The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London

Kuna hii article nimeitoa kwenye Tanzania Daima laleo 25/07/07


Ukishangaa ya Balaliiiii utaona ya Ka-damage!

Mpayukaji Msemahovyo



WANAKAYA bado wanaulizia marekebisho ya mikataba ya kijambazi ya madini yao.

Hata kabla ya kupewa jibu la haja, mara wanaletewa msiba mwingine! Laiti angekuwa Mtume Paulo angesema: “Nyinyi Wadanganyika wapumbavu nani aliwaroga kuwa mikataba imebadilishwa?”

Wakati uchafu wa Bunch of Thieves (BoT) haujapoa tunaletewa tusi jingine kuwa Omulangila Nshomile Nazimia Kadamage ameishabadilisha mbinu ya kusaini mikataba ya madini.

Kweli waliposema wanabadilisha mikataba hatukujua kuwa kumbe wanabadilisha mbinu ya ulaji zaidi. Kweli wamebadilisha.

Badala ya kufanyia ufuska wao Bongo sasa wanaufanyia Ulaya!

Balaliiii naye katushangaza kuwa licha ya sisi kuwa tegemezi havunji genge lake la wezi! Mkuu naye utadhani hana madaraka na kaya yake!

Bwana Kipaza Sauti (Speaker) naye eti naye kavunja maadili ya kijiwe kumwokoa mhalifu wa kawaida! Yaani kaya hii tangu baba aondoke imeingiliwa!

Hayo ni mahojiano ya ndani kwa ndani wakati mzee mzima nikiangalia muuza kahawa anavyochanganya makemiko yake.

Maana leo nimejilawa baada ya mshirika wa bedroom kuunusa upepo wa shumbwengu langu la Migomigo. Si kitimoto hicho, yaani usiku kucha!

Mara nastuliwa na sauti ya mgosi Machungi. “Mgosi mbona unafikiia sana utadhani unataka kusaini mikataba ya madini kue Andani kwa maikia!”

Kufumba na kufumbua naona timu nzima imetia guu. Inaonekana hawa washirika wanatoka kuweka sigara kubwa.

Mara Mbwa Mwitu anadakia. “Mgosi usinichafulie siku yangu kwa kunikumbusha hawa tumbiri. Yaani kaya imekuwa kama mfuko wa chizi kila kibaka kujichotea anavyotaka!”

Makengeza naye alivyochangamka baada ya kulipuliza! Analamba mic. “Wazee leo mada ni ujambazi wa wakubwa kwenye ofisi za umma. Wanaziuma huku ukapa ukituuma sisi umma!

“Kumbe ndiyo maana wanatuita umma maana wanatuuma kweli kweli! Kweli sisi ni umma na wao ni waumma umma tena kwa uma na mrija!”

”Du, kijiwe hiki! Sina hamu. Utadhani wale Magiriki ambao Msomi huwa anatolea mifano!” Mkuru anamtazama Msomi na kuendelea. “Hebu Msomi nikumbushe majina ya wasomi hawa.”

Msomi huku akitabasamu anaibusu mic. “Yupo rafiki yangu kipenzi na msomi mwenzangu Socrates, Plato, Sophocles, Herakritos, Demakritos, Cicero, Cassenius Lucinius Luculus na mimi msomi mwenyewe, Mkata vimeo vya kaya hii, pia yu...”

Kabla ya kuendelea kupayuka majina ya magwiji hawa, Makengeza anaingilia. “Msomi imetosha. Maana Mukurusi, Demokrasihasi du! Kweli wenzetu mlivibukua vitabu!”

Msomi anabwia kahawa yake maana tangu bajeti ianze kuuma hana jeuri ya kubwia tangawizi na vitumbua kama awali.

Anasema: “Mimi, akina Slaa, Mbowe na wengine ndiyo wasomi ambao hatuko tayari kubakwa kisiasa ili tuibakishe nchi yetu. Kisa eti kuhongwa pesa chafu kama kwenye uchafu alioongelea Mgosi.”

Mzee Kidevu naye analamba mic. “Nyie hamjui. Mkuu aliposema mikataba ya akina Tuni tuni, Vigoda, Vyenge na Miramba na wenzao wengine hamkumuelewa.

“Alimaanisha kwa kuiboresha na kusainiwa Ulaya tena kwa mama mwenyewe. Kweli Kamaragi kajua kututenda.”

“Du! Hii kubwa mzee Kidevu,” alichomekea Mpiga picha Kapende.

“Ni kweli kwa watu hawa hata kubomoa kwao ni kujenga. Hukusikia wakisema maisha bora kwa kaya yanawezekana tusijue wanamaanisha wao na washikaji zao!

“Hujasikia wakitutia madole machoni wakisema eti kaya ni kama dege linalopaa wakati lilishabutuka na kuungua?”

Msomi kashikwa pabaya. Anakatua mic tena. “Mie naona huyu Nshomile angebadilisha jina na kujiita Ka-damage. Maana kama ni kusababisha damage (uharibifu) ameishaongeza mafuta kwenye moto. Je, hapa wa kulaumiwa ni nani?”

Anajijibu mwenyewe. “Hapa mkuu hatuna. Mie nshawambia siku nyingi kuwa kaya imegeuzwa gheto la wezi kujizolea.

“Angekuwa ni mtu mwenye kuambilika ningemshauri amteue Katelefoni Mpenda kuchukia vyombo vya habari ili awakoromee wawekezaji. Au anakoromea vyombo vya habari kwa vile havimpi ten percent?

“Sijui na wanaopinga ukeketaji wako wapi! Maana ukeketaji si wa mwili tu. Kuna ukeketaji wa kiakili ambao ni mbaya sana. Hakuna udhalilishaji kama kutaka maelezo yasiyokuwapo kisa uzushi na upuuzi wa kawaida!”

”Msomi umeongea kama Mukurusi, hatujakuelewa,” analalamika mzee Maneno.

Msomi anavaa jezi tena. “Hamkuona mzee Ruxa alivyochoka na huu usanii na hadi uvumilivu ukamshinda akaamua kuwapa live?

“Kumbe kaya hii ni shamba la ngedere kujifunzia kuharibu mazao! Angalia Balalii. Angalia Mheshimiwa Richmond, mkuu hawagusi au ndiyo huo uswahiba?

“Mzee Kidevu kanitoa tongo tongo. Kumbe wanaharamu hawa na matapeli ni sawa! Umma unauuma! Unaahidi Kanani kutaswaga kwenda Misri! Kurekebisha mikataba unabadili staili ya ulaji! Badala ya kupeana cha mbele hapa wanatumana kwenda kupeana walipotulangulia rada!

“Hapa kaya itajipindua pamoja na kuwa na genge la mapinduzi ya umma.” Anakatua kashata huku akijifuta jasho. Anabwia kidogo kahawa na kuendelea. “Tangu kufa mzee, kaya hii imekumbwa na balaa la kusimamiwa na vibaka huku wakialikana na kuzidi kutusukumizia ulofa.

“Halafu wapo wapuuzi sijui wamekatiwa! Eti wanasema Tuni tuni apewe nishani! Kama ni nishani ya umachinga sawa lakini si ya uadilifu.

“Kama kuna nishani ya ulaji basi apewe Balaliiii.”

Kabla ya kuendelea kutambaa naye Mbwa Mwitu anaanza upuuzi wake. “Msomi samahani sikukuelewa. Umesema inaonekana akina Nshomile wamekatiwa nini? Maana nimesikia ukisema wanakwenda kwa mama ili waibake kaya. Hii ni salsafa ngumu.”

“Mbwa nawe acha ushamba. Ni falsafa siyo salsafa,” Mzee Kidevu anaamua kumkosoa Mbwa Mwitu. Vicheko si kawaida hadi tunawasahau majambazi wetu kwa kitambo!

Mpemba naye kapata upenyo. “Yakhe mie nshasema siku za nyuma. Hapa watu wasipoanka kama Pemba wataendelea lia lia weee huku hawa watu waendelea kujizolea ‘mdebwedo’.

“Sie tuligoma tukafanya muafaka ingawa baadaye watu fulani tuwajua, wakauvuruga na Alhamdulillah wemebaki historia tena chaafu!” Anapiga chafya na kuendelea.

“Mie wallahi nawaapia masafu ya Mtume kama Wabara mtaendelea lala na lelemama hii bila kufahamu wallahi mtajajuta siku moja. Hapa lazima watu wajitokeze na kutukua haki yao. Vinginevo twafanyiwa usanii nasi twabweteka.”

Mpayukaji nami napata mwanya isitoshe mahasira niliyo nayo kutokana na kulazwa kitimoto na mshirika wangu we acha tu. Naanza kutambaa. “Je, wapinzani huwa wanaelewa somo? Wanangoja nini kuandaa maandamano na migomo ili tujue hii kaya ni mali ya nani.

“Maana inavyoonekana kundi hili litakuja kutuuza halafu litimkie huko wanakoendea kutuchuuzia kwenye madangulo yao.”

”Tuuzwe mara ngapi mzee mzima?” Anadakia mzee Maneno.

”Mzee mwenzangu umenena. Kama kweli hii kaya ingekuwa yetu na wezi wetu wangeelewa na kukubali hivyo mtu kama Balaliii au Ka- Damage wangekuwa wameishatimuliwa na saa nyingine wangekuwa Ukonga wakitubia makosa yao.

“Yaani tumezidiwa na Mu-7 ambaye tulimkomboa juzi tu ameweza kuwatia korokoroni majambazi waliojifanya marafiki zake.

“Alijua asipofanya hivyo umma usiotaka kuumwa utaelewa kuwa ni washirika wake kama ambavyo kaya yetu imeanza kuamini kutokana na vibaka kupewa kila aina ya ulinzi huku wakitafutwa majambazi wa vijibenki kwani Benki Kuu siyo benki sawa na ile ya Mwanga au ni kwa vile uvunjaji umeanzia ndani kwa kutumia kalamu badala ya bunduki?”

kijiwe kikiwa ndiyo kinanoga si lilipita Limousine la Balalaliiiii na ka-damage, tukaamka kulitupia mawe, likatimua mbio!

Mpayukaji@yahoo.com
 
................Wakati uchafu wa Bunch of Thieves (BoT) haujapoa tunaletewa tusi jingine kuwa Omulangila Nshomile Nazimia Kadamage ameishabadilisha mbinu ya kusaini mikataba ya madini.

Kweli waliposema wanabadilisha mikataba hatukujua kuwa kumbe wanabadilisha mbinu ya ulaji zaidi. Kweli wamebadilisha...........................

Badala ya kufanyia ufuska wao Bongo sasa wanaufanyia Ulaya!..............kijiwe kikiwa ndiyo kinanoga si lilipita Limousine la Balalaliiiii na ka-damage, tukaamka kulitupia mawe, likatimua mbio!



Hizo mbio zilikuwa kama hizi?

1646.jpg
 
CHADEMA yalia na Karamagi

na Lucy Ngowi

CHAMA cha Demekrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeungana na mbunge wake, Zitto Kabwe (Kigoma Kaskazini), kushikilia bango suala la serikali kusaini mkataba mpya wa madini nje ya nchi kabla hata kumaliza kupitia upya mikataba ya madini yenye utata.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema hayo jana alipokuwa akitoa tamko la Kamati Kuu ya chama hicho kuhusu hali ya taifa katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Makao Makuu ya chama hicho, Dar es Salaam.

Alisema hali hiyo inathibitisha ukosefu wa dhamira ya kweli ya Serikali ya CCM kuhakikisha Watanzania wananufaika na rasilimali ambazo Mungu amewajalia na ni kinyume cha ahadi ya Rais Jakaya Kikwete ambayo aliitoa wakati wa uzinduzi wa Bunge.

“Kwa kuwa serikali imeonyesha kiburi katika kuhakikisha kuwa mikataba inawekwa wazi hata kwa Bunge, Kamati Kuu inatoa mwito kwa vyama vya wanasheria na vikundi vya haki za binadamu kuchukua hatua zinazostahili,” alisema Mbowe.

Alisema Kamati Kuu inaitaka CHADEMA kushirikiana na vyama vya siasa kuendelea kuhamasisha nguvu ya umma katika kulinda na kutetea maslahi ya taifa.

“Hakuna jambo la kawaida katika suala hilo, tutaendelea kulishikia bango suala la Karamagi kwenda kusaini mkataba nje. Tutaendelea kulifumua suala hili kwa kuwa tuna taarifa za kina. Tunaitaka serikali ichukue hatua kama serikali itaminya hili, sisi tutalifumua,” alisema Mbowe.

Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo, katika Bunge la bajeti linaloendelea pamedhihirika kuwa serikali haitaki upinzani kwa kuwa kuna ushuhuda wa kimazingira na hata kimatendo.

Mbowe alisema Kamati Kuu ya CHADEMA inaona kuwa Bunge la Tanzania linaelekea kupoteza uhalali wake wa kuwa chombo kinachowakilisha umma wote wa Tanzania, kwa kuwa limejigeuza kuwa chombo cha chama kimoja cha CCM kwa vitendo vyake.

“Wabunge wa CCM wanaingiza ushabiki wa kisiasa katika mambo yenye maslahi kwa taifa kwa ujumla wake. Ni mkakati wa serikali kuufifisha na kuunyong’onyeza upinzani,” alisema Mbowe.

Aliwataka wananchi wasimame kidete kuhakikisha wawakilishi wao wanatanguliza mbele maslahi ya raia na si maslahi ya vyama vyao na kama wanapingana na matakwa ya umma, basi wawanyime kura katika chaguzi zijazo.

Alitumia fursa hiyo kwa kusema Kamati Kuu ya CHADEMA inaipongeza kambi ya upinzani bungeni kwa kuwasilisha bajeti mbadala, kwa kuwa ilipendekeza hoja nzito kuhusu vyanzo mbadala vya mapato na kupunguza matumizi ya serikali.

“Tunalaani utamaduni wa mawaziri na wabunge wa CCM kuweka mbele ushabiki wa kisiasa, ambao kimsingi hausaidii taifa letu wala wananchi wetu,” alisema.

Mbowe alisema kuwa Kamati Kuu inamtaka Rais Kikwete amwajibishe Waziri wa Fedha, Zakhia Meghji kwa kuwa anachezea maisha ya Watanzania.

Alisema Meghji alilidanganya Bunge kwa kuwa serikali imeshindwa kudhibiti hali ya mfumo wa soko holela na inaelekea kuongoza kwa majaribio.

Akizungumzia elimu ya juu, Mbowe alisema wapo wanafunzi ambao wameshindwa kuchangia asilimia 40 ya masomo yao na hatimaye wamezuiliwa kufanya mitihani katika vyuo vya Tumaini Iringa, Ustawi wa Jamii, St. Augustine Mwanza na vingine.

Aliishauri serikali kutoa utaratibu wenye kuwawezesha wanafunzi hawa kufanya mitihani yao kama ambavyo ilifanyika kwa Chuo cha Kilimo Morogoro (SUA) na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Awali, Mbowe alisema kuwa taifa limezidiwa na mzigo wa ufisadi kwani orodha ya ufisadi, matumizi makubwa na matumizi yasiyo na lazima ni ndefu, wakati nchi inateketea watawala wananeemeka.

“CHADEMA inalaani hali hii na kufadhaishwa na ukimya ama ucheleweshaji wa Rais Kikwete. Rais ameonekana kuwa na kigugumizi kikubwa kuhusiana na ufisadi.

“Madhila yanayolikumba taifa rais anastahili lawama asilimia 100. Kama anawalea wasaidizi wake na kukaa kimya, anachangia ufisadi,” alisema Mbowe.

Alimalizia kwa kusema kuwa hali ya taifa letu hairidhishi na hivyo jitihada za kila mwananchi zinahitajika katika kuhakikisha uwajibikaji wa viongozi na raia katika kulirejesha taifa letu katika mwelekeo mwafaka wa demokrasia na maendeleo.

Katika hali ya kujiamini mwenyekiti huyo wa CHADEMA alimtahadharisha Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba kuwa yuko mbioni kuanza kuwafuata wananchi kwa kutumia helikopta yake.

Alitoa kauli hiyo baada ya kuulizwa na waandishi wa habari ni kwanini kila anapokwenda katibu huyo anafuata.

“Namwambia Makamba ajitayarishe kwani karibu nitaanza kuruka na helikopta yangu sijui yeye atafanyaje. Safari hii Makamba atanifuatilia, lakini hatanipata, mufilisi kabisa,” alisema.
http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/8/4/habari1.php
 
Zitto kawasilisha hoja yake ya Buzwagi/Karamagi, imewasumbua sana CCM MPs wamekua wakijibu hoja badala ya kuchangia, wamechanganyikiwa kishenzi.

Asubuhi hadi saa 7 ilikua live TVT na Star TV, but jioni wakachomoa hakuna cha LIVE, maana saa hizi Zitto anajibu hoja na kuwabana, amekua kama Waziri aliyewasilisha, anapewa saa nzima kujibu hoja za wabunge lakini nasikia humo ndani wanamchanganya kila saa anasimama MBUNGE ama Waziri anasema, "KUHUSU UTARATIBU".

Star TV walianza saa 11 kuonyesha mechi then wakaanza Bongostar, then kipindi cha afya yetu na sasa ni matangazo tu ya biashara. HII NI AIBU KWA UTAWALA BORA NA DEMOKRASIA, waliona wananchi wataona wanavyodhalilika na jinsi wasivyotetea maslahi yao

Hoja inatupwa baada ya CCM kushinda kwa kura.

Sasa Mbunge wa Mchinga, mwalimu wa zamani wa Usalama wa TAifa, Mudhihir M. Mudhihr anawasilisha hoja ya kutaka Zito asimamishwe ubunge kwa kusema uongo. Hoja inajadiliwa na wengi,
anaanza Dr Slaa anasema hakubaliani na hoja ya kumsimamisha ubunge zitto kwa sababu hakuna ushahidi wa kusema uongo wa zitto haujathibitishwa. Haya wataendelea na baadaye atakuja John Malecela


Dr Slaa anasema, "
 
Ndio tatizo la kukurupuka. Siku Zitto alipomtuhumu Karamagi na kuahidi kuleta hoja binafsi...ndio akawa amejifunga kitanzi. Baada ya kutoa hoja ndio akaanza research...iliyo-lead kwenye ukweli kwamba alikurupuka...kuna wakati alikwishaamua asiwasilishe hoja hiyo baada ya kukosa data. Lakini kwakuwa aliahidi kwa mbwembwe hakukuwa na njia zaidi ya kuwasilisha hoja dhaifu....baada ya Karamagi kujibu, ikaonekana kwamba huyu Mheshimiwa aliongopa na wenzake sasa ndio wanamtwanga kwa hoja ya kusimamishwa Ubunge kwa kusema uongo. Hata hivyo, mimi nadhani ni hoja ya kipuuzi ya kutaka asimamishwe Ubunge. Mimi nadhani wamuache aumbuke na uongo wake manake hii ni tabia yake ya kusema uongo kutafuta umaarufu.
 
Kama kuna anayejua hoja yenyewe ailete hapa tuione.

Mara ya mwisho jambo lililokuwa limeongelewa ni kuwa waziri Karamagi alikwenda kutia saini mkataba wa madini Buzwagi wakati bado serikali inashughulikjia utaratibu mpya wa mikataba ya madini. Waziri akajibu kuwa mgodi ule wa Buzwagi ni mdogo sana na wala hakukuwa na haja ya kusubiri utaratibu mpya. Je uwongo uliomo kwenye hoja ya namna hiyo ni upi?
 
Ndio tatizo la kukurupuka. Siku Zitto alipomtuhumu Karamagi na kuahidi kuleta hoja binafsi...ndio akawa amejifunga kitanzi. Baada ya kutoa hoja ndio akaanza research...iliyo-lead kwenye ukweli kwamba alikurupuka...kuna wakati alikwishaamua asiwasilishe hoja hiyo baada ya kukosa data. Lakini kwakuwa aliahidi kwa mbwembwe hakukuwa na njia zaidi ya kuwasilisha hoja dhaifu....baada ya Karamagi kujibu, ikaonekana kwamba huyu Mheshimiwa aliongopa na wenzake sasa ndio wanamtwanga kwa hoja ya kusimamishwa Ubunge kwa kusema uongo. Hata hivyo, mimi nadhani ni hoja ya kipuuzi ya kutaka asimamishwe Ubunge. Mimi nadhani wamuache aumbuke na uongo wake manake hii ni tabia yake ya kusema uongo kutafuta umaarufu.

Wewe nani kakwambia Zito anasema uongo.... unatumia authority ipi ya kudai kuwa Zito ameongopa..... Mjadala unaendelea na kwa mujibu wa aliyeanzisha hoja TV zimeskip kuonyesha live

Wewe huku unakurupuka kudai Zito anaongopa...
Wewe bado hujathibitisha madai mazito uliyomwaga hapa kuwa AC alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Zito na sasa unataka kuanza mengine?

grrrrrrrrrrr muongo kwa uongo!
 
Kama kuna anayejua hoja yenyewe ailete hapa tuione.

Mara ya mwisho jambo lililokuwa limeongelewa ni kuwa waziri Karamagi alikwenda kutia saini mkataba wa madini Buzwagi wakati bado serikali inashughulikjia utaratibu mpya wa mikataba ya madini. Waziri akajibu kuwa mgodi ule wa Buzwagi ni mdogo sana na wala hakukuwa na haja ya kusubiri utaratibu mpya. Je uwongo uliomo kwenye hoja ya namna hiyo ni upi?

Kila kitu kinaanzia na kitu kidogo na kuendelea kuwa kikubwa. Yeye ana uhakika gani madini yaliyochini ni kidogo, (Is he a geologist?). Ndio uhalalishaji wa wizi wa kijinga wanafikiri sisi wote hamnazo, isitoshe hicho kidogo sio chake binafsi ni cha Tanzania na sisi ndio tunataka mikataba mipya kwa rasilimali zetu sio yeye. Yeye kazi yake ni kusikiliza anayotumwa na wale anaowawakilisha na sio vinginevyo.
 
..mwaka huu ni wa kihistoria katika nchi hii!

..kashfa nyingi za rushwa zinaikumba nchi!

..ufujaji wa mali ya umma nao umeripotiwa kwa kiasi kikubwa!

..bunge kuwa sehemu ya kuibuliwa mambo na kuzimwa mambo ilhali ukweli unafahamika!

..wafujaji wa mali ccm wanachukuliwa hatua!tunasubiri serikalini!

..hii yote ni zawadi anayotuletea JK,kiaina!
 
Zitto kawasilisha hoja yake ya Buzwagi/Karamagi, imewasumbua sana CCM MPs wamekua wakijibu hoja badala ya kuchangia,

wamechanganyikiwa kishenzi.

Asubuhi hadi saa 7 ilikua live TVT na Star TV, but jioni wakachomoa hakuna cha LIVE, maana saa hizi Zitto anajibu

hoja na kuwabana, amekua kama Waziri aliyewasilisha, anapewa saa nzima kujibu hoja za wabunge lakini nasikia humo

ndani wanamchanganya kila saa anasimama MBUNGE ama Waziri anasema, "KUHUSU UTARATIBU".

Star TV walianza saa 11 kuonyesha mechi then wakaanza Bongostar, then kipindi cha afya yetu na sasa ni matangazo tu

ya biashara. HII NI AIBU KWA UTAWALA BORA NA DEMOKRASIA, waliona wananchi wataona wanavyodhalilika na jinsi

wasivyotetea maslahi yao

Hoja inatupwa baada ya CCM kushinda kwa kura.

Sasa Mbunge wa Mchinga, mwalimu wa zamani wa Usalama wa TAifa, Mudhihir M. Mudhihr anawasilisha hoja ya kutaka Zito

asimamishwe ubunge kwa kusema uongo. Hoja inajadiliwa na wengi,
anaanza Dr Slaa anasema hakubaliani na hoja ya kumsimamisha ubunge zitto kwa sababu hakuna ushahidi wa kusema uongo

wa zitto haujathibitishwa. Haya wataendelea na baadaye atakuja John Malecela

Adam Malima, kasema watasikitika kumkosa kwenye Kamati ila anastahili adhabu hata ya kukosa mikutano minne ya BUnge kwa kusema uongo, yeye alithibitika kusema uongo hajachukuliwa hatua.

Zitto kasema yuko tayari kwa maamuzi yoyote yatakayotolewa na Bunge..

Malecela sasa anasema
 
Kila kitu kinaanzia na kitu kidogo na kuendelea kuwa kikubwa. Yeye ana uhakika gani madini yaliyochini ni kidogo, (Is he a geologist?). Ndio uhalalishaji wa wizi wa kijinga wanafikiri sisi wote hamnazo, isitoshe hicho kidogo sio chake binafsi ni cha Tanzania na sisi ndio tunataka mikataba mipya kwa rasilimali zetu sio yeye. Yeye kazi yake ni kusikiliza anayotumwa na wale anaowawakilisha na sio vinginevyo.

Mchezo mtamu huu...Zitto kakutana na mafioso...na kwenye hili wadau wanadai ni mtu na mume mwenzie kwa AC. I hope wote walitumia mpira.
 
Humu tutakuwa tunagombana "kiitikadi' baada ya kujali mambo ambayo ni manufaa kwa walio wengi bila kujali vyama vyao!.Zitto alikuwa anahoji ni Vipi Waziri Karamagi kaenda kusaini Mkataba wa madini huko Uk,wakati serikali kwa Tamko lake yenyewe na kwa kupitia Mkuu wa Nchi walisema wana-review mikataba yote ya madini na kutosaini mikataba mingine!.Ni nini kosa la Zitto hapo? kwani si kweli kwamba Waziri Karamagi kasaini Mkataba wa madini wa Buzwagi?.Au Buzwagi ipo Burundi?

Huyu Mswahili Mdhihiri Mdhihiri ni mnafiki tu!,anajua tosha kuwa kabebwa kufikia hapo alipo,alipandishwa kiajabu ajabu kutoka kwenye Street Red Line, Ulinzi wa Viongozi hadi kwenye Uwaziri,na hata huo Ubunge wa Mchinga anaupata kwa migongo ya wapambe wake!Hana haki kuomba kusimamishwa Ubunge kwa Zitto!,inabidi tuwe serious sasa!!!!,Zitto anawakilisha watu wa Kigoma (na ndio waliompigia kura),hatima yake ya uwakilishi itaamuriwa na watu hao!na sio hawa wapambe wanaojipendekeza kwa kumtukuza na kujikomba kwa EL (Kumbukeni kimbelembele cha Mdhihir wakati wa kutajwa kwa Lowasa kuwa PM huko Dodoma).Kwa wale mnaomlaumu Zitto,mlitaka afanye research gani?
 
I wish ningeona huo mjadala live maana kwa jinsi ninavyoliangalia hili suala CCM wanajimaliza wakati wanamjenga Zitto kwa wananchi...I hope Mzee Malecela hajajiingiza kwenye hiki kitanzani...

Watundu waliopo Dodoma mkishindwa kupata Video records basi hata audio records zitatosha....

Tanzanianjema
 
Good vacation for him and those who might need his maverick and contributions......kaka wakati wa kujipanga upya...karibu mapumzikoni..

Tanzanianjema
 
Maskini Zitto,
Wamemkomoa tu! SiSiEmU bwana- sasa imedhibitika ni uwongo gani amesema?
Ila itampandisha sana charti kisiasa!
 
Leo sisemi kitu ila ni aibu tupu kwa TAIFA LETU.... WATANZANIA WATATUSHANGAA SANA
 
Back
Top Bottom