True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

125
Nawezaje kumficha babu mambo ya hatari kiasi kile? Nilitokwa machozi huku babu akijipa kazi ya kunituliza.

Babu hata usingesema yote hayo, nikata shauri ya kukueleza kila kitu tangu usiku nilipoingia kulala, nipo tayari kukwambia kila kitu pasipo kuficha hata 1.

Nilianza kumsimulia babu kila tukio tangu nilipokutana na yunge mdogo na mkubwa mpaka kuanzisha nao uhusiano na mpaka yunge kunipeleka kwenda kujionea kilinge cha wachawi mpaka niliponusurika kufyekwa shingo na mzee yule wa kiwanjani pamoja na yule mama mnene ambao walikuwa hoi vitandani kutokana na pigo moja hatari la upembe wa yunge.

Katika kumsimulia mkasa ule, nilijipa angalizo kutomtaja bibi hata mara moja, na hatimae nilimaliza kumsimulia babu stori ile na yeye kuanza kunitwanga maswali.

Ebu nambie bila kuficha, ni nani mwingine unaemjua ulimwona kilingeni?
Mimi: mwingine niliemwona pale ni kijana mmoja ambae alikuwepo uwanjani siku niliyoenda kufanya mazoezi pale uwanani.

Niambie ukweli mwanangu, je bibi yako hukumwona kule?
Daah!!!

Endelea boss
 
126
Nimekuwa na hisia siku nyingi kwamba huenda mke wangu nae anajishughulisha na kikundi hicho cha walozi, lakini kama hujui ni kwamba mtu ukijiingiza anga hizo lazima kuna kiingilio utakitoa (kafara ya mtu wa karibu yako zaidi) lakini licha ya kutega mitego yangu yote sijawahi kumnasa bibi yako na kujihakikishia kwamba ni mshirikina, japo niponae miaka mingi sijawahi kuona dalili zozote za kumhusisha na ulozi japo ndoto zangu huwa zinaniambia ni mtu hatari sana.

Jambo lingine ambalo hunifanya nipuuze mawazo yangu ni kwamba tangu nimemuoa hatujawahi kufiwa na mtoto, hata mjukuu mmoja, na hata mimi mpaka leo nipo hai, je kama anajihusisha na ulozi basi yeye anatoaga sadaka gani? Alizidi kuongea babu.

Ebu sasa nambie ulimwona ama hukumwona? Alinitega babu.

Niliinamisha kichwa pembeni nikiwaza kwamba nikimwambia babu akajua kwamba bibi ni mlozi itakuwaje pale nyumbani, siuvunjifu wa amani utatokea? Naikiwa hivyo pale hapatakalika kamwe, niliwaza sana.

Basi usjali mwanangu, uso wako tu unaeleza wazi, inuka.!
 
Back
Top Bottom