TikTok inagaragaza YouTube iliyokuwa ikisumbua kwa miaka mingi

Mimi situmii sana tiktok, lakini naomba niseme ni moja kati ya mtandao unaokuja kwa kasi hivyo kuwa mshindani namba 1 wa youtube.
Kwa sasa hawajaifikia youtube, lakini hiyo haiondoi ukweli kwamba ni threat namba 1 wa youtube, ndiyo maana Marekani wanaipiga vita ili kumuokoa youtube ambayo ni ya Mmarekani.
Marekani ndivyo alivyo, kumbuka hata Huawei alifanyiwa figisu baada ya kuonekana ni threat kwa Iphone/Apple. Ni mbinu za kijasusi za Mmarekani ili kuokoa makampuni yao yanayopata ushindani mkali kutoka kwa Wachina.
Hivyo wote mnaoibeza tiktok kaeni mkijua ni kweli inaleta threat kwa usitawi wa youtube.
 
Tiktok ni muhimu kwa wakata viuno ila kwa watu wanatafuta contents za kuelimisha, kujifunza kitu kama tutorials za kurekebisha vifaa na na uzalishaji lazima YouTube iwe muhimu kwao.

Tiktok mtandao wa kujazana ujinga na upuuzi, vitu vya muhimu vichache
 
TikTok imekuja kummaliza kabisa YouTube aliyekuwa akisumbua kwa miaka mingi. YouTube hana mvuto kwasasa kila simu ya kijana anayefahamu nini maana ya utandawazi basi ana App ya TikTok kwenye simu yake.

Wengi wanajitahidi ku Uninstall App ya YouTube ila bahati mbaya inakuja Pre Installed kwenye simu za Android isingekuwa hivyo basi YouTube ingeshafutwa kwenye simu za vijana wengi.

YouTube ni mbovu kwenye impression haiwezi kusukuma video za Creators kwa watazamaji automatically mpaka promotion itumike wakati TikTok inapeleka content mbele ya watazamaji automatically ilimradi uwe na content nzuri.

TikTok kusumbuliwa Marekani kwamba itazuiwa hiyo ni njama ya YouTube kutaka kumng'oa kwasababu ya yeye kupoteza mvuto sokoni hapendwi tena.

Natabiri kifo cha YouTube kwa siku zijazo hilo halina ubishi TikTok akitaka kummaliza kabisa YouTube aruhusu Video za mpaka lisaa limoja au zaidi pia aboreshe mfumo wa malipo makubwa kwa Creators hapo YouTube atakufa kabisa.
Twitter naye yupo kwenye mpango wa kummaliza YouTube kwa kuruhusu Video ndefu.
Tokotoko ndiyo nini?
 
Kuna siku npo dukani akaja mteja kununua bidhaa na amelipa anataka risiti ya efd. Muhusika wa sku zote hayupo.

Ilibidi nimpigie akashauri nizame youtube na kweli nikatoa risiti fresh tu.

Binafsi Youtube haina mpinzani. Hiyo Tiktok hata kuinstall sijawahi kuwaza.
 
Back
Top Bottom