poleni sana wahanga wenzangu mliokuwa mmelizwa na tigo pesa kwa mfumo wa kununua muda wa hewani. Nilipatwa na mkasa huo takribani wiki moja iliyopita kwa kiasi cha zaidi ya tsh. 20,000/. Nililipoti tatizo hilo kwa ofisi za tigo pale mlimani city wale warembo wakanishauri niorodheshe jina langu, namba yangu na kiasi kilichokwamishwa na mtandao, sikusita nami nilikuta orodha ndefu sana nami pia nikatia jina langu. Nimekaa kwa muda sasa lakn leo tigo wamenitumia ujumbe wa kuniomba radhi na salio langu limeongezeka kwa kile kiwango ambacho kilikwamishwa na mtandao.
Poleni sana tigo kama kweli mtandao wenu umeingiliwa na hackers, lkn kama ni uzembe wenu no thanks on this foolish!
Naomba sana wadau ambao wamelizwa kwenda manualy ofisi za tigo kila kitu kipo poa.
Kwa kweli tigo wanaboa lkn kuhama siwezi kiukweli kabisa
Japo siku hizi wamezidiwa...na wizi ni mwingi. Siwezi hama ajili ya kupatikana nje ya nchi. Kwan nautumia nkiwa hapa hapa ndani ya nchi.