Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,908
- 945
MHE. ZAYTUN SWAI ASISITIZA KUACHANA NA UTALII WA KIMAZOEA, TWENDE NA UTALII WA KIMKAKATI
"Sekta ya Maliasili na Utalii ni ya muhimu sana kwa kutuingizia fedha za kigeni, tumeona zaidi ya asilimia 25 ya fedha za kigeni inatokana na Sekta ya Maliasili na Utalii, pia asilimia 17 ya pato la Taifa linachangiwa na Sekta ya Maliasili na Utalii" - Mhe. Zaytun Swai, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha
"Sekta ya Maliasili na Utalii inachangia ajira kwa watanzania, ajira za moja kwa moja na zisizo rasmi takribani Milioni 1.6 ya watanzania wameajiriwa katika sekta ya Maliasili na Utalii. Mnyororo wa Sekta ya Maliasili na Utalii ni mrefu sana na unafugusa Sekta ya usafirishaji na kilimo" - Mhe. Zaytun Swai, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha
"Tukiilea Sekta ya Utalii inaweza kuchangia asilimia 50 ya upatikanaji wa dollars 💵 hapa Tanzania 🇹🇿. Nampongeza Rais Samia kwa kuitangaza Sekta ya Utalii kimataifa. Naiomba Wizara ya Maliasili na Utalii ifanye kazi zaidi ili kuendana na kasi ya Rais Samia" - Mhe. Zaytun Swai, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha
"Ni lazima tuondokaneni na Utalii wa Kimazoea ili twende na Utalii wa kimkakati. Tutafanya hivi kwa kushirikiana na Sekta Binafsi ili kuweza kujenga miundombinu mbalimbali hususani hoteli zenye hadhi ya kimataifa ya kulaza wageni wetu" - Mhe. Zaytun Swai, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha
"Tanzania ina vyumba 122,532 vya kulala wageni, lakini nchi jirani wana vyumba zaidi ya Milioni 2. Nchi zilizoendelea kwenye Utalii kama Seychelles 🇸🇨, Mauritius 🇲🇺 na Kenya 🇰🇪 waliondokana na Utalii wa mazoea wakaenda kwenye Utalii wa kimkakati" - Mhe. Zaytun Swai, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha