mchunguzi nilishaona Hakuna haja.....Ya kuchukua Finger prints
Shahidi: Hitaji la Kuchukua Finger Prints lilikuwa baada ya Kumpekua Mshitakiwa Namba Moja na baada kukuta Kijitabu ikabidi sasa Kuchukua Finger Prints. Wakati nachukua Maelekezo Mshitakiwa wa pili ilikuwa tarehe 07 August 2020 kabla ya Kupata Kijitabu hicho.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kama Ulichukua Sampuli za Finger Prints za Pistol inavyodaiwa kukutwa na Mshitakiwa wa Pili. Sasa wewe Kama Mchunguzi ni kwanini hukuchukua Finger Prints na Sampuli za DNA.
Shahidi: Mimi sikuona haja ya kuchukua Finger Prints kwa sababu.......Mshitakiwa tulikuwa naye, Tunafanya Finger prints kama Mshitakiwa amevunja na hayupo Sisi Hatukuwa na hitaji hilo kama alivyo uliza wakili.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kuwa Kwa kipindi Chote baada ya Kupata nia ya Uhalifu, kama ulimtaarifu Kiongozi aliyelengwa Ole Sabaya, kama ulimpatia taarifa. Ukasema hukumpati na wala Kamati ya Ulinzi ya mkoa wa Kilimanjaro, ni kwanini sasa.
Shahidi: Tulikuwa kuwa na....Uhakika wa Taarifa zetu, hatukuona sababu za kuwaambia Watu wengine kwa kuwa tunge Create Pressure.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Wakati Mtuhumiwa wa kwanza anakamatwa palikuwa na Askari Jeshi na Ukasema Hakukuwa na Askari Jeshi
Shahidi: Hapakuwa na Askari Jeshi kwa sababu Mimi Ndiyo nilikuwa Arresting Officer na Nikisaidiwa na Inspector Mahita pamoja na ASP Mahita
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusiana na Maandamano Ukasema ni Sheria Inaruhusu lakini kwa Kufuata taratibu eleza Unamaana gani?
Shahidi: Ni kweli Sheria Inaruhusu Maandamano lakini kuna Sheria zingine pia zinaweka taratibu kuwa kabla ya Kufanya Maandamano awe amepata kibali
Wakili wa Serikali: Kibali gani
Shahidi: Cha Polisi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali Kuhusiana na Mtu wa Pili katika Maelezo yake kuwa Mtu Mmoja anaitwa Kakobe, Ukasema ukabaini Kuwa Mtu huyo anayeitwa Kakobe ndiyo Moses Lijenje, eleza ni wakati gani ulibaini
Shahidi: Wakati tunawakamata Watuhumiwa walikuwa wawili......lakini tulikuwa tuna Taarifa wapo watatu, Tukiwauliza Yupo wapi Mwenzetu Wakasema anaitwa Kakobe ambaye ndiyo Lijenje.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali kuhusiana na Sheria ya Ushahidi Wakati wa Onyo Kuwa section one na Two hukuweka, Ukasema hiyo ni Curable, Ulikuwa unamaanisha nini.
Shahidi: Haiwezi Kuathiri Maelezo ya Kuonywa
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji tunaomba Tukomee hapa.
Jaji: anaandika Kidogo
JAJI: Upande wa Utetezi
Kibatala: Mheshimiwa Tumekubaliana kuwa hatuna Pingamizi lolote
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji tuna Shahidi Mwingine lakini Kabla ya Kuendelea naye tunaomba ahirisho fupi, Ikiwezekana tuweze Ku resume Saa 5:30.
Jaji: Maombi yanakubaliwa, tutarudi Mahakamani saa Tano na Nusu.
Jaji: Kama tumekukwaza Kwa niaba ya Mahakama naomba Radhi, Naomba Radhi kwa niaba ya Utetezi na Ninakushukuru Kwa Ushahidi wako.
Jaji anatoka Mahakamani
---------
JAJI anaingia
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021
Wakili wa Serikali Kidando: Wapo tayari Kuendelea na Mashahidi
Jaji: Upande wa Utetezi Mpo tayari
Kibatala: Tupo tayari kwa ruhusa yako Mheshimiwa
Jaji: Shahidi wa Pili
Wakili wa Serikali: Shahidi amefuatwa
Mahakama ipo kimya ina subiri shahidi aingie
Shahidi amefika
JAJI: Majina shahidi: JUSTINE ELIYA
Jaji: Umri wako
Shahidi: Umri 31, Kabila Mmeru, Dini Mkrito, Shughuli Mkulima
Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama hii kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa ni kweli, kweli tupu Eenheeeee Mwenye Mungu nisaidie
Wakili wa Serikali: Ataongozwa na Wakili wa Serikali Abdallah Chavula
Jaji: Karibu
Wakili wa Serikali: Nitakuwa nakuhoji Maswali utakuwa unajibu kwa Kuelekea kwa Mheshimiwa Jaji
Wakili wa Serikali: Majina yako yapi:
Shahidi: Justine Eliya Kaaya
Wakili wa Serikali: Bw Kaaya Kwa sasa Shughuli zako ni Zipi?
Shahidi: Kilimo na Biashara
Wakili wa Serikali: Kilimo cha aina gani
Shahidi: Cha Mboga Mboga na Nafaka
Wakili wa Serikali: Unamaanisha nini
Shahidi: Mboga Mboga Nyanya, Vitunguu na Karoti na Nafaka, namaanisha Mahindi na Maharage
Wakili wa Serikali: Shughuli hizi unazifanyia wapi
Shahidi: Arumeru Mkoani Arusha
Wakili wa Serikali: Wateja wako hasa ni wanunuzi wa hayo mazao ni akina nani?
Shahidi: Ni watu tofauti Watanzania na Wageni wanaokuja Mkoa wa Arusha
Wakili wa Serikali: Unazifanyia wapi
Shahidi: Mkoani Arusha, wilaya ya Arumeru, Longido na Wilaya ya Arusha Mjini.
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Mwaka 2017 wewe Maskani yako yaliku a ni wapi?
Shahidi: Nilikuwa naishi Longido
Wakili wa Serikali: Wilaya ya Longido ipo Mkoa gani
Shahidi: Arusha
Wakili wa Serikali: Hapo Wilaya ya Longido ulikuwa unajishughulisha na Shughuli zipi?
Shahidi: Kupiga Picha na Kilimo katika Wilaya ya Arumeru
Wakili wa Serikali: Mwaka 2017 ulikuwa unajishughulisha na Kilimo cha aina gani
Shahidi: Nilikuwa nalima Karoti
Wakili wa Serikali: Wateja wako walikuwa ni akina nani?
Shahidi: Waliotoka Sokoni na baadhi ya watu pale Arusha
Wakili wa Serikali: Tueleze sasa hii Shughuli ya Kupiga Picha nayo, Ni Shughuli gani?
Shahidi: Picha za Mnato kwa kutumia Camera na Simu
Wakili wa Serikali: Ulikuwa ukiwapiga akina nani
Shahidi: Viongozi wa Serikali na Viongozi wa Kisiasa
Wakili wa Serikali: Unaweza ukatuambia ni akina nani hasa
Shahidi: Dr. Steven Kemomo Kiruswa Mbunge wa Longido
Wakili wa Serikali: Mwingine
Shahidi: Mrisho Gambo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Gabriel Daqaro aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Na wengine wengi
Wakili wa Serikali: Hao umewataja wa Ki-serikali, Je wa kisiasa
Shahidi: Lengai Ole Sabaya
Wakili wa Serikali: Huyu Lengai Ole Sabaya ulikutana naye wapi mara ya kwanza?
Shahidi: Mwaka 2017 Uchaguzi Mdogo wa Marudio Jimbo la Longido, Akanitaka nikamsaidie Kupiga Picha katika Shughuli zake zingine Mbalimbali
Wakili wa Serikali: Nini Kilijiri wakati huo baina yako wewe na yeye?
Shahidi: Alikuwa Diwani wa Kata ya Kisambasha, Wilaya ya Arumeru alivutiwa na Upigaji wangu wa picha
Wakili wa Serikali: Alikutaka ukamsaidie Wapi?
Shahidi: Katika kata yake ya kisambasha, Wilayani Arumeru
Wakili wa Serikali: Ulipokea Vipi Ombi hilo
Shahidi: Nilimkubalia kwa kuwa ilikuwa ni fursa kwangu
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama baada kukubali lile Ombi Utaratibu wa Ufanyaji kazi wenu ulikuwaje
Shahidi: Longido ni Mbali, hivyo ilinipasa kuhama Longido na Kuhamia Arusha, Nyumbani Kwa Lengai Ole Sabaya, Sehemu Inaitwa Kibanda Maziwa SAKINA
Wakili wa Serikali: Ulifanya kazi na Ole Sabaya na kuishi kwenye Nyumba yake kwa muda gani?
Shahidi: Mwaka 2017 Mpaka Mwaka 2018 July Alipoteuliwa Kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai
Wakili wa Serikali: Wewe ulienda kuishi wapi baada ya Kuteuliwa?
Shahidi: Nilienda Kuishi naye Hai Mkoani Kilimanjaro katika Makazi ya Mkuu wa Wilaya
Wakili wa Serikali: Kwenye hiyo Nyumba ya Ole Sabaya ulikuwa ukiishi na nani?
Shahidi: Yeye Mwenyewe Sabaya na Mke wake Jesca
Wakili wa Serikali: Ulipokuwa ukiishi naye wewe hasa ulikuwa Ukifanya Shughuli zipi
Shahidi: Kufanya Shughuli zake ndogo Ndogo ikiwemo Kumpelekea Nguo zake Dry Cleaner, Ikiwemo Kumpelekea Chai na Chakula Ofisini Kila Siku.
Wakili wa Serikali: Katika hiyo Nyumba ya Mkuu wa Wilaya Hai, Lengai Ole Sabaya Ulikuwa ukiishi na nani?
Shahidi: Nilikuwa nikiishi naye, yeye Mwenyewe na Mke wake.
Wakili wa Serikali: Umeishi Pale kwa Muda gani?
Shahidi: Kutoka July 2018 Mpaka Mwezi wa 10, 2018
Wakili wa Serikali: Nini kilitokea?
Shahidi: Niliamua Kurudi Longido Kuendelea na Shughuli zangu Nyingine sababu nikiacha Mchumba na Kutaka Kusimamia Shughuli zangu zingine za Kilimo.
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama sasa Mwaka 2018 uliporudi Longido unaweza Kukumbuka watu gani katika Medani za Kisiasa Ulianza Kufanya nao Mawasiliano
Utetezi: OBJECTION, Quite Leading kwa Kutaka Kuuliza ni watu gani wa Kisiasa Ulifanya Mawasiliano nao.
Wakili wa Serikali: Shahidi hebu tuambie Ulifanya Mawasiliano na Watu Gani?
Shahidi: Siku Moja nikiwa nyumbani nilipigiwa simu kwenye simu yangu Airtel 0693006700 kutoka kwenye namba ya Airtel 0784779944 na Mtu aliyejitambulisha Kuwa ni Freeman Mbowe
Wakili wa Serikali: Akakwambia kitu gani?
Shahidi: Nilishtuka sana akaniuliza Ujambo?. Nikamwambia sijambo akasema anashida ya Kuniona
Wakili wa Serikali: Ukafanyeje?
Shahidi: Nikamuuliza Upo wapi, Akajibu yupo Arusha
Wakili wa Serikali: Ukajibu Kitu gani,
Shahidi: Nikamwambia Nipo Longido kwa sasa Siwezi Kuja kwa sababu ya Changamoto ya Usafiri
Wakili wa Serikali: Nini Kikatokea?
Shahidi: Akaniambia Chukua Gari Noah Gharama Nitakuja Kulipa Ukifika Arusha. Kwa sababu ya Ile hofu nikamwambia siwezi Kuja
Wakili wa Serikali: Hofu ya Nini?
Shahidi: Kwanza Nikiongozi Mkubwa lakini Pia sina Ukaribu na Yeye
Wakili wa Serikali: Baada ya Kumueleza hayo nini Kilitokea
Shahidi: Aliniambia Subiri nakupigia, akakata simu.
Shahidi: Baada ya Muda akaniambia nipo Njiani nakufuata Longido.
Wakili wa Serikali: Muitikio wako ulikuwaje?
Shahidi: Kwa kuwa alisema yupo Njiani nakuja nikasema wacha nisubiri nisingeweza Kumzuia
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama nini kilitokea
Shahidi: Baada ya Dakika 40 alinipigia Simu kuwa Njoo hapa Uwanja wa Mpira
Wakili wa Serikali: Uwanja wa Mpira wa wapi?
Shahidi: Ndani ya mji Mdogo wa Longido
Wakili wa Serikali: Baada ya Kumueleza hayo Ulichukua hatua zipi?
Shahidi: Nilichukua Bodaboda na Kwenda
Wakili wa Serikali: Tuambie yaliyojiri
Shahidi: Akunichukua Bodaboda Nikaenda mpaka Uwanjani, na Kukuta Gari inaunguruma
Wakili wa Serikali: Ilikuwa ni Majira ya Muda gani
Shahidi: Saa 3 Usiku
Wakili wa Serikali: Baada ya kukuta gari,
Shahidi: Akaniambia Sogea hapa kwenye Gari Kwa namba ile ile ya 0784779944, Akaniambia ingia Kwenye gari Chief acha Kuogopa
Wakili wa Serikali: Kwenye Gari kulikuwa Kuna watu wangapi?
Shahidi: Nilimkuta yeye na Dereva na Nyuma ya upande wa Dereva palikuwa na Mwanamke
Wakili wa Serikali: Alikwambia Dhumuni lake lilikuwa na Ujumbe gani?
Shahidi: Akaniambia kuwa Lengai anamsumbua Sana
Wakili wa Serikali: Lengai ni nani..?
Shahidi: Mkuu wa Wilaya ya Hai
Wakili wa Serikali: Endelea
Shahidi: Akataka nimpatie Taarifa na Shughuli anazofanya pamoja na Watu anaofanya nao kazi pale Hai
Shahidi: Nikamwambia haitowezekana, kwa sababu mimi Sipo tena kwa Sabaya
Wakili wa Serikali: Ulipomueleza haya, yeye alifanya nini?
Shahidi: Akaniambia yeye Kiongozi Mkuu wa Chama Cha Upinzani Kwenye Nchi hii, Hivyo atafanya Vyovyote vile anavyoweza ili nirudi kwa Sabaya Kuendelea na Kazi
Wakili wa Serikali: Muitikio wako Ulikuwa ni Upi?
Shahidi: Nikamwambia haitowezekana kwa sababu nimechagua Kufanya Shughuli zangu Binafsi
Wakili wa Serikali: Nini Kilitokea?
Shahidi: Akaniambia samahani kwa Usumbufu wa Kunisumbua na akanipa TSh Laki 3
Wakili wa Serikali: Nini kikaendelea?
Shahidi: Akaniambia ni za Usumbufu, Tutawasiliana
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea
Shahidi: Tuliagana na aliondoka
Wakili wa Serikali: Baada ya Yeye Kuondoka wewe Ulielekea wapi
Shahidi: Baada ya kushuka kwenye Gari nilimpigia Ole Sabaya simu lakini hakupokea simu
Wakili wa Serikali: Wewe Ulienda wapi sasa
Shahidi: Nilibakia pale pale kwenye Uwanja na Kumpigia Dr Steven Kiruswa na Kumueleza kilichotokea?
Wakili wa Serikali: Wewe sasa Ulienda wapi?
Shahidi: nilirudi Nyumbani Kwangu
Wakili wa Serikali: Ulirudi Vipi Nyumbani kwako
Shahidi: Niliita Bodaboda nikarudi Nyumbani Kwangu
Wakili wa Serikali: Ni wakati gani tena Ulikuja kuwasiliana na Mtu uliye mtaja kuwa ni Freeman Mbowe pale uwanjani?
Shahidi: Mwaka 2020 Mwanzoni alinipigia Simu kupitia Whatsap
Wakili wa Serikali: Kwa namba ipi?
Shahidi: Kwa namba ile ile ya 0784779944
Wakili wa Serikali: Alikuwa na ujumbe gani
Shahidi: Akasema tumepotezana sana Chief
Wakili wa Serikali: Alikupa ujumbe gani?
Shahidi: Akasema anataka tuonane
Wakili wa Serikali: Wapi?
Shahidi: Moshi, wakati huo nilikuwa Arusha
Wakili wa Serikali: We Ukasemaje?
Shahidi: Ngoja nimalizie Kumwagilizia Shambani huku nikishamaliza nitakuja
Wakili wa Serikali: Nini kilitokea Kutokana na ahadi yenu?
Shahidi: Baada ya Kumalizia Shughuli zangu nilipanda Costa na Kumpigia Simu Kwamba naenda
Wakili wa Serikali: Ulipanda Costa Kuelekea wapi?
Shahidi: Moshi Kilimanjaro
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama ukifika hadi wapi?
Shahidi: Baada ya Kumpa Taarifa kuwa Nipo kwenye gari akasema nishuke Machame road.
Wakili wa Serikali: Kwa namba ipi?
Shahidi: ile ile ya 0784779944
Wakili wa Serikali: Ulipomueleza akakupa Maelekezo yepi?
Shahidi: Akaniambia nishuke Machame Road
Wakili wa Serikali: Ipo wapi?
Shahidi: Ipo Wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro
Wakili wa Serikali: Tueleze sasa baada ya Kupewa Maelekezo hayo nini kilitokea?
Shahidi: Nilishuka kwenye Gari nikapiga tena simu
Wakili wa Serikali: Simu ipi?
Shahidi: Namba yake ile ile ya 0784779944
Wakili wa Serikali: Ulipompigia simu nini kilitokea?
Shahidi: Akaniambia ni subiri hapo nakuja
Wakili wa Serikali: Nini kilijiri?
Shahidi: Baada ya Muda akinipigia simu kuniambia, Umefika, umekaa Upande upi, Akaniambia Vuka kaa Upande wa Kulia.
Wakili wa Serikali: We Ulikutana na nini?
Shahidi: Palikuwa na Barabara ya kwenda Machame na Nyingine kwenda Arusha na Nyingine Moshi
Wakili wa Serikali: Nini kikatokea?
Shahidi: Ilikuja Gari aina ya Land cruiser V8 Yenye Mlingoti na Bendera ya Bunge ikiwa na Plate Namba zilizoandikwa KUB
Wakili wa Serikali: Nini kilitokea?
Shahidi: Ilisimama Upande wangu, ikashusha Kioo Upande wa Abiria, nikamuona Mwenyekiti akaniambia Panda
Wakili wa Serikali: Baada ya Kuambiwa Upande nini kili tokea?
Shahidi: Alishuka Mtu kutoka Siti ya Nyuma akaniambia pita nikaingia kwenye Gari
Wakili wa Serikali: Enheeeee
Shahidi: Ile gari ilienda Muelekeo wa Kwenda Machame, Baadae tukaingia sehemu ambayo nilikuja Kugundua Hotel ya Aishi
Wakili wa Serikali: Palikuwa na watu gani kwenye Gari?
Shahidi: Palikuwa na Dereva na huyo Mlinzi wake aliyenipisha nikaingia kwenye Gari
Wakili wa Serikali: Mahusiano yenu ya Dereva na huyo Mlinzi kabla ya Siku hiyo yalikuwaje?
Shahidi: Tulikuwa hatufahamiani
Wakili wa Serikali: Ulijuaje aliyekupisha kuwa ni Mlinzi wake
Shahidi: Baada ya Yeye Kunitambulisha kuwa ni Mlinzi lakini pia ni Diwani wa Kata ya kiboriloni
Wakili wa Serikali: Baada ya Dakika 08 Mlifika wapi Vile?
Shahidi: Hotel ya Aishi Machame Wakili wa Serikali: Wewe ulitambuaje
Shahidi: Sababu ya Kibao Kilichoandikwa Aishi Hotel
Wakili wa Serikali: Tueleze sasa yaliyotokea
Shahidi: Baadae tulishuka kwenye Gari Mimi, yeye na Yule Mlinzi wake
Wakili wa serikali: Mlivyoshuka nini Kiliendelea?
Shahidi: Tulielekea Upande wa Mgahawa
Wakili wa Serikali: Umekuwa ukielezea Yeye na Mlinzi wake. Mlinzi wake na Yeye nani?
Shahidi: Freeman Mbowe
Wakili wa Serikali: Baada ya kushuka kwenye Mgahawa
Shahidi: Akasema tuongee kidogo sababu anamikutano kwenye jimbo lake akaniambia niagize Chakula
Wakili wa Serikali: Muda huo ilikuwa saa ngapi?
Shahidi: Saa Saba Mchana
Wakili wa Serikali: Wakati anakutaka Mkutane Moshi ilikuwa ni Saa Ngapi?
Shahidi: Saa Mbili Asubuhi
Wakili wa Serikali: Wewe Safari yako Kuelekea Moshi ulianza Saa ngapi?
Shahidi: Saa Tano kasoro
Wakili wa Serikali: Ulianzia wapi hiyo saa Tano kasoro
Shahidi: Sehemu inaitwa Kilala Wilaya ya Arumeru
Wakili wa Serikali: Alikwambia nini sasa?
Shahidi: Akauliza Mnampango gani Juu ya Mkutano inayoendelea Jimboni
Wakili wa Serikali: Jambo gani lingine alikwambia
Shahidi: Akaomba nimtajie wale wasaidizi wa Sabaya alipokuwa anatembea nao
Wakili wa Serikali: Wewe ulimwambia nini
Shahidi: Nilimwambia sina Taarifa yoyote ya kumwambia kwa wakati ule
Wakili wa Serikali: Nataka kuhusu hayo Majina
Shahidi: Nikimtajia Majina na Yule Diwani akawa anaandika kwenye Kikaratasi
1.Japhet Rwendela
2.Vedastus sibula
3.Mtoto wa Mkulima
4.Sylvester Nyegu
5.Binti wa kichaga
6.Mwalimu Doreen
7.Watson Malimumgu
JAJI: Mtoto wa Mkulima na Binti wa Kichaga ni Majina?
Shahidi: Ndiyo Majina nilivyokuwa nayafahamu wanayatumia kwenye Mitandao
Wakili wa Serikali: Kipi Kingine alikueleza
Shahidi: Nilitoa hizo namba kwenye simu niliwatajia Wakaziandika
Wakili wa Serikali: Lipi lingine alikueleza
Shahidi: Akasema atashughulika nao tutawasiliana na Wewe na Mimi baadae
Wakili wa Serikali: Nini kilitokea Baina yako wewe na yeye?
Shahidi: Akaniaga kasema atanitumia Chochote jioni
Wakili wa Serikali: Ulisema Chochote umaanisha nini?
Shahidi: Gharama zangu za Nauli
Wakili wa Serikali: Ilikuwaje baada ya hiyo ahadi
Shahidi: Hakutimiza hiyo ahadi na pia hakunitafuta baada ya pale
Wakili wa Serikali: Baada ya Makutano yenu pale Aishi Hotel wewe ukielekea wapi?
Shahidi: Nilirudi Arusha
Wakili wa Serikali: Ni wakati gani Mwingine uliwasiliana na Mbowe?
Shahidi: Mwezi 07 Mwaka 2020
Wakili wa Serikali: Tarehe ngapi?
Shahidi: Sikumbuki tarehe
Wakili wa Serikali: alikutafuta kwa namna gani
Shahidi: Alinipigia kwa Njia ya Mtandao wa Whatsap
Wakili wa Serikali: Kwa namba ipi
Shahidi: 0784779944
Wakili wa Serikali: ujumbe wake ulikuwa nini
Shahidi: Nipo Dar es Salaam nakuja Moshi, Naomba tuonane Nina Jambo la Kuzungumza na wewe
Wakili wa Serikali: Wakati huo wewe ulikuwa wapi
Shahidi: Shambani Kwangu Maji ya Chai
Wakili wa Serikali: Majira ya Saa ngapi
Shahidi: Mchana wa Saa Nane
Wakili wa Serikali: Ulichukua hatua zipi baada ya Ujumbe huo
Shahidi: Nikafanya Shughuli zangu, nikaanza Safari ya kwenda Moshi
Wakili wa Serikali: na ulienda Moshi kwa aina gani ya Usafiri
Shahidi: nikipanda Basi la Kilimanjaro Kutokea singida
Wakili wa Serikali: ahadi ilikuwa Mkutane Majira gani
Shahidi: alisema Saa 1 atakuwa amefika Moshi
Wakili wa Serikali: baada ya Kupanda Basi la Kilimanjaro ulifikia wapi
Shahidi: Moshi stendi
Wakili wa Serikali: wakati unashuka ilikuwa Majira gani
Shahidi: Saa 1 Usiku
Wakili wa Serikali: ikawaje
Shahidi: nilimpigia Simu Freeman Mbowe kuwa nimefika
Wakili wa Serikali: Kwa namba gani
Shahidi: 0784779944
Wakili wa Serikali: akasemaje
Shahidi: nichukie Pikipiki nimfuate Keys Hotel
Wakili wa Serikali: Baada ya Maelekezo hayo nini kilitokea
Shahidi: Niliita Bodaboda Nikaenda Hadi Keys Hotel na baada ya Kufika Keys Hotel nikampigia Freeman Mbowe kwamba Nimefika
Wakili wa Serikali: Kwa namba ipi
Shahidi: 0784 779944, Nikamwambia nimefika, Akasema namtuma Msaidizi wangu anifuate
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo nini kilitokea
Shahidi: alikuja Dereva wake ambaye namtambua kwa Jina Moja la Willy
Wakili wa Serikali: Nini hasa kilikufanya Umtambue
Shahidi: Siku nakutana naye kwa Mara ya Kwanza Machame ndiye aliyekuwa anamuendesha na Alinitambulisha
Wakili wa Serikali: Kule Nyuma ya Hotel Ulipoenda, Nyuma ya swimming ukikutana na Jambo gani
Shahidi: waliniambia Mheshimiwa Yupo Kwenye Kikao, Tukae hapa tukiwa tunasubiria amalizie Kikao
Wakili wa Serikali: ukiacha wewe na Dereva nani Mwingine Mlikaa naye
Shahidi: tulikaa na Mlinzi wake alikuwa baunsa baunsa Kidogo
Wakili wa Serikali: Ulifahamu Vipi huyo Baunsa baunsa ni Mlinzi wake
Shahidi: Willy aliniambia, huyo ni Mlinzi wa Mheshimiwa usiwe na wasi wasi
Wakili wa Serikali: nini kiliendelea hapo Mlipokuwa mmekaa
Shahidi: tulikula baada ya kula Mlinzi wake akaenda Kule alipokuwa Mwenyekiti Freeman Mbowe, na baada ya muda alirudi na Kusema tunaondoka
Wakili wa Serikali: Wewe SHAHIDI ulijuaje Kuwa Kule alipo Mwenyekiti ndipo alikuwa Mwenyekiti
Shahidi: Ilikuwa ni sehemu ya wazi tulikuwa tumetengenishwa na Swimming Pool
Wakili wa Serikali: tueleze wakati hayo yanatokea ilikuwa ni Majira ya saa ngapi
Shahidi: Saa tatu kasoro Usiku
Wakili wa Serikali: aliporudi na kuwaambia sasa mnaomdoka, nini kilitokea
Shahidi: Tulinyanyuka wote na kuelekea Kule alipo Freeman Mbowe
Wakili wa Serikali: tueleze wakati hayo yanatokea ilikuwa ni Majira ya saa ngapi
Shahidi: Saa tatu kasoro Usiku
Wakili wa Serikali: aliporudi na kuwaambia sasa mnaomdoka, nini kilitokea
Shahidi: Tulinyanyuka wote na kuelekea Kule alipo Freeman Mbowe
Wakili wa Serikali: Mlipoelekea huko alipokwepo Mwenyekiti nini Kilitokea
Shahidi: akatuambia pole sana kwa kutuweka, Baada ya muda Mlinzi wake akatufungulia Mlango wa Gari, Naye Mwenyekiti akaingia kwenye gari na nyuma ya Dereva akaingia aliyekuwa mlinzi wa Chadema Joyce Mukya
Mimi NikaKaa Katikati na Nyuma akakata Mlinzi wake
Wakili wa Serikali: Mlielekea wapi
Shahidi: tukitoka keys Hotel tukaelekea Mwelekeo wa Arusha
Wakili wa Serikali: iliwafikisha wapi
Shahidi: Aishi Hotel
Wakili wa Serikali: We Ulijuaje Kuwa Mmefika Aishi Hotel
Shahidi: nilishafika pale, haikuwa mara ya kwanza
Wakili wa Serikali: nini Kilitokea
Shahidi: aliwaambia watangulie ndani sisi tuna Kikao kifupi
Wakili wa Serikali: Kikao Kifupi mlifanya nani na nani
Shahidi: Freeman Mbowe, Mlinzi wake. Dereva alipotaka Kujumuika akamwambia hiki Kikao ni Cha watu watatu
Wakili wa Serikali: Hebu tuambie sasa, Mahusiano yako na Huyu Mtu unayesema ni Mlinzi, kabla yakikuwaje
Shahidi: nilikuwa sifahamiani naye
Wakili wa Serikali: Kwenye hicho Kikao mliongea Maswala gani
Shahidi: alinitambulisha kwanza kuwa Huyu ni Mlinzi wake anaitwa Khalfani Bwire na Msiri wake na hivyo niwe huru Kuzungumza naye
Wakili wa Serikali: yeye Mlinzi alikuwa wapi
Shahidi: tulikuwa tumekaa naye Upande wa kushoto
Wakili wa Serikali: Kikao chenu Mlizungumza Mambo yepi
Shahidi: alikuwa ananiambia nitaje tena Majina ya wale Vijana na Namba zao za simu na kazi wanazozifanya kwa Sabaya
Wakili wa Serikali: Wewe baada ya kukutaka Ufanye hivyo Ulichukua hatua gani
Shahidi: Kabla ya kuanza kuwataja nikamtaka Mlinzi wake akachukue kalamu na Karatasi ilituweze kuandika
Wakili wa Serikali: Baada ya hayo Maelekezo ikawaje
Shahidi: alirudi na kalamu na Karatasi Nikaanza Kuziandika
Wakili wa Serikali: Wewe Majina na namba za Simu za hao watu wewe ulizitoa wapi
Shahidi: nilikuwa nawafahamu tangu nafanya kazi kwa Sabaya
Wakili wa Serikali: hizo namba za Simu ulizitoa wapi wewe
Shahidi: nilizitoa kwenye simu
Wakili wa Serikali: Majina ya akina nani shahidi:
1. Japhet Rwendela
2. Vedastus sibula
3. Mtoto wa Mkulima
4. Sylvester Nyegu
5. Binti wa kichaga
6. Mwalimu Doreen
7. Watson Malimumgu
8. Enock kirigiti
Baada ya pale aliniambia nimtajie sehemu anazopenda kutembelea Mheshimiwa Sabaya
Wakili wa Serikali: Ulimtajia Sehemu gani
Shahidi:
1. Cocoriko Annex iliyopo Arusha
2. Cocoriko ya kijenge
3. The Don, Ipo karibu na Tanzania Breweries
4. Milestone Park iliyopo Sakina
Na hotel anazolala Sabaya
1. SG resort Iliyopo Sakina Arusha
2. Golden Crest Hotel ipo Arusha
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama baada ya kuwa wewe Umetoa Taarifa hizi ulifanya nini
Shahidi: Nilimuuliza mwenyekiti haya Majina na hizi sehemu unataka za Nini?
Akaniambia hilo niachie Mimi kazi yako hapa Imeisha.
Wakili wa Serikali: Lingine nini lilijitokeza baada ya mazungumzo yake
Shahidi: akaniambia nimkabidhi Khalfani Bwire Yake majina, Khalfani BWIRE akasema huyu Sabaya ni Mtu Mdogo sana Nitamchezesha. Baada ya pale Mwenyekiti akaniambia kazi Ndiyo inaanza rasmi kuanzia sasa hivi nitakuwa na Kulipa Mshahara
Wakili wa Serikali: ilikuwa ni Majira ya saa ngapi
Shahidi: Takribani saa 4 usiku
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama wewe baada ya yale Mazungumzo Ulielekea wapi
Shahidi: alisema wewe utapewa Chumba utalala hapa baada ya muda kuwa Umekwenda
Wakili wa Serikali: kingine
Shahidi: ilibidi nilale kwa sababu nisingepata Usafiri wa Kwenda Arusha
Wakili wa Serikali: nini kilifuatia
Shahidi: Kesho yake Asubuhi alinipatia TSh Laki Mbili kwenye namba yangu ya 0754916666 kutoka Airtel Money yenye namba 0784 779944.
Wakili wa Serikali: baada ya hapo Ulielekea wapi
Shahidi: Nilirudi Arusha kuendelea na Kazi zangu za Shambani
Wakili wa Serikali: Ni wakati Mwingine upi tena Ulikuja kuwasiliana tena na Mwenyekiti
Shahidi: hatukuwasiliana tena kwa sababu tarehe 25 August 2020 nilikamatwa na Askari wa Jeshi la Polisi
Wakili wa Serikali: Ulikamatiwa wapi
Shahidi: Makumira, Wilaya ya Arumeru nikiwa napanda CRDB, USA RIVER
Wakili wa Serikali: ulikuwa unapelekea CRDB pesa za Nini?
Shahidi: Nimetoka Kuuza Mazao Shambani
Wakili wa Serikali: Mazao gani
Shahidi: Karoti
Wakili wa Serikali: Ulikuwa umewauzia watu gani
Shahidi: Watu wa Mount Meru, wao walikuwa wanapeleka Game site huko Ngorongoro
Wakili wa Serikali: ulikuwa na Kiasi gani
Shahidi: Dollar za Kimarekani 1100 na TSh Millioni Moja Laki Moja na Kumi na Saba Pamoja na Euro 240
Wakili wa Serikali: baada ya Kumatwa nini Kilifuata
Shahidi: Nilikamatwa nikapakizwa Kwenye gari ni kapeleka Kituo Kikuu cha Arusha
Baada ya Lisa Moja Nilienda Kupekuliwa Nyumbani kwangu
Na Baadae Kusafirisha Kuletwa Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama zile pesa zako zilikuwa wapi
Shahidi: zilikuwa Mikono Mwa Askari pamoja na Simu zangu
Wakili wa Serikali: ilikuwaje hizo fedha
Shahidi: walinipekua kutoka katika mifuko yangu wakasema ni Noti bandia
Wakili wa Serikali: walipokukamata walikueleza wanakukamata kwa Makosa gani
Shahidi: Kwamba Nina tuhuma za kujihusisha Kula njama za kufanya Vitendo Vya ugaidi
Wakili wa Serikali: tueleze sasa Ulipofikishwa Dar es Salaam nini kilikusibu
Shahidi: Baada ya kufikishwa kituo cha polisi Dar es Salaam nilifanyiwa mahojiano na afande Mahita
Wakili wa Serikali: baada ya Mahojiano
Shahidi: Niliweka lockup Mpaka nilipofikishwa Mahakamani Kisutu
Wakili wa Serikali: Mahakamani Kisutu Ulipofikishwa ulifikishwa kwa sababu zipo
Shahidi: nilifungukiwa mashitaka Mbalimbali ikiwemo Kushiriki Vikao Vyakutenda Mambo ya kigaidi, Kula Njama za kutenda ugaidi, Kesi ya Utakatishaji wa Fedha
Wakili wa Serikali: Eleza Mahakama sasa Kwa kuanza na Khalfani Bwire we ulikutana naye wapi kabla ya Kuunganishwa naye
Shahidi: Nilikutana naye akiwa Keys Hotel na Aishi Hotel akiwa na Freeman Mbowe
Wakili wa Serikali: VIPI kuhusiana na Mohammed Ling'wenya
Shahidi: huyo sifahamu nilikutana naye Mara ya Kwanza Gerezani
Wakili wa Serikali: VIPI kuhusiana na Adam kasekwa
Shahidi: huyo simfahamu pia
Wakili wa Serikali: baada ya kuwa umeunganishwa kwenye kesi hiyo Mahakama ya kisutu ulipeleka wapi
Shahidi: Nilipelekwa Gereza la Ukonga
Wakili wa Serikali: ulikuwa na akina nani
Shahidi: kila mtu alikuwa na wing yake, Nilikuwa na Khalfani Bwire na baadae kaongezeaka Mtu anaitwa a Khalid Athuman na Baadae akaongezeka Mohamed Ling'wenya akitokea Segerea
Wakili wa Serikali: Umekuwa kwenye kesi ile kwa muda gani
Shahidi: Kwa Miezi 11
Wakili wa Serikali: Nini kilitokea Shahidi: aliletwa Mheshimiwa Mbowe Siku ya 26 July 2021 alitukuta tukiwa na Khalfani Bwire, akasema Poleni sana Nimekuja kuwatoa.
Wakili wa Serikali: Baada ya Kauli hiyo nini Kilitokea
Shahidi: Asubuhi watu wa Magereza walikuja Kusema tujiandae tunaenda Mahakamani Kesho yake 27 July 2021 tulipelekwa Kisutu Mbele ya Hakimu Mzee Simba Mimi, Khalid Athuman (Mshitakiwa 05) na Gabriel Muhina (Mshitakiwa wa 6)
Mwanasheria akasema bada ya Upelelezi, Sisi hatuhusiki kwa hiyo tumefutiwa mashitaka kwa kifungu kidogo Baada ya pale niliondoka kutoka Mahakamani kwenda kwa Mdogo wake Kitunda Kesho yake nikarudi Mahakamani Kwa Mwendesha Mashitaka Kuuliza Vitu vyangu
JAJI: ni sehemu ya Ushahidi wenu kwamba alienda Mdogo
Wakili wa Serikali: Hapana Mheshimiwa
Shahidi: Kesho yake nilipoenda Kisutu Kuuliza Utaratibu wa fedha zangu wakanielekeza niende Central Police Dar es Salaam Nikaenda Kuonana na Inspector Swila akaniandika Maelezo baada ya Kuniandika a maelezo akanipa Vitu Vyangu
Wakili wa Serikali: Umemtaja Mtu anaitwa Freeman Mbowe, Khalfani Bwire, Mohamed Ling'wenya, Just unaweza Kuwatambua
Shahidi: Ndiyo, wapo hapa mahakamani
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba sasa awatambue Hapa Mahakamani
JAJI: Utetezi
Kibatala: Hatuna Pingamizi
SHAHIDI anatembea anaenda Kumtaja Kila Mmoja kwa Jina Lake
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji siye ni hayo tu
JAJI: upande wa Utetezi
Jaji: mkizingatia ni Muda wa Mapumziko
Kibatala: tunaweza za Kushauriana nao?
Jaji: sawa Kibatala" tunapendekezo kwamba tukuombe Tu-break Kwa Dakika 30
Jaji: Saa 8:25 tutarudi tena Kuendelea
Jaji anatoka.
Jaji amerudi
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021, inatajwa
Jamhuri Kolamu yao ipo Vile vile
Upande wa Utetezi Kolamu yao Ipo Vile vile
Utetezi: wanaomba wanamtambulishe na wamjumuishe Wakili Nashon Nkungu Kwa sababu alikuwa Mahakama Kuu kwenye kesi Nyingine Asubuhi ya Leo.
Jaji: Sasa tulikuwa tumebakiza Upande wa Cross examination na ningependa Kuanza na wakili wa Mshitakiwa namba Moja
MTOBESYA: Nitakuwa sahihi nikisema kwamba katika Ushahidi wako hukutoa uthibitisho Wako wako kwamba Ulikuwa Ukifanya kazi kwa Ole Sabaya
Shahidi: Siyo sahihi
Mtobesya: Mwambie sasa Mheshimiwa Jaji ni uthibitisho upi Umetoa Mbele ya Mahakama hii
Shahidi: Muulize Mheshimiwa Mbowe ndiyo atakwambia kama nilikuwa nafanya kazi.
Jaji: Mbowe siyo shahidi
Jaji: labda Wakili urudie swali
Mtobesya: Ni sahihi Kwamba umesema ulikuwa unafanya kazi na Ole sabaya
Shahidi: sahihi
MTOBESYA: ni sahihi sasa kwamba Hukutoa chochote Mahakamani Kuthibitisha
Shahidi: Ndiyo sikutoa
Mtobesya: Umesema katika Ushahidi Wako kuwa ulikuwa unasafikiri Kutoka Longido kuja Moshi na kutoka Arusha Kuja Moshi ulikuwa unatumia Usafiri gani
Shahidi: Usafiri wa Umma
MTOBESYA: Ni matumaini yangu kuwa Ulipanda Basi la Umma unapewa Ticket
Shahidi: inategemea na hilo Basi
MTOBESYA: Mwambie Sasa Mheshimiwa Jaji kwamba wewe hukutoa Ticket
Shahidi: Si kutoa Ticket kwa sababu nilipandia Njiani.
MTOBESYA: kwa hiyo nipo sahihi kwamba huku safiri kwa sababu hukutoa Ticket wala Uthibitisho Wako wowote hapa Mahakamani
Shahidi: Siyo sahihi, Siyo lazima uwe na Ticket kuthibitisha.
Mtobesya: Okey Tunashukuru
Mtobesya: Tangu Ukutane na Mbowe Mpaka Unakutana na Inspector Swila ni Muda umepita
Shahidi: Umeuliza Swali siyo Sahihi
JAJI: ukuliza na Mawakili wa Serikali Wamenyamaza na Mahakama haijaingilia Ujue hilo swali ni sahihi, utatakiwa ujibu. kama hufahamu Shahidi Jibu sifahamu.
Mtobesya: Tangu huyo unayemuita Mbowe Mkutane ni Muda gani umepita
Shahidi: Mwaka moja na Nusu
Mtobesya: Kuna lolote alikuachia afande Swila baada ya kukuandika Maelezo
Shahidi: Hakuna aliloniachia baada ya Kuandika Maelezo akanipa Vitu vyangu nikaondoka
Mtobesya: kwa hiyo swila hakukwambia kwamba Siku Moja Maelezo yako anayoandika yatatumika kama Ushahidi
Shahidi: Hakuniambia
Mtobesya: alichokiandika Alikupa ukakisoma
Shahidi: Ndiyo alinipa nikasoma
Mtobesya: Ukajiridhisha Kwamba ulichokisema ni sahihi
Shahidi: ni sahihi, Ndiyo
Mtobesya: Hakuna Wakati alikwambia kuwa Umpatie kila kitu, umwambie unakijua
Shahidi: Hapana
Mtobesya: Unauhakika ulichoandika ndicho Ulichosema Leo Mahakamani
Shahidi: Ndiyo hichohicho
Mtobesya: Kwa Bahati nzuri sisi Mawakili wa Utetezi tuna nafasi ya Kupewa Nyaraka za Maelezo mliyoandika Mheshimiwa Jaji naomba nipewe Original Document ya hii, Na Msingi wangu wa Kuomba Ni Kifungu cha 164 cha Sheria ya Ushahidi
Mawakili wa Serikali Hatuna Pingamizi Mheshimiwa Mtobesya anatembea Kumfuata Shahidi alipo
Mtobesya: pitia Nyaraka hii Kama ndiyo Swila aliyoyaandika na Kama Ulikubali kuwa sahihi
Shahidi: Haya Ndiyo Maelezo yangu ya Kwanza
Mtobesya: Unaweza Kusoma?
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Soma tarehe kisha soma Mtu aliyeandika ni nani
Shahidi: Ndiyo haya
MTOBESYA: naomba Nikuulize kuhusu hii Statement yako dhidi ya Ulichokisema Leo 1. Nionyeshe kwenye hiyo Statement sehemu ilivyoandikwa kwamba huyo uliyemuita Mheshimiwa Mbowe kuwa yule alikuwa Mlinzi wake na Msiri wake
Wakili wa Serikali: OBJECTION Kwa Mujibu wa Kifungu cha 154 anatakiwa a Muonyeshe Shahidi hicho analichokisoma, yeye amefanya Vice versa
Mtobesya: Sijapata Msingi wa Objection ya Ndugu yangu Robert Kidando Nilianza Kutengeneza Msingi kwa Kuuliza Je alichokisema hapa ndiyo kilichopo kwenye Statement, Sasa Kama anataka twende hivyo tutaenda
Jaji: Hapana tuwasaidie Wateja wetu
Wakili wa Serikali: Provisory Mstari wa Nne ndiyo inakataza
JAJI: tueleze Nyie Mmelewa nini
Wakili wa Serikali: Maamuzi ya Kifungu Hichi Yametolewa Uamuzi na Mahakama ya Rufaa katika kesi ya Lilian Otesi Vs Jamuhuri, namba 77 katika Rufaa ya Jinai ya Mwaka 251 Mwaka 2008 katika Mahakama Ya Rufaa. Katika kesi hii Ukurasa wa 25 Mahakama ilisema yafuatayo; Kinachozungumzwa pale ni sawa na Kifungu namba 154 cha Sheria ya Ushahidi Kama Kilivyo gawanyika Maeneo Mawili Eneo la kwanza, Shahidi anaweza Kudodoswa kupitia Maelezo yake aliyoyaandika Nyuma Eneo la Pili anaweza Kuhojiwa kuhusu Maswala yake hayo hayo bila Kumuonyesha Maelezo yake Lakini kama anadhamiriwa kumpima Mkanganyiko wake shahidi, Kuna Utaratibu unaotakiwa Kufuatwa. Na hivyo kabla ya a kuthibitisha amuelekeze kwanza, Tofauti na Yeye kaenda na Kumfuata
Mtobesya: Rafiki yangu anarejea Vifungu viwili Tofauti Walitaka hayo ningefika huko kwa sababu hata a kesi ya Alberto Mendez imejadili hayo na Mimi nilikuwa ni sehemu ya Ile kesi. Kwa hiyo nafahamu ninachofanya.
Wakili wa Serikali: kifungu 164 hakisimami Pele yake, Kusimama kwake kunatemegea Kifungu cha 154 Na huo ndiyo Msimamo wa Mahakama
Mtobesya: Tusaidiane Mheshimiwa Jaji dhumuni la Kifungu cha 164 ni Kumchanganya (contradict) Shahidi
Wakili wa serikali: Mimi nilikuwa nimeanza Kwenye kifungu cha 154,Sikuwa nimefika huko
Jaji: wao wanasema Wana hukumu ambayo wanaweza Kutu Supply, nafikiri ni Vyema basi tuweze Kuona tu
Mtobesya: hili swala linaweza Kuibuka tena Mbeleni tunaomba Liwe Cleared kabisa na Mahakama
Wakili wa Serikali: tunaomba Dakika 15
Jaji: sawa tunaahirisha Kwa Dakika 15
Unaachiwa huru kwa masharti ya kuja kutoa ushahidi wa uongo Tangu lini Machame ikawa Wilaya ya Moshi.
Jaji bado hajarejea mpaka sasa
Jaji Kaingia
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 imetajwa
Robert Kidando: Kolamu yao Ipo Vile vile na anasema wapo tayari Kupokea Maelekezo ya Mahakama
Jaji: Muda Mfupi wakati wa Dodoso na Upande wa Utetezi, Upande wa Utetezi waliomba Mahakama iruhusu itoe Maelezo yaweze Kutumika kwa Nakala halisi p4 Baada ya Mawakili wa Utetezi Kusimama Upande wa Serikali Walisimama na Kusema Utaratibu haukufuatwa
Jaji: Baada ya hapo pande zote zilisema kuna Maamuzi nikaomba Maamuzi hayo
1. Nyaraka inatakiwa itolewe, hilo limeshafanyika
2. Nyaraka hiyo inapaswa Isomwe Katika Maeneo anayotaka Kumuuliza Maswali Ili Kumcontradict
Jaji: Mahakama hii inasema Kwakuwa huo ndiyo Utaratibu basi Unatakiwa Ufuatwe na Kuendelea na Shughuli Wakili wote wanasimama na Kushukuru ishara ya Kukubaliana Maamuzi ya Jaji.
Mtobesya: Anarudi kwa Shahidi na anaomba Mahakama Impatie tena Nyaraka anaweza kuisoma Shahidi anaanza Kusoma Alishawahi KUWA Msaidizi wa Katibu wa CCM Longido Amesomea Hotel Management Alishawahi Kufanya kazi na Sabaya kama Msaidizi wake Na aliacha kazi kwa Sabaya kwasababu alitaka Kurudi Longido na alienda kwa ajili ya Kumfuata Mchumba wake Anarudia kuwa alipigiwa simu na Freeman Mbowe, Kwamba alifuatwa Longido. "Freeman aliniambia kuwa nilitumia Elfu 50 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Hai Mama Helga na kumtomgoza
Shahidianaendelea kusoma: Nilishangaa Sana Kwamba alijuaje kwa sababu ilikuwa ni kweli nilimtomgoza Alinipigia Simu Tukutane Moshi Alinipigia niende Keys Hotel Na Siku Nyingine tulienda Aishi Hotel
Mtobesya: Soma eneo linalosema Mimi nilikwenda Kwa Kutumia Nauli yangu. Umeona?
Shahidi: anapekua
Shahidi: Mimi nilikwenda Kwa Kutumia Nauli yangu, na Nilipofika alikuja Kunichukua
Mtobesya: Eleza Mahakama Kwamba huyo Mlinzi alikuwa Diwani wa Kiboriloni
Shahidi: Nilisema
MTOBESYA: elezea Sasa hapo Katika Maandishi yako humo kuna Mlinzi anaitwa Bwire
Shahidi: Mheshimiwa Jaji MI Leo nilikuwa nafafanua.
Mtobesya: hakuna mahala Kwenye Statement inaonyesha kuna Mlinzi anaitwa Bwire
Shahidi: Statement Haionyeshi
Mtobesya: kwenye Statement yako kuna sehemu inasema Baada ya Kukutana Mara ya Pili, kwamba Ulimtajia Majina huyo Mbowe watu wanaotembea na Sabaya?
Shahidi: Majina hayajaandikwa hapa kwenye Statement
Mtobesya: Ulipokutana Mara ya Tatu ulisema Ulimtajia pia Majina, hayo Majina yapo kwenye Maelezo Yapo?
Shahidi: Hayapo
Mtobesya: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali na huyo uliyemuita Mbowe ulimpigia Sabaya na Baadae Mbunge uliyemjulisha, Je hayo yapo kwenye Statement Yako?
Shahidi: hayapo
Mtobesya: pia wakati wakili wa Serikali anakuongoza nilisikia Majina ya Hotel na Club ulizotaja kwa Majina yake, Hizo Taarifa zipo humo kwenye Statement Yako?
Shahidi: Hazipo
Mtobesya: Wakati wakili wa Serikali anakuongoza Huyo uliyesema ni Bwire alitamka Sabaya ni Mtoto Mdogo atamchezesha, Je yapo kwenye Statement?
Shahidi: Hayapo
Mtobesya: Wakati wakili wa Serikali anakuongoza a umesema wewe unajishughulisha na Kilimo na Ukasema unavyofanya Kilimo, Je yapo hapo kwenye Statement..?
Shahidi: Hayapo
Mtobesya: Soma kwa Sauti Kuanzia Sehemu unayosema kuwa Ulikuwa Msaidizi wa Katibu wa CCM Shahidi anasoma Kuwa alikuwa Msaidizi wa Katibu wa CCM na mwanaharakati wa CCM.
Mtobesya: Wakati wakili wa Serikali anakuongoza ulisema kuwa wewe Ulishawahi kuwa Msaidizi wa CCM.
Shahidi: Hapana
Mtobesya: Je ungependa Maelezo uliyoyaongea Leo yaingie kwenye Ushahidi wako?
Shahidi: Ndiyo kwa sababu nimeongea Chini ya Kiapo ningependa yaingie kama Ushahidi
Jaji: Upande wa Serikali
wakili wa Serikali: Hatuna Pingamizi
Mheshimiwa Jaji anaandika Mahakama ipo Kimya
MTOBESYA amerudi kukaa katika Eneo lake
Jaji: kwa sababu imeombwa na Shahidi Kuwa Maelezo hayo hayajapingwa Na Mahakama, na haijapingwa na Upande wa Mashitaka basi Mahakama Imepokea Maelezo hayo Kama Kielelezo namba 1.
Mtobesya: naomba Kuendelea Mheshimiwa
MTOBESYA: Nitakuwa sahihi nikisema Kwa kipindi hicho Mpaka Unaandika Statement ulikuwa unajishughulisha na siasa
Shahidi: Siyo sahihi Kwa sababu Mimi ni Mwandishi ninayepiga Picha Siyo Mwanasiasa
Mtobesya: Kwa hiyo wewe siyo Mwanachama
Shahidi: Siyo Mwanachama Wa Chama Chochote
Mtobesya: Ni lini Uliacha kuwa Mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi
Shahidi: Sijawahi Kuwa Mwanachama wa Chama chochote Kile
Mtobesya: Hujawahi Kuwa Karibu na Viongozi wa Kisiasa
Shahidi: Nimesema kuwa nimekua karibu na Viongozi wa Serikali na Siasa
Mtobesya: Unaweza Kumtajia Mheshimiwa Jaji ni akina nani uliwahi Kuwa nao karibu
Shahidi: Mrisho Gambo, Daqaro, na Sabaya
MTOBESYA: hujawahi Kuandika Barua ukiwa Gerezani Kwa Viongozi wa Kisiasa wakusaidia kwenye kesi iliyokuweka Jela?
Shahidi: Sijawahi
Mtobesya: hujawahi Kutembelewa na Viongozi wa Kisiasa Ukiwa Gerezani?
Shahidi: sijawahi
Mtobesya: Ulikutana na Mheshimiwa Mbowe Gerezani tarehe ngapi
Shahidi: Tarehe 26 07 2021
MTOBESYA: Maelezo yako umeandika Lini
Shahidi: Siku Mbili baada ya Kutoka Gerezani
Mtobesya: na Umesema wakati Umefika Mahakamani Kisutu Siku hiyo, mlielekezwa nini Siku hiyo
Shahidi: Baada ya Upelelezi Kukamilika tumeonekana hatuna hatia tena
Mtobesya: Unakumbuka Namba ya Kesi Uliyokuwa umeshitakiwa nayo
Shahidi: sikumbuki Mtobesya: Naweza Kusema Kesi namba 63 ya Mwaka 2020
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Unakumbuka Mashitaka uliyoshitakiwa nayo wewe Binafsi
Shahidi: Kushiriki Vikao Kula Njama za kutenda Vitendo Vya ugaidi na Utakatishaji
Mtobesya: Kwa Niaba ya Mshitakiwa wa Kwanza naomba tuishie hapa
Mheshimiwa Jaji naitwa John Mallya
Mallya: shahidi Nina Mswali Machache, Jibu kwa Sauti
Mallya: Diwani analipwa TSh ngapi
Shahidi: sifahamu
Mallya: Diwani analipwa posho TSh Ngapi
Shahidi: sifahamu
Mallya: Kwa ufahamu wako wewe Sabaya alikuwa anakulipa Kutoka Mfuko gani
Shahidi: sifahamu
Mallya: Kwa hiyo wewe hukutaka kabisa Kujua kama anaiba au anatoa wapi
Shahidi: sikujua Mallya: alikuwa anakulipa TSh ngapi
Shahidi: Laki tatu
Mallya: Kwa Picha au Kwa Mwezi
Shahidi: Kwa Mwezi
Mallya: Mheshimiwa naomba Kielelezo namba D1
Mallya: Soma Hapo Mwanzoni Shahidi: nilianza Harakati za Kisiasa na Kuwa Msaidizi wa Katibu wa CCM
Mallya: Umemtaja Mrisho Gambo alikuwa Chama Gani
Shahidi: CCM
Mallya: Sabaya alikuwa Chama gani
Shahidi: CCM
Mallya: Daqaro Mkuu wa Wilaya Alikuwa Chama gani
Shahidi: Mkuu wa Wilaya hana Chama
Mallya: Unasema Sabaya alikuwa Diwani wa Chama gani
Shahidi: CCM
Mallya: halafu Magufuli akamteua kuwa Mkuu wa wilaya
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa mKuu wa Wilaya hana Chama ila Magufuli alimteua Sabaya wa CCM
Shahidi: Ndiyo alimteua akiwa CCM
Mallya: hapa karibu Umesikia kabla ya Sabaya kufungwa Miaka 30 aliomba Mahakama impungzuie Adhabu sababu anamchumba, Wewe Umesema Sabaya alikuwa na Mke
Shahidi: Mimi najua Sabaya alikuwa na Mke
Mallya: Kwa hiyo Kule Kadanganya Mahakama
Shahidi: sijui yeye sasa
Mallya: nimesikia Ulimtajia Mheshimiwa Freeman Mbowe, Sylvester Nyegu
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Umesikia Kuwa Mahakama Imemfunga Kwa Makosa ya Ujambazi Arusha
Shahidi: Ndiyo nimesikia
Mallya: Soma Statement yako hapo Mlipokuwa Mwishoni Mwa Mwaka 2017
Shahidi anasoma
Mallya: Kwa hiyo Hapa ulisema Mwishoni Mwa 2018, Mahakama ichukue lipi
Shahidi: Aliye andika atakuwa amekosea
Mallya: Soma Hapo Juu
Shahidi: Mimi nathibitisha kuwa Maelezo haya ni Sahihi
Mallya: Sasa wakati gani tujue upo sahihi hapo Umethibitisha Upo sahihi na Leo unasema tuchukue ya leo Kwamba Uliacha kazi kwa Sabaya 2017 na Leo unasema uliacha kazi 2018, Hapo Chini Maelezo uliyosaini yana maana gani
Shahidi: Yana maana ya Uthibitisho
Mallya: Mkuu wa Wilaya analipwa TSh ngapi
Shahidi: Sifahamu
Malya: Sabaya alikuwa anakulipa TSh ngapi
Shahidi: Laki tatu
Mallya: alikuwa anatoa wapi
Shahidi: sifahamu
Mallya: umesema Sabaya alikuwa anaongozana na Watu 7 au 8, Je walikuwa wanalipwa na nani
Shahidi: sifahamu, Walikuwa ni MARAFIKI zake
Mallya: wakati Unatoa Majina Mwaka 2017 na Ukaja kuyatoa tena Mwaka 2018 kwanini ulikuwa nayo.
Shahidi: walikuwa MARAFIKI zangu
Mallya: ulipokamatwa Arusha alikuhoji Afande Mahita
Shahidi: Ndiyo
Mallya: hayo aliyokuhoji umeyatoa hapa Mahakamani?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: je umeshawahi kuyatoa hayo Maelezo kwa Maana Karatasi kwa Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Siyo kazi yangu
Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba ajibu swali langu
Jaji: Je aliyatoa lakini
Mallya: nataka iingie kwenye Rekodi ya Mahakama
Mallya: Ulipokutana na Mbowe Gerezani alikwambia Nimekuja kuwatoa na Kesho yake ukatoka kweli
Shahidi: Ni sahihi nilitoka
Mallya: baada ya Kufutiwa kesi ulienda Central Kufuata Vitu vyako
Shahidi: Ni sahihi, Nilienda Central kwa Inspector Swila nikatoa Maelezo, ndiyo Nikapewa vitu Vyangu
Mallya: Kwa hiyo Mahakama irekodi kuwa ulipewa Vitu Vyako baada ya Kuandika Maelezo
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Ni hayo tuh Mheshimiwa Jaji
JAJI: hujamuuliza kama alipotoka Gerezani alienda kwa MChumba wake
Mahakama KICHEKO
JAJI: Kesho tunaweza kumaliza Mapema Je tunaweza Kupata Shahidi Mwingine
Wakili wa Serikali: Bado hatuna Uhakika tulikuwa tunahangaika kumpata
Jaji: basi Jitahidini Msijiandae Kumkosa
Jaji: basi nahairisha Mpaka kesho ambapo Upande wa utetezi watamalizia Kuuliza Maswali ya Dodoso Kisha Upande wa Mashitaka watarudi kwaajili ya Re examination
Jaji: naahirisha Mpaka Kesho saa 3 kamili