KadaMpinzani
JF-Expert Member
- Jan 31, 2007
- 3,715
- 86
2007-08-27
Na Simon Mhina
Mwenyekiti wa TLP, Bw. Augustine Mrema, amesema wapinzani wameunda vikosi viwili, cha anga na nchi kavu kwa ajili ya kuishambulia CCM.
Aidha, amesema ili kutekeleza azma hiyo, wameshakamilisha mipango ya kupata helikopta zingine nne.
Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, mwanasiasa huyo alisema mipango ya wapinzani kuzunguka nchi nzima na kuwaeleza wananchi juu ya kilichomsibu Mbunge Zitto Kabwe, imepangwa na viongozi wote.
Alisema maneno aliyonukuliwa akiyasema Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Bw. James Mbatia yametungwa na CCM.
"Mimi CCM naijua sana, wameshajua wamejifunga wenyewe na sisi tunataka tuongezee bao lingine! Wameunda vitengo vingi vya propaganda, kikiwemo kile cha kwenye vyombo vya habari," alisema.
Hata hivyo, Bw. Mrema alisisitiza kuwa mbinu hizo chafu haziwezi kuwavunja nguvu kwa vile sio mpya, na kwamba CCM walizitumia dhidi yake na upinzani kwa miaka mingi.
"Propaganda ya kwanza ilikuwa kwamba Mrema ni CCM, ya pili wakasema Mrema ni mbinafsi, sasa wameona tumeungana, wanaanzisha fitina, lakini wamekwama," alisema.
Alisisitiza kuwa mwaka 2010, wataweka mgombe mmoja wa urais na mbunge mmoja wa upinzani kila jimbo.
Bw. Mrema alisema wapinzani wamegundua kila walikopita kwamba wananchi wamefurahishwa na muungano wao.
Alisema itakuwa ni kituko cha mwaka kwa viongozi wa upinzani kuvunja umoja huo.
Hata hivyo, alisema hakuna uwezekano wa umoja huo kuvurugika kwa sababu hakuna mkakati wanaopanga, bila kushirikishana wote.
Kuhusu 'brigedi' za mashambulizi, Bw. Mrema alisema wameamua kuunda kikosi cha anga na kile cha ardhini.
Akifafanua, alisema kama ilivyo katika vita ya kawaida, mashambulizi ya anga yanarahisisha, lakini hayawezi kuleta ushindi, bila kushuka chini.
Alisema kikosi cha anga ambacho kitatumia helkopta hizo, kitaongozwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Bw. Freeman Mbowe.
Alisema kikosi hicho, kitakachowajumuisha makomandoo kadhaa kama Zitto Kabwe, kitakuwa na lengo la kufanya mashambulizi ya nguvu katika vijiji na miji, ambayo ni ngome ya CCM, tena kwa haraka na kwa muda mfupi.
Alisema kikosi cha ardhini, ambacho ndicho chenye jukumu kubwa, kitakuwa na viongozi watatu, Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), James Mbatia (NCCR) na yeye mwenyewe.
Alisema viongozi hao watakuwa na jukumu la kupita kwa miguu sehemu ambazo zilifikiwa na helkopta, kwa ajili ya kuzisafisha na kuziteka.
Alisema safari hizo zimeshaanza na CCM wameshagundua mkakati huo na kuona hatari inayowakabili, na ndio maana wameanza propaganda kupitia vyombo vya habari.
SOURCE: Nipashe
Na Simon Mhina
Mwenyekiti wa TLP, Bw. Augustine Mrema, amesema wapinzani wameunda vikosi viwili, cha anga na nchi kavu kwa ajili ya kuishambulia CCM.
Aidha, amesema ili kutekeleza azma hiyo, wameshakamilisha mipango ya kupata helikopta zingine nne.
Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, mwanasiasa huyo alisema mipango ya wapinzani kuzunguka nchi nzima na kuwaeleza wananchi juu ya kilichomsibu Mbunge Zitto Kabwe, imepangwa na viongozi wote.
Alisema maneno aliyonukuliwa akiyasema Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Bw. James Mbatia yametungwa na CCM.
"Mimi CCM naijua sana, wameshajua wamejifunga wenyewe na sisi tunataka tuongezee bao lingine! Wameunda vitengo vingi vya propaganda, kikiwemo kile cha kwenye vyombo vya habari," alisema.
Hata hivyo, Bw. Mrema alisisitiza kuwa mbinu hizo chafu haziwezi kuwavunja nguvu kwa vile sio mpya, na kwamba CCM walizitumia dhidi yake na upinzani kwa miaka mingi.
"Propaganda ya kwanza ilikuwa kwamba Mrema ni CCM, ya pili wakasema Mrema ni mbinafsi, sasa wameona tumeungana, wanaanzisha fitina, lakini wamekwama," alisema.
Alisisitiza kuwa mwaka 2010, wataweka mgombe mmoja wa urais na mbunge mmoja wa upinzani kila jimbo.
Bw. Mrema alisema wapinzani wamegundua kila walikopita kwamba wananchi wamefurahishwa na muungano wao.
Alisema itakuwa ni kituko cha mwaka kwa viongozi wa upinzani kuvunja umoja huo.
Hata hivyo, alisema hakuna uwezekano wa umoja huo kuvurugika kwa sababu hakuna mkakati wanaopanga, bila kushirikishana wote.
Kuhusu 'brigedi' za mashambulizi, Bw. Mrema alisema wameamua kuunda kikosi cha anga na kile cha ardhini.
Akifafanua, alisema kama ilivyo katika vita ya kawaida, mashambulizi ya anga yanarahisisha, lakini hayawezi kuleta ushindi, bila kushuka chini.
Alisema kikosi cha anga ambacho kitatumia helkopta hizo, kitaongozwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Bw. Freeman Mbowe.
Alisema kikosi hicho, kitakachowajumuisha makomandoo kadhaa kama Zitto Kabwe, kitakuwa na lengo la kufanya mashambulizi ya nguvu katika vijiji na miji, ambayo ni ngome ya CCM, tena kwa haraka na kwa muda mfupi.
Alisema kikosi cha ardhini, ambacho ndicho chenye jukumu kubwa, kitakuwa na viongozi watatu, Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), James Mbatia (NCCR) na yeye mwenyewe.
Alisema viongozi hao watakuwa na jukumu la kupita kwa miguu sehemu ambazo zilifikiwa na helkopta, kwa ajili ya kuzisafisha na kuziteka.
Alisema safari hizo zimeshaanza na CCM wameshagundua mkakati huo na kuona hatari inayowakabili, na ndio maana wameanza propaganda kupitia vyombo vya habari.
SOURCE: Nipashe