Uko nje ya nyumba yako na rafiki zako huku unacheza na mtoto wako mchanga ukiwa umejifunga taulo ghafla unapomrusha juu hewani taulo inaanguka! T.E.N.S.I.O.N
Umepanga kwenda kujua wazazi wa dem wako na ukiwa safarini mzee anatema mate ya tumbaku ndani ya gari na unamtusi vilivyo kufika kwa kina dem wako unapata yuleyule mzee ndio babake! T.E.N.S.I.O.N
Mwanamke umefumaniwa live na mumeo ukivunja amri ya sita nje ya ndoa lakini mumeo anajifanya hana noma na wewe,anachukulia poa tu,hakupigi wala kukuuliza lolote kuhusu kosa lako.
Ukiwa safarini ndani ya basi,umenunua vocha ya sh.10000,unaikwangua na ku-copy namba zake halafu unaitupa nje,unajaribu ku-send,unaambiwa namba ya vocha uliyoingiza haipo.Masikini kumbe uli-copy namba vibaya.>Tension!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.