Mugongo Mugongo
JF-Expert Member
- Nov 8, 2006
- 223
- 8
Zitto aliwasilisha vizuri hoja yake nzito yenye vipengele muhimu kumi na moja. Karamagi akajibu kipengele kimoja baada ya kingine (kwa vijembe huku akinukuu vifungu mbalimbali vya sheria za madini na mapato alivyovitumia Zitto, akieleza jinsi Zitto alivyovitumia kulipotosha bunge). Na hapo ndipo alipowapiga bao wengi waliokuwa wanafuata mkumbo.
Kilichotokea ni kwamba majibu ya Karamagi yakawachanganya waliokuwa wamejiandaa kuunga mkono hoja kiasi kwamba wakabaki kuchanganyikiwa wakati wa kuchangia. Kungekuwa na uwezekano wa kujitoa, leo hii wabunge wengi wangemwomba spika aondoe majina yao. Hakuna mbunge hata mmoja aliyeweza kuoanisha hoja za Zitto na majibu ya Karamagi. Inaonyesha walikuwa wamekariri majibu, sasa baada ya Karamagi kumchambua Zitto wakabaki kujiumauma kiasi cha kufikia hatua ya kumwombea msamaha Zitto kwamba alikuwa anahitaji kueleweshwa (Maulida Komu). Wengine wakaanza kusoma vifungu vya Katiba vinavyompa mbunge kinga ya kutoshtakiwa kutokana na atakayochangia bungeni kana kwamba walishaamua kwamba Zitto kadanganya. .. walichanganyikiwa kweli kweli.
Hoja ikabadilishwa ikawa kwamba Kamati Teule iundwe ili kusafisha jina la Karamagi lililochafuliwa na tuhuma hizo. Hapo ndipo nikachoka kabisa. Aliyefurahisha zaidi ni Chacha Wangwe maana hakujua hata anachangia hoja ipi. Leo kwa kweli ilikuwa ni vichekesho tu bungeni.
Leo Karamagi nami kanishangaza manake huwa hajui Kiswahili fasaha lakini leo kakomaa...na kum-reduce Zitto to almost nothing. Kachambua kipengele kimoja baada ya kingine, kwa data na kwa kujiamini. Kila mtu kaona kwamba Zitto alisema uongo ili kutaka umaarufu. Bado nadhani kumfungia sio jawabu, mimi nadhani ile aibu ya kwamba kadanganya, katoa data za uongo ingetosha (ingawa huyu bwana hana uso wa haya hata anapogundulika kasema uongo).
Kama alivyosema Maulida Komu, Mbunge mwenzake wa CHADEMA, anachohitaji Zitto ni kueleweshwa (ingawa shida yake ni kujifanya mjuaji).